Je, Biblia ya ukweli/Halisi ni ipi?

Je, Biblia ya ukweli/Halisi ni ipi?

Mkuu wayahudi wanadai kulikuwa na fixed canon ya vitabu 39 vya agano la kale...... Ethiopian orthodox nayo inadai kuna fixed canon ya vitabu 81 ambavyo wao walivitunza ila wayahudi walivipoteza mfano book of Enoch... Hivyo kiufupi kila mtu anavutia upande wake lakini kila kanisa linasema hiyo kanuni ilikuwa planned na Roho mtakatifu ndio sasa najiuliza

1. Je wote wapo sahihi?
2. Je Roho mtakatifu anakinzana?
3. Kma hakinzani kwanni kila dhehebu liwe na Biblia yake?
4. Je kma mmoja ndio yupo sahihi na wengine wamepotoka kwa kupunguza/ongeza namba ya vitabu nini hatma yao ?

I hope hoja imeeleweka mkuu
Jibu la swali la 1..hakuna vitu au majibu yanayotofautiana halafu tukasema sahihi

2:kwani roho mtakatifu ameandikwa kwenye agano la kale ?ninachofahamu roho mtakatifu amekuja baada ya Yesu kuondoka
3:kukinzana kwa madhehebu ni mfumo tu wa kidunia
4:hitimisho ni neema au motoni
 
Kwa uelewa wangu mdogo nilionao, ninachokijua kuhusu Biblia kwa ufupi tu ni kwamba, kwa miaka mingi saana watu mbalimbali wenye karama mbalimbali kama vile manabii wamekuwa wakivuviwa uwezo ama kufunuliwa Neno La Mungu kwa uwezo Wa Mungu Mwenyewe.

Tena wengine walipewa na maagizo kabisa na Mungu wayaandike mambo yale waliyo onyeshwa katika mawe makubwa ili kila mtu anayepita katika njia hiyo ayasome sana hata aweze kuyakariri.

Mafunuo mengine waliyopewa watumishi Wa Mungu na kuyatekeleza kwa vitendo yaliandikwa na waandishi na kuhifadhi kumbukumbu, sasa hizo kumbukumbu baada ya miaka mingi baadaye ndiyo vile vizazi vilivyofuata wakawa wakielimishana kumjua Mungu wakitumia zile kumbukumbu kama rejea.

Na yapo mambo mengi saana yaliyotendeka na kufundishwa ila yamewekwa machache tu ili kutoa mwongozo kwa msomaji Wa Biblia apate kuamini na kufanya sawasawa na maagizo ya Biblia.

Biblia imeweka wazi kabisa kuwa yapo mambo mengi sana hata yangeandikwa yasingetosha katika kitabu, kimsingi msomaji mzuri Wa Biblia ni yule anayesoma kwa Imani na kutumia muda Wa kutosha kutafakari kile anachokisoma, hapo ataona uhalisia Wa Kitabu.

Kwa hiyo, kuwepo kwa wingi au uchache Wa vitabu katika Biblia kunaweza kusiondoe uhalisia Wa Neno La Mungu isipokuwa kunampunguzia wigo Wa kupata maarifa zaidi msomaji, isipokuwa kama tafsiri ya kitabu hicho haitakuwa sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimekuelewa mujarabu kabisa maana umepangilia hoja kwa mtiririko mzuri sana ila sasa kuna situation ya Zero-sum game naiona hapa..... kwamba mmoja anapata na mwingine anakosa kabisa na hii ndio inanitatiza

Mfano martin luther alisema kitabu cha waebrania na Esther havikutakiwa kuwepo kwenye Bible maana havikushushwa na Mungu na akaenda mbali na kuvifuta kwenye Biblia yake toleo la kwanza kabisa

Kwa mfano huu je nitakuwa sawa nikisema waliocompile hizi Bible walitumia akili zao wenyewe na sio Roho mtakatifu kama wanavyodai maana sielewi kivipi protestant wenzake waseme hivyo 66 wamepewa na Roho mtakatifu alafu luther hapo hapo aseme naye Roho mtakatifu kamtuma kuvifuta Esther na waebrania huoni hapi kuna controversy??

Na kama mmoja wao ndio kweli katumwa na Mungu kucompile hivo vitabu je nini hatma ya hao wengine whether protestant au catholic ambao ndio watakuwa wako wrong side of the coin..... Na pia kama mmoja wao kakosea kwanini Mungu ameruhusu Neno lake livurugwe na maamuzi ya watu wachache waliotumia akili zao binafsi??

Embu nisaidie hapa mkuu
 
Kuna hoja moja hapa umeizungumzia kimsingi inahitaji uwe ni mtu Wa elimu sana ili kuthibitisha maana ni aghalabu sana kupata reference yake kutoka kwenye Biblia yetu tunayoisoma.

Ni kuhusu uwepo Wa wanadamu wengine hata kabla ya Adamu na Eva, kwa kuhusisha tu kwamba kulikuwepo na nchi ya kush magharibi mwa bustani ya Eden.

Unajua Biblia wakati mwingine inapozungumzia nchi Fulani si lazima kuwepo na wanadamu wanaishi huko, kwa sababu nchi kibiblia kwa tafsiri nyingine ni ardhi, wala si lazima mpaka kuwepo wanaoishi ndani yake. Rejea kitabu cha Mwanzo sura ya kwanza kabisa.

Pia nimependa ulivyoleta hoja yenye nguvu kuhusu mtu mweusi, kimsingi mtu halisi ni roho, mwili ni makazi ya roho hiyo hivyo awe ni mtu mweusi, mweupe, mwekundu au blue siyo issue

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuhusu Adam kuwa sio mtu wa kwanza kibiblia ni ngumu kuprove ingawa kitabu cha Ezekiel na ufunuo ukivisoma kwa makini vinatoa clue kubwa sana ya wanadamu wengine kuwepo kabla ya Adam ila napaswa watu wafahamu kuwa Biblia haitaji watu baki bali watu ambao walikuwa na impact kwenye storyline mfano Adam alikuwa na watoto kibao ila wanatajwa 3 pekee..... Na ndio maana paulo akasema Enoch ni mtu wa saba baada ya Adam ilihali Adam alikuwa na watoto kibao wengine ila Biblia haikuwatambua bali ikatambua lineage ya Seth pekee n.k

Sipendi kuchanganya science na Bible maama vinakinzana ila kuna double standards huwa naziona mfano Radiometric dating ya mifupa ya Pharaoh wanaotajwa kwenye Biblia mfano Ramses II inapoint miaka 3000 iliopita ambapo ni consistent na miaka ya Biblia na watu wa dini hufurahi sababu wanaona proof ya maandiko yao kuwa ni credible lakini wakati huo huo mashine hiyo hiyo na formula hiyo hiyo ikipima fuvu let's say ya Neaderthal huko Hispania ya sasa ikaonekana lina zaidi ya miaka 40,000 sasa hapa huwa wanakataa wanasema science inapinga Biblia na inapotosha sasa hapa which is which??
 
Nikushukuru kwanza kwa kukiri kuwa BIBILIA ni mkusanyiko wa vitabu vingi. Kutoka kwa manabii na waandishi wengine mfano Matthew etc.
Sasa tukirudi kwenye mada, Bibilia ipi sahihi? Jibu ni moja tu. ZOTE ZIPO SAHIHI.
Nasema hivi kwasababu.
1. Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu vingi Vinavyoelezea HISTORIA kati ya MUNGU na WANADAMU Kuanzia Uumbaji, Uasi, Ukombozi na hatima ya maisha baada ya haya.
Hii ndio hasa point ya msingi.
2. Maandiko yanaposema Hata yodi moja ya Totari haitaondoka/ Usiongeze wala kupunguza neno ina maana kubwa na inabidi uitazame kwa upana wake. Mfano umesema Hata Yesu alifanya marejeo ya maandiko kutoka vitabu walivyokuwa navyo Wayahudi kabla hajazaliwa. Na katika kurejea huko alichukua vitabu baadhi si vyote na sikitabu kizima. Alifanya hivi, ni ili afikishe ujumbe kamili uliokusudiwa.
Ukiangalia kuanzia Mwanzo - Ufunuo habri inayozungumzwa hapo ni moja tu. Tofauti inakuja kwenye tafsiri na jinsi mwandishi alivyoandika ila ujumbe unaozungumzwa ni ule ule.
Mfano: Matthew Luke and John wote hawa wameelezea kufufuka kwa Yesu. Antajwa Malaika, Kaburi, Yesu amefufuka na wanawakewaliokwenda kaburini. huyu kasema waliingia, mwingine walikuta malaika nje mwingine nk. ila jibu la MALAIKA hapo ni moja tu, AMEFUFUKA kama alivyosema.
Ikumbukwe vitabu vyote ulivyotaja havijakatazwa kusoma ikiwa unahitaji kuongeza maarifa zaidi(Kama nilivyosema mwanzo kuwa IT is all about a History of God and Man. That is what Bible is all about.
Kwahiyo kuwa na uchache wa vitabu au kuwa navyo vingi hakuifayi Bible kuwa siyo sahihi, maadam zote zina kiri UWEPO wa Mungu; Uumbaji; Uasi wa Mwanadamu, Kukombolewa kwake(Mwanadamu) na Hatima ya maisha yake baada ya hapa duniani.
Hata ukisoma Torati kwenye Bibilia ya RC ndiyo hiyo hiyo unaikuta kwenye Lutheran etc.

Karibuni tuendelee kujifunza.
Mkuu nimekusoma pia ila kuna concept moja tunaisahau ntaeleza kwa mfano nilioutoa hapo juu..... Ethiopia Tawahedo church yaani Orthodox linatumia kitabu cha Enoch ambacho kwa kiasi kikubwa kinapingana na Biblia ya RC na protestant mfano kinasema malaika walizaa na binadamu kitu ambacho Biblia ya protestant inakataa kwa kumquote Yesu akisema malaika hawanaga jinsia sasa mpaka hapo kuna crisis ya mmoja ni mkweli mwingine ni muongo maana haiwezekana Enoch na Yesu wote wawe sawa. Sasa nachojiuliza kama Ethiopia hawako sahihi kukiweka book of enoch yaani kuilisha Biblia maneno yasiyo ya kweli je Mungu anapendezwa?? Kama hapendezwi si ina maana wamekosea? Je si itakuwa na maana Biblia mmoja wapo kati ya hizo mbili itakuwa haijapewa baraka na Roho mtakatifu?? Na kama haijapewa je Biblia ipi sasa ni sahihi?? Na kama mmoja tu ndio sahihi nini hatma ya madhehebu yenye watu mabilion kutumia Biblia yenye upungufu?? Na kwanini Mungu karuhusu neno lake lipotoshwe assuming that mmoja kati ya hizo biblia mbili kapotosha kuhusu malaika kuzaa na binadamu??

I hope hapa utanielewa kwamba zote haziwezi kuwa sawa..... Je Biblia halali ni ipi kwa vigezo hivi

Ahsante
 
Mkuu kuhusu Adam kuwa sio mtu wa kwanza kibiblia ni ngumu kuprove ingawa kitabu cha Ezekiel na ufunuo ukivisoma kwa makini vinatoa clue kubwa sana ya wanadamu wengine kuwepo kabla ya Adam ila napaswa watu wafahamu kuwa Biblia haitaji watu baki bali watu ambao walikuwa na impact kwenye storyline mfano Adam alikuwa na watoto kibao ila wanatajwa 3 pekee..... Na ndio maana paulo akasema Enoch ni mtu wa saba baada ya Adam ilihali Adam alikuwa na watoto kibao wengine ila Biblia haikuwatambua bali ikatambua lineage ya Seth pekee n.k

Sipendi kuchanganya science na Bible maama vinakinzana ila kuna double standards huwa naziona mfano Radiometric dating ya mifupa ya Pharaoh wanaotajwa kwenye Biblia mfano Ramses II inapoint miaka 3000 iliopita ambapo ni consistent na miaka ya Biblia na watu wa dini hufurahi sababu wanaona proof ya maandiko yao kuwa ni credible lakini wakati huo huo mashine hiyo hiyo na formula hiyo hiyo ikipima fuvu let's say ya Neaderthal huko Hispania ya sasa ikaonekana lina zaidi ya miaka 40,000 sasa hapa huwa wanakataa wanasema science inapinga Biblia na inapotosha sasa hapa which is which??
Nakuelewa sana, ukiangalia sana kibiblia unaona tangu kuumbwa kwa mwanadamu Wa kwanza (yaani Adam) mpaka sasa ni kama miaka elfu 5 hivi, ila bado Biblia inaelezea miaka mingi sana hata kabla ya uumbaji.

Pia kama unavyosema Biblia imekuwa ikielezea zaidi kile kizazi ambacho Mungu amekuwa karibu nacho, ingawaje wapo watu wengi saana nje ya mtiririko Wa Adam, Seth na wengineo.

Ila ningependa unipatie hivyo vifungu katika kitabu cha Ezekiel na Ufunuo nijisomee huenda nitapata kitu cha ziada. Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nimekusoma pia ila kuna concept moja tunaisahau ntaeleza kwa mfano nilioutoa hapo juu..... Ethiopia Tawahedo church yaani Orthodox linatumia kitabu cha Enoch ambacho kwa kiasi kikubwa kinapingana na Biblia ya RC na protestant mfano kinasema malaika walizaa na binadamu kitu ambacho Biblia ya protestant inakataa kwa kumquote Yesu akisema malaika hawanaga jinsia sasa mpaka hapo kuna crisis ya mmoja ni mkweli mwingine ni muongo maana haiwezekana Enoch na Yesu wote wawe sawa. Sasa nachojiuliza kama Ethiopia hawako sahihi kukiweka book of enoch yaani kuilisha Biblia maneno yasiyo ya kweli je Mungu anapendezwa?? Kama hapendezwi si ina maana wamekosea? Je si itakuwa na maana Biblia mmoja wapo kati ya hizo mbili itakuwa haijapewa baraka na Roho mtakatifu?? Na kama haijapewa je Biblia ipi sasa ni sahihi?? Na kama mmoja tu ndio sahihi nini hatma ya madhehebu yenye watu mabilion kutumia Biblia yenye upungufu?? Na kwanini Mungu karuhusu neno lake lipotoshwe assuming that mmoja kati ya hizo biblia mbili kapotosha kuhusu malaika kuzaa na binadamu??

I hope hapa utanielewa kwamba zote haziwezi kuwa sawa..... Je Biblia halali ni ipi kwa vigezo hivi

Ahsante
Kuna kitu kimoja ni vizuri ukakijua mkuu, katika roho kila kitu kinawezekana! Habari ya kwamba malaika hawana jinsia inaweza ikawa sawa maana wao ni roho, na pia wanao uwezo vile vile Wa kufanya kizazi kwa wanadamu kwa sababu, wakiwa katika maumbo yao halisi hawawi kama mwanadamu Wa kawaida, na pia wanao uwezo Wa kuwa kama mwanadamu Wa kawaida hata ukadhania ni mwanadamu mwenziyo kumbe si mwanadamu. L

Kwa hiyo hilo la jinsia lisikuletee ukakasi mkuu. Fikiria ni kwa nini Mungu akamwambia yule joka Wa zamani ibilisi, kuwa amelaaniwa kuliko wanyama Wote Wa mwituni na kwa tumbo atatembea na kula mavumbi ya nchi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nimekusoma pia ila kuna concept moja tunaisahau ntaeleza kwa mfano nilioutoa hapo juu..... Ethiopia Tawahedo church yaani Orthodox linatumia kitabu cha Enoch ambacho kwa kiasi kikubwa kinapingana na Biblia ya RC na protestant mfano kinasema malaika walizaa na binadamu kitu ambacho Biblia ya protestant inakataa kwa kumquote Yesu akisema malaika hawanaga jinsia sasa mpaka hapo kuna crisis ya mmoja ni mkweli mwingine ni muongo maana haiwezekana Enoch na Yesu wote wawe sawa. Sasa nachojiuliza kama Ethiopia hawako sahihi kukiweka book of enoch yaani kuilisha Biblia maneno yasiyo ya kweli je Mungu anapendezwa?? Kama hapendezwi si ina maana wamekosea? Je si itakuwa na maana Biblia mmoja wapo kati ya hizo mbili itakuwa haijapewa baraka na Roho mtakatifu?? Na kama haijapewa je Biblia ipi sasa ni sahihi?? Na kama mmoja tu ndio sahihi nini hatma ya madhehebu yenye watu mabilion kutumia Biblia yenye upungufu?? Na kwanini Mungu karuhusu neno lake lipotoshwe assuming that mmoja kati ya hizo biblia mbili kapotosha kuhusu malaika kuzaa na binadamu??

I hope hapa utanielewa kwamba zote haziwezi kuwa sawa..... Je Biblia halali ni ipi kwa vigezo hivi

Ahsante
Kwa mtizamo wa kibibilia(Kiimani zaidi). kuna haja ya kuangalia historia ya mwandishi wa kitabu pia. Kama ulivyosema Bible ya kigiriki ya mwanzo KK ilikuwa na 46 books hivi, ila Jews wakaweka 37 books. Why walikuja na hiyo? Tuanzie hapo.
na vipi katika hizo 46 books Enock kitabu chake kilikuwepo? je alikiandika baada ya Yesu kuja na kuondoka.
Kwanini nauliza haya, ili tuende sambamba na why Enoch book is not included.
Kama nilivyotangulia kusema kwenye quote yangu kuwa Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu. na vinaelezea HISTORIA ya MUNGU na MWANADAMU.
katika hili Wakristo wanamuangalia YESU kuwa ndiye mkombozi na ni msema kweli. Na ukweli huo ndio ulipelekea hata Wayahudi wakawa hawamtaki mpaka kufikia kumuua ili litimie andiko. japo wao walikuwa na kitabu lakini hawakuifahamu hiyo. Ndiyo maana alisema Baba wasamehe maana hawajui walitendalo.
Sasa ikiwa Yesu alisema malaika hawazai wala kuoa. Enoch ni nani hata aseme walizaa? alijifunza kwa nani, au nabii yupi aliwahi kuongea hivyo kwa mfano!

Linapokuja suala la Christianity and the Bible. Hapa hata wayahudi hawakukubali kumfuata Christ. isipokuwa wale aliokuwa nao na waliopata bahati ya kukutana naye(kina Paul). Hivyo basi. Ni hakika kabisa wakatokea wapotoshaji wa maandiko na kutaka watu wayatumie kumbe hayana ukweli.
Cha kujivunia hapa ni uhuru aliotupatia MUNGU wa kuchagua lililojema na la kufaa kuufikilia ule uzima wa milele(Eternity Life).
Hii ni kuwa huru kuhoji kila ulionalo kabla hujalikubali na kuliamini.
Hao Waethiopia kuwa nacho hicho kitabu ni chaguo lao kwa uhuru wao.
Narudia tena kusema Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu, hivyo hakuna Bibilia ya ENOCH. Kuna vitabu Saba, kumi au mia haifanyi isiwe sahihi. Usahihi ni je, Ujumbe wake unasema nini juu ya MUNGU na MWANADAMU.
Katika ukusanyaji wa vitabu hivi pia ulizingatia mambo mengi mfano historia ya mwandishi, nini anataka jamii ijifunze kwalo(Ujumbe uliopo ndani yake), ulinganifu na wengine(Hapa nazungumzia kilichokusudiwa kufundishwa kinalingana na wengine japo amelezea kwa uandishi wa namna yake) nk.

Labda nikuulize kidogo.
Mjadala wako ni kwaajili ya kitabu cha ENOCK au kuna lingine?
Karibu.
 
Wacha porojo wewe, jibu ni ipi bibilia ya kweli?
Ni ile inayosema baada ya Yesu atakuja mtume wa mwisho ambaye ni Mohamed(S.A.W)
Sema Takbiiiir!
Back to the topic
Ilimradi msingi haujaharibiwa ,hakuna haja ya kuuliza ipi ni sahihi.
Hakuna biblia inayomkataa Mungu na hakuna inayotukataza tutende yaliyo mema.
Ingekuwepo inayotuambia tujilipue,hiyo ningeikataa.
 
Yesu kristo alisema "Kizazi hiki chatafuta ishara ,na kamwe hakitaziona"

Kuna baadhi ya watu wanapost mada kwa kudhani wana upeo mkubwa bila kujua " wananakili mtandaoni " maoni ya watu mtandaoni na kutumiwa na mpinga kristo,roho chafu hutumia watu "dhaifu " kufikisha ujumbe.

Original version:" Kizazi kibaya na cha zinaa chataka ishara ;wala hakitapewa ishara ,isipokuwa ishara ya Yona"
 
Jibu kwa mtoa mada "dhaifu" ni kwamba biblia ya kweli ipo ndani ya nafsi yako ukisema uitafute hauto ipata
 
Ni ile inayosema baada ya Yesu atakuja mtume wa mwisho ambaye ni Mohamed(S.A.W)
Sema Takbiiiir!
Back to the topic
Ilimradi msingi haujaharibiwa ,hakuna haja ya kuuliza ipi ni sahihi.
Hakuna biblia inayomkataa Mungu na hakuna inayotukataza tutende yaliyo mema.
Ingekuwepo inayotuambia tujilipue,hiyo ningeikataa.
Mkuu msingi gani haujaharibiwa?? Martin Luther Biblia yake ya protestants ya kwanza kabisa kuitafsiri kutoka kilatin kwenye Biblia ya wakatoliki alisema vitabu vya Waebrania,Yakobo na Esther havifai kabisa na kwamba vinapotosha sasa huoni mambo mazuri yalioandikwa humo hasa waebrania yatapoteza watu kibao kwenye msingi wao wa imani??

Pia Kitabu cha Henoko biblia ya orthodox kinasema malaika walizaa na Binadamu na ndio ilipelekea gharika ila Biblia ya protestants inasema dunia ilijaa dhambi ndio gharika likaja..... Sasa huoni tayari hapo kuna jambo kubwa sana limepotoshwa kati ya hizi Biblia mbili? Je story ya Nuhu kwako haina msingi wowote kwenye imani hasa linapokuja suala la kuepuka dhambi, kuwa mtakatifu n.k

Bila kusahau jehovah witness wanatumia Apocalypse of Abraham ambao unaelezea ufunuo tofauti kabisa na Biblia ya protestant kupitia ufunuo wa yohana sasa huoni wameshakinzana hivyo wote hawawezi kuwa sahihi hasa ukizingatia unabii ni jambo la msingi sana likipotoshwa madhara yake ni makubwa sana.

Je bado unakubaliana kuwa biblia zote zinaongea lugha moja??
 
Jibu kwa mtoa mada "dhaifu" ni kwamba biblia ya kweli ipo ndani ya nafsi yako ukisema uitafute hauto ipata
Oooh ok Kwahiyo hizi nilizotaja zote ni feki tu si ndio maana yake?? Ina maana wakristo wote wamepotoshwa mpaka sasa kwa kutoambiwa Biblia ya kweli ipo ndani ya nafsi na sio kwenye makaratasi?? Na kama Biblia ipo kwenye nafsi kwanini basi Mungu aliwapa mitume maagizo kuwa waandike maneno yake na wayasambaze ilihali angeweza kusema na watu kupitia BIBLIA ZA NAFSINI mwao??
 
Oooh ok Kwahiyo hizi nilizotaja zote ni feki tu si ndio maana yake?? Ina maana wakristo wote wamepotoshwa mpaka sasa kwa kutoambiwa Biblia ya kweli ipo ndani ya nafsi na sio kwenye makaratasi?? Na kama Biblia ipo kwenye nafsi kwanini basi Mungu aliwapa mitume maagizo kuwa waandike maneno yake na wayasambaze ilihali angeweza kusema na watu kupitia BIBLIA ZA NAFSINI mwao??

"Wana macho nao hawaoni,wana masikio nao hawasikii"
 
Kwa mtizamo wa kibibilia(Kiimani zaidi). kuna haja ya kuangalia historia ya mwandishi wa kitabu pia. Kama ulivyosema Bible ya kigiriki ya mwanzo KK ilikuwa na 46 books hivi, ila Jews wakaweka 37 books. Why walikuja na hiyo? Tuanzie hapo.
na vipi katika hizo 46 books Enock kitabu chake kilikuwepo? je alikiandika baada ya Yesu kuja na kuondoka.
Kwanini nauliza haya, ili tuende sambamba na why Enoch book is not included.
Kama nilivyotangulia kusema kwenye quote yangu kuwa Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu. na vinaelezea HISTORIA ya MUNGU na MWANADAMU.
katika hili Wakristo wanamuangalia YESU kuwa ndiye mkombozi na ni msema kweli. Na ukweli huo ndio ulipelekea hata Wayahudi wakawa hawamtaki mpaka kufikia kumuua ili litimie andiko. japo wao walikuwa na kitabu lakini hawakuifahamu hiyo. Ndiyo maana alisema Baba wasamehe maana hawajui walitendalo.
Sasa ikiwa Yesu alisema malaika hawazai wala kuoa. Enoch ni nani hata aseme walizaa? alijifunza kwa nani, au nabii yupi aliwahi kuongea hivyo kwa mfano!

Linapokuja suala la Christianity and the Bible. Hapa hata wayahudi hawakukubali kumfuata Christ. isipokuwa wale aliokuwa nao na waliopata bahati ya kukutana naye(kina Paul). Hivyo basi. Ni hakika kabisa wakatokea wapotoshaji wa maandiko na kutaka watu wayatumie kumbe hayana ukweli.
Cha kujivunia hapa ni uhuru aliotupatia MUNGU wa kuchagua lililojema na la kufaa kuufikilia ule uzima wa milele(Eternity Life).
Hii ni kuwa huru kuhoji kila ulionalo kabla hujalikubali na kuliamini.
Hao Waethiopia kuwa nacho hicho kitabu ni chaguo lao kwa uhuru wao.
Narudia tena kusema Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu, hivyo hakuna Bibilia ya ENOCH. Kuna vitabu Saba, kumi au mia haifanyi isiwe sahihi. Usahihi ni je, Ujumbe wake unasema nini juu ya MUNGU na MWANADAMU.
Katika ukusanyaji wa vitabu hivi pia ulizingatia mambo mengi mfano historia ya mwandishi, nini anataka jamii ijifunze kwalo(Ujumbe uliopo ndani yake), ulinganifu na wengine(Hapa nazungumzia kilichokusudiwa kufundishwa kinalingana na wengine japo amelezea kwa uandishi wa namna yake) nk.

Labda nikuulize kidogo.
Mjadala wako ni kwaajili ya kitabu cha ENOCK au kuna lingine?
Karibu.
Mkuu nimekusoma kabisa hoja yako kuhusu swali lako labda nieleze hivi
1. Nauliza sababu Ethiopia wamekiweka hiko kitabu cha Henoko kwenye Biblia yao huku RC na protestants hawajakiweka na humo kina kinzana vitu vya msingi kabisa mfano Unabii wa siku za mwisho, uumbaji wa Mungu, ukombozi wa wanadamu mfano wakati wa Nuhu biblia inatuonyesha walifanya dhambi ila Nuhu alikuwa mtakatifu ndio maana kaachwa lakini henoko anasema Nuhu hakupona sababu ni mtakatifu bali kwakuwa tu hakuwa ana damu ya wanefili sasa vitu kma hivi vinauwezo wa kuua imani ya wakristo n.k hivyo hoja yangu hapa sio enoko tu bali kuonyesha kwamba Biblia zote haziko sawa so haziwezi zote kuwa halali na haziwezi zote kuwa Zimevuviwa na Roho mtakatifu maana naamini Roho hawezi jiachanganya

Mfano mwingine ufunuo wa siku za mwisho umeelezewa tofauti kabisa kwenye Book fo Abraham kinachotumiwa na Bible ya mormons sasa huoni inaweza potosha mamilion ya watu ikiwa kila biblia ina ufunuo tofauti wa kuja kwa Yesu?? Main point hapa nilitaka tukubaliane kwamba Biblia moja tu ndio itakuwa sahihi na zingine ni batili sasa basi hiyo halali ni ipi?? Na ambayo sio halali nini hatma ya hayo makanisa kama yamepotoshwa miaka yote hii?? Na kwanini Mungu aruhusu maneno yake yaongezewe uongo hadi kusababisha mamilion ya watu wapotezwe??

I hope umeelewa nachotaka kuraise hapa
 
Unatafuta njia ya kufungwa huu uzi, hayo mapicha tumeyazoea
Na majibu nilishakupa zaidi ya mara 1000
Ñjoo kwenye hoja, Ipi biblia sahihi?

Ni wazimu wa maswali [emoji117]
IMG_20190114_112532_166.jpg
eti ibi Maktaba sahihi [emoji350] [emoji15]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yesu kristo alisema "Kizazi hiki chatafuta ishara ,na kamwe hakitaziona"

Kuna baadhi ya watu wanapost mada kwa kudhani wana upeo mkubwa bila kujua " wananakili mtandaoni " maoni ya watu mtandaoni na kutumiwa na mpinga kristo,roho chafu hutumia watu "dhaifu " kufikisha ujumbe.
Na hii ndio shida ya wafia dini mada za kujengana mnasema nimetumwa na mpinga kristo kwahiyo kuhoji kwanini Biblia zinakinzana ni UPINGA KRISTO?? kwahiyo wewe unaona sawa Biblia ya kanisa la Mormon kusema Abraham alipewa gauni la shetani kuvaaa ilihali Biblia yako inasema Abraham ni baba wa imani??

Sasa mimi nayefukua huu uovu na hao mormons nani ndio anatumika na shetani?? Je martin luther aliyesema kitabu cha waebrania ni UPUUZI na mie nayefukua ''uovu'' huo wa luther nani anatumika na shetani

Embicile!!
 
Back
Top Bottom