verify
JF-Expert Member
- Dec 31, 2024
- 1,311
- 3,139
- Thread starter
- #141
Upo sahihi pia,Biblia imeanza kwa kusema hapo mwanzo(time) M-ngu aliziumba Mbingu(space) na Nchi(matter) sasa swali ni kuwa je kuna kiumbe chochote kinaishi nje ya hayo mambo matatu?
Kama jibu ni hapana basi hakukuwa na chochote hapo kabla ya mwanzo.
Lakini nielewe hapa kwamba Mungu amekuwepo tangu enzi, hivyo ukuu na uwezo wake haukuanza na uwepo wetu wala hautaishia kwetu. Kwa hiyo, sioni ugumu kusema kwamba kabla yetu huenda kulikuwepo viumbe wengine. Vivyo hivyo, mwisho wa uwepo wetu haumaanishi mwisho wa uumbaji wa Mungu anaweza kuumba viumbe wengine hata baada yetu. Kwa mtazamo huo, tunaweza kusema kwamba kabla ya kizazi chetu huenda kulikuwepo viumbe zaidi, ingawa hili bado linabaki kuwa nadharia na si jambo lililothibitishwa.
Benoit sijui umepata picha nini najaribu kusema hapa ?