Je, Kikwete ni mdini?

Je, Kikwete ni mdini?

Mods, na wana JF,

Haitakuwa busara kwa thread hii kuipeleka sehemu ya dini, inajulikana sehemu hiyo haifikiwi na watu wengi hapa JF ikiwa mimi mmoja wapo.

Ni matumaini yangu kuweza kuiaccess hii thread na kuona mijadala ikichangiwa ili kuweza kujua ukweli.


Sitegemei kuwa JF/Mods wapo kwa ajili ya kuchochea chuki dhidi ya Serikali iliyopo madarakani kwani kama itakuwa ni hivyo basi wanafanya jambo la hatari sana linaloweza kutugharimu. Tumeona ile thread ya OIC ikiachiwa kuchangiwa na kila mtu na mwenye kila tusi dhidi ya dini ya kiisamu na kejeli akiachiwa kwa marefu na mapana. Kwahiyo sioni sababu ya hii thread ya kisiasa zaidi kutupiwa huko kusikojulikana.


Mwisho napenda kutoa angalizo:

Sio haki kuhamisha thread ya mtu na kuipeleka sehemu asiyokuwa na access nayo. Hapa JF ni sehemu ya kutoa mawazo na kila mmoja aheshimiwe mawazo yake na sio kufungwa na kutupwa kapuni.

Kuna tetesi Zimeenea mtaani kuwa baada ya JK kuingia madarakani aligomea ruzuku iliyokuwa ikitolewa na Serikali kuendesha makanisa pamoja na taasisi zinazoendeshwa na makanisa katoliki nchini kama shule, hospitali na vyuo. "The Government shall provide financial assistance to Church institutions and shall seek financial assistance to Church run social services in its bilateral negotiations with foreign governments"

source
:The Memorandum of Understanding between the Government of the United Republic of Tanzania and the Tanzania Episcopal Council (TEC) and the Christian Council of Tanzania-page 3 (attached herewith)

Nasikia JK aliwaambia kuwa nchi hii haina dini na itakuwa ubaguzi kuwapa ruzuku watu wa dini moja na kuwaacha wa dini nyinginezo akatolea mfano kuna waislam, wabudda, masingasinga, wahindu na wasiokuwa na dini je hao hawana haki ya kupewa ruzuku? na serikali ikitoa ruzuku kwa hawa wote itawezaje kujiendesha? Basi bora mkose wote. Hapo naona JK aliona mbali sana ila hakujua kama anajiharibia yeye na chama chake. Na ndio maana kwa kutumia mlango wa nyuma kuna chama kikasimamisha watumishi wa Mungu kwa wingi na kufanikiwa kupenya kila pembe ya Tanzania. Inasemekana Kanisa liliplay part kubwa kwa mafanikio ya chama fulani. Na hizo zilikuwa ni hasira za watumishi wa kanisa.

KUNA TETESI KUWA WAFUATILIAJI WA MAMBO WAMEITHIBITISHIA SERIKALI UBADHIRIFU MKUBWA WA RUZUKU ILIYOKUWA INATOLEWA NA SERIKALI SAMBAMBA NA MISAMAHA YA KODI. MISAMAHA HII YA KODI NI ILE YA UAGIZWAJI MAGARI NA VITU MBALIMBALI KUPITIA TRUSTEES ZA MAKANISA. NA TANGU KUANZA KUBANWA KUMEKUWA NA UAIGIZAJI WA VITU MDOGO TOFAUTI NA HAPO MWANZO, MAANA INASEMEKANA WAJANJA WALIKUWA WANATUMIA MWANYA HUO KUJINUFAISHA.

Ukiunganisha picha itaona hapo ndio chanzo hasa cha timbwili hili mnaloliona leo lililo vikwa ngozi ya vyama vya siasa ( upinzani ). Hapo awali Wakristo na CCM walikuwa chanda na pete. Ilikuwa ni kosa la jinai kwa mkristo mwenye imani kuwa upinzani ndio maana hata viongozi wao wengi mwaka 2005 walisema JK "chaguo la Mungu"

Leo hii ukitia pua tu JF na maeneo mengi kwenye mitandao na mitaani utakutana na shutuma kuwa JK ni Mdini, lakini hawatoi facts za udini wake.

Je, JK ni mdini?

Orodha ya Baraza la Mawaziri na Manaibu wa Wizara 26 za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2010 - 2015


  1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora - Mathias Chikawe (Mkristo)
  2. Waziri wa Nchi, Oisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu - Steven Wassira (Mkristo)
  3. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma - Hawa Ghasia
  4. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Waziri wa Muungano - Samia Suluhu Hassan
  5. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Waziri wa Mazingira - Dk. Terezya Luoga-Hovisa (Mkristo)
  6. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge - William Lukuvi (Mkristo)
  7. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji - Mary Nagu (Mkristo)
  8. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - George Mkuchika (Mkristo)
  9. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (i) - Aggrey Mwanri (Mkristo)
  10. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (ii)Kassim Majaliwa -
  11. Waziri Wizara ya Fedha - Mustapha Mkullo
  12. Naibu Waziri Wizara ya Fedha (i) - Gregory Teu (Mkristo)
  13. Naibu Waziri Wizara ya Fedha (ii) - Pereira Ame Silima
  14. Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi - Shamsi Vuai Nahodha
  15. Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi - Balozi Khamis Suedi Kagasheki
  16. Waziri wa Katiba na Sheria - Selina Kombani (Mkristo)
  17. Waziri Wizara ya Mambo ya Nje - Bernard Membe (Mkristo)
  18. Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje - Mahadhi Juma Mahadhi
  19. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa - Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi
  20. Waziri Wizara yaMaendeleo ya Mifungo - Dk. Mathayo David Mathayo (Mkristo)
  21. Naibu Waziri Wizara ya Maendeleo ya Mifungo - Benedict Ole Nangoro (Mkristo)
  22. Waziri Wizara ya Mawasiliano Sayansi ya Teknolojia - Profesa Makame Mnyaa M'barawa
  23. Naibu Waziri Wizara ya Mawasiliano Sayansi ya Teknolojia - Charles Kitwanga(almaaruf Mawe Matatu) (Mkristo)
  24. Waziri Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi - Profesa Anna Kajumulo-Tibaijuka (Mkristo)
  25. Naibu Waziri Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi - Goodluck Ole Medeye (Mkristo)
  26. Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii - Ezekiel Maige (Mkristo)
  27. Waziri Wizara ya Nishati na Madini - William Mghanga Ngeleja (Mkristo)
  28. Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini - Adam Kighoma Ali Malima
  29. Waziri Wizara ya wa Ujenzi (Barabara na Viwanja vya Ndege) - Dk. John Pombe Magufuli (Mkristo)
  30. Naibu Waziri Waziri Wizara ya wa Ujenzi - Dk. Harrison Mwakyembe (Mkristo)
  31. Waziri Wizara ya Uchukuzi - (Reli, Bandari, Usafiri wa Majini) - Omary Nundu
  32. Naibu Waziri Wizara ya Uchukuzi - Athuman Mfutakamba
  33. Waziri Wizara ya Viwanda na Biashara -Dk. Cyril Chami (Mkristo)
  34. Naibu Waziri Wizara ya Viwanda na Biashara - Lazaro Nyalandu (Mkristo)
  35. Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi - Dk. Shukuru Kawambwa (Mkristo)
  36. Naibu Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi - Philipo Mulugo (Mkristo)
  37. Waziri Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii - Dk. Haji Hussein Mpanda
  38. Naibu Waziri Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii - Dk. Lucy Nkya (Mkristo)
  39. Waziri Wizara ya Kazi na Ajira - Gaudensia Kabaka (Mkristo)
  40. Naibu Waziri Wizara ya Kazi na Ajira - Dk. Makongoro Mahanga (Mkristo)
  41. Waziri Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto - Sophia Simba
  42. Naibu Waziri Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto - Umi Ali Mwalimu
  43. Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo - Emmanuel John Nchimbi (Mkristo)
  44. Naibu Waziri Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo - Dk. Fenela Mukangala (Mkristo)
  45. Waziri Wizara ya Ushirikiano Afrika Mashariki - Samuel John Sitta (Mkristo)
  46. Naibu Waziri Wizara ya Ushirikiano Afrika Mashariki - Abdallah Juma Abdallah
  47. Waziri Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika - Profesa Jumanne Maghembe
  48. Naibu Waziri Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika - Christopher Chizza (Mkristo)
  49. Waziri Wizara ya Maji - Profesa Mark James Mwandosya (Mkristo)
  50. Naibu Waziri Wizara ya Maji - Gerson Lwinge (Mkristo)

Jumla yote ni 50 kati yao wakristo 32 na waislam 18.

Wakristo 64%
Waislam 36%

Ukiangalia wakuu wa mikoa na wilaya utaona wakristo ni wengi zaidi ya waislam sasa sijui na sifahamu huo udini wa JK upo wapi???

Mwenye data tafadhali azilete jamvini.


Kuna habari za hivi punde ni kuwa kuna makampuni zaidi ya 80 ya clearing and forwarding yamefungiwa kwa sababu mbalimbali kubwa hasa ubabu mashi. Inajulikana kwenye sekta hii watu wa kutoka mkoa fulani wameishikilia kwa asilimia zaidi ya 80. Inasemekana sifa ya watu wanaotoka huko ni ujanja mwingi na ni wakwepaji wakubwa wa kodi na walitumia vizuri sana nafasi ya kuwa na udugu kuanzia uwaziri mpaka kamishna wakati wa Che Nkapa.

Ushauri kwa JK, Mkuu wee endelea kukaza buti watu walipe kodi kwa manufaa ya nchi usijali tunakusapoti kwa maana hawana shukrani Serikali imewaachia wamekula sana kodi kupitia ukwepaji na misamaha hewa lakini wamekuwa mbele kunyea kambi.

kwa ukweli watu kama wewe wananikera sana,tunajua umetumwa lakini wewe na waliokutuma iko siku mambo haya yatawatokea puwani.upuuzi mtupu jamani hivi ninyi watu flani mnaotaka kumsafisha JK mtafanya hivyo mpaka mbinguni?mbona mengine hamyasemi?au mnataka tuanze kumwaga kila kitu hapa itakuwa haibu.

BUT FRIEND TIME IS KNOCKING ON THE DOOR..........
 
Tuache udini watanzania tuna ishi kwa raha lakini kwa nini suala hili liibuke wakati huu kwani 2005-2010 JK si yulyule
 
Mbona huongei chuo cha Tanesco MORO KUWA CHUO CHA WAISLAM, Hujagusia shule kama SONGEA BOYS, SANGU secondary, Tabora Boys kama zilikuwa za catholic, na kwa taarifa yako NHC nyingi ni za wahindi nenda uendako miji mingi mikubwa ya tanzania ilijengwa na wahindi na ndio wengi walionyan'anywa nyumba wala sio waislam, Old Moshi ilikuwa ya wahindi leo ya serikali hausemi, Makamba mwislam aliwahi kusema wakati wenzetu wakristo wanakwenda shuleni kupata elimu dunia sisi waslam tulikuwa tunakwenda madrasa.

Idadi ya mawaziri wakristo inatakiwa hivyo au ilitakiwa kuwa kubwa zaidi ya hapo nafikiri wajua idadi ya wakristo na waislam ipo tofauti ukibisha hamnazo,

Mimi nimekuwa nikifuatilia hoja za waislam kuhusu udini na mengineyo nimeona mara nyingi sio tatizo lao bali wanamatatizo ya inferiority complex ambayo inasababishwa na maustaaadh wasokuwa na data bali kupandikiza chuki na mifarakano katika jamii kama wewe. Na uende uendako JF haitafungiwa kama sababu ni dini
 
Mbona huongei chuo cha Tanesco MORO KUWA CHUO CHA WAISLAM, Hujagusia shule kama SONGEA BOYS, SANGU secondary, Tabora Boys kama zilikuwa za catholic, na kwa taarifa yako NHC nyingi ni za wahindi nenda uendako miji mingi mikubwa ya tanzania ilijengwa na wahindi na ndio wengi walionyan'anywa nyumba wala sio waislam, Old Moshi ilikuwa ya wahindi leo ya serikali hausemi, Makamba mwislam aliwahi kusema wakati wenzetu wakristo wanakwenda shuleni kupata elimu dunia sisi waslam tulikuwa tunakwenda madrasa.

Idadi ya mawaziri wakristo inatakiwa hivyo au ilitakiwa kuwa kubwa zaidi ya hapo nafikiri wajua idadi ya wakristo na waislam ipo tofauti ukibisha hamnazo,

Mimi nimekuwa nikifuatilia hoja za waislam kuhusu udini na mengineyo nimeona mara nyingi sio tatizo lao bali wanamatatizo ya inferiority complex ambayo inasababishwa na maustaaadh wasokuwa na data bali kupandikiza chuki na mifarakano katika jamii kama wewe. Na uende uendako JF haitafungiwa kama sababu ni dini

umesahau Pugu secondary -catholic, minaki sec-anglica, muhimbili hosp-anglican
 
Zanzibar vipi?unasema mnaweza mbona wasionyeshe mfano kuwa hiyo dini unayosema huku imekandamizwa???????????Naomba masuala ya dini tuwaachie hao wanaofaidi kwa kutujaza ujinga wa dini.Tuongelee maendeleo yetu na mustakabali wa Taifa.Je wao walipeleka hoja kwa serikali wakanyimwa hiyo ruzuku???Kanisa lina hospitali KCMC,Bugando,vyuo St.August,Tumaini etc ambavyo hakuna ubaguzi wa huduma.Ni kwa nini basi watumie sadaka za wakristo tu?Ndio maana wanaiomba serikali na yenyewe ichangie au basi leteni sadaka za msikitini nazo zitumike kwenye maendeleo ya jamii,na sio kulalamika kuwa wakristo wanapendelewa.Lete data na hoja,tusipeane nafasi kutokana na dini.Namkumbuka jamaa mmoja tukiwa A Level alijikita sana kwenye dini akapata 0,wenzake waliojikita kwenye masomo wakafaulu Je ikitokea nafsi ya uongozi tumpe aliyesoma akapata div.1 au anayekuja na hoja ya udini huku alishindwa akapata 0.Amua mwenyewe sokomoko.
 
Zanzibar vipi?unasema mnaweza mbona wasionyeshe mfano kuwa hiyo dini unayosema huku imekandamizwa???????????Naomba masuala ya dini tuwaachie hao wanaofaidi kwa kutujaza ujinga wa dini.Tuongelee maendeleo yetu na mustakabali wa Taifa.Je wao walipeleka hoja kwa serikali wakanyimwa hiyo ruzuku???Kanisa lina hospitali KCMC,Bugando,vyuo St.August,Tumaini etc ambavyo hakuna ubaguzi wa huduma.Ni kwa nini basi watumie sadaka za wakristo tu?Ndio maana wanaiomba serikali na yenyewe ichangie au basi leteni sadaka za msikitini nazo zitumike kwenye maendeleo ya jamii,na sio kulalamika kuwa wakristo wanapendelewa.Lete data na hoja,tusipeane nafasi kutokana na dini.Namkumbuka jamaa mmoja tukiwa A Level alijikita sana kwenye dini akapata 0,wenzake waliojikita kwenye masomo wakafaulu Je ikitokea nafsi ya uongozi tumpe aliyesoma akapata div.1 au anayekuja na hoja ya udini huku alishindwa akapata 0.Amua mwenyewe sokomoko.

Ushahidi wa malengo haya unaonekana wazi kwenye vitabu vya Jan P van Bergen Development and Religion in Tanzania: Sociological soundings on Christian participation in rural transformation, John C. Sivalon Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, Frieder Ludwig Church & State in Tanzania: Aspects of a Changing Relationship, 1961–1994. Uchunguzi wa vitabu hivyo pamoja na vya Bwana Mohamed Said na Dkt. Hamza Njozi unaonyesha vipi Kanisa lilivyoitumiya Dola ya Tanganyika na baadaye ya Tanzania kujiimarisha ndani ya nchi kwa kuwazuwiya Waislam wasipige hatua za kimaendeleo zitakazoweza


Kwaheri Ukoloni, Karibu Uhuru! 299
kuwapita Wakristo.
Tafauti na Waislam, wakala za kujitoleya na taasisi za Kikristo zinatowa mchango mkubwa katika huduma za kiafya na za kiilimu Tanzania. Huduma nyingi za kiafya katika sehemu za vijijini huwa zinatolewa na taasisi hizo ambazo zinapata misaada kutoka kwa wafadhili wa taasisi za kimataifa. Inakuwa ni vigumu kwa Waislam kupata misaada kutoka nchi za Kiislam na taasisi za kimataifa. Upande mmoja wameelemewa na vita vya kipropaganda dhidi ya Waarabu Waislam na utumwa wa Waislam ambavyo vinawaghadhibisha na kuwakimbiza wafadhili Waislam na taasisi za Kiislam. Au zitatafutwa taasisi za Waislam ambazo zimejaa ufisadi na kuwafanya wafadhili Waislam na taasisi za Kiislam zikataye kuwasaidiya Waislam kwa kupitiya taasisi hizo. Baina ya mifarakano yote hiyo Wakristo wanaongeza na wanaongezewa nguvu na waumini wenzao kutoka nchi za Magharibi.
Tarehe 21 Februari mwaka 1992, Baraza la Kikristo Tanzania na Baraza la Maaskofu Katoliki walitiya saini Mkataba wa Maridhiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoandaliwa na Profesa, Dokta, C. R. Mahalu wa Kitengo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na kutiwa saini na Edward Ngoyai Lowassa kwa niaba ya Serikali, Elinaza Sendoro kwa niaba ya Baraza la Kikristo Tanzania, na Josephat Lebulu, kwa niaba ya Baraza la Maaskofu Katoliki.
Mkataba wa Maridhiano una lengo zuri la kuendeleza huduma za afya na ilimu katika jamii na unaikalifisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania:
…itajitahidi kujumuisha misaada ya kifedha kwa ajili ya huduma za jamii zinazomilikiwa na ‘Makanisa' itakapokuwa katika mazungumzo ya kuomba misaada husuusan mazungumzo yake na Jamhuri ya Kifedirali ya Ujerumani. Uwezekano kama huo uangaliwe pia itakapokuwa na mazungumzo na wafadhili wengine.22
Wakati Zanzibar ilipotaka kujiunga na shirika la Kiislam la Organization of Islamic Conference (OIC), Askofu E. Sendoro wa Mkataba wa Maridhiano alitahadharisha juu ya uamuzi wa kitendo hicho kwa kusema: "Zanzibar ikiwa ni Dola ya Kiislamu, itaendeleya kuwa sehemu ya Muungano? Bunge la Muungano litakuwa na dhamana juu ya Zanzibar au lipo kwa ajili ya Tanzania Bara?"23
Askofu Sendoro kalikozesha suala la Zanzibar kutaka kujiunga na OIC na kulifanya ni suala la Zanzibar kutaka kuwa Dola ya Kiislam. Kwani Mkataba wa Maridhiano ambao lengo lake kubwa ni kuendeleza huduma za kijamii za Kanisa katika sekta za ilimu na afya ulikuwa na lengo la kuifanya Tanzania kuwa Dola ya Kikristo? Kwa vile Mkataba wa Maridhiano ni mkataba baina ya Taasisi zisizo za kiserikali na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jee, ulipata baraka za Baraza la Wawakilishi la nchi ya Zanzibar na Bunge la Jamhuri ya Muungano au ilionekana kuwa hakuna haja ya kufanya hivyo?

From the book Kwaheri Ukolonin Karibu Uhuru page number 209 - 300
 
nimekupata vizuri sasa tukija kwenye hili la dini ni lazima tuangalie madhehebu ya dini ili kuyawakilisha vizuri au mtu akiwa ni mkristu basi ni mkristu tu; kwa mfano, tuhakikishe Wakatoliki, Walutheri na Wapentekoste nao wanakuwa represented vizuri kama vile Sunni, Shia, Answar?

Kitafute kitabu Cha Haridh Ghasany kwakuwa upo nje itakuwa rahisi kukipata kisha soma kuanzia ukurasa wa 299 - 300 utaona mikakati ya ukristo kuukandamiza uslam na hata mapinduzi ya zanznibar ni kuogopa dola ya kiislam mwandishi ameelezea kwa kina na kunukuu vitabu kadha wa kadha vilivyo andikwa na wazawa pamoja na wazungu. Dont miss nadhani ukikisoma utachangia hoja kwa upeo mkubwa na hutakuwa mnafiki.

Shukran
 
hakuna anayesema kikwete ni mdini,...kikwete ni fisadi..acheni kujadili mada isiyo na faida kwa taifa,mtu yoyote asiye na uwezo wa kujenga hoja anakuja na hoja ya udini kama kikwete sasa hivi na huyo mfuasi wake:embarrassed:
 
Washindwe kabisa wote wanaotaka kutugawa kwa misingi ya dini zetu wakati kuwa Kiongozi si sababu ya kuanzishwa dini.

Najua ni njama za mafisadi kutaka kuendelea kukaa madarakani huku wakiendelea kuitafuna nchi yetu.

Mimi najua kati yangu mimi na wewe hakuna udini ila watu wachache wakiwemo mafisadi ndo wanaitumia udini ili kutufunga macho na kutugawa,
Amkeni muwe macho..............
 
Kikwete mdini sana tu...baraza lake limejaa waislamu 33 na wakristo 17..damn! isitoshe sipendi kuona hao 17 kwanza hawana uwezo, hawajasoma, hawafai kabisa...wakristo wanachapa kazi bana sio mchezo...angalia ngeleja..umeme hakuna mgao, angalia sophia simba..hana mchezo, angalia mkuchika hana utani...JK ondoa hao 17 weka watu waliosoma achana na madrasasultul...hawana elimu...

JK anawaogopa wakristo period!
 
kigezo cha baraza la mawaziri nadhani si jibu sahihi la hili swali/hoja ni kwamba anakandamiza dini au thebu gani na kupendelea lipi lakini nadhani serikali haina dini
 
Imagine ingekuwa waislam wamesign huu mkataba wa siri...

Naona nchi ingebiruka juu chini


waislam walianzisha shule au hospitali wakanyimwa ruzuku??na hizo shule si walikuwa wanasoma wa dini zote??na hospitali si wanatibiwa wote??tatizo la waislam badala ya kujenga shule na hospitali wanajenga madrasa na misikiti ili wawajaze chuki watoto..ukweli ni kwamba waarabu wamewarithisha mawazo ya kimaskini...eti siku hizi kuna seminari za kiislam,thank god wameiga kitu positive labda uhalifu utapungua
 
Imagine ingekuwa waislam wamesign huu mkataba wa siri...

Naona nchi ingebiruka juu chini


waislam walianzisha shule au hospitali wakanyimwa ruzuku??na hizo shule si walikuwa wanasoma wa dini zote??na hospitali si wanatibiwa wote??tatizo la waislam badala ya kujenga shule na hospitali wanajenga madrasa na misikiti ili wawajaze chuki watoto..ukweli ni kwamba waarabu wamewarithisha mawazo ya kimaskini...eti siku hizi kuna seminari za kiislam,thank god wameiga kitu positive labda uhalifu utapungua


Wewe ni mdini na una chuki na waislamu..nenda kasome uislamu with positive mind..
 
Tanzania Haina Udini na Haitakuwa na Udini Kamwe. Hizi Posts Kama Hii Inaonyesha Jinsi Gani Baadhi ya Wananchi Mnataka Tuzungumzie Issues Kwenye Angle ya Udini. Yes JK Aliiba Kura Lakini I am Not Going to Accuse Him Kwamba ni Mdini Thats Enough. Hii Nafasi ya Kijamii Inamalengo ya Kujenga Inchi kwa Kuelimishana na Tanzania is Great Country In Terms of Religious and Tribalism Issues Ukilinganisha na Inchi Nyingi Africa. Ukiangalia Wengi Tunaojadili Hizi Issues ni Vijana wa Tanzania na Kama Sisi Vijana Tunaelekea Kupandikiza Udini, Tutaiharibu Tanzania na Tutarudi Nyuma Kama Kenya na Rwanda. Its Ok Kuwa Critical na Government Bila Kudiscuss Issues za Dini na Ukabila...

"Lets Put Forward Discussions That Build Our Democracy and Development Initiatives"

tatizo swala la udini kalianzisha rais(kama kweli ni rais halali),should anything destructive happen to this country as far as religion is concerned,JK must be held responsible,he has planted a very bad seed,its sad but i must admit i begin to hate him for that:redfaces:
 
tatizo swala la udini kalianzisha rais(kama kweli ni rais halali),should anything destructive happen to this country as far as religion is concerned,JK must be held responsible,he has planted a very bad seed,its sad but i must admit i begin to hate him for that:redfaces:

Ulitakiwa kumpongeza ..wewe mwenyewe mdini
 
This post from Sokomoko is one of the post that need to be discussed and im very happy for bringing this matter here coz majority of us here in JF tunaeneza propaganda za ajabuajabu kuhusu Kikwete na Uislam.

Big up sokomoko
 
Naelewa ninachosema. Mimi sikubaliani na suala la ubaguzi wowote kama ni la udini, au rangi. Ninachosema kwamba kuna watu ambao wanapinga kwamba TZ haina udini wakati wananchi wake na rais wake wameconfirm kwa nchi TZ kuna udini. Suala la population kati ya hizi dini ni kuonyesha jinsi gani TZ ipo ktk tatizo kubwa zaidi kwa sababu hatuna statistic zinazoonyesha population kati hizi dini mbili.

UNAPOSEMA RAIS AMECONFIRM KUWA KUNA UDINI UNAMAANISHA NINI??RAIS AMECONFIRM KUNA UDINI??AMECONFIRM VIPI???ALIMTAJA NANI NI MDINI ZAIDI YA MAJUNGU NA KUISHIWA SERA ILI IONEKANE WAKRISTO WANAMPINGA SABABU YA DINI YAKE NA SI UTENDAJI WAKE MBOVU!!!FIKIRI KABLA HUJAONGEA KITU...USIMWAMINI SANA RAIS WAKO MAANA KWENYE KAMPENI HIZI AMETUONYESHA YEYE NI NANI,..HE CAN STOOP SO LOW FOR POWER...SHAME ON HIM
 
Naelewa ninachosema. Mimi sikubaliani na suala la ubaguzi wowote kama ni la udini, au rangi. Ninachosema kwamba kuna watu ambao wanapinga kwamba TZ haina udini wakati wananchi wake na rais wake wameconfirm kwa nchi TZ kuna udini. Suala la population kati ya hizi dini ni kuonyesha jinsi gani TZ ipo ktk tatizo kubwa zaidi kwa sababu hatuna statistic zinazoonyesha population kati hizi dini mbili.

UNAPOSEMA RAIS AMECONFIRM KUWA KUNA UDINI UNAMAANISHA NINI??RAIS AMECONFIRM KUNA UDINI??AMECONFIRM VIPI???ALIMTAJA NANI NI MDINI ZAIDI YA MAJUNGU NA KUISHIWA SERA ILI IONEKANE WAKRISTO WANAMPINGA SABABU YA DINI YAKE NA SI UTENDAJI WAKE MBOVU!!!FIKIRI KABLA HUJAONGEA KITU...USIMWAMINI SANA RAIS WAKO MAANA KWENYE KAMPENI HIZI AMETUONYESHA YEYE NI NANI,..HE CAN STOOP SO LOW FOR POWER...SHAME ON HIM

Napenda nikusihi ndugu yangu utumie maneno yasiyoweza kuleta madhara ni kweli kuwa kila mmoja ana uhuru wa kuongea au kutoa mawazo lakini uhuru una mipaka yake. Nchi hii hakuna marais wawili so take care
 
Kwa hiyo hata kama hao waislam wamefeli utawapa tu nafasi ya kusoma na walopass unawaacha??u would be the worst president since the creation of the planet earth
 
Back
Top Bottom