Je kuna haja ya wanandoa kupekuana simu zao au kuacha kupekuana na kikubwa ni heshima itawale
Kwanza nianze kwa kusema nyakati hizi simu zetu za mikononi ndio zimekuwa adui mkubwa wa ndoa na mahusiano yetu,sasa hivi huhitaji kupeleleza kwa majirani kuhusiana na mwenendo wa mkeo au mumeo,unachohitaji ni kupekua simu ya mwenza na mara paap file hili hapa
Sasa kwa wale ambao mnanifuatilia story ambazo huwa nazileta kila usiku hapa jukwani,utagundua kwamba hawa wanandoa au wapenzi wamekuwa wakiaminiana na kufurahia ndoa zao bilashida yoyote ile, na wengi waliokutwa barabarani walikuwa ama wanaenda Shopping na wenza wao,au hospital au kwenye starehe na mahala Pengine popote pale wakiwa wanafuraha kabisa
Lakini mambo yalibadilika pale tu simu zilipopekuliwa na kugundulika usaliti ndani yake
Kwa maana nyingine watu wamekuwa wakiishi kwa furaha kana kwamba hakuna usaliti unaofanyika huko nje,kikubwa waliheshimiana kama wanandoa au wapenzi,huku kila mmoja akificha makando makando yake
Na haya ndio maisha yetu ya kila siku,iwe Afrika au Ulaya au Asia,binadamu ni wale wale kinachotofautiana labda mazingira na nyakati za kufanyia huo usaliti
Je wazee wetu huko nyuma hawakuchapiwa? Jibu ni kwamba walichapiwa na hata kulea watoto ambao sio wao walilea pia
Ila walijua haya mambo yapo ndio maana walijaribu kuenda nayo sawa,na matokeo yake ndoa zilidumu sana,si kwasababu walijua kinachoendelea kwa wenza wao na kukubaliana nacho,ila kwa kutotaka kujua nini kinaendelea kwa wenza wao.
Kwa maana ya kwamba hawakutaka kupepelezana na kufuatilia kila nyendo ambazo wenza wao wanapita,na hiyo ndio siri kubwa ya ndoa zao kudumu
Mathalani mume anaposafiri na ukizingatia kipindi kile hakuna simu za kupeana taarifa kwamba narejea nyumbani,alikuwa akirudi kutoka safari,hafiki moja kwa moja nyumbani,ila atapitia kijiweni na kutoa taarifa nyumbani kwake kwamba amerejea kutoka safari, ama kwa kutuma mtu apeleke koti nyumbani kwake au kipaseli,lakini lengo kubwa ni kutoa taarifa kwamba iam back
Hii maana yake hata pale home kama wife ana mtu pale basi asafishe njia kwakuwa mwenye mji karudi,kwahiyo akifika asikute sintofahamu yoyote ile
Kwa maana nyingine wazee wetu walikuwa wanatumia kila namna ya njia ili tu wasikutane na shida kwenye ndoa zao,hawakutaka stress kabisa kana kwamba walikuwa wanajua,if you want trouble you will get trouble,and if you want peace basi jiweke mbali na kutafuta trouble.
Hivyo ndivyo walivyoishi na kweli walipata amani ndani ya nafsi zao na ndoa zilidumu sana, matukio walikuwa wanapigana lakini stahili ya maisha waliyoishi hayakuathiri maisha yao ya ndoa,kwakuwa hawakutaka kujua au kutafuta shida,hawakutaka kufumaniana,hawakutaka kupelelezana
Sasa sisi ambao kila kukicha tunatafuta kupelelezana,kila kukicha tunataka kufumaniana,ndio ambao tunaongoza kuharibika kwa ndoa zetu na mahusiano yetu
Lakini lau tungeishi kama huko wazee wetu walivyoishi naamini kabisa tungezeeka pamoja
Kupepelezana kuna faida na hasara zake,miongoni mwa faida ni kuepukana na maradhi,kuepuka kulea watoto ambao sio wako,na kuepuka hila mbali mbali za kimapenzi
Lakini hasara zake naona ndio kubwa zaidi,ikiwemo kusambaratika kwa familia,maana siri zikisha fichuka ni asilimia chache sana ya ndoa ambazo zinaweza kuendelea kuwepo,lakini nyingi huvunjika na kupotelea mbali
Hapo msingi mzima wa maisha ya ndoa unakufa,watoto wanakuja kupata tabu,mpango mzima wa familia unatetereka
Ukiniuliza mimi kipi ni bora,kati ya kupekuana na kupeleleza au kuishi kwa kuaminiana na kuheshimiana,nachagua kuishi kwa kuaminiana na kuheshimiana,kwasababu hapa napata amani ya roho na nafsi pia
Nitampenda mwenza wangu siku zote,na nitafurahia maisha ya ndoa
Lakini nikichagua kupelelezana na kuchunguzana,siku zote nitaishi kwa hofu na kukosa raha,kila tukio la mwenza kuchelewa kurudi kazini nitahisi katoka kuchapwa,kila simu yake inapokuwa busy nitahisi anaongea na mabwana zake,kwahiyo utajikuta kila tukio ambalo hata la kawaida utalitafutia majibu ambayo yatakuumiza na kukukosesha raha
Na kibaya zaidi kadri utakavyokuwa na mawazo hasi ndivyo ubongo wako utazidi kukuonyesha mazingira ambayo utaamini ni ya kweli,lakini kumbe kiuhalisia ni hisia zako tu basi.
Kikubwa watu waheshimiane,hata kama labda una mpango wa kando basi hakikisha amani ya mwenza wako inaendelea kutamalaki,acha dharau kwakuwa tu unabebishwa huko nje,kumbuka hao wa nje wanakupenda kwasababu una ambaye anakutunza,siku ambayo utamwambia nimeachwa nae huyo anachapa lapa,kwakuwa hakujipanga kufanya majukumu yote ambayo mumeo au mkeo anayafanya
Kwahiyo tambua siku zote embe ni tunda la msimu tu ila nazi itaendelea kuwepo siku zote au waswahili wanasemwa usiteme Big G kwa karanga za kuonjeshwa
Alamsik!