Kuna jambo la kuvutia sana katika Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu; na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji.” Aya hii inaweza kutufanya tujiulize swali ambalo mara nyingi tunalipita: nini kilitokea kabla ya hali hii ya ukiwa na utupu? Biblia haitoi maelezo ya moja kwa moja kwamba kulikuwa na vita au viumbe waliokuwa wakiishi duniani kabla ya mwanadamu, lakini ukitazama kwa jicho la udadisi, unaweza kujiuliza ikiwa kulikuwa na tukio fulani lililosababisha hali hiyo ya machafuko. Labda kulikuwa na mabadiliko makubwa, labda machafuko, au hata vita lakini haya ni mawazo ya kutafakari, si ukweli uliothibitishwa na maandiko.
Kama tunaruhusu akili ichunguze zaidi, tunaweza kujiuliza je, “ukiwa na utupu” ilikuwa hali ya mwanzo kabisa, au ilikuwa matokeo ya jambo lililotokea kabla ya simulizi kuanza? Mungu anaonekana kuleta nuru, mpangilio na uhai katika mazingira yaliyoelezwa kuwa na giza na vilindi vya maji. Hii inaweza kutufanya tufikirie uwezekano wa “reset” ya uumbaji si kwamba Biblia inasema Mungu alifanya reset baada ya vita, bali kama hypothesis ya kifalsafa. Huenda kulikuwa na historia ambayo haijaelezwa huenda hakuna kitu kilichokuwepo kabla yake. Pengo hilo ndilo linaloifanya akili iulize.