JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Ertugrul Bey win-one Fake P ShesRise_1 hebu toa ufafanuzi hapa usitumie AI tumia uelewa wako

Kesho kidunia ipoje?
Tunaambiwa muda wa Tokyo upo mbele kuzidi wa Dar hivyo, sasa Tokyo ni kesho Dar ni leo, maana yake mtu wa Tokyo anayajua yaliyoyokea kesho?

Kama hajui basi hio kesho ni ya kwenye kalenda tu na sio kesho halisi kote Dar na Tokyo ni leo lakini kisaa na kikalenda ni kesho?

Tokyo 05:16AM 19th August 2026, tomorrow
Dar es Salaam 11:16PM 18th August 2026, today
Hope ulipata majibu
 
Nurse aacha kazi na kujiuza, tangu aache kazi ni mwaka mmoja umetimia mume hajui chochote

Karibu sana kwenye uzi mkubwa kabisa "Usiku wa Manane" hapa jamii forums,hapa tunasanuana, tuna have fun na tunaelimishana pia

Leo tupo Kisumu,leo kuna kubwa kuliko,ukisikia kazini kuna kazi basi ndio leo,ndoa hizi zina mambo sana,lakini tuendelee tu kuoa na kuelewa ndio asili ambayo ameumbwa nayo mwanadamu

Huyu mke ni nesi na mume ni bank teller, tangu wawe pamoja wana miaka mitano sasa,na wana mtoto wa miaka 2

Kama kawaida kila mtu huwa anamuamini mwenzake sana,ingawa host wa show huwa na kauli yake moja kwamba " usimsifu mtu public kuwa ni msafi" nakuballiana nae kabisa,hata wewe msomaji wangu pamoja nami, usifanye hivyo ipo siku utashangazwa sana

Huyu dada kwanza Mashaallah kaajaliwa mshepu wa namba nane,figure la kuwafanya wanaume wakodoe macho,lakini mishepu hii ingawa tunaipenda ila ina gharama Zake ambazo uwe tayar kuishi nazo,ikiwemo kupigiwa,kuchunwa sana na kufanywa fala in the name of love.

Wadada hawa marafiki kama watatu waliamua kuacha kazi kwa kufanya ukahaba wa kutoka na wazungu na watu wa high profile.,kwahiyo sometimes dada anaaga kwenda semina sehemu anakaa siku kadhaa kumbe huko anajiuza

Kuna meseji ilisomeka, mwenzake anamwambia ni mara ya pili sasa unapata infections, kwahiyo kama walikuwa wanaambiana wawe makini zaidi, lakini kuna text nyingine huyu mke anamwambia mwenzake yule mzungu ni govi na nimeenda nae kavu kavu

Kupitia meseji mbali mbali imegundulika kazi yao ni kujiuza,na walikuwa wanapata doo kweli kweli /wanapata pesa nyingi sana

Mfano mume anasema siku moja mke kaja na bonge la screen,kumuuliza akasema amepewa zawadi kazini, na mume akaendelea kusema huko kwa nyumba kuna vitu vyenye thamani sana.

Lakini katika chat zao inaelekea waliazimia kabisa kuja kuwa reach,maana wanasema tumejitolea kuacha kazi kwa shughuli hiyo hivyo lazima wapambane

Kuna siri moja pia imeibuka kupitia text hizo,inaelekea kuna dada mmoja miongoni mwao aliuwawa na mzungu,na wao wanajua kila kitu,ndio mume akamwambia mke wewe utakuwa unajua siri ya kifo cha mwenzenu au mmeshirikiana kumuua

Ebu fikiria katika maelezo ya awali kabla ya siri kugundulika alikuwa anakosa muda wa kuonana na binti yake in the name of kazi nyingi,anarudi late sana halafu anaondoka asubuhi sana,kumbe hata kazi yenyewe alishaaacha,

Kama mwanaume how does it feel, ukute saa nyingine hata unyumba hupati kumbe mke anafanya ujinga,mfano mume anakumbuka kipindi fulani alitaka kuichapa mke akatoa visababu,kumbe ndio kipindi hiko ako na infections

Wakati mwingine mume unanyimwa game kumbe wife hashaharibu huku so anaona soo ishu ikabuma au anakuokoa na infections

Haya mke mwaka mzima kaacha kazi na anaondoka na kurudi kama kawaida,guys tujifunze kusoma patterns, naamini kabisa kama mwamba angekuwa makini nauwakika kuna kitu angegundua,kwasababu naamini kabisa kuna nyakati lazima ratiba za kwenda na kurudi kazini hazikuwa sawa

Ndio maana nasema hapa tusisome hizi story kama burudani tu,bali kama masomo ambayo yatakufungua ufahamu wako kuchukua hatua za kusoma nyendo ambazo hazieleweki, mfano kila wakati mwenza wako anasema ana semina semina,tena huwa zinaongozana ongozana,je ushawaza kujua ukweli wa hizo semina?

Mwisho wa siku jamaa akamvua mke wake pete ambaye sasa tumuite mbwa Pete ya ndoa na kuondoka nayo,na kumwambia yeye huwa hapigi wanawake au kuwamwagia asidi,la sivyo angemtimba pale pale,na mwisho akamwambia aje home kuchukua vitu vyake tu tena atavikuta mlangoni

Kama haitoshi nilitaka kusahau,kwenye meseji mke alikuwa anamwambia mwenzake kwamba "anajilaumu kwa kuolewa mapema sijui ni presha kutoka kwa ndugu,maana mama alimpenda sana huyo kijana" hapo hapo alidhamiria baadae kuja kuwa reach single mother kwa kumuacha mume wake"

The fun thing is, alipoambiwa anaachwa basi alijiliza na kupiga magoti kwamba asiachwe,wakati kiuhalisia alipanga aje amuache baby baba wake, guys wanawake silaha yao kubwa ni kujiliza na kughala ghala chini usipokuwa makini unaweza kumsamehe chap,kuwa makini usiingie kwenye huo mtego, kanuni ni moja tu ukimfumania msaliti ni kuachwa tu period

Mwisho wa siku jamaa alimshukuru sana host wa kipindi kamsaidia kumsanua kuhusu huyo mke wake,mume anasema he had a big plans for her wife,so afadhali amejua mapema

Ladies msipende sana hela mpaka mkasahau afya zenu, just imagine huyo ni nesi na mtalaamu wa afya lakini alikuwa anachapwa kavu kavu,hata mume alimuuliza " hivi hiyo kada ya afya ulisomea nini sasa hata kama hujui kuthamini afya yako.


View: https://youtu.be/cHkBLYKx0JM?si=F2655L5efB9nCdHS

Wadau mambo ni mengi na muda ni mchache

Mpaka wakati mwingine

Alamsiki!
 
Back
Top Bottom