Nikushukuru kwanza kwa kukiri kuwa BIBILIA ni mkusanyiko wa vitabu vingi. Kutoka kwa manabii na waandishi wengine mfano Matthew etc.
Sasa tukirudi kwenye mada, Bibilia ipi sahihi? Jibu ni moja tu. ZOTE ZIPO SAHIHI.
Nasema hivi kwasababu.
1. Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu vingi Vinavyoelezea HISTORIA kati ya MUNGU na WANADAMU Kuanzia Uumbaji, Uasi, Ukombozi na hatima ya maisha baada ya haya.
Hii ndio hasa point ya msingi.
2. Maandiko yanaposema Hata yodi moja ya Totari haitaondoka/ Usiongeze wala kupunguza neno ina maana kubwa na inabidi uitazame kwa upana wake. Mfano umesema Hata Yesu alifanya marejeo ya maandiko kutoka vitabu walivyokuwa navyo Wayahudi kabla hajazaliwa. Na katika kurejea huko alichukua vitabu baadhi si vyote na sikitabu kizima. Alifanya hivi, ni ili afikishe ujumbe kamili uliokusudiwa.
Ukiangalia kuanzia Mwanzo - Ufunuo habri inayozungumzwa hapo ni moja tu. Tofauti inakuja kwenye tafsiri na jinsi mwandishi alivyoandika ila ujumbe unaozungumzwa ni ule ule.
Mfano: Matthew Luke and John wote hawa wameelezea kufufuka kwa Yesu. Antajwa Malaika, Kaburi, Yesu amefufuka na wanawakewaliokwenda kaburini. huyu kasema waliingia, mwingine walikuta malaika nje mwingine nk. ila jibu la MALAIKA hapo ni moja tu, AMEFUFUKA kama alivyosema.
Ikumbukwe vitabu vyote ulivyotaja havijakatazwa kusoma ikiwa unahitaji kuongeza maarifa zaidi(Kama nilivyosema mwanzo kuwa IT is all about a History of God and Man. That is what Bible is all about.
Kwahiyo kuwa na uchache wa vitabu au kuwa navyo vingi hakuifayi Bible kuwa siyo sahihi, maadam zote zina kiri UWEPO wa Mungu; Uumbaji; Uasi wa Mwanadamu, Kukombolewa kwake(Mwanadamu) na Hatima ya maisha yake baada ya hapa duniani.
Hata ukisoma Torati kwenye Bibilia ya RC ndiyo hiyo hiyo unaikuta kwenye Lutheran etc.
Karibuni tuendelee kujifunza.
Mungu pekee ndiye ajuaye ni lini Wakristo wataweza kutoa nakala sahihi (asilia) ya kitabu chao (Biblia).
Mtu atashangaa, juu ya idadi ya matoleo ya Biblia yaliyopo leo hii.
Kila moja linatofautiana na jingine, ndio, kila moja linadai kuwa yeye ndio toleo asilia. Matolea yote hayo yameshawahi kutangaza duniani kuwa, yenyewe ni ufunuo mtakatifu.
Rejeo lao lililo tayari lipo katika (2 Timotheo 3:16), isemayo
“Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho...” Lakini kile wasichokifahamu Wakristo ni kuwa, “Kwa hakika, yaliyomo katika Biblia zao si Maandiko matakatifu isipokuwa ni hekaya, fikra, matukio na tamaduni tu
Tatizo hilo linachanganya zaidi pale tunapojua kuwa baadhi ya matoleo ya Biblia yana vitabu vingi zaidi kuliko mengine.
Toleo la Orthodox (OVC), lina
vitabu 86;
Toleo la Charismatic (CV), lina vitabu 76;
Toleo la Roman Catholic (RCV), lina
vitabu 73;
na matoleo yote ya Kiprotestanti yana
vitabu 66 likiwemo The New World Translation of the Holy Scripture [1984] (NW), linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova na matoleo mengine kama vile the King James [1611-1942] (KJ), American Standard [1901-1944] (AS), Rivised Standard [1971] Second Edition (RS) Jerusalem Bible [1966] (JB), Good News Bible (1954: iliyochapwa 1956), Ronald A, Knox (Kx), New International Version (NIV), na motoleo mengine yasiyo na idadi.
Zaidi ya hayo, vipi kuhusu hoja ya Warejeaji wanosifika wa Biblia ya the Rivised Standard Version (RS), Rivised Edition ya 1952, na kwa Agano Jipya, Second Edition ya 1971, by Wm. Collins Sons & Co. Ltd. Iliyochapwa na Canadian Bible Society, isemayo katika Utangulizi wake:
(1)
“Naam, Toleo la King James lina dosari kubwa mno.... dosari hizo ni nyingi sana na hatari sana kiasi cha kupelekea kuitishwa wito wa kurekebishwa kwa tafsiri yake ya Kingereza.”
(2) “Toleo la King James la Agano Jipya liliegemea katika mandiko ya Kigiriki yaliyoharibiwa kimakosa” Vipi kuhusu hoja ya Mashahidi wa Yehova katika chapa ya Mwamko ya Septemba 1951 inayoeleza; “Biblia ina makosa 50,000!”
Na vipi kama nikisema, kinyume na imani yetu, kuwa “
Katika Waandishi wanne wa Injili Hakuna hata mmoja aliyekuwa Mwanafunzi wa Yesu (AS).” Katika (Luka 6:14-16 na Marko 3:17) tunaona yametajwa majina ya wanafunzi kumi na wawili na Yesu (AS). Huku majina Mathayo na Yohana yamo, na majina Marko, Luka na Paulo hayajatwaja.
Hata hivyo, kutokana na nukuu zifuatazo, utagundua kuwa hizo Injili mbili zinatajwa kuwa ni za Mathayo na Yohana kwa kuwaheshimu tu, kwani ziliandikwa na mtu wa tatu. Soma nakala halisi ya mstari wa (Mathayo 9:9):
"Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani aitwaye Mathayo, akamwambia nifuate. Akaondoka akamfuata."
Na katika (Yohana 21:24):
"Huyu ndiye yule mwanafunzi ayashuhudiaye haya, na aliyeyaandika haya; nasi twajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli?"
Katika aya ya kwanza, mwandishi anasimulia tu kile kilichotokea kati ya Yesu (AS) na Mathayo, huku katika aya ya pili, ni wazi kuwa kiwakilishi “nasi” kinawakilisha mwandishi.
Hebu kwa sasa tutafakari juu ya kile kilichosemwa na waandishi wawili wa Kikristo kuhusu kuundwa kwa Biblia:
“Wakati mwingine, Wanukuzi wanatia kile kisichokuwemo katika maandishi, pia kile wanachokifikiria kitakuwemo. Mnukuzi anaweza kuamini kumbukumbu zinazobadilika, au anaweza kuunda maandiko kwa mujibu wa mtazamo wa madhehebu anayoyafuata. Kwa kuongezea katika matoleo na manukuzi ya Mapadri wa Kikristo, takriban (Miswada) ya Mandiko Matakatifu elfu nne ya Wagiriki [MSS], ilijulikana kuwa ipo. Kwa hiyo, tofauti za usomaji ni jambo la kuzingatiwa.”[1]
Kwa hiyo Injili ziliundwa, na ambazo kiwaziwazi, ziliakisi mitazamo ya ufahamu wa mahitajio na matumizi ya jamii za waandishi. Kwao wao, vitu vya kimila vilitumika, lakini kulikuwa hakuna kusita katika kukibadilisha kile kisichoendana na lengo la mwandishi.”[2]
[1] J.R., dummelow: Commentary on the Holy Bible, p. 16. – (see – Mrs. Ulfat Aziz-Us-Samad: “Islam and Christianity”, 1984, Presidency of Islamic Research IFTA and Propagation, Riyadh, Kingdom of Saud Arabia p.7).
[2] T.G. Tucker: The History of The Christian in the Light of Modern Knowledge, p. 320. (Ibid, p. 6).