JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Anko ndani ya anniversary ya kumbukumbu ya kifo cha mkewe,amejikuta ameulewa mzigo wa mtoto wa dada yake

Kuna watu huwa hawatambulishwi mizigo ya kuvunja chaga,kitendo cha kumtambulisha hilo bonge la dada ujue kinachofuatia ni lawama

Homeboy aliamua kwenda na mwenza wake kuuungana na anko wake kwenye kumbu kumbu ya kifo cha mkewe aliyefariki kwa covid

Lakini kumbe nyuma ya pazia anko akaulewa ule mzigo,wakabadilishana namba na demu wa chalii bila chalii mwenyewe kujua

Huku maisha ya kijana na demu ni changamoto,muda wa kulipa kodi umefika na mwamba mfukoni hapaja eleweka,manzi akiuliza je inakuwaje,mwamba anatoa ahadi tu

So manzi akaamua kutangaza shida kwa anko na anko naye hana baya ukichukulia kwamba mzigo ameulewe

Changamoto ya pili,ilifika siku ya wapendanao,mwamba yupo job anapambana,huku demu anaona wenzake wanafanya mitoko akaona huu ujinga haiwezekani yeye kukaa nyumbani wakati anko anaweza kumtoa out,ingawa bwana wake alimwambia atamtoa out tar 15 February siku moja baada ya Valentine kupita, hilo haliku mfanya bibie akatishe ratiba yake ya kula Valentine day tar 14

Demu anasema hakika anko wa bwana wake alimtreat vizur sana,akajisikia furaha sana,alipoulizwa ilikuwaje ukatoka out na anko na kutembea nae,akajibu ni tamaa tu imempata,akaulizwa tamaa ni mara moja lakini mbona nyie mmekutana mara nyingi,akaishia kuomba msamaha

Akaulizwa ebu sema ukweli hapa kwenye kamera je unampenda anko,mtoto akasema ndio

Basi bwana wake mpambanaji akamwambia basi nenda kwa anko wangu kwakuwa unampenda,mtoto anabaki kusema sasa tumezaa mtoto inakuwaje na wewe ndio baba mtoto wangu,mwamba hakuelewa somo akasepa

Hayo ndio maisha ya mapenzi,hakika lolote linaweza tokea na kwa wakati wowote ule

Video hii hapa,cheki mwenyewe zigo la kuvunja chaga,usije ukasema Ertugrul bey analeta sound tu


View: https://youtu.be/cw6uZlBomLk?si=2qBt9_rori6z9ylQ

Alamsik!
 
Back
Top Bottom