JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Nimefungua uzi huu kutokana na kuwa na janga la kukata usingizi usiku. Kama na wewe ni mmojawapo naomba tuungane pamoja hapa kwa kuandika ulipo na unafanya nini kwa wakati huo baada ya kukosa usingizi.

Muda wa jukwaa ni kuanzia saa 6 usiku mpaka 11 asubuhi. Mimi hapa leo tangu nimeamka nimeamua KUFANYA IBADA Tuuuu!
7:37
 

Matumizi ya pesa yasichukue nafasi kubwa katika mapenzi yenu.



Iwe ni mwanamke au mwanaume, ukiona mahusiano yenu kwa kiasi kikubwa yanategemea pesa ili yaendelee, basi ni wakati wa kutafakari kwa makini. Nimesema mwanamke au mwanaume kwa sababu siku hizi hata wakina dada wengi wana uwezo wao wa kifedha.

Wapo wanaowatunza na kuwasaidia wapenzi wao pale wanapoona kuna upendo wa kweli.

Lakini mahusiano ambayo furaha yake, amani yake na hata uwepo wake unategemea pesa, hayo si mahusiano yenye msingi imara. Mara nyingi mmoja anakuwa anamtumia mwenzake kwa maslahi yake binafsi.

Juzi kati nakumbuka mdau mmoja alisema, "Nikikumbuka gharama nilizotumia kubembeleza penzi, roho inaniuma sana." Ukweli ni kwamba utaumia sana ukigundua ulitumia muda, nguvu na fedha nyingi kuokoa mahusiano ambayo kumbe upendo wenyewe haukuwepo.

Mtu anayekupenda kwa dhati atakuhurumia. Ni kweli anaweza kuhitaji msaada wako mara chache, lakini haiwezi kuwa kila wakati. Yule ambaye hana mapenzi ya kweli kwako hatajali hali yako. Kitu kikubwa anachokitafuta ni kile anachoweza kupata kutoka kwako, na akishakipata ataendelea na maisha yake.

Kama kuna red flag ambayo wapenzi wanapaswa kuiangalia kwa makini, basi ni namna pesa zinavyoathiri mahusiano yao. Ukiona mwenzako anabadilika ghafla kwa sababu umeshindwa kumpa pesa, kutatua shida yake kwa wakati, au umemwomba akupe muda kidogo, kisha anaanza kununa, kukukwepa au kukunyima upendo, hiyo ni ishara ya kutafakari kwa kina. Inawezekana kinachothaminiwa si wewe, bali kile unachokitoa.

Love should not be negotiated. Mapenzi ya kweli hayapaswi kuwekwa mezani kama biashara yenye masharti. Anayekupenda kwa dhati atakuelewa hata unapokwama. Badala ya kukuongezea presha, atakuwa bega lako la kutegemea na leso yako ya kufuta machozi.

Lakini ukigundua kwamba bila pesa hakuna tabasamu, hakuna ucheshi, hakuna ukaribu, na furaha yote inarudi tu pale unapotoa fedha, basi ni vyema kushtuka mapema kabla hujapoteza zaidi ya pesa zako. Unaweza kupoteza pia amani ya moyo wako.

Mapenzi ya kweli hujengwa juu ya uaminifu, heshima, kuelewana na kujali, si ukubwa wa pochi.

Alamsiki!
 
Back
Top Bottom