kagumyamuheto
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 286
- 3
wakati nasoma o-level pale Maengo sec - Dodoma, kuna mwalimu (maaraufu - Kifutu - mhaya) aliwahi kula kiapo cha kunifukuza shule au yeye aache kazi. kisa eti mimi ni muislamu. nilikuwa nakaa bweni la Mwenge na kila mara nikienda kuchota maji pale kwake karibu na bweni akinifukuza. alikuwa mwalimu wa A-level na mimi nipo O-level. sasa nikawa najiuliza kwa nini mimi tu? baadae nikagundua kuwa ananichukia kwa vile nilipendelea kuvaa kofia. alifikia mahala akishinikiza nipewe suspension na nikapewa lakini niliappeal na mwalimu TETE akanisimamia na nikashinda na kuendelea na shule. huyu mwalimu alikuwa muumini sana wa kanisa. hiyo ndiyo hali halisi.
hayafai kusemwa haya lakini yamefanyika mengi. mimi nilimsamehe kwani hakujua maana ya mafundisho ya Biblia - mpende adui yako!
tuweni na nia safi mioyoni mwetu na pale penye uovu hata kama unafanywa na muumini au kiongozi wako tusimame kwenye utaifa na uzalendo. nchi hii ni yetu sote. hakuna mwenye haki juu ya mwingine. turejee historia na tuone akina nani walipigania uhuru wa nchi hii. je, sio wale wanaokaa madrasa na kula ubwabwa kama tunavyowabeza sasa?
hayafai kusemwa haya lakini yamefanyika mengi. mimi nilimsamehe kwani hakujua maana ya mafundisho ya Biblia - mpende adui yako!
tuweni na nia safi mioyoni mwetu na pale penye uovu hata kama unafanywa na muumini au kiongozi wako tusimame kwenye utaifa na uzalendo. nchi hii ni yetu sote. hakuna mwenye haki juu ya mwingine. turejee historia na tuone akina nani walipigania uhuru wa nchi hii. je, sio wale wanaokaa madrasa na kula ubwabwa kama tunavyowabeza sasa?