Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,431
- 1,045
Soma hii series kisha uamue mwenyewe!
Hadithi inaanzia hapa:
Ikafuatiwa na…
Nini kikafuata?
Na sasa:
Kiambatanisho
Je, sasa unamwamini Jason Bourne walau katika hili?
Hadithi inaanzia hapa:
Jason Bourne
RIPOTI YA UCHUNGUZI BINAFSI JUU YA UGONJWA WA DR HARISON MWAKYEMBE 12/10/ 2011 (Kama hukupata kuisoma, isome hapo chini mwisho kabla Invisible haja iondoa tena)
Ikafuatiwa na…
HALI YA WAGONJWA DR MWAKYEMBE, MWANDOSYA NA ZITTO -INDIA
JASON BOURNE
TEL:
ID :
Hali ya Mwakyembe
Katika jamii inayoamini maombi kuwa ni sehemu ya uponyaji, basi yatupasa watanzania wenye mapenzi mema na Mh Mwakyembe tufanye hivyo tena haraka sana. Kwa mda wa dk20 nizokaa ndani ya chumba chake maalumu chenye vihami sumu, kwakweli nilitokwa na machozi.
Mh hali yake ni mbaya! Nadhani mtu mzima akisema hali ni maya bila shaka mnatambua.
Hali ya Mwandosya:
Mh Mwandosya sikuweza kumuona live hii ni kutokana na mahali alipolazwa kuwa mbali kidogo na hapo alipo Mwakyembe, Taarifa nilizo zipatata kutoka kwa Daktari Virmandh Gaemr mmoja wa madaktari wanaomtibu Mwandosya ni kuwa hali yake haina tofauti sana na ya Mwakyembe.
Hayo ndiyo niliyoyaona kwa macho yangu!
Asanteni sana.
Nini kikafuata?
…… hatimae yale maneno mengi na kelele za wizara ya afya leo zimezimwa pale shangingi liliposogelea ndege ya Emirates na huku gari la kubebea wagonjwa kutoka Swiss port likijisogeza kwa ukaribu zaidi, kuashiria kuna mtu anashuka akiwa ndani ya wheelchair ama stretcher.
Hatimae gari likajisogeza pembeni na kukaribia kwenye Landcruiser gafla mikono ya shupavu Prof Mwandosya ikajitokeza kushukuru watanzania
na kwa maombi yao na ukarimu wao.
Na sasa:
Monday, 12 December 2011 20:42 Naibu Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe
Patricia Kimelemeta
NAIBU Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, amerejea nchini akitokea Hospitali ya Apollo nchini India alikolazwa kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wa ngozi. …..
Kiambatanisho
Jason bourne said:
Ripoti ya Uchunguzi Binafsi juu ya Ugonjwa wa DR HARISON MWAKYEMBE 12/10/ 2011
Baada ya kushauriwa na afisa mwandamizi wa JF bwana PAW kuwa niifanyie marekebisho kidogo hii ripoti na mimi bila hiyana nimefanya hivyo. Ni matumaini yangu kuwa japo uhalisia kamili wa ripoti utakuwa umepungua lakini nitawaomba kuweni wavumilivu.Vilevile nitawaomba radhi wale mtakao kerwa na mpangilio mbovu wa hii ripoti, hii ni kwa kuwa mimi si mtaalamu sana wa uandaaji wa ripoti.
RIPOTI YA UCHUNGUZI BINAFSI JUU YA UGONJWA WA DR HARISON MWAKYEMBE 12/10/ 2011
JASON BOURNE
TEL:*********
ID************Hatua ya kwanza:
Niliamua kujua kama ni kweli kalishwa sumu au laa. Na watu nilio wahusisha katika kujua huko ni TISS.
Katika uchunguzi niliweza kuzungumza na LTK wapatao kumi na tano.
Wote maelezo yao yalifanana kwa maana ya (walishiriki kupanga na kutekeleza kumlisha sumu Dr Harison Mwakyembe) Hatua walizopitia:
- Maboharia wawili
- Wapanga mikakati wawili
- Mkuu wa LTK
- Vijana wa kazi kumi
Kwa mujibu wa maelezo ya LTK/D00/B1 mkuu wa kitengo hicho ambae kwa kweli niliongea nae kama rafiki yangu wa karibu ndie aliyenipa mwangaza wakufanikisha kazi yangu.
Katika misheni hii watu wengi wanatakiwa KUFA, nitawataja wale muhimu tu:
1. Wilblod Slaa
2. Samweli Sitta
3. Harison Mwakyembe
4. Said Kubenea
5. Mark Mwandosya Mnamo ijumaa ya tarehe 01/10/2010 saa 4:25, kikao kikuu cha mikakati kilikalika Moven Pick kikihudhuriwa na watu sita,
Baada ya mjadala wa saa moja uliogusa magumu inayokumbana serikali na watu walio waona wao ni vikwazo na waliosababisha magumu hayo, ndipo wakaibuka na listi ya wanaotakiwa kusalimisha uhai wao:Bada ya hapo kesho yake TISS/B1 alikutana na LTK/D00/B1 na kumpa amri ya misheni hiyo na orodha kamili ya watuhumiwa bila kumwambia sababu za mauaji hayo, zaidi alisema "nahitaji ripoti ya utekelezaji".
- TISS/A001 XXX
- TISS/B1
- TISSB32
- TISS/B5
- TISS/A6
- TISS/F5
.....
Je, sasa unamwamini Jason Bourne walau katika hili?