Msaliti wa mapenzi anastahili adhabu ambayo itamfanya siku nyingine awaze mara mbili kufanya usaliti
Na hii ni mahsusi kwa wanandoa, kwasababu kwa watu ambao hawaishi pamoja inakuwa haina uzito sana,au ni ngumu kuitekeleza
Kwanza ifahamike mwanandoa msaliti haadhibiwi kwa makofi au kipigo,au kwa namna yoyote ile ya kudhuru mwili,bali adhabu yake inakuwa ya kisaikolojia zaidi
Lakini kabla ya kutekeleza adhabu hii,unatakiwa umwambie kabisa mwenza wako kwamba yani kuanzia sasa hivi mambo hayatakuwa kama ilivyozoeleka mpaka pale utakapo kuwa sawa.
Punguza baadhi ya mambo ambayo ulikuwa unayafanya hapo awali wakati usaliti haujatokea
Mathalani kama mlikuwa mnakula chakula pamoja,au ulikuwa huli chakula mpaka arudi,basi Sasa anza kula peke yako,kama ni mke mtengee chakula mumeo na muache mezani ale peke yake, hii itamfanya atafakari sana makosa yake na kujiuliza what is the next step huyu mtu anafikiria nini, je hiki chakula kaniwekea sumu nini
Kama ulikuwa hulali mpaka muende wote kulala,now wahi kwenda kulala au Chelewa kwenda kulala,ilimradi aone Kuna utofauti wa mambo na yaliyo kuwa zamani
Kama mlikuwa mnakawaida ya kupiga mastory na kuulizana habar za kazi au za harakati mbali,now kausha piga kimya tu,ni salamu na mambo mengine yaende kimya kimya
Linapokuja swala la kuhondomola chakula cha usiku,piga stop,mwambie mwenzako haupo sawa kwa yale yaliyo tokea,mpaka utakapo kaa sawa
Kumbuka hapa haununi ila unapunguza tu baadhi ya mambo ambayo mmekuwa mkoyafanya pamoja wakati mkiwa na furaha
Na vile vile inakupa nafasi ya kutafakari bila kukurupuka,kuhusiana na kuachana na mwenza wako au laa,maana wakati mwingine,unaweza kufanya maamuzi ya ghafla kutokana na hasira ukajikuta baadae unajutia
Au kama ni mume mwambie mkeo aende kwao kwanza akapumzike upate nafasi ya kutafakari kwa hilo lililotokea
Sasa kwa kipindi ambacho mko mbali ndio utajua je huyu mtu anafaa kusamehewa au laa,je mapenzi yangu kwake ni makubwa kuliko makosa yake,maana kama mapenzi yako kwakwe ni makubwa kuliko makosa basi ni rahisi kumsamehe na hutojutia
Njia hizi huwa zinamfanya mkosaji ajitafakari sana,kwasababu zinaruhusu akili yake kuona tatizo alilolisababisha,na kuona madhara ambayo amesababisha,hivyo atajitafakari na huenda akaona athari ya jambo hili kama atarudia tena ujinga wake
Lakini kwa mwanamke,fanya mambo haya hali ukijua una kipato chako,pale ambapo mume akikata mahitaji ili akunyong'onyeze ili uombe poo,anakuta upo ngaangali na maisha yanaendelea kama kawaida
Kumbuka kumsema mwenza wako kwa watu kwa usaliti alioufanya,hapo haumfundishi kitu,sana sana atazidi kufanya hivyo kama kukukomoa
Kumtukana kwa alichofanya hautamfunza kitu sana sana utamtia hasira na kufight buck
Hapa unaact cool lakini unampa somo ambalo atabakia nalo siku zote,na atajiuliza next time nikizingua je itakuwaje
Hakuna mateso mazuri kama ya kisaikolojia,ebu chukulia kwamba mumeo au mkeo kakufumunia lakini ana act normal kana kwamba nothing happened, trust me usiku unaweza usilale kwa amani unawaza fikiria anataka kunichinja kimya kimya nini,hapo ndio utakuta kama ni mke huyo anasepa kwaoo kwa wazazi wake
Halafu ukiulizwa Baba vipi kuna shida gani na mwenzio mbona kaja huku,hapo unajibu hakuna shida yoyote ile labda yeye ndio aleze labda kuna shida gani mpaka ameondoka nyumbani
Wakati mwingine huhitaji kutumia mabavu na hasira kumfunza mtu adabu unatumia akili tu
Alamsiki!