Je, Kulikuwa na Machafuko Kabla ya Mwanadamu?

Je, Kulikuwa na Machafuko Kabla ya Mwanadamu?

Haiwezekani mtu awepo bila kuzaliwa kutoka kwa mwanamke.
Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa mwanamke alikuwepo kabla ya Dunia na Ulimwengu kuwepo? Kwa sababu umesema kila mtu kazaliwa na mwanamke tangu milele, na dunia ina mwanzo.

Walikuwa wanazaliana wakiwa wapi, angani? Acha ucheshi bhana!
 
Sawa kimsingi kuna tafsiri inadai hivyo lakini ni muhimu kutenganisha na kile ambacho maandiko yenyewe yanasema.
Tukianzia na wazo la Gap theory kwendana na hiyo mwanzo 1:2 inasema kulikuwa na kipindi kirefu ambacho kitu kilitokea kwa mfano uasi wa viumbe wa kidogo na dunia ikawa ukiwa.

Kwa baadhi ya wanaoitafsiri hudhani uumbaji ulianza kwanza kisha tukio la uharibifu alafu ndiyo dunia kuwa ukiwa na tupu (tohu wabohu) mwishowe Mungu kuipanga upya. Lakini ni interpretation si jambo ambalo Mwanzo 1:2 inalielezea moja kwa moja.

Biblia inazungumzia viumbe wa kiroho na uasi wa shetani katika sehemu mbalimbali nafikiri hapa rejea hata kitabu cha Ufunuo wa Yohana 12:7 lakini sasa kwa bahati mbaya hainganishi waziwazi uasi huo na Mwanzo 1:2 ndiyo maana bado haijathibitishwa kuwa kulikuwa na viumbe wakaharibu dunia .

Hilo haijathibitishwa na maandiko yenyewe ila zinabaki kuwa nadharia tu brother.
Atleast umeweza kunijibu, kwamba zimebaki kuwa nadharia kwasababu hakuna kilicho andikwa Asante I'm satisfied mkuu.
 
Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na chanzo, Hata chanzo cha kila kitu kitahitaji kuwa na chanzo chake kingine.

Hivyo kutakuwa na msururu mrefu wa vyanzo vingi visivyokuwa na mwisho.

Hii inaitwa infinite regress of causes.

An infinite regress of causes is an endless chain of events where every cause has its own prior cause going back forever. There is no first event, no start, and no uncaused beginning.

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho exist chenyewe tu bila chanzo.

Na kama si lazima kwamba kila kilichopo kinahitaji kuwa na chanzo, Hata Ulimwengu na vyote vilivyomo except man-made things, Havina na wala havihitaji kuwa na chanzo.

Sikweli.

Ni makisio na makadirio tu.

Kwa sababu hakuna aliye hesabu hizo billion years.

Ni watu tu walikisia.
no uncaused beginning.
 
Hii nadharia yako ya steady state Theory kwamba ulimwengu hauna mwanzo ilishapitwa na wakati na ikatupwa kule tangu miaka ya 1960 baada ya kugundulika kwa cosmic microwave background radiation.
Kama Ulimwengu lazima uwe na mwanzo, Kabla ya Ulimwengu kuanza, Huko ulipokuwa kulianzaje?

Maana mwanzo na wenyewe hauwezi kuanza from nothing.

Unless otherwise, hakuna mwanzo.
 
no uncaused beginning.
Kama no uncaused beginning,

Kwa maana hiyo basi, Hapapaswi kuwa na chochote kilichoanza chenyewe pasipo beginning.

An infinite regress of causes is an endless chain of events where every cause has its own prior cause going back forever. There is no first event, no start, and no uncaused beginning.

Hivyo kutakuwa na msururu mrefu wa vyanzo vingi visivyokuwa na mwisho.

Pasipo kukoma.

Endlessly to infinity.
 
Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa mwanamke alikuwepo kabla ya Dunia na Ulimwengu kuwepo? Kwa sababu umesema kila mtu kazaliwa na mwanamke tangu milele, na dunia ina mwanzo.

Walikuwa wanazaliana wakiwa wapi, angani? Acha ucheshi bhana!
Mkuu una hoja nzuri naendelea kufuatilia mjadala
 
Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa mwanamke alikuwepo kabla ya Dunia na Ulimwengu kuwepo? Kwa sababu umesema kila mtu kazaliwa na mwanamke tangu milele, na dunia ina mwanzo.

Walikuwa wanazaliana wakiwa wapi, angani? Acha ucheshi bhana!
Ulimwengu umekuwepo milele na binadamu na viumbe wengine wamekuwepo milele ndani ya ulimwengu wakizaliana.

Hata sisi binadamu ni part ya Ulimwengu. Tumekuwepo milele.
 
Kama no uncaused beginning,

Kwa maana hiyo basi, Hapapaswi kuwa na chochote kilichoanza chenyewe pasipo beginning.

An infinite regress of causes is an endless chain of events where every cause has its own prior cause going back forever. There is no first event, no start, and no uncaused beginning.

Hivyo kutakuwa na msururu mrefu wa vyanzo vingi visivyokuwa na mwisho.

Pasipo kukoma.

Endlessly to infinity.
Kuongeza utegemezi usio na mwisho haukiondoi chanzo huru kuwepo.
 
Kama Ulimwengu lazima uwe na mwanzo, Kabla ya Ulimwengu kuanza, Huko ulipokuwa kulianzaje?

Maana mwanzo na wenyewe hauwezi kuanza from nothing.

Unless otherwise, hakuna mwanzo.
Ndio maana huwa tunasema chanzo cha kwanza kabisa cha ulimwengu hakiwezi kuwa na mwanzo. Kinapaswa kuwa kitu chenye nguvu ambacho hakijaumbwa, hakijazaliwa, na kiko nje ya muda na nafasi.

Wewe ndio ulikuwa unalazimisha kila kitu lazima kizaliwe na mwanamke!
 
Ulimwengu umekuwepo milele na binadamu na viumbe wengine wamekuwepo milele ndani ya ulimwengu wakizaliana.

Hata sisi binadamu ni part ya Ulimwengu. Tumekuwepo milele.
Acha kukariri neno milele kama wimbo wa taifa! Kama binadamu tumekuwepo milele, mbona hakuna hata fossil moja ya binadamu iliyopatikana kwenye tabaka la ardhi la zama za dinosaurs?
 
Kama kawaida yako kuandika nonsense 😂😂 .

Umetupa jina la nadharia ya kizungu ili uonekane una akili, lakini huna mstari wa kuisimamisha.
Huwa mnatumia mistari gani kusema watoto wa adamu walioana wao kwa wao kaka na dada (incest) wakazaa wakajaza dunia ?
 
Huwa mnatumia mistari gani kusema watoto wa adamu walioana wao kwa wao kaka na dada (incest) wakazaa wakajaza dunia ?
Watakujibu kwasababu Abraham alimuoa dada yake sara, nothin special
 
Hadithi za Biblia ni stori uchwara zilizojaa logical contradictions.

Achana na hadithi zisizo na kichwa wala miguu.
Ni hadithi kwako usiye jua Biblia. Kasome na fanya utafiti kuhusu Biblia ndio uje na conclusion kwamba ni hadithi. Kwa mfano amri kumi ni hadithi? Au kuambiwa kuwa watakufa?
 
Ndio maana huwa tunasema chanzo cha kwanza kabisa cha ulimwengu hakiwezi kuwa na mwanzo.
If nothing comes from nothing.

Hata hicho chanzo cha kwanza cha ulimwengu, Hakiwezi kukwepa kanuni hii.

Hicho chanzo cha kwanza cha ulimwengu hakiwezi kutokea tu from nothing.

Kama chanzo cha kwanza cha ulimwengu kinaweza kukwepa kanuni hii ya " nothing comes from nothing" Basi hata Ulimwengu wenyewe unaweza kukwepa kanuni hii.

Na ulimwengu ukawa ndio mwanzo wenyewe. Bila kuhitaji chanzo kingine.

Lakini tukisimama kwenye kanuni hii ya nothing comes from nothing . Tunarudi kule kwenye infinite regress of causes.

An infinite regress of causes is an endless chain of events where every cause has its own prior cause going back forever. There is no first event, no start, and no uncaused beginning.

Ambapo, Hapapaswi kuwa na chochote kilicho anza chenyewe tu, from nothing.

Hivyo kutakuwa na msururu mrefu wa vyanzo vingi visivyokuwa na mwisho. Pasipo ku stop!
Kinapaswa kuwa kitu chenye nguvu ambacho hakijaumbwa, hakijazaliwa, na kiko nje ya muda na nafasi.
Hata Ulimwengu si lazima uwe umeumbwa.

Na wala ulimwengu hauhitaji kuumbwa.

Lakini kama ni lazima ulimwengu uwe uliumbwa, Hata huyo muumbaji wa ulimwengu atahitaji kuumbwa.

Na huyo muumbaji wa muumba ulimwengu atahitaji kuumbwa.

Patakuwa tena na msururu mrefu wa waumbaji wengi, pasipo kukoma.

Kama kuumbwa ni lazima basi ulazima huu itabidi u-apply kwa kila kitu. Including huyo muumbaji mwenyewe.

Kumu exclude huyo muumbaji kwenye "ulazima wa kuumbwa" halafu kufosi vitu vingine viwe viliumbwa ni kufanya logical fallacy inaitwa special pleading fallacy.

The special pleading fallacy happens when someone applies a general rule to everyone else, but claims an unjustified exception for themselves or their topic. It relies on a double standard and changes the criteria mid-argument without a valid reason.

Kwa hiyo kama kuumbwa ni lazima. Basi ulazima huu ni kwa kila kitu. Pasiwepo chochote kile kilicho exist chenyewe bila kuumbwa. Including huyo muumbaji.

Wewe ndio ulikuwa unalazimisha kila kitu lazima kizaliwe na mwanamke!
Binadamu ndio anazaliwa na mwanamke.

Viumbe wengine vinazalina vyenyewe.
 
Huwa mnatumia mistari gani kusema watoto wa adamu walioana wao kwa wao kaka na dada (incest) wakazaa wakajaza dunia ?
Mwanzo 5:4 inasema wazi kabisa Adamu alizaa wana wa kiume na wa kike. Kama Mungu asingepanga dada zao wawepo, Kaini angemuoa nyani wa porini?
 
Ndio maana nasema hizo hadithi za Biblia ni hekaya za kutungwa zisizo na ukweli wowote ule.

Ni hadithi za kutungwa tu, sawa na hekaya za Abunuwasi, Hadithi za Esopo na hadithi za Kalume kenge.
Nani alitunga hizo hadithi?
 
Mwanzo 5:4 inasema wazi kabisa Adamu alizaa wana wa kiume na wa kike. Kama Mungu asingepanga dada zao wawepo, Kaini angemuoa nyani wa porini?
Sasa hii theory yako ina tofauti gani na pre-adamite theory iliyo sehemu ya mleta uzi?😂
 
Wamefanikiwa kwa kiasi fulani.

Wamefanikiwa kupumbaza watu wengi hasa waafrika wasiotaka kutumia akili zao kufikiri wanabaki kuaminishwa ujinga.

Kuna mazuzu mpaka leo hii, karne ya 21 wanaamini kuna maisha bora baada ya kufa.

Hawapambani wawe na maisha bora hapa duniani. Wanasubiri maisha ya kufikirika huko mbinguni.

Maandiko ya kidini, Biblia ikiwemo imechangia pakubwa kuwapumbaza.
Akina nani hao?. Wakati Biblia inasema asiye fanya kazi na asile. Unajikanyaga sana.
 
Back
Top Bottom