Je, Biblia ya ukweli/Halisi ni ipi?

UTANGULIZI
Historia ya Biblia ya kikristo ni ndefu jinsi vitabu vilivyopatikana lakini ntaandika kwa kifupi sana na mengine tutaandaika tunavyozidi kuchangia kwenye uzi huu. Na pia nitoe rai mapema kuwa uzi huu sio wa kidini bali wa kielimu/historia hivyo sitegemei watu kurushiana matusi ya kuhusu dini sijui Mungu yupo au hayupo!! N.k
View attachment 993939
Prologue
Biblia ya kikristo ni mjumuiko wa vitabu mbalimbali vya manabii/Mitume wa Mungu ambao vimejumuishwa pamoja ili kutoa muongozo wa kiimani kwa wakristo kote ulimwenguni. Biblia inatambulika kama iliandikwa na vitabu kujumuishwa kwa uweza wa MUNGU hivyo ni kitabu kitakatifu, lakini kilichonishtua ni kugundua kwamba kati ya wakristo wanatumia Biblia tofauti kabisa yaani Wakatoliki Biblia yao ina vitabu 73, waprotestant vitabu 66, Orthodox Tawahedo (Ethiopia) ina vitabu 81 hili limenifanya nifungue uzi ili tumalize mkanganyiko huu na naomba tusome taratibu na kwakuelewa mada inazungumzia nini kabla ya kuchangia kwa kuongozwa na ushabiki au mihemko.

Historia
Wayahudi (Israel) walikuwa wanaandika maandiko wanayovuviwa na Mungu wao Yahweh tokea miaka 600 kabla ya Yesu na walikuwa na fixed canon ya vitabu 24 (39 ukivigawa) mpaka kipindi cha nabii wa mwisho Malachi 400 BC hivyo inasemekana ndio vitabu pekee vilivyokuwepo. kufikia karne ya 4 kabla ya kristo (KK) wayahudi waliokuwa uhamishoni hasa misri walitafsiri vitabu vya agano la kale vilivyoandikwa kiebrania kwenda kigiriki na kuzaa Biblia iliofahamika kama ''Septuagint''.... Biblia hii ilipata ushawishi sana kuliko ya kiebrania na ieleweke kwamba ni Biblia hii ndio imetumika mpaka na Yesu alipokuwa akinakili maandiko ya agano la kale kiufupi 70% ya quotes kutoka agano la kale kwenye vitabu vya Agano jipya vimetolewa kwenye Greek Septuagint. Kufikia hapa kukawepo na Biblia mbili kuu hivyo twende pamoja.
View attachment 993940
Mgogoro
Ikumbukwe Septuagint ilijumuisha vitabu vya kimafundisho ambavyo Hebrew bible haikuvitambua vitabu hivi vinajumuisha Macabees, Sirach,Wisdom of solomon n.k. Sasa ikafika mahali Septuagint (kigiriki) ikawa inatumika zaidi kuliko maandiko ya kiebrania (wayahudi) hivyo kwa mujibu wa mwanahistoria Heinrich Graetz ikabidi kikundi cha wayahudi kikutane kwa kilichoitwa council of Jamnia kilichofanyika 70 Baada ya kristo ambapo ndio kiliweka msimamo wa vitabu gani vya biblia ya kiebrania ndio vitambulike kwa wayahudi wote yote hii ili kuzuia upepo wa Biblia ya Greek sepruagint na hivyo hapa wakawa na msimamo wa vitabu vichache hasa vya agano la kale 39 tofauti na 46 vya septuagint. Hivyo tokea hapa madhehebu tofauti ya kikristo yakachukua Biblia mojawapo ya pande hizi mfano RC wao waliendelea na Greek Septuagint ambayo ndio ilitumiwa na mitume ila waprotestant wao waliamua kuendelea na Hebrew Bible wakiamini ndio halali na haijachakachuliwa pia madhehebu mengine kma Tawahedo Orthodox na mengineo yalikuwa na misimamo yao juu ya vitabu fulani hivyo utakuta baadhi ya makanisa yana vitabu kati ya hivyo 39 hadi 46 vya agano la kale.

Martin Luther
Karne ya 16 kiongozi wa wanamabadiliko/protestants walioamua kujitenga na ukatoliki Dr. Martin Luther naye aliamua kufanya tafsiri ya Biblia kwenda lugha ya kijerumani. Kiliandikwa 1520-34 na katika kuifanyia majumuisho naye alitaka kupunguza vitabu 7 vya agano jipya vikiwemo Ufunuo,Yuda,Waebrania na Yakobo n.k kwa kile alichokiita kwamba "havikuwa na uvuvio wa Roho mtakatifu" na hata leo hii kwenye Luther bible cha waprotestant hivyo vitabu 4 vimewekwa vya mwisho kabisa katika biblia yao na nakala za mwanzoni viliwekwa kundi moja na vitabh vilivyoitwa ''apocrypha''.

Pia luther alikipinga vikali kitabu cha esther nakutaka kifutwe kutoka kwa Biblia. Alisema hakina uvuvio wa Roho mtakatifu maana hakuna mahala kinamtaja MUNGU!! Martin luther alipinga pia uwepo wa kitabu cha James/Yakobo kwenye Biblia sabau kwanza kiliandikwa karne ya 2 ambapo muandishi wanayedai ni Yakobo kaka yake yesu alishakuwa amekufa toka mwaka 67 BK hivyo aliona kma ni kilifojiwa tu.
View attachment 993938

HITIMISHO
Sasa baada ya kuwa nimepitia baadhi ya hoja za wana JF humu hasa zinazogusa maslahi ya kikristo huwa wana conclude kuwa Biblia haina makosa maana ilivuviwa na Roho mtakatifu sasa nilikuwa nataka wajuzi mnisaidia maswali yafuatayo

1.je kauli hii inapotolewa huwa ina maana ya Biblia ipi ambayo ilivuviwa na Roho?

2. Je Biblia gani ni halali

3. Manabii wanasema usiongeze au kupunguza neno kwenye Vitabu vyao sasa Je kama mmoja ndio yupo sahihi ina maana wengi wamepotoshwa??

4. Na kama wamepotoshwa je nini hatma ya ukristo kama wahuni wachache wanaweza ongeza maneno au kupunguza kwenye Biblia

5. Swali la mwisho naamini MUNGU anaona haya makosa Je ina maana karuhusu neno lake lipotoshwe?? Na kama sio kwanini mpaka sasa kaacha wahuni wachezee NENO lake.

Naomba kuwasilisha

Cc: ningeomba Moderator kina Active na Mhariri msihamishe uzi huu jukwaa la dini ili niweze kupata mawazo ya wana JF wote hta wasio na access na jukwaa la dini, nitashukuru kwa hilo.
Nimeisoma kwa kutulia, nimeona huo mkanganyiko wa vita ya kugombea kutambulika kwa chapisho fulani kati ya hayo mengi
Kimsingi sioni tatizo kwa muktadha wa kuwa dini na imani ni vitu vinavyoathiriwa na tamaduni, mila na desturi... Hivyo katika kueneza neno la Mungu kuna mahali kulipatikana upinzani wa kutaka kuongeza ama kupunguza kitu... Lakini bado msingi mkuu haujaathiriwa kabisa

Jr
 
Tz mbongo , umeuliza ni katiba ya nchi gani ? Maadam mimi ni Mtz ni katiba ya nchi yangu , na nikiwa nje nafuata katiba ya nchi husika . Kwangu mimi katiba hasa ya nchi yangu ni kitabu kitakatifu kwani muongozo wote na kanuni za kuishi zipo pale . Watu walioandaa na kuipitisha kwa wananchi wanajulikana na tukakubaliana nao .

Sent using Jamii Forums mobile app
Unataka kusema hii katiba inayotumika sasa Tz katika nchi yako imeandaliwa na kupitishwa na watu wanaojulikana na wananchi wamekubaliana nao?
 
Katiba inayotumika maadam ni msahafu wetu tuna uwezo wa kurekebisha mambo .Umeshasikia kamati ya kurekebisha biblia ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuuliza kama hii katiba inayotumika sasa imepitishwa na watu wanaojulikana na wananchi wamekubaliana nao? Hujajibu halafu unakimbilia kusema inawezekana kubadili baadhi ya mambo,wakati zoezi la katiba mpya tumeona kilichotokea.
 
Ni mila na desturi zipi zilizoharibiwa na zingesaidia vp katika kuleta maendeleo?
Hebu fafanua mkuu maana haya mambo huwa hamtoi ufafanuzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna jamii yoyote katika ulimwengu isiyokuwa na mila na desturi zake. Kilichofanyika ni kuzivuruga ili tuzione hazina maana tukumbatie za kwao ili tufishwe kifikra. Na katika hilo walifanikiwa ndo maana wewe hapo ambaye ni zao la malengo yao unaendelea kuwatetea.
Tulikuwa na tiba zetu za asili ambazo zilisaidia sana kwenye afya. Wakajitahidi kuzififisha - lakini imekuja kugundulika kwamba hizo tiba zetu ndizo hizo sasa wanaboresha na kuturudishia kwa gharama kubwa sana.
1. Naamini unajua vyema kampuni ya DNLG wanatumia miti ipi kutengeneza dawa then wanapiga hela.
2. Naamini kama wewe ni mfuatiliaji unajua thamani ya mti wa mlonge ambao unaonekana ni mti wa kipekee kwenye tiba.
3. Kila kabila ilikuwa na namna yake ya kuabudu na kile walichokiabudu lilirudisha majibu tarajiwa. Niwe wazi katika hili ... huko mkoani Kagera ilikuwa mtu akikutenda ubaya ukamlilia Kaihula Nkuba - ilikuwa haipiti mwezi radi inashuka na kutoa tahadhari ili mtenda dhambi ajirudi.
Sijui kwenye makabila mengine lakini kote kulikuwa na utaratibu wa kuendesha ibada na kujiongoza ili jamii iendelee kustawi.
Ni mengi ambayo wamebeba na kufanyia kazi; utashangaa ukihitaji historia ya Karagwe unaipata Germany badala ya kuipata Karagwe penyewe. Leo hii ndo wanajitokeza wazungu wengine eti wanataka kuwekeza kwenye mambo ya makumbusho - hata huko kuna kitu wamelenga.
Kwa ujumla ukitaka kuiharibu jamii haribu historia yake, haribu mila na desturi zake - na katika hilo walifanikiwa
 
Hatuelewani , point ni watu wasiojulikana ila katiba watu wanajulikana ila ni upeo wa kufikiria katika kupokea hiyo katiba . Ni swala tu la umoja bila woga kudai katiba kulingana na maisha yetu . Angalia Kenya walivyofanya na wanaendelea kuichambua . Ila biblia ikisema rangi nyeusi ni nyeupe "ndio mzee" hakuna ubishi ! Hebu hoji kuhusu uumbaji wa Adam na Eva , utaitwa taahira

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna maneno ya Mungu na tafsiri ya maneno ya Mungu.
Maneno ya Mungu utayasikia kutoka ndani yako kwa sababu Mungu yuko ndani yako. Yule anayehubiriwa makanisani ni mungu wa deal. - toa ndugu toa - Mungu wa kweli anakuongoza kwenye kutambua mema na mabaya toka ndani yako. Hawa wanaotafsiri maneno ya Mungu ni deal tu. Ona walivyojimilikisha ardhi, mahekalu, vyuo n.k. kwa kivuli cha dini zao.
Hautakuja kuyajua hayo mpaka pale utakapokuwa umefunguka jicho la rohoni - jicho la tatu. Mnamchangia mchungaji / mtumishi wa mungu mahela wakati wahumini wanahangaika na maisha.
Imeandikwa Dini ya kweli ni hii - saidia wajane, maskini na yatima - mengine mbwembwe tu. Sio kwamba napinga dini ila kuna umuhimu wa kuchunguza kwa kina wanaosambaza hizo dini nyuma ya pazia wana nini?
 
Hakuna jamii yoyote katika ulimwengu isiyokuwa na mila na desturi zake. Kilichofanyika ni kuzivuruga ili tuzione hazina maana tukumbatie za kwao ili tufishwe kifikra. Na katika hilo walifanikiwa ndo maana wewe hapo ambaye ni zao la malengo yao unaendelea kuwatetea.
Tulikuwa na tiba zetu za asili ambazo zilisaidia sana kwenye afya. Wakajitahidi kuzififisha - lakini imekuja kugundulika kwamba hizo tiba zetu ndizo hizo sasa wanaboresha na kuturudishia kwa gharama kubwa sana.
1. Naamini unajua vyema kampuni ya DNLG wanatumia miti ipi kutengeneza dawa then wanapiga hela.
2. Naamini kama wewe ni mfuatiliaji unajua thamani ya mti wa mlonge ambao unaonekana ni mti wa kipekee kwenye tiba.
3. Kila kabila ilikuwa na namna yake ya kuabudu na kile walichokiabudu lilirudisha majibu tarajiwa. Niwe wazi katika hili ... huko mkoani Kagera ilikuwa mtu akikutenda ubaya ukamlilia Kaihula Nkuba - ilikuwa haipiti mwezi radi inashuka na kutoa tahadhari ili mtenda dhambi ajirudi.
Sijui kwenye makabila mengine lakini kote kulikuwa na utaratibu wa kuendesha ibada na kujiongoza ili jamii iendelee kustawi.
Ni mengi ambayo wamebeba na kufanyia kazi; utashangaa ukihitaji historia ya Karagwe unaipata Germany badala ya kuipata Karagwe penyewe. Leo hii ndo wanajitokeza wazungu wengine eti wanataka kuwekeza kwenye mambo ya makumbusho - hata huko kuna kitu wamelenga.
Kwa ujumla ukitaka kuiharibu jamii haribu historia yake, haribu mila na desturi zake - na katika hilo walifanikiwa
Unazungumzia madawa yetu asili,unataka kusema kwa mfano wachina au wakorea hadi sasa wanatumia madawa na tiba zao za asili kwamba hawatumii tiba za kizungu kama tufanyavyo sisi waafrika?
 
Unazungumzia madawa yetu asili,unataka kusema kwa mfano wachina au wakorea hadi sasa wanatumia madawa na tiba zao za asili kwamba hawatumii tiba za kizungu kama tufanyavyo sisi waafrika?
Hapo umenipata - asilimia 75 ya wachina wanatumia madawa ya asili na wameboresha hadi wana viwanda vya kutengeneza madawa ya asili yasiyokuwa na chemicals;

Fuatilia Cuba waliokataa muingiliano na mataifa ya kufuata mlengo wa magharibi wana sifa zifuatazo:-
1. Vifo vya watoto na wajawazito viko chini sana kwa sababu wao hawaamini kwenye hizi chanzo zinazosambazwa kiholela.

2. Life span ya mcuba iko juu kwa sababu anatumia kile chenye manufaa kwa afya yake.

Njooo nchi za Afrika, Ebora, Ukimwi, Maralia, homa ya ini n.k yaani kumekuwa kama dampo la maradhi. Viongozi wetu wanakubali kila kitu pasipo kuuliza wataalam kama kina madhara au la!

Umeona kwenye tiba tu - hata nyimbo wasanii wetu wameishapoteza mwelekeo wa nyimbo za asili zao.
 
Hatuelewani , point ni watu wasiojulikana ila katiba watu wanajulikana ila ni upeo wa kufikiria katika kupokea hiyo katiba . Ni swala tu la umoja bila woga kudai katiba kulingana na maisha yetu . Angalia Kenya walivyofanya na wanaendelea kuichambua . Ila biblia ikisema rangi nyeusi ni nyeupe "ndio mzee" hakuna ubishi ! Hebu hoji kuhusu uumbaji wa Adam na Eva , utaitwa taahira

Sent using Jamii Forums mobile app
Haueleweki point yako hasa ni ipi? Ni kwamba biblia haijulikani imepatikana vp ama imetungwa na nani? Au kwamba biblia haifanyiwi maborekebisho?
 
Hapo umenipata - asilimia 75 ya wachina wanatumia madawa ya asili na wameboresha hadi wana viwanda vya kutengeneza madawa ya asili yasiyokuwa na chemicals;

Fuatilia Cuba waliokataa muingiliano na mataifa ya kufuata mlengo wa magharibi wana sifa zifuatazo:-
1. Vifo vya watoto na wajawazito viko chini sana kwa sababu wao hawaamini kwenye hizi chanzo zinazosambazwa kiholela.

2. Life span ya mcuba iko juu kwa sababu anatumia kile chenye manufaa kwa afya yake.

Njooo nchi za Afrika, Ebora, Ukimwi, Maralia, homa ya ini n.k yaani kumekuwa kama dampo la maradhi. Viongozi wetu wanakubali kila kitu pasipo kuuliza wataalam kama kina madhara au la!

Umeona kwenye tiba tu - hata nyimbo wasanii wetu wameishapoteza mwelekeo wa nyimbo za asili zao.
Kwahiyo mkuu unataka kuniambia mimi nikienda china sehemu kubwa ya matibabu nitakayokutana nayo ni matibabu ya tiba za asili kuliko matibabu ya kizungu?
 
Maneno ya Mungu utayasikia kutoka ndani yako kwa sababu Mungu yuko ndani yako. Yule anayehubiriwa makanisani ni mungu wa deal. - toa ndugu toa - Mungu wa kweli anakuongoza kwenye kutambua mema na mabaya toka ndani yako. Hawa wanaotafsiri maneno ya Mungu ni deal tu. Ona walivyojimilikisha ardhi, mahekalu, vyuo n.k. kwa kivuli cha dini zao.
Hautakuja kuyajua hayo mpaka pale utakapokuwa umefunguka jicho la rohoni - jicho la tatu. Mnamchangia mchungaji / mtumishi wa mungu mahela wakati wahumini wanahangaika na maisha.
Imeandikwa Dini ya kweli ni hii - saidia wajane, maskini na yatima - mengine mbwembwe tu. Sio kwamba napinga dini ila kuna umuhimu wa kuchunguza kwa kina wanaosambaza hizo dini nyuma ya pazia wana nini?
Mkuu mie nimezungumzia kuhusu maneno ya Mungu na tafsiri ya maneno ya Mungu,sasa hayo sadaka na wahubiri yanaingia vp kwa nilichokieleza?
 
Yes naelewa mfano Biblia ya orthodox ya Ethiopia ina vitabu 81 meaning kuna maneno ya Mungu ya vitabu zaidi ya Biblia ya RC yenye vitabu 73 pekee.... Je hapo huoni maneno ya Mungu yameongezwa na kupunguzwa??

Pia kuna hoja inasema Biblia ilikuwa compiled kwa msaada wa Roho mtakatifu sasa inakuaje Roho awaambie Orthodox wawe na vitabu vingi alafu protestants wawe na vichache?? Na kama sio ningependa utumie fursa hii kukanusha rasmi kwamba kuna Biblia ambazo hazijawa compiled kwa msaada wa Roho ili iwe mwanzo na mwisho kwa wakristo wa JF kuja na hoja hiyo kwenye mada za humu

Ubarikiwe

Kuongeza ima kupunguza tbs hii hapa
IMG_20181217_203655_665.jpg
sasa utuwekee Biblia Ambayo inaenda kinyume na maagizo hayo Hata allah Ameitakasa Biblia Takatifu
IMG_20190116_105357_777.jpg
sasa wewe usie jua kusomana kazi yako uongo na uzushi na kudhania
IMG_20181122_114934_220.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuongeza ima kupunguza tbs hii hapa View attachment 995961 sasa utuwekee Biblia Ambayo inaenda kinyume na maagizo hayo Hata allah Ameitakasa Biblia Takatifu View attachment 995978 sasa wewe usie jua kusomana kazi yako uongo na uzushi na kudhania View attachment 995984

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nadhani hapo mwanzo niliweka rai kabisa huu uzi sio wa kidini na hakutakiwi kuwa na mijadala ya kukashifu dini za watu wala personal attacks otherwise uzi utahama kama mlivyoharibu ule uzi wa Book of Enoch

Hoja hapa ni Biblia gani ni sahihi kati ya vitabu 66,73 au 81?? Sasa hayo ya Quran hayajibu sababu hata hiyo Aya ya Quran haijasema hiyo Bible anayosema iko perfect ni ipi ya protestant?? RC au Tawahedo?? So bado haijajibu swali kabisa

Bottom line ni kwamba **** watu mnakuja na hoja kwamba Bible canon ilishushwa na Roho mtakatifu sasa nachojiuliza ina maana Roho mtakatifu anajipinga kiasi ashushe Canon tofauti kwa wakristo?? Na kama sio Je ina maana mmoja ndio yuko sahihi na wengine wamepotoka?? Na kama wengi wamepotoka nini hatma ya ukristo kama watu wamepotezwa miaka yote hii na hawajajikomboa??

Haya maswali ukiyajibu kisomi utakuwa umetusaidia ila ukiingiza udini hapa unakuwa hauna mchango wowote maana huwezi jua majibu yako yanaweza badili watu imani humu so jitahidi uwe positive kwenye mijadala yanayogusa imani yako.
 
Mkuu kwenye bible kuna mstari unasema hivi "kila neno lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho "
Kwa iyo wanaotumia vitabu vingi/ vichache wote wapo sawa.
....

Hawawezi kuwa sawa sababu wingi na uchache havifanani. Lazima kuna wengine watakuwa na ziada na wengine kinyume chake,tena ukizingatia suala nyeti la imani lenye kuangalia mustakabali wa waja na hatima yao. Hapa umakini wa dharura unatakiwa uchukue nafasi yake.
 
Hata allah Ameitakasa Biblia Takatifu
emoji117.png

Hivi huwa unajisikiaje unapo andika uongo wa wazi ?

Kwanini unapenda kuizungumzia Qur'an wakati hujui chochote juu ya Qur'an ? Tazama ulichokiandika na kaisome tena hiyo aya ya 115 katika sura ya 6 (Al An'am). Utuonyeshe ni wapi imezungumzia ?

Umenukuu tena aya ya 24 katika sura ya 18 (Al Ahkaf). Jaribi kuwa mkweli hata kwa bahati mbaya. Aya zote zina zinaelezea utukufu wa Qur'an.

Sasa jaribu kujenga kielimu wala si kibubusa na kufanya ghishi.
 
Back
Top Bottom