mgunga pori
JF-Expert Member
- Jul 23, 2016
- 4,093
- 4,912
Nchincha mwiba huoNakumbuka mwaka 2016 kuna mdau mmoja wa JF nilikuwa napenda sana uchangiaji wake kiasi cha kumfuata privately. Tukawa tunachat dhamira ikiwa ni kuja kutongozana hii yote kwa taswira tu niliomjengea kichwani mwangu kama pisikali fulani maana hatukuwa tumeshea picha. Ila kwa story zake alikuwa ni corporate lady umri wa makamo. Na michango yake yote ilikuwa anatoa kama binti.
Siku moja kulikuwa na tafrija Bank ya Diamond Trust wateja walialikwa tawi la Masaki. Kuna msela tulikuwa sehemu moja tunapiga stori kama wawakilishi wa kampuni zetu za ajira. Ikiwa tunachezea simu zetu huku tukiongea ghafla akanionyesha article JF huku akisema subiri a log in ili acomment. Si ndio kuona yule demu wangu wa inbox ndio msela kupitia log in details maana hakuficha.
Sikusema chochote ila baada ya hapo nilimblock kabisa. ID yake nikiangalia sasa hivi ilikuwa active mara ya mwisho 2018.
Nimetaja jina la eneo tulikokutana ili mwamba kama yupo humu kwa ID nyingine ajue kuwa nilimshtukia kuwa ni dume na hata mpaka leo sijui alikuwa na nia gani. Maana wasifu wake wa kazi aliotumia nikiwa na chat nae unashabihiana na ule wa uhalisia katika udume wake na hili nilijua tulipokuwa tunapiga story bank.
Toka siku hiyo nachukulia ma member wote humu kuwa ni madume kama mimi tu.



