Je, Kikwete ni mdini?

Je, Kikwete ni mdini?

Kuna jambo ambalo huwa nashindwa kuelewa kwanini watu wanasoma halafu hawatafakari mambo kisayansi. Dini na haswa katika nchi kama Tanzania siyo kitu cha kuringia. Kwanza kabisa hakuna aliye na uthibitisho kuwa dini yake ni bora kuliko nyingine. Pili sidhani kwamba kuna didni inayofundisha (kutoka maandishi ya mitume) kuwa umchukie mwenzako, jirani yako, kuikashifu dini yake, kuidharau dini yake, kujenga chuki hadi kumtoa roho kwa sababu ni dini tofauti na yako. Baada ya kusema hayo sidhani kuwa anayeweza kuandika kashfa kwa dini nyingine anaifahamu dini yake vyema. Anajifanya tu na ni kibaraka wa watu wenye kutafuta watu walio na akili nyepesi kufuata matakwa yao tena kwa kudanganywa na pesa kidogo tu. Ni jambo la kusikitisha kuwa hatufiki mahali tukakubali kuwa hata kama dini moja katika nchi na haswa kama Tanzania kuizidi dini nyingine hilo siyo jambo la kuanzia mipango ya uadui. Badala yake ingekuwa ni changamoto ili kila mwenye dini ya kweli rohoni ajitahidi kuingia kwenye ushindani kielimu na kiuchumi ili kuyamudu maisha na bila kulewa chuki na jirani yake. Dini, mtu hukaa nayo moyoni mwake ikifanya kazi ndani yake na matendo yake ndiyo yanayoonyesha kitu au hazina aliyo nayo moyoni mwake. Na jamii iliyomzunguka hutambua hilo kirahisi kabisa.
Jambo la muhimu kujiuliza ni je huoni kuwa ulizaliwa huna dini yoyote na ungeweza kuwa dini yoyote wakati unalelewa na wale waliokulea? Au waliokuelimisha?? Sasa iweje leo hii imechukua hata jukumu la kuikashifu dini ya jirani yako? Mtu yeyote mwenye akili timamu aliyeelimika na hswa Mtanzania anatakiwa kuelewa kuwa udini hauna nafasi dunia ya leo na tunaomba aliye na hisia hizo ajifunze na kuacha mara moja kupima wenzake kwa vigezo vya aina hiyo. Ajipime yeye mwenyewe kwanza na ajielimishe kistaarabu. Halafu arudi atuandikie mambo mema zaidi hapa JF. Hatuna muda mwingi wa kupoteza!
 
Tanzania Haina Udini na Haitakuwa na Udini Kamwe. Hizi Posts Kama Hii Inaonyesha Jinsi Gani Baadhi ya Wananchi Mnataka Tuzungumzie Issues Kwenye Angle ya Udini. Yes JK Aliiba Kura Lakini I am Not Going to Accuse Him Kwamba ni Mdini Thats Enough. Hii Nafasi ya Kijamii Inamalengo ya Kujenga Inchi kwa Kuelimishana na Tanzania is Great Country In Terms of Religious and Tribalism Issues Ukilinganisha na Inchi Nyingi Africa. Ukiangalia Wengi Tunaojadili Hizi Issues ni Vijana wa Tanzania na Kama Sisi Vijana Tunaelekea Kupandikiza Udini, Tutaiharibu Tanzania na Tutarudi Nyuma Kama Kenya na Rwanda. Its Ok Kuwa Critical na Government Bila Kudiscuss Issues za Dini na Ukabila...

"Lets Put Forward Discussions That Build Our Democracy and Development Initiatives"
 
Hebu hizi topic za Kikwete na udini tafadhali zifungeni kwani zinachefua moyo!

KILA SIKU NI HAYO HAYO HAKUNA JIPYA
 
Hebu hizi topic za Kikwete na udini tafadhali zifungeni kwani zinachefua moyo!

KILA SIKU NI HAYO HAYO HAKUNA JIPYA
Kisha muache kulalamika kama JK mdini. Maana mmeshindwa kutoa ushuhuda mioyo yene inauma kwa ukweli.
 
Tanzania Haina Udini na Haitakuwa na Udini Kamwe. Hizi Posts Kama Hii Inaonyesha Jinsi Gani Baadhi ya Wananchi Mnataka Tuzungumzie Issues Kwenye Angle ya Udini. Yes JK Aliiba Kura Lakini I am Not Going to Accuse Him Kwamba ni Mdini Thats Enough. Hii Nafasi ya Kijamii Inamalengo ya Kujenga Inchi kwa Kuelimishana na Tanzania is Great Country In Terms of Religious and Tribalism Issues Ukilinganisha na Inchi Nyingi Africa. Ukiangalia Wengi Tunaojadili Hizi Issues ni Vijana wa Tanzania na Kama Sisi Vijana Tunaelekea Kupandikiza Udini, Tutaiharibu Tanzania na Tutarudi Nyuma Kama Kenya na Rwanda. Its Ok Kuwa Critical na Government Bila Kudiscuss Issues za Dini na Ukabila...

"Lets Put Forward Discussions That Build Our Democracy and Development Initiatives"

Jamaa wametumia sana hiyo propaganda ya nchi yetu haina udini kujinufaisha. Ila kila lenye marefu halikosi ncha na hakuna mwanzo usio na mwisho. Kelele zao bila hoja ni sawa na ulimi hautoboi puto.
 
Jamaa wametumia sana hiyo propaganda ya nchi yetu haina udini kujinufaisha. Ila kila lenye marefu halikosi ncha na hakuna mwanzo usio na mwisho. Kelele zao bila hoja ni sawa na ulimi hautoboi puto.


Takataka
Takataka
Takataka
Takataka
Takataka
Takataka








 
Waislamu wenzangu lini tutaelimika tuache ujinga na sisi tuendelee?
 
wanatumia rasilimali kujinufaisha halafu wanajidai hakuna udini. udini upo sana tu. mbona huwa wakali linapokuja swala la waislam lkn yao hunyamza kimya?

Ona mpumbavu mwingine huyu! Mwenzako anauliza Je Kikwete ni mdini? badala ya kujibu hoja unaleta uharo
 
KWELI jK NI MDINI KAUACHIA UBALOZI WA VATICAN UNANAWIRI. MBONA MKAPA ALIPITISHA SHERIA ZA KUZUIA WAISLAM WASIENDELEE? SHERIA YA UGAIDI

wanatumia rasilimali kujinufaisha halafu wanajidai hakuna udini. udini upo sana tu. mbona huwa wakali linapokuja swala la waislam lkn yao hunyamza kimya?

Ona unachoandika uko kama taahira! Mkapa huyo huyo aliwapa chuo kikuu ili mpunguze Madrassa
 
hahaha, zanzibar inalipuwa? Hata ukiokota hela unarudisha ? Tutaenda rwanda kufanya mauaji ya kimbali kama walivyofanya maaskofu kwenye makanisa

Hujui kule kuna Kanisa zimepigwa na mabomu ya Al queda. Nyie endeleeni kujenga misikiti na Madrasa ya kutosha na kufuga ndevu nyingi
 
Hivi kwanini watu wengi sana bado wana mawazo ya kizamani kwamba wao ndio wasomi na wengine hawakwenda shule.hivi mliokwenda shule mbona mnaongea humu jf bila data za kisomi,hakuna fact,mipumba mitupu.kama nynyi ndio wasomi wenyewe basi naisikitikia sana Nchi yangu Tz .Elimu yenu ndio mmetufikisha hapa tulipo kama nchi 90% ya watu ni masikini.kama matunda yenu ya kuwa na elimu ndio tupo hapa basi darasa langu la saba tosha kabisa.
 
Jamaa lina akili za uji-uji, kila waziri mwenye jina angalau moja la kiingereza ama la "kizungu" ana note "Mkristo", mawazo yake yanamtuma ukristo ni jina! Ukristo ni IMANI syo jina! kuna wapagani humo kwenye baraza hata milango ya makanisa hawaijui una wabambikia ukristo! Huu ni wehu kabisa. Nchi hii ina watu wa madhehebu mbalimbali, yaani dini za kuletwa na za kienyeji na wasio na dini, mbona huwaonyeshi?

Hao mawaziri wengi wao wanategemea Waganga wa jadi na wachawi kufanikisha mambo yao unawataja kuwa ni wakristo! Hujui unachojadili zaidi ya uji uji kwenye kichwa chako. Tafuta imani zao wanazo ziamini siyo jina "nyambafu"
 
@sokomoko: kwa mtizamo wangu jibu la swali lako ni HAPANA, SI MDINI;

Hata hivyo naona nawe mwenyewe umeingia katika mtego wa madai na hofu batiri zinazopikwa na watu pasi msingi. Kosa la mtelezo ulichokifanya katika mada yako ni hili:

Kwa vile 2x2 = 2+2 = 4
sasa unasema 3x3 = 6

Sokomoko, Kiongozi Mkuu wa nchi au yeyote hawezi kuonyeshwa kuwa si mdini au ni mdini simply kwa kutoa hesabu ya Mawaziri na Wakuu wa Mikoa / Wilaya n.k Ukifanya hivyo asubuhi na mapema Wahindu, Wapagani, Wabidha n.k nao watabisha katika mlango wango uwape hesabu yao mapema vinginevyo watakurudisha na kusema ama serikali yetu ni wadini wa Uislam au Ukristo! Je ni vipi watu kwa kutumia mahesabu yako watasema kuhusu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Tafadhali sana kuwa makini katika kuleta hoja zenye kuleta mshikamano wa Kitaifa badala ya kuchochea hisia ambazo hakika mimi binafsi nasema hatuna udini isipokuwa kuna wachache wanataka tuelekee huko.

Kwa kifupi njia unayoitumia ni sawa na ile wengine pia wenye ufinyu wa mawazo wanaitumia kutoa lawama za udini.

Nakuuliza je ni halali kuassume kwamba idadi ya Watanzania wenye sifa za kuajirika ni sawa kati ya Wakristo na Waislamu na kwamba tukiteremka katika sifa (profile) zao kitaaluma, kiuzoefu, kimaadili na hata kiutashi pia utapata idadi sawa yaani 50% kila moja. kama jibu la swali langu ni hapana basi huna haja ya kuonyesha asilimia kujaribu kuprove kuwepo kwa udini au kutokuwepo kwa udini.

Mimi kawaida yangu namsubiri yeye anayedai kuwa Rais wetu ni Mdini, ndiye atuhakikishie hilo na nakwambia kuwa hakuna anayeweza kutuonyesha hilo.

Zaidi ya yote, Sokomoko unasema,

Nasikia JK aliwaambia kuwa nchi hii haina dini na itakuwa ubaguzi kuwapa ruzuku watu wa dini moja na kuwaacha wa dini nyinginezo akatolea mfano kuna waislam, wabudda, masingasinga, wahindu na wasiokuwa na dini je hao hawana haki ya kupewa ruzuku? na serikali ikitoa ruzuku kwa hawa wote itawezaje kujiendesha?

Hakika huu ni uzushi na kuleta Sokomoko fanya tu assigment yako ujue hadi unaposoma maandishi yangu sasa ni Vyuo vingapi na Vituo vya Afya hususani hospitali teule ngapi zinaendelea kupewa ruzuku mpaka leo!.

True, 2 x 2 = 2+ 2 but 3x3 is not equal to 3+3
 
Kikwete siyo mdini tu, bali pia ni mjinsia, mkabila na mbaguzi wa rangi: wanawake ni 10% tu kwenye baraza lake la mawaziri wakati kwenye general population idadi yao ni 50%! What's more: singasinga 0%: shree rajneesh hindu mandal 0%: wakwere 0% ukitoa yeye mwenyewe (na zaidi ya hapo karibu 80% ya makabila yaliyopo Tanzania hawana mwakilishi katika baraza jipya la mawaziri): half-caste 0%: hata wakongo nao hawamo ingawa hawakutakiwa kuwamo! Of course, bila kusahau wazungu 0% ambao wana-subsidize 50% ya bajeti yote ya serikali...
 
Mkuu Kibunago I have to say I agree with you. Tatizo la watu kama Sokomoko siyo kwamba wana advocate usawa wa dini zote bali wanacho lalamikia ni kujihisi (kwa sababu siyo fact) kwamba watu wa dini nyingine wapo juu zaidi. Kama kweli Sokomoko angekua ana advocate usawa asinge angalia tu Wakristo na Waislamu bali pia Singa Singa, Wapagani, Wahindu etc. Sasa yeye haoni hizi dini zingine lakini ana taka kutuaminisha kwamba yeye si mdini.

Pili, mimi namuona mtu ambae kafikia hatua ya kuhesabu watu wa dini gani wapo wangapi kwenye baraza ndiyo mdini. Wengi wetu tume kua tukiangalia kama walio wekwa wana faa au laa bila kuzingatia dini ila yeye kaamua kuangalia fulani ni wa dini gani bila hata kujua kwamba jina na dini ni vitu viwili tofauti.

Mimi nishamsoma huyu Sokomoko na watu wa design yake. Wanajua dini ni sensitive issue kwa hiyo wanajua jinsi ya kuprovoke. Huku katika jamii sijawahi kuona wala kusikia Waislamu au Wakristo wakilalamikia uwepo wa udini ila ni humu JF ndiyo una sikia story zote hizi. Mtu ambae haja wahi kukanyaga Tanzania akisoma baadhi ya post humu anaweza akafikiria Tanzania haku kaliki kumbe that is far from the truth.

Dawa nzuri ya kukomesha watu kama hawa ni kuto kujibu post zao kabisa kwa maana mtu mmoja akijibu tu basi mtiririko wa pumba unaanza. Tanzania hamna such thing as udini. Tatizo ni wale wachache ambao kwenye kila ngazi wana taka kuangalia nani ana tokea dini fulani tena siyo hata dini zote bali dini mbili tu na bado mtu ana jiita si mdini.

Mwisho ningependa kuwauliza swali wanaJF. Je kati ya hawa mdini ni nani? Yule anayempinga mtu kutokana na dini yake au yule anayemtetea mtu kutokana na dini yake? Maana humu JF kuna members wana tetea watu kwa ajili wao ni dini moja lakini bado wana nguvu za kuita watu ambao wanampinga huyo mtu kutokana na dini yake kuwa ni mdini. Wote ni wale wale tu!
 
Mwisho ningependa kuwauliza swali wanaJF. Je kati ya hawa mdini ni nani? Yule anayempinga mtu kutokana na dini yake au yule anayemtetea mtu kutokana na dini yake? Maana humu JF kuna members wana tetea watu kwa ajili wao ni dini moja lakini bado wana nguvu za kuita watu ambao wanampinga huyo mtu kutokana na dini yake kuwa ni mdini. Wote ni wale wale tu![/B]

Mwanafalsafa1, hakuna mdini ambaye anakubali kuwa yeye ni mdini! Kila mtu anayetaka kuzungumzia udini anazungumzia udini wa watu/mtu mwingine. Ukimuuliza kama yeye ni mdini atakana kabisa na kudai kwa kumtuhumu yeye udini basi wewe ndiye mdini! Soma mada zote zenye kuhusu udini utakuta hakuta hata moja ambapo mwanzishaji au mchangiaji anakiri kuwa yeye ni mdini!
 
Mwanafalsafa1, hakuna mdini ambaye anakubali kuwa yeye ni mdini! Kila mtu anayetaka kuzungumzia udini anazungumzia udini wa watu/mtu mwingine. Ukimuuliza kama yeye ni mdini atakana kabisa na kudai kwa kumtuhumu yeye udini basi wewe ndiye mdini! Soma mada zote zenye kuhusu udini utakuta hakuta hata moja ambapo mwanzishaji au mchangiaji anakiri kuwa yeye ni mdini!


Kingine kinacho nishangaza mkuu ni kwa nini kila mtu ghafla anajifanya yeye ni mwanasheria wa Kikwete? Kama Kikwete angeona haja ya kujitetea dhidi ya hizi shutuma si angejitetea? Sasa iweje leo Kikwete supposedly kuitwa "mdini" kuwaume wengine zaidi ya "mtuhumiwa" mwenyewe?

Hii ndiyo sababu inayo pelekea mimi kusema udini wanauona hawa waleta mada wa JF tu. Kama kweli general public inge kuwa ina fikiri hivyo basi tungeona na Kikwete mwenyewe ange jibu tuhuma either directly or indirectly. Sasa leo ina shangaza mheshimiwa mwenyewe kanyamaza lakini wengine ndiyo wanampigia tarumbeta humu ndani. Why?

The only conclusion I can reach is that ishu hapa siyo Kikwete. Waleta mada wenyewe ni wadini na wanatumia mgongo wa Kikwete kuleta hoja zao kwa kujidai tuhuma zina wauma kuliko "mlegwa" mwenyewe. Kama zipo tuhuma zidi ya Kikwete kuwa mdini wacha ajibu mwenyewe. Let's hear it from the horses mouth. JK ana bigger platform ambayo kama ange amua anaweza kuitumia kujitetea. Sasa leo wakina Sokomoko wana taka kutuaminisha kwamba Kikwete ni mnynge sana kiasi kwamba ana hitaji msaada wao kujitetea.
 
Back
Top Bottom