kwanza unafanya kosa la kulinganisha nyanya na embe! JF siyo nchi mtu huwezi kujianzishia ya kwako! Mtu anayeikandia JF kwa vile ni "tawi la chadema" na hao wana "chadema" wanamuacha achangie na kuwakandia aidha hazimo au haoni contradictions. Kama JF ni ya chadema (sijui kama wewe ni mmoja wa wanaomini hivyo) sasa wale wasio na vyama na wana CCM au wa vyama vingine kwanini wakeshe hapa?
Ukweli ni kuwa hapa ni mahala pa wote na chadema siyo mmiliki au mwenye hisa hapa. Sasa hili watu hawataki kuambiwa. Yaani, forum ya chama ambacho mwenyekiti wake anaitwa mbakaji wa watoto wadogo bado inaendelea kuvumilia mawazo ya mtu yule yule?
Kama tukiamini japo kwa sekunde kuwa hii ni ya chadema, then Chadema wako mbali sana kwenye uhuru wa mawazo ukilinganisha na chama chenye miaka zaidi ya hamsini!
Ndio maana nikajenga hoja kuwa kama watu wanaona hii ni ya chadema, kwanini wasianzishe ya CCM na sisi tukeshe huko tukiwatukana viongozi wao tuone wao watavumilia kiasi gani.
Nungwi, usiwe na shaka mimi ni kama wewe sina chama na sijapiga magoti mbele ya chadema wala kutoa sadaka kwa CCM! na kitu pekee kwangu ni Tanzania.