ArD67
JF-Expert Member
- Nov 14, 2016
- 2,817
- 2,044
Ndugu! Ktk nchi yenye mchanganyiko wa dini kama Tanzania,,,,, dini ya kati huwa inazaliwa. Ulichokiongea hapo kina nusu uislamu na nusu yake ukristu. Hakikubaliki chote kwa upande wowote ule.Aliyekataa kumsujudia(kumtukuza)Adam ni Iblisi,Iblisi ndio alikiwa miongoni mwa malaika,alipoasi ndio akawa iblisi.Hivi ni viumbe wawili tofauti,kuna jini na Iblisi,ndio masna mtu akifanya jambo ovu,kama kubaka,hasemi jini kanipitia,asema shetani kanipitia au iblisi kanipitia.
Kwenye Qur'an(sio tafsiri),aliyetajwa ni Iblisi,hakuandikwa shetani,ndio maana unaposoma tafsiri ya Qur'an,husomi Qur'an,unasoma tafsiri ya Qur'an.
Uislamu unafundisha kwamba, Mungu ameumba viumbe vya aina tatu vyenye kujitambua (utambuzi), malaika (nuru), majini (moto) na binadamu (udongo). Tofauti ya malaika na hivi viwili vilivyosalia ni utashi, malaika ni maroboti hayawezi kujiamulia cha kufanya. Hivyo hawawezi kamwe kufanya dhambi. Lucif–ER huyu alikuwa ni uzao wa majini,, aliyeishi mbinguni. Nature yake ikamruhusu kufanya dhambi.
Kuhusu majina shetani na ibilisi, kwanza ni yenye asili ya kiebrania yakimaanisha uasi na upinzani. Hili si jina halisi la kiumbe bali la matendo. Lucifer ni shetani na ni ibilisi.
Inshu ya kukataa kumsujudia Adamu kuwa ndo kosa la Lucifer, hili ni fundisho la uislamu tu. Ukristo haufundishi hilo. Ukristu unasema tamaa ya mamlaka ilimuwaka akatamani naye akae siti ya mola wake.
Ukristu unafundisha kwamba Lucifer alishaanguka zamani sana, kabla ya uwepo wa Eva. Na inawezekana alishajaribu mbinu nyingi kumuangusha Adam akashindwa,,,, Eva alipoumbwa aliutumia udhaifu wake. "si huyu Eva uliyeniletea "
Quiz, Adam aliishi miaka mingapi kabla ya Eva kuumbwa? Ikumbukwe siku moja ya Mungu ni sawa na miaka 1000 ya kwetu.