Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Muda wa kazi unaisha saa 9, wengine wanaweza kuchelewa kidogo, muda wa watoto kutoka kwenye masomo pia ni saa 9, bado wikiend mpo wote nyumbani, so ni suala la kuamua unatumiaje muda wako tu, kuwa na familia ama kufanya mambo mengine. Mtoto kutaka jambo sio lazima apitie kwa mama,inategemea na jambo lenyewe, kuna mambo mengine anataka kwa mama kisha anapitia kwa baba, anafanya vice versa. Sema sasa kama baba hatumii muda na watoto, wanaweza wakawa wanamuogopa hata kufanya maongezi nae, ndio case unayomaanisha nadhani
Hujasema kweli. Muda wa kazi unaisha saa tisa, je kazi hiyo unaifanyia nyumba ya pili? Je, watoto wote wanarudi saa 9 nyumbani? Je, majukumu ya kazi yatakuacha siku zote utoke saa tisa, usisafiri kikazi n.k?

Kwa hiyo unapinga mtoto kuwa karibu na mama zaidi? Unapinga hili?
 
As far as gender matters are concerned ;there's no turning back

Men simply have to brace for impact
Not a laughing matter bt hamna namnaa
Wanawake ndio wana feel nock on effect. Wanazalishwa na kuachwa. Wanatumika na kuchoshww kisha siku zao zikipita wanaandamana kwenda kwa RC. Wananung'unika siku hizi wanaume hawaoi, wanawachomachoma tu na kuwaacha.

Godly women will always be the happiest on planet earth!!
 
Pole,mtoto anahitaji mapenzi ya baba na mama,

bond husaidia mtoto ajifunze social skills.

..mtoto aweze kuinteract na both men and women#

,sasa nyie mliolelewa mama akiwa 'kijakazi' na baba akiwa na Authoritarian Personality

huwa mna difficulties ikija relationship na wanawake……

..sitashangaa nyie watu mkiwa bado singles au mahusiano yenu yana walakini..lol...

kupiga kelele wanawake wasome na wafanye kazi sio u feminist..

These are demands put by our environment...

simply mtu mmoja hawezi kuprovide kila kitu

inabidi tusaidiane,

sasa kusaidiana huko kusiishie kwenye bills peke yake

na majukumu ya nyumbani pia...

nyie mliolelewa kwenye familia mnazodai hazikua za kifeminist..

mtapata tabu sana.

simply wanawake 'mliojijengea' picha vichwani mwenu..hawa exist in this modern world...

mnawatafuta 'mama' zenu katika relationship zenu..??

hamjui zama zimechange??

No wonder mnakuja na topics wanawake wamepokwa na jamii...

Wanawake wapo,ila mnasearch in the wrong fields...

Due to changes in the environment, our ancestors had to move from one place to the other...

Demands put by our environment,means both of us need to work..

ni hivyooo
Hao unaosema hawa exist wapo sana tu, God fearing women waliotunza asili yao. Nami nikuambie tu I have a happy marriage contrary to what you wish. Mtoto katika miaka yake ya awali atahusiana na mama zaidi kwa sababu ana muda naye mwingi hata baada ya kumwachisha ziwa. Kijana wa kiume akikua huambatana na baba yake zaidi lakini pia atakuwa na muda na mama yake, ndivyo ilivyo kwa mtoto wa kike kwa mama.

Social skills zinakuwa imparted hivyo, kila mzazi ana nafasi yake kwa wakati wake. Sisi tuliolelewa kwenye maisha hayo unayoyakashifu tuna amani sana kuliko hiki kizazi cha nyoka, kinachokidai kuzibuka lakini wanaishia kunasa kwenye tundu bovu.

Na kama unaamini mwanamume ndiye mwenye kuumia kwenye huu upuuzi, basi kweli haimo ndani yako. Hayuko mwanamume aliyekwenda kutafuta dawa ya kupata mke, ama kwenye nyumba za ibada, ama kwa waganga. Waganga wa jadi wamezidi kuwa wengi kwa sababu ya wanawake kuhitaji huduma, hawana amani tena. Bisha na hili
 
Kuhusu uhusiano wa mwanamke na mwanaume katika ndoa; mwanaume anajukumu la KUMPENDA mke wake, naye mke analojukumu la KUMTII mume wake (Wakolosai 3:18-25, Waefeso 5:22-23).

Lakini pia, mwanamke ni msaidizi wa mwanaume (Mwanzo 2:18). Kumbe huo ndio mpango wa Mungu tangu mwanzo alipowaumba mwanaume na mwanamke.

Ndio maana hata Historia inatufundisha kuwa; tangu mwanzo wa jamii zetu zilizokuwa primitive, bado kulikuwa na mgawanyo wa majukumu.

Kazi ya mwanaume ilikuwa ni kutafuta kipato kwa kuchimba mizizi, kuvuna matunda, na baadae kuwinda na kulima huku mwanamke alikaa na watoto nyumbani kuwalea na kutunza familia.

Mungu hajaweka usawa kati ya mwanaume na mwanamke. Ndio maana mwanaume analinganishwa na kichwa na mwanamke analinganishwa na mwili. Utofauti huu unatufanya tuhitajiane.

Kichwa hakiwezi kufanya kitu bila mwili, wala mwili bila kichwa. Utofauti huu ndio unatufanya tukamilishane. Wala usichukuliwe kama utumwa.

Kama kila mtu atasimama na kuitambua nafasi yake kwenye jamii hamna wazo wala fikra za utumwa kwenye ndoa hilijambo lazima watu walione.
 
Ujinga huo aliouandika
Nadhani wewe ndio hujamuelewa mleta mada, pengine kamsome tena
Dunia imebadilika, kila mtu ana haki ya kupata fursa ya elimu na kufanya kazi yoyote kama anaweza kuifanya
Kama hupendi pole, ndio mambo yalivyo na yataendelea kuwa hivyo, haturudi karne ya 19 tena
Dada Nadhani ume interpret hii topic kwa jinsi unavyotaka wewe na sio kwa jinsi muandishi alivyo iwasilisha.

Hakuna mahali panaposema kwamba mwanamke hatakiwi kupata fursa ya elimu wala kufanya kazi kwani hizo ni haki za msingi ya kila mtu, na kujaribu kwa namna yoyote kuzuia mwanamke asipate haki hizi ni kosa la uvunjanji wa haki za binadamu.

Unachopaswa kuelewa hapa ni kwamba kinachopigiwa kelele ni namna elimu inavyotumika ambavyo ni kinyume na makusudio yake. Elimu anayopewa mwanamke leo hii imekuwa twisted kiasi kwamba ina mpotosha zaidi kuliko kumjenga.

Imagine kuna mwenzako hapa anasema eti amesoma hili asiwe mtumwa na utumwa wenyewe ni kuwa tegemezi. Sasa huyo kweli kaelimika au kapotoshwa?

Kwamba ukiwa tegemezi basi wewe ni mtumwa, hivi hii ndio maana sahihi ya utumwa kweli?

Hii elimu inayoitwa "ukombozi wa mwanamke" ina dosari kubwa mno na imewameza wengi. Kwanza inamuaminisha akishakuwa na uhuru wa kiuchumi basi mwanaume kwake ni kitu cha ziada tu na hivyo anaweza akaishi kama mwanaume na yeye.

Tunafahamu kuwa na maarifa ni kitu kizuri, lakini maarifa hayo yasiwe nyenzo ya mashindano yasiyokuwa na tija. Na kwa bahati mbaya sana wengi wameangukia kwenye hili kundi.

Dunia imebadilika ndio lakini mabadiliko hayo faida zake ziko outweighed na hasara na kwenu nyie walengwa sio rahisi kuliona hili sana sana mtaona mko mahali pazuri.
 
Wanawake ndio wana feel nock on effect. Wanazalishwa na kuachwa. Wanatumika na kuchoshww kisha siku zao zikipita wanaandamana kwenda kwa RC. Wananung'unika siku hizi wanaume hawaoi, wanawachomachoma tu na kuwaacha.

Godly women will always be the happiest on planet earth!!
Mbona unataja wanawake wenye shida tu ?
Hamna wanaume wenye shida?

Na hamna wanawake wanaofurahia maisha simply bcz wamejiendeleza kwa namna flani?.

Naona una bias flani hivii
Mwanaume kutokuoa sio hoja he also remains single like the woman..
Na siku akioa ataoa mwanamke na si mwanaume mwenzake..ts even..ndoa ya wawili jmn..y u feel women always loose and men always win?..reality haiko hivo

If Godly women were only the happiest wasingekimbilia upepo wa kisulisuli vile😅
 
Dada Nadhani ume interpret hii topic kwa jinsi unavyotaka wewe na sio kwa jinsi muandishi alivyo iwasilisha.

Hakuna mahali panaposema kwamba mwanamke hatakiwi kupata fursa ya elimu wala kufanya kazi kwani hizo ni haki za msingi ya kila mtu, na kujaribu kwa namna yoyote kuzuia mwanamke asipate haki hizi ni kosa la uvunjanji wa haki za binadamu.

Unachopaswa kuelewa hapa ni kwamba kinachopigiwa kelele ni namna elimu inavyotumika ambavyo ni kinyume na makusudio yake. Elimu anayopewa mwanamke leo hii imekuwa twisted kiasi kwamba ina mpotosha zaidi kuliko kumjenga.

Imagine kuna mwenzako hapa anasema eti amesoma hili asiwe mtumwa na utumwa wenyewe ni kuwa tegemezi. Sasa huyo kweli kaelimika au kapotoshwa?

Kwamba ukiwa tegemezi basi wewe ni mtumwa, hivi hii ndio maana sahihi ya utumwa kweli?

Hii elimu inayoitwa "ukombozi wa mwanamke" ina dosari kubwa mno na imewameza wengi. Kwanza inamuaminisha akishakuwa na uhuru wa kiuchumi basi mwanaume kwake ni kitu cha ziada tu na hivyo anaweza akaishi kama mwanaume na yeye.

Tunafahamu kuwa na maarifa ni kitu kizuri, lakini maarifa hayo yasiwe nyenzo ya mashindano yasiyokuwa na tija. Na kwa bahati mbaya sana wengi wameangukia kwenye hili kundi.

Dunia imebadilika ndio lakini mabadiliko hayo faida zake ziko outweighed na hasara na kwenu nyie walengwa sio rahisi kuliona hili sana sana mtaona mko mahali pazuri.
Its twisted simply because men twisted it first

It used to be kisa mwanaume ana elimu na pesa mwanamke utaisoma namba..utanyanyasika mana jamaa anakupangia anavotaka yeye smtimes bila kujali how you feel...japo sio wote ila baadhi
Ss sikuhz women have that pia naona ndo mana wanaume mnateseka...

Afterall si wanawake wote wanatumia elimu zao vibaya..jifunzeni kuchagua tu vizuri
 
Hili linapaswa kuwa mjadala wa kitaifa na hizi taasisi za kimataifa zinazotetea huwa zinafanya hivi kwa maslahi ya nani?

Amini usiamini ni kwa maslai yao,kwani wanajua misingi yote ipo ndani ya familia na kama wakifanikiwa kuharibu huo msingi maadili hayatakuepo na watao athirika hapa ni watoto.
 
kiazi mbatata wee ....navyompenda Mama yangu, na ninvyosimaam kwa ajili ya mama yangu..

Niwe nmekosa nn?? Hihihi kaone ,kapanya weee
Amekugusa sehemu husika?mbona umecatch feelings ss?.

Tujaribu kuja na walau hoja na si maneno ya kejeli/matusi
 
Its twisted simply because men twisted it first

It used to be kisa mwanaume ana elimu na pesa mwanamke utaisoma namba..utanyanyasika mana jamaa anakupangia anavotaka yeye smtimes bila kujali how you feel...japo sio wote ila baadhi
Ss sikuhz women have that pia naona ndo mana wanaume mnateseka...

Afterall si wanawake wote wanatumia elimu zao vibaya..jifunzeni kuchagua tu vizuri
Hakika sio wote na ndio maana mada imeletwa mezani ili tujifunze na kukumbushana masuala haya muhimu kabisa kwani kupotoka huku ndio kunakopelekea kuzalishwa kwa taifa dhaifu lisilo na dira.
Huwa nasikitika sana kwa aina fulana ya malezi hasa yatolewa na baadhi ya akina Mama wanao ona wamejitosheleza(wenyewe wanadai hawataki kutawaliwa)na kulea mtoto kwa aina fulana ya taratibu za Hollywood basi mtoto hakanywi wala kuhojiwa kwa lolote yeye junior atafanya atakalo hata kama ni upuuzi.
Sasa hoja kama hizi zisipopenyezwa na jamii kutambua athari zake kwa kizazi cha kesho basi lazima tuamini na kufahamu kuwa kama taifa tutashindwa pakubwa
 
Dada Nadhani ume interpret hii topic kwa jinsi unavyotaka wewe na sio kwa jinsi muandishi alivyo iwasilisha.

Hakuna mahali panaposema kwamba mwanamke hatakiwi kupata fursa ya elimu wala kufanya kazi kwani hizo ni haki za msingi ya kila mtu, na kujaribu kwa namna yoyote kuzuia mwanamke asipate haki hizi ni kosa la uvunjanji wa haki za binadamu.

Unachopaswa kuelewa hapa ni kwamba kinachopigiwa kelele ni namna elimu inavyotumika ambavyo ni kinyume na makusudio yake. Elimu anayopewa mwanamke leo hii imekuwa twisted kiasi kwamba ina mpotosha zaidi kuliko kumjenga.

Imagine kuna mwenzako hapa anasema eti amesoma hili asiwe mtumwa na utumwa wenyewe ni kuwa tegemezi. Sasa huyo kweli kaelimika au kapotoshwa?

Kwamba ukiwa tegemezi basi wewe ni mtumwa, hivi hii ndio maana sahihi ya utumwa kweli?

Hii elimu inayoitwa "ukombozi wa mwanamke" ina dosari kubwa mno na imewameza wengi. Kwanza inamuaminisha akishakuwa na uhuru wa kiuchumi basi mwanaume kwake ni kitu cha ziada tu na hivyo anaweza akaishi kama mwanaume na yeye.

Tunafahamu kuwa na maarifa ni kitu kizuri, lakini maarifa hayo yasiwe nyenzo ya mashindano yasiyokuwa na tija. Na kwa bahati mbaya sana wengi wameangukia kwenye hili kundi.

Dunia imebadilika ndio lakini mabadiliko hayo faida zake ziko outweighed na hasara na kwenu nyie walengwa sio rahisi kuliona hili sana sana mtaona mko mahali pazuri.
Haha mbona mnaumia sana mwanamke kumuona mwanaume kama kitu cha ziada?.

Hio ndo mentality ya baadhi ya wanaume..imeanzia upande wa kiumeni...
Mwanaume anaona mwanamke ni chombo cha starehe, asiestahili kupiga hatua ktk yale anayopenda maishani na vitu vingine km hivyo ambavyo si vizuri kwa binadamu yoyote
 
topic za Lizarazu , Nyenyere , Carlos The Jackal , Jokajeusi wote hawa hawajui upendo wa mama..mnajihangaisha bure..lol. ……………..
Naona unanijua sana mimi na familia yangu wewe dada.

Ila nikwambie tu mama yangu sio mwanamke wa cancerous generation of women ambao na wewe ni mmoja wao.

Mama yangu ni mwanamke anayefahamu nafasi yake kifamilia na kijamii kwa ujumla na wala hapana shaka juu ya hilo.

Mama yangu sio mwanamke anaendekeza mashindano yasiokuwa na tija ambayo hayana mwisho mzuri.

Mama yangu sio mwanamke aliyepumbazwa na tamaduni mpyaa zinazohalalisha kila aina ya upuuzi.

Mama yangu sio muhamasishaji na mbishi anayetete mambo ya kijinga kijinga kisa tu yanafanywa na watu wa jinsia yake.

Mama yangu sio mjinga wa kuona single motherhood ni kitu cha kawaida mpaka kufikia hatua ya kuhamasisha kabisa.

Mama yangu ni mtu mwenye upendo wa dhati kwanzia kwa familia yake mpaka kwa wanajamii wanaomzunguka.

Mama yangu ni mwanamke bora kabisa aliyezaliwa kwenye kizazi bora cha wanawake na hichi ambacho kinaonekana kilichopotea.
 
Inapendeza kama hata wewe unafahamu fika kwamba huu mfumo tunaoambiwa kwamba umeletwa kwa ajili ya kuwasaidieni nyie wanawake kwa namna jinsi unavyo kuwa practiced unaleta athari nyingi kuliko faida kwa walengwa.

Athari zake zinaweza zisionekane kwa urahisi sasa hivi lakini tukaziona hapa baadae au hata kwenye matukio mbali mbali mfano kama kwenye ajali kama ulivyo ona kwenye comment yangu iliyopita.

Sasa nije kwenye hiyo kauli ya baba yako aliyokwambia juzi.


Juzi juzi baba yangu amenitamkia kuwa alinisomesha nisiwe mtumwa. Naamini wengi wanaonekana hivi wakiwa nyumbani wanalea. Hebu niambie ni nani anayependa utumwa.

Kwa kuangalia tu hii kauli baba yako Nathubutu kusema yeye ni aina ya wazazi ambao wameshiriki kikamilifu kuharibu kizazi cha wanawake wa sasa.

Baba yako anaamini mwanamke asiyesoma ni lazima atakuwa ni tegemezi tu kwa mwanaume na huo utegemezi yeye anauona ni utumwa, sasa hili asiingie kwenye huo utumwa basi lazima asome sana...INASIKITISHA SANA KWA KWELI.

Naamini kabisa tangu udogoni kwako amekuwa akikujengea hii mindset kwamba kusoma=kuepuka manyanyaso ya mwanaume na mpaka sasa hivi umekuwa nayo na hujawahi kuona tatizo kwenye hilo.

Mbali na huu mfumo tulionao wazazi pia wamechangia sana kuwaharibu wanawake hasa nyie wasomi kwa namna jinsi walivyowalea.

Mzazi anampa binti yake elimu hili aje aitumie kama mbadala wa kuishi bila mwanaume. Yaani elimu inakuwa ni replacement ya mwanaume maishani mwake.. Very pathetic mindset.

Umewahi kujiuliza ni kwanini wanawake wengi wasomi ndoa zinawashinda? Sababu moja wapo kubwa ni kuwa na hii mindset waliojazwa na wazazi wa aina ya baba yako.

Wanawake wengi wasomi wawapo ndoani wakikutana na changamoto hawaitumii elimu yao kama nyenzo ya kutatua changamoto hizo na badala yake elimu hiyo wanaifanya plan B(mbadala wa mume baada ya kuachika) pale mambo yasivyoenda jinsi wanavyotaka wao.

wanawake hao wasomi ni rahisi sana kusema maneno kama "tuachane" "usinibabaishe" "ninaweza kuishi bila wewe" hata pale changamoto ndogo tu inapojitokeza. Yote hii ni kwa sababu tu wanaweza kujitegemea kupitia elimu zao na wameshaukimbia ule utegemezi(utumwa) na hii tafsiri ya neno utumwa kwao inaenda mpaka kwenye utii.

Elimu zao zinawaondolea ile haiba na nafasi ya mwanamke kwa mwanaume na kujikuta anakuwa mshindani badala ya msaidizi ndio maana ni ngumu sana kwao kuwa na ndoa thabiti, sululisho pekee la kukabiliana na changamoto za ndoa huwa wanaona ni kuvunja ndoa.

Nadhani umewahi kuona comments zangu humu nikisistiza kuwa mwanamke msomi hafai kuwa mke. Ninasema vile kwa kumaanisha wala sio maigizo.

Na ni kweli hamfai kuwa wake.

Angalia mfano kama wewe hapo tayari sasa hivi unaona eti mwanamke anayefanya kazi ya kulea tu watoto nyumbani huyo ni mtumwa!!! How?

Kwa maana nyingine unaniambia kwamba mwanamke anayechakalika sawa na mwanaume huyo ndio kajikomboa toka utumwani kitu ambacho si sahihi kabisa.

MWENYEZI MUNGU hakuwa mjinga kumfanya mwanamke kuwa tegemezi wa mwanaume na kumuepusha na shuruba zote za kazi kama ambavyo wazazi wa siku wanavyowaaminisha nyie mabinti.

Haya sasa hivi mmetoka kwenye huo utumwa mmeingia kwenye kushindana na wanaume Nadhani athari zake wewe mwenyewe unaziona.

Kushindana kwenu na wanaume kumepelekea wengi wenu kuishi bila wenza na mnajikuta mna majukumu mengi sana ya kuyakabili kuliko hata wale mnaowaona wako utumwani(tegemezi).

Na majukumu hayo mazito mliyojipachika yanawaleteeni athari za kiakili kwanzia nyie mpaka kwenye familia zenu.

Kuna observation moja ilifanyika nchini UK watoto waliolelewa na single parents na wale waliolelewa na wazazi wote wawili walikuwa wanaulizwa kama wanatamani kuishi maisha wanayoishi wazazi wao pale watakapokuwa watu wazima.

Karibia watoto wote wanaolelewa na single parents walisema hawatamani kabisa kuishi maisha ya wazazi wao, kwa sababu wazazi wao(single parents) wana struggle sana namna ya kubalance familia na careers zao, na hivyo watoto hao kujikuta muda mwingi wanauokosa ule ukaribu wa mzazi.

Na hii ni ukweli mtupu single mothers wengi(ambao hawako tena utumwani) hawana muda wa kukaa na familia sababu ya kukimbizana na majukumu.

Haya yote yameletwa na huu mfumo unaoshabikiwa na wengi ambao umefanya wengi kuwa na mentality kama hii aliyonayo baba yako ya kuamini utegemezi ni utumwa.
Kiuhalisia utegemezi siyo utumwa, lakini wanaume wengi ndiyo wamefanya wanawake waamini hivyo.

Kwa sababu kuna wanaume wanaona kama kuwahudumia wake zao ni kuwafanyia favour, kwahiyo wana haki ya kuwapiga na kuwanyanyasa wake zao vyovyote wanavyojisikia kwa sababu wanajua kuwa wanawategemea na hawana pa kuenda.

Hata tukiangalia mada nyingi humu za kuhusu uchumba na ndoa utasikia wanaume wengi wakisema "mimi mwanamke niliyemtolea mahari hawezi kunibabaisha", unaweza kuona ni jinsi gani kuna wanaume wanaona kama kutoa mahari ni kuwafanyia favour wanawake na ndiyo maana wanaona kama wana haki miliki za kuwapiga au kuwanyanyasa wake zao wanavyojisikia.

Kwahiyo mimi nadhani wanaume waache kuwa na mitazamo ya ajabu kwamba eti "kufanya kitu fulani ni kumfanyia mwanamke favour hivyo naweza kumfanya chochote ninachojisikia" hii ndiyo inafanya wanawake waone kama kuwa wategemezi kwa wanaume ni utumwa.
 
Hujasema kweli. Muda wa kazi unaisha saa tisa, je kazi hiyo unaifanyia nyumba ya pili? Je, watoto wote wanarudi saa 9 nyumbani? Je, majukumu ya kazi yatakuacha siku zote utoke saa tisa, usisafiri kikazi n.k?

Kwa hiyo unapinga mtoto kuwa karibu na mama zaidi? Unapinga hili?
Exceptions are okay..ndio maisha
Muhimu wazazi kutengeneza muda zaidi kuwa karibu na kuweka mazingira salama ya mtoto na kumfuatilia kadri utakavyoweza anapokua

miezi 4 ya mwanzo u can stay full time na mtoto kwa waajiriwa...kwa wafanyabiashara hata mwaka..
Then unaenda kazini masaa machache for 6 months zinazofuata by miezi 10 hadi mwaka mtoto kafika mbali sana
Mda unakua nao mzuri tu kumfuatilia
Mama ajipange namna ya kuwaattend watoto
They grow and they grow fast..

U cant be around your child 24/7 no matter how much you love them..but you can create comfort and security hata kama haupo

Ukifa mtoto hatoishi kwani?..
 
Mbona unataja wanawake wenye shida tu ?
Hamna wanaume wenye shida?

Nataja walio wengi, exception cases zipo ila majority.

Na hamna wanawake wanaofurahia maisha simply bcz wamejiendeleza kwa namna flani?.

Nimepata kuzungumz na wanawake wengi waliohesabika kufanikiwa, wote walonyesha kuumizwa na kutokuwa na ndoà. Mfano mwingine ni Sophia Simba aliwahi kuhojiwa live kwenye TV na alikiri hayo. Wanawake waliojiendeleza na wakawa na ndoa imara wana furaha kuliko waliojiendeleza na kubaki kudanga mitaani. Kuna tofauti kati ya mwanamke mwenye ndoa na asiye na ndoa, hata heshima yao ni tofauti, huo ndio ukweli.

Naona una bias flani hivii
Mwanaume kutokuoa sio hoja he also remains single like the woman..
Na siku akioa ataoa mwanamke na si mwanaume mwenzake..ts even..ndoa ya wawili jmn..y u feel women always loose and men always win?..reality haiko hivo

Sina bias, nayatazama maisha katika uhalisia. Mwanamume akiamua kuoa anaoa, mwanamke akiamua kuolewa anasuniri ampate mwanamume, the difference is clear. Wote wakishatumikia anasa wakaamua kuingia kwenye ndoa, mwanamke atategemea bahati wakati mwanamume atachagua amtakaye. Nimekosea wapi hapo?
If Godly women were only the happiest wasingekimbilia upepo wa kisulisuli vile

Kukimbilia upepo w kisulisuli sio kipimo cha godly women. Mwanamke mcha Mungu hawezi kuwemo kwenye kundi lile la wanawake walio desperate. Huyu hufichwa katika Bwana na mwanamume amwonaye ni yule aliye sahihi tu, that is the Bible. Uliowaona hapo ni wale waliokwenda kanisani kutafuta muujiza wa ndoa.
 
Naona unanijua sana mimi na familia yangu wewe dada.

Ila nikwambie tu mama yangu sio mwanamke wa cancerous generation of women ambao na wewe ni mmoja wao.

Mama yangu ni mwanamke anayefahamu nafasi yake kifamilia na kijamii kwa ujumla na wala hapana shaka juu ya hilo.

Mama yangu sio mwanamke anaendekeza mashindano yasiokuwa na tija ambayo hayana mwisho mzuri.

Mama yangu sio mwanamke aliyepumbazwa na tamaduni mpyaa zinazohalalisha kila aina ya upuuzi.

Mama yangu sio muhamasishaji na mbishi anayetete mambo ya kijinga kijinga kisa tu yanafanywa na watu wa jinsia yake.

Mama yangu sio mjinga wa kuona single motherhood ni kitu cha kawaida mpaka kufikia hatua ya kuhamasisha kabisa.

Mama yangu ni mtu mwenye upendo wa dhati kwanzia kwa familia yake mpaka kwa wanajamii wanaomzunguka.

Mama yangu ni mwanamke bora kabisa aliyezaliwa kwenye kizazi bora cha wanawake na hichi ambacho kinaonekana kilichopotea.
Hongera kwa mama ni mfano wa kuigwa
Ila umepanic
 
Back
Top Bottom