Je, Biblia ya ukweli/Halisi ni ipi?

Mkuu yote yanafanana lakini muongozo,sheria,Amri,maagizo ya Mungu n.k yapo katika kila kitabu cha Nabii au Mtume.... Sasa kimoja kinapoachwa na kanisa fulani huoni kuna maagizo ya Mungu yataachwa?? Je huoni tayari wanakinzana na mistari hii miwili

Mkuu ukisoma kitabu cha matendo ya mitume wakati ambapo ndimi za moto ziliwashukia wale mitume ambao kiuhalisia ndio kanisa la kwanza (Kama ntakua nimekosea mtanirekebisha katika hili) walivyotoka pale kila mmoja aliongea kwa lugha tofauti. Kwa iyo wale waliopokea neno la Mungu kila mmoja alilitafsiri kwa jinsi alivojaliwa na roho wa Mungu.
Nadhan Roman ndio waliochangia kwa kiasi kikubwa mpaka Leo hii kuna biblia nyingi zenye tafsir tofauti
....
 
Mkuu dog 1 kwanza shukrani kwa kuchukua muda wako na kuandaa hoja nzito namna hii iliyoshiba kwa hilo nikupongeze ila kuna maeneo ningependa unieleweshe kidogo

1. Suala la kwanza niliuliza nisaidiwe ni Biblia ipi ilifunuliwa na Roho mtakatifu maana kila dhehebu hudai Biblia ya certain number ya vitabu imevuviwa na Roho mtakatifu sasa kwenye majibu yako sijaona (oops labda sijasoma vizuri) umegusia hilo..... Na je kama Biblia zote zilivuviwa ma Roho mtakatifu ili ziwe compiled kwa namba ya vitabu hivo je ina maana Roho mtakatifu anakinzana mwenyewe?

Pia kwenye jibu lako la #1 umegusia uzito wa vitabu vilivyoachwa hasa vya deuterocanonical kwa kunipa list ya vitabu vya muhimu zaidi kwa wakristo.... Na kimojawapo umetaja ni waebrania. Sasa basi Luther Bible ilipropose Waebrania kifutwe kabisa kwenye tafsiri ya Biblia ya kijerumani Je unaona hii ni halali?? Na kama sio huoni tayari kuna Biblia zimekosa uhalali mfano hiyo Luther Bible??

2. Jibu hili nimeridhika ingawa lipo too general.... Mfano naposema uhalali namaanisha kati ya Septiagint,hebrew/masoretic,Tawahedo,luther bible n.k je ipi ina canon credible zaidi kuliko yenzake mfano Book of Enoch inatambulika kwa mainstream christians kuwa ni kitabu feki ila Ethiopian orthodox church wanatumia let alone macabees 3 and 4 ambapo Catholic na protestants wanavikataa kuwa halali ila Orthodox wanaona ni halali je inawezekana kweli Kitabu kimoja kiwe feki kwenye Biblia moja na kiwe halali biblia ingine?? Huoni hapo lazima mmoja kaingia chaka/kapotosha hivyo Biblia yake sio halali??

3.mkuu labda sijakuelewa je ina maana ni halali mtu kupunguza au kuongeza neno kww Biblia kwa sababu tu ni ufunuo na Torati pekee ndio zimekataza kuongeza maneno kwenye maagizo ya Mungu?? Mfano huoni kutoa neno moja tu kwenye Biblia kunaweza poteza maana nzima ya mstari fulani mfano
images (44).jpg


Swali la 4 bado valid if at all utakubali kuwa Martin luther ama catholic walipotosha juu ya msimamo wa kitabu cha waebrania na Esther.... Maana haiwezekani mmoja aseme sio halali na akifute kwenye Biblia alafu mwingine aseme ni halali alafu wote wawe sawa.... Sidhani kama hii ni sahihi.... Hivyo basi between Orthodox,Luther,RC lazima mmoja ndio yupo sahihi sasa basi kma wengine ndio wamepotosha je nini hatma ya kanisa kama mtu anaweza kuamka asbuhi tu na kufuta au kuongeza kitabu chochote kwenye Biblia?

5. Licha ya hoja yako nzito ila hili swali lipo valid bado yaani inakuaje Mungu awaache tu Ethiopia waongeze book of Enoch ilihali RC walikikataa tokea mwanzo..... Je kwanini Mungu hajaingilia kuepusha huu uhuni wa watu wachache kupanga vitabu kwa maslahi yao.

Shukrani
 

Attachments

  • images (45).jpg
    images (45).jpg
    24 KB · Views: 74
Lakini katika kitabu Cha ufunuo pale Yohana anaposema Usipunguze wala kuongeza ni kwa kile kitabu cha ufunuo tu sio Biblia yote maana kitabu cha ufunuo kiliandikwa chini ya uangalizi wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo mkuu kwa maelezo yako ni kwamba ni sahihi kupunguza maneno ya MUNGU sababu tu aliyeonya ni Yohana peke yake?? Ikimaanisha kwakuwa ushoga au uzinzi ukipingwa na Mtume mmoja basi haiwi dhambi kwenye vitabu vya mitume wengine yaani Biblia ni kisiwa??

Mimi nilidhani kitabu kimoja kikisema wizi ni dhambi basi ina apply kwa Biblia nzima na sio kwa specific book peke yake.

Anyway tukiikubali hoja yako kuwa kupunguza ni sawa Je hapo Biblia bado itakuwa imekuwa arranged na Roho mtakatifu kma wanavyodai wakristo?? Je Roho mtakatifu anaweza kuarrange vitabu tofauti kwenye kanisa moja hadi jingine?? Na kama ni hivyo ina maana anakinzana?? Na kama hakinzani je ina maana wanaosema Roho ndio kapangilia vitabu wanapotosha??

Ubarikiwe

Cc mitale na midimu Son of Gamba Mnabuduhe SALA NA KAZI
 
Lakini hili jibu lako linakinzana na maneno ya walioandika Biblia... Mfano Mtume Yohana wa ufunuo alisema msiongeze au kupunguza neno kwenye maandiko ya Mungu sababu mtatupwa KUZIMU..... sasa basi huoni makanisa mengine kuwa na vitabu pungufu au nyongeza tayari wamekinzana na maandiko hivo kufanya Biblia zao kuwa batili

Karibu
Biblia ambayo ilishwahi kutolewa ambayo haijapunguzwa hata kitabu kimoja kilichoandikwa na mitume,yaani kila kitabu kilichoandikwa kipo.Bilblia hiyo ipo?,na kama ipo ni ipi?
 
Hivi Yohana anasema msiongeze/ kupunguza neno kwenye biblia au kwenye ufunuo wake? Maana mimi navyojua wakati anapata ufunuo biblia haikuwepo kwahiyo hawezi zungumzia biblia!
Lakini hili jibu lako linakinzana na maneno ya walioandika Biblia... Mfano Mtume Yohana wa ufunuo alisema msiongeze au kupunguza neno kwenye maandiko ya Mungu sababu mtatupwa KUZIMU..... sasa basi huoni makanisa mengine kuwa na vitabu pungufu au nyongeza tayari wamekinzana na maandiko hivo kufanya Biblia zao kuwa batili

Karibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biblia ina historia ndefu sana. kwa mtumiaji wa kawaida inabidi tu aiache kama ilivyo na aamini kilichopo.
Maandiko ya kale yaliandikwa na wafuasi wa musa, amabavyo ndiyo vitabu vitano vya kwanza vya biblia, vinaitwa PENTATUCH. hivi ni vitabu vya mwanzo, kutoka, walawi, hesabu na kumbukumbu la torati.

Baadae walikuja manabii kama vile isaya, Amosi n.k. Inasadikiwa Amosi ndio kitabu kikongwe kabisa miongoni mwa vitabu vya manabii. sitaki kuandika kuhusu mgawanyiko wa vitabu vya biblia maana si mada husika hapa.

Biblia ilikuja kutafsiriwa kwenda kigiriki, kama mleta mada alivyopambanua. Hapa mkanganyiko ndio ulipoanzia. Walikuwepo watafsiri wengi na kwa awamu mbalimbali waliotafsiri biblia kutoka kiebrania hadi kigiriki. Ikumbukwe kuwa Tafsiri zingine zote za biblia zilitafsiriwa kutoka machapisho (tafsiri) ya kigiriki.

katika kutafsiri maandiko kwenda kigiriki, wapo waliotafsiri wakiwa mashariki ya kati (samahani mji nimeusahau) na wapo waliotafsiri wakiwa katika mji wa Alexandria- Misri. Hapa ndipo kulipotokea mkanganyiko wa vitabu vya biblia kutofautiana katika tafsiri. Mfano wayahweist (YAHWEST) wana tafsiri yao na wapo wengine (da, ukilaza wangu umesababisha nisahau majina ya watafsiri wengine, mtanisamehe) wana tafsiri tofauti. Hadi leo ukiangalia vitabu vya biblia vina tafsiri mbalimbali, mfano kitabu cha mwanzo katika biblia ya KING JAMES VERSION ni tofauti na kitabu cha mwanzo katika biblia zingine. Kiuhalisia hizi ni tafsiri tu, si aina za biblia, kulingana na origin ya watafsiri.

sasa basi, baada ya utawala wa RUMI kushiaka hatamu, watawala wa kipindi hicho walikuwa na mamlaka makubwa ya kuchagua tafsiri na vitabu vya kutumia. Kuna vitabu vingi sana ambavyo vimetelekezwa au kuachwa kwa sababu ya matakwa ya watawala. mfano mdogo na hai ni vitabu vya deutorokanoni (kanuni ya pili) vinavyotumika na madhehebu ya kikatoliki duniani kote lakini havitumiki na madhehebu mengine.

Hebu nijaribu kujibu maswali ya mleta hoja japo kidogo...

1.je kauli hii inapotolewa huwa ina maana ya Biblia ipi ambayo ilivuviwa na Roho?
Biblia ni mkusanyiko wa vitabu mbalimbali, vipo vya manabii, vya historia, injili, barua za mitume n.k. Ukiachilia mbali tafsiri mbalimbali za biblia, kiujumla biblia ni moja. tofauti iliyomo katika tafsiri haiondoi uhalisia wa biblia. Pia vitabu vingine kutotumika na madhehebu mengine, pamoja na ukweli kwamba kuna vitabu vingine vimepotea kabisa (vingine inasadikiwa vimefichwa na ROMA) bado msingi wa biblia unabaki pale pale.

vitabu visivyokuwa maarufu au vilivyopotea (mfano vitabu vya matendo ya YESU na mataendo ya PETRO) au vinavyotumiwa na baadhi ya madhehebu (mfano vitabu vya sira, wamakabayo, Thobiti, n.k) havina misingi mikubwa ya kiimani au kiroho, zaidi vinasaidia kufundisha historia ya wahusika au matukio flani. mfano kuna kitabu kinaeleza namna yesu alivyokua, yaani matendo yake akiwa kijana. Kinasema mengi kama vile jinsi mama yake yesu (mariam) alivyokuwa akitembea na yesu sehemu mbalimbale wakitenda miujiza na kuponya watu. Pia kitabu cha matendo ya petro kinatoa hadithi moja inayosema petro alikuwa na mtoto mlemavu lakini petro mwenyewe alikataa katakata kumponya... kitafute ukisome mwenyewe utafurahia hadithi hizi.

kwa kifupi, vitabu vya kiroho ni vile vya musa (pentatuch) na vya manabii. vingine ni vya Ayubu, methali, maombolezo n.k na vitabu vinne vya injili. Kuna barua za mtume paul pia vinasaidia kirao, bila kusahau kitabu cha waebrania.

2. Je Biblia gani ni halali
Biblia halali ni ile inayozingatia tafsiri halali, bila kujali ni nani alitafsiri au ilitafsiriwa wapi na lini. Kwa maana nyingine hakuna biblia haramu. Biblia ni mkusanyiko wa vitabu rasmi vilivyotokana na tafsiri rasmi.


3. Manabii wanasema usiongeze au kupunguza neno kwenye Vitabu vyao sasa Je kama mmoja ndio yupo sahihi ina maana wengi wamepotoshwa??
Ukiachana na kitabu cha ufunuo, ambacho mwandishi wake anajiita Yohane na kilichoandikwa katika kisiwa cha kupro, hakuna kitabu kingine kinachozungumzia kuongeza ua kuongeza neno. Kinachoepukwa ni kupotosha au kotoa tafsiri isiyo sahihi. Biblia imetoa wigo mkubwa kwa watafsiri, si kama Quran ambayo imekataza kabisa mchezo wowote wa kuchezea maandishi yake.

Katika tafsiri za biblia, hakuna atakaesema yuko sahihi au hayuko sahihi. Kimsimngi maana haijapotoshwa, isipokuwa watumiaji ndo hupotosha maana kutokana na imani zao au namna ya kutafsiri maandiko hayo.


4. Na kama wamepotoshwa je nini hatma ya ukristo kama wahuni wachache wanaweza ongeza maneno au kupunguza kwenye Biblia

5. Swali la mwisho naamini MUNGU anaona haya makosa Je ina maana karuhusu neno lake lipotoshwe?? Na kama sio kwanini mpaka sasa kaacha wahuni wachezee NENO lake.


Kwa maelezo hayo bila shaka hakuba haja ya kujibu maswali namba nne na tano.
cc zitto junior
Umebobea sana katika Theolojia.Hongera.

Swali la nyongeza ni kwa nini baadhi ya vitabu havijawekwa katika biblia mathalani kitabu cha Enoch.
 
Biblia ambayo ilishwahi kutolewa ambayo haijapunguzwa hata kitabu kimoja kilichoandikwa na mitume,yaani kila kitabu kilichoandikwa kipo.Bilblia hiyo ipo?,na kama ipo ni ipi?
Hiyo Biblia huenda ilikuwepo zamani enzi za kina Obadiah au mordechai ila kwa sasa sidhani kama ipo complete Bible maana **** vitabu ambavyo vilikuwa considered kwenye Hebrew canon ila kwa sasa vinatambulika kama Lost Books mfano Book of samuel the seer,Chronicles of Nathan the seer n.k.

Ila hyo ni history kabla hata Yesu hajaja ila toka amekuja vitabu ambavyo ni canonical vinajumuisha kati ya 66 hadi 81 ndio hapo mzizi wa mada kwamba kwa Biblia zilozopo je ipi ni credible in terms of numbers tukiassume mmojawapo ndio halali kuliko zingine.

Ni hayo tu
 
Hivi Yohana anasema msiongeze/ kupunguza neno kwenye biblia au kwenye ufunuo wake? Maana mimi navyojua wakati anapata ufunuo biblia haikuwepo kwahiyo hawezi zungumzia biblia!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ndio napojiuliza ina maana kila kitabu cha Biblia ni kisiwa?? Yaani Musa akikataza uzinzi basi anaongea na waisrael sio watanzania au wakristo?? Tukienda kwa staili hii ina maana hata amri 10 za Mungu kwakuwa zilitolewa kwa Waisrael basi watanzania hazituhusu si ndio maana yake mkuu ??
 
Umepewa akili itumie kuutafuta ukweli.
Biblia inaongelea mambo ya mashariki ya kati, haiongelei mambo ya Mwanamalundi wala Mkamantale. Hivyo kwa kuyajua hayo tu ni dhahili kwamba ina mapungufu na haifai kutumiwa na ulimwengu wote.
Ukiangalia wachina ambao hawakuikubali wamepiga hatua na Mungu anawabariki kwa kuwa hawakukubali kudanganywa. Afrika iliyokuwa imebarikiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu - imeadhibiwa kwa sababu tulipokea uongo toka kwa wezi (wazungu) na Mungu akachukia.
Wewe jiulize inakuwaje mtu anasimama anahubiri watu kusameheana wakati yeye kwenye miongozo yake hakuna neno msamaha.
J.K aliwahi kusema hivi "za kuambiwa weka na za kwako"
 
Umepewa akili itumie kuutafuta ukweli.
Biblia inaongelea mambo ya mashariki ya kati, haiongelei mambo ya Mwanamalundi wala Mkamantale. Hivyo kwa kuyajua hayo tu ni dhahili kwamba ina mapungufu na haifai kutumiwa na ulimwengu wote.
Ukiangalia wachina ambao hawakuikubali wamepiga hatua na Mungu anawabariki kwa kuwa hawakukubali kudanganywa. Afrika iliyokuwa imebarikiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu - imeadhibiwa kwa sababu tulipokea uongo toka kwa wezi (wazungu) na Mungu akachukia.
Wewe jiulize inakuwaje mtu anasimama anahubiri watu kusameheana wakati yeye kwenye miongozo yake hakuna neno msamaha.
J.K aliwahi kusema hivi "za kuambiwa weka na za kwako"
Mbona wazungu wamekubali kudanganywa na bado wameendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom