Gavana
JF-Expert Member
- Jul 19, 2008
- 33,635
- 8,955
Nikushukuru kwanza kwa kukiri kuwa BIBILIA ni mkusanyiko wa vitabu vingi. Kutoka kwa manabii na waandishi wengine mfano Matthew etc.
Sasa tukirudi kwenye mada, Bibilia ipi sahihi? Jibu ni moja tu. ZOTE ZIPO SAHIHI.
Nasema hivi kwasababu.
1. Bibilia ni mkusanyiko wa vitabu vingi Vinavyoelezea HISTORIA kati ya MUNGU na WANADAMU Kuanzia Uumbaji, Uasi, Ukombozi na hatima ya maisha baada ya haya.
Hii ndio hasa point ya msingi.
2. Maandiko yanaposema Hata yodi moja ya Totari haitaondoka/ Usiongeze wala kupunguza neno ina maana kubwa na inabidi uitazame kwa upana wake. Mfano umesema Hata Yesu alifanya marejeo ya maandiko kutoka vitabu walivyokuwa navyo Wayahudi kabla hajazaliwa. Na katika kurejea huko alichukua vitabu baadhi si vyote na sikitabu kizima. Alifanya hivi, ni ili afikishe ujumbe kamili uliokusudiwa.
Ukiangalia kuanzia Mwanzo - Ufunuo habri inayozungumzwa hapo ni moja tu. Tofauti inakuja kwenye tafsiri na jinsi mwandishi alivyoandika ila ujumbe unaozungumzwa ni ule ule.
Mfano: Matthew Luke and John wote hawa wameelezea kufufuka kwa Yesu. Antajwa Malaika, Kaburi, Yesu amefufuka na wanawakewaliokwenda kaburini. huyu kasema waliingia, mwingine walikuta malaika nje mwingine nk. ila jibu la MALAIKA hapo ni moja tu, AMEFUFUKA kama alivyosema.
Ikumbukwe vitabu vyote ulivyotaja havijakatazwa kusoma ikiwa unahitaji kuongeza maarifa zaidi(Kama nilivyosema mwanzo kuwa IT is all about a History of God and Man. That is what Bible is all about.
Kwahiyo kuwa na uchache wa vitabu au kuwa navyo vingi hakuifayi Bible kuwa siyo sahihi, maadam zote zina kiri UWEPO wa Mungu; Uumbaji; Uasi wa Mwanadamu, Kukombolewa kwake(Mwanadamu) na Hatima ya maisha yake baada ya hapa duniani.
Hata ukisoma Torati kwenye Bibilia ya RC ndiyo hiyo hiyo unaikuta kwenye Lutheran etc.
Karibuni tuendelee kujifunza.
Tuwekee wazi biblia ipi hapa inasema ukweli ???
All versions are not saying the same thing