Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Hawa watumishi wenyewe ni perpetrators wa huu mfumo haribifu na una maslahi sana kwao sio wa kuwaamini kabisa.

Yaani hawa sijui wanasaiokolojia,wachungaji, wahamasishaji, wasululishi wa migogoro ya ndoa ni washirika wazuri sana wanao prolog huu unaoitwa ukombozi wa mwanamke.

Na tusigemee kabisa kama watasaidia hata kupunguza athari zitokanazo na huu mfumo maana unafaida kwao.

Uwepo wa matatizo yetu ya kijamii hususani ya mahusiano ndio uhai wa maslahi yao, siku matatizo hayo yakiisha hata maslahi yao pia yatakuwa hatarini.

Kama umewahi kuwafuatilia hawa akina Chris mauki,Eddy makenge na wengineo mara nyingi huwa wanaongea vitu ambavyo wanawake wanapenda kuviskia. Mara nyingi wanaongelea sana makosa ya wanaume na kufunika funika makosa ya wanawake na hata ushauri wanaoutoa ni ushauri unaoharibu zaidi kuliko kujenga sema wanajitahidi kucheza na saikolojia ya wanawake.

Na wanafanya vile makusudi kabisa ila wanachoangalia wao ni account zao kuongezeka unene.
Ni sawa kabisa mkuu, mimi nawaona kama wenye kutumia udhaifu wa fikra za wanawake ili kuwateka na kujipatia faida. Lakini Neno la Mungu litasimama na kweli yake itajidhihirisha
 
Gombeni sana na kulalama sana ila mkumbuke mfumo usio wa haki unaoitwa mfumo dume ndiyo uliomfanya mwanamke kutafuta jinsi ya kujikomboa. Mfumo mpya mnaoulilia kuwa ni mbaya siyo mpya bali ni ule ule sema sasa una jinsi zote mbili na mkuki kwa nguruwe unakuwa mchungu. Huyu Mungu tunayemtaja hapa kuwa alimweka mwanaume kuwa mtawala na mwanamke mtawaliwa (if at all maana nakumbuka aliwatuma kutawala/kutiisha nchi) hakusema kumtawala mwanamke ni kumnyanyasa na kumdharau. Angetaka iwe hivyo angeumba mwanamke ambaye hana akili wala vipawa na angeweza kabisa kulea watoto wake kama wafanyavyo hayawani. Lakini kitendo cha kuwapa wote ufahamu na jukumu la kutiisha nchi alitaka hawa watu washirikiane kwa upendo kila mmoja katika nafasi yake na waheshimiane.

Kilichotokea ni mtawala kuwa mbinafsi na kutawala kidikteta - kusahau kuwa mwenzie ni binadamu kamili mwenye utashi na matamanio ya asili ya upendo na uhuru. Vipigo ni vya mwanamke, uduni ni wa mwanamke, kazi duni ni za mwanamke, matusi ya kudhalilisha ni ya kike. Yaani chochote cha mwanamke ni duni. Mwanaume akikosea anaambiwa anafanya mambo ya kike na akiambiwa hivi anaumia; mwanamke akifanya yampasayo mwanadamu kufanya anaambiwa anaigiza uanaume! Mwanaume ni mtu, mwanamke ni kiumbe. Kiumbe dhaifu. Mwanamke si kiumbe cha kufananishwa nacho. Ni fahari kufananishwa na simba au jogoo lakini si mwanamke.

Sasa mambo yamebadilika. Maendeleo ya Sayansi na uchumi yanasukuma mabadiliko katika mahusiano ya kijamii. Mfumo wa sasa hauruhusu mahusiano ya mtawala asiyejitambua na mtawaliwa asiyejitambua. Kujitambua ndo habari yenyewe - mtu mmoja mmoja mpaka taifa. Ukila na kipofu vizuri utakula muda mrefu na yeye ataridhika. Ukimdhulumu utampa fursa ya kujihoji na kuhoji kisha nafasi yako itatikiswa maana hukutumia maarifa bali kiburi cha kumiliki nyenzo za kutawalia (mali na elimu). Sasa huyu mnyonge baada ya kujitambua kuwa hastahili kutendewa vibaya anaanza harakati za kujikomboa. Naye anaanza kutaka kukaa alipo mtawala ili naye apate ahueni. Na ahueni anaipata kweli wala tusidanganyane kuwa mwanamke mwenye uhuru wa kimaarifa na kiuchumi ana tabu kama mwanamke ambaye hana hivi vitu na anajitambua lakini hana jinsi. Asiyejitambua hana shida. Jambo usilolijua halikusumbui. Ndiyo wife material naskia.

Sasa mwanamke akishapata nyenzo za uhuru hawezi kuenenda tofauti na mfumo kandamizi uliopo. Naye atakuwa mkandamizaji. Kwa hiyo mfumo dume na mfumo jike yote ni mifumo kandamizi. Watanyanyasika wanawake na wanaume wote ambao hawana nyenzo za uhuru. Kimsingi wanaume ni waathirika wakubwa zaidi kwani si rahisi kukaa kwenye nafasi ya "mtu duni" kwani anaathirika mara mbili: hana vyenzo za uhuru wala urahisi wa kupata mwenzi kwani nyenzo hizo ni vigezo vikuu. Mwanamke mwenye nyenzo za uhuru akikosa mwenzi anakuwa amekosa kitu moja, si vyote, na kama amevuka kiwango cha kushikiliwa kimaadili na jamii anaweza kutumia nyenzo zake kuwachezea wanaume walio kwenye nafasi duni. Uhuru si sawa na upweke. Sasa mwanaume ukose nyenzo za uhuru - upweke utakuhusu, manyanyaso yatakuhusu maana anayekuweka mjini ndiye anakuendeshea maisha. KILA MWANAMKE NA KILA MWANAUME ATAFUTE SANA KUJITEGEMEA KIAKILI NA KIUCHUMI.

Mwisho, mfumo sahihi wa kijamii ni mfumo wa haki (just). Tunaposema haki sawa kwa wote tunamaanisha binadamu wote ni sawa bila kujali ulemavu au jinsi ya mtu. Mfumo unaoheshimu utu wa mtu kwanza kabla ya kuja kwenye uanamke, ulemavu, utoto au uzee ndiyo mfumo bora. Mwanamke angechukuliwa kama mtu kwanza halafu mwanamke baadae tusingefika hapa. Pia tusichanganye mabadiliko ya kiuchumi na mabadiliko ya nafasi ya mwanamke. Mwanamke miaka mingi huko nyuma na mpaka sasa ni mzalishaji mkuu. Wa wakati ule alikuwa akizalisha karibu na nyumbani na anakwenda shamba na mtoto anamchimbia shimo anamuweka au anamuweka mgongoni. Lakini sasa shughuli za kiuchumi zimepanuka na makazi yamekuwapo ya vijiji na miji. Si jambo geni kwa mwanamke kuacha mtoto nyumbani na kwenda kutafuta. Mimi nina miongo minne sasa na niliachwa sana kwa mama mkubwa mpaka mama atakaporudi toka shambani au sokoni na alipokwenda kujiendeleza kielimu niliachwa kwa babu na bibi. Mama yangu mwenyewe mwenye miongo 7 alianza shule akiwa na miaka 10 kwa kuwa alikuwa akimlea mdogo wake wakati mama yake akizalisha mali. Tusichanganye mada. Kazi ndiyo utu. Tujipange upya zama zimebadilika.
Such a bloody third wave feminist.

Kwa jinsi ulivyoandika hili bandiko lako unaonekana kabisa wewe ni miongoni mwa Supremacy fighters!

Na nnamini kabisa wewe utakuwa hauna ndoa wala mahusiano yenye afya. Sababu you are too competitive unnecessarily.

Hata huo uhuru wako wa kiuchumi unautafuta kwa ajili ya kushindana na mwanaume, hili ufanye vitu vilivyozoeleka kufanywa na wanaume na upewe heshima anayopewa mwanaume na sio vinginevyo.

Na uthibitisho wa wewe kutaka kukaa kwenye nafasi ya mwanaume ni hapo unaposema "ukiwa na nyenzo za uhuru unaweza ukawachezea wanaume utajavyo na maisha yako yote unaamini mwanaume amekuwa juu ya mwanamke kwa sababu ya umiliki wa mali/pesa wa si vinginevyo...unamchekesha.

Halafu shida yenu nyie 3rd wave feminists wala sio haki sawa, bali nyie mnataka kuwa dominant(mfumo jike) na ndio maana mmejaa uanaume mwingi na imagination kibao.

Pia nikukumbushe Mungu kutuumba wote tukiwa na ufahamu sawa, haimaanishi kwamba tutakuwa sawa kwenye kila kitu, ufahamu tu peke yake hautoshi kumfanya mwanamke aweze kukaa kwenye nafasi ya mwanaume kama ambavyo fikra zako zinakwambia.

-Mungu alitupa ujasiri kuliko nyie
-Mungu alitupa uvumilivu kuliko nyie
-Mungu alitupa uwezo wa ku contol ubinafsi tofauti na nyie
-Mungu alitupa urahisi wa kuzi control hisia zetu na kuzeweka mbali pale tunapofanya maamuzi tofauti na nyie
-Mungu alitupa uimara wa kimwili kuliko nyie.

Hizo ni baadhi tu ya tofauti za mwanaume na mwanamke ambazo ni sababu kwanini mwanamke halingani/hayuko sawa na mwanaume.

Na pia kaa ukifahamu tu pamoja na huo uhuru wako wa kiuchumi lakini bado mwanaume ataendelea kuwa ndio mwenye privilege na wewe utaishi kwa kumtegemea sana maisha yako yote.
9740921_cfhj39quuaea52s_jpeg6ea917839e87a84d131c03848e4d2ff2.jpeg
 
Hapawezi kuwa na usawa kati ya mwanaume na mwanamke maisha yakaenda....
Wamama na wadada tunaweza kuwa na haki sawa ya kupata huduma za kijamii kama elimu, ajira, biashara, burudani etc lakini hatuwezi kuwa sawasawa na wanaume wala wanaume hawaezi kuwa sawa na wanawake kwani kila mmoja ana majukumu ambayo aliumbiwa

Kwenye imani zetu tumejifunza toka awali kabisa kwenye uumbaji mwanaume ni nani na mwanamke ni nani pamoja na majukumu yao. Pia desturi zetu hazikua mbali na imani zetu kuhusu hili.

Mambo yale ya Beijing tuyaache Beijing, sisi tuishi kwa asili yetu binadamu ilivyo na pia miongozo ya imani zetu

Maoni yangu binafsi
Andiko fupi lakini lenye ujumbe mzito kwa jamii. Mwenyezi Mungu akutie nguvu daima.
 
article yangu ipi? sijaandik article mimi, nime comment. Msingi wa kinachoongelewa nimekielewa, anasema mwanamke arudi kwenye majukumu yake ya ki traditional kama kupika na kulea watoto, na mwanaume ndio awe mtafuta kipato
Yap, nimesema hayo. Na kwakuongezea tu, elimu yamwanamke ilenge kumboresha kwenye kutekeleza majukumu yake ambayo umekiri ni ya kitraditional. Hakuna kilicho juu ya malezi ya watoto, kutokutekeleza hilo ni dhambi kubwa.
 
Ujinga huo aliouandika
Nadhani wewe ndio hujamuelewa mleta mada, pengine kamsome tena
Dunia imebadilika, kila mtu ana haki ya kupata fursa ya elimu na kufanya kazi yoyote kama anaweza kuifanya
Kama hupendi pole, ndio mambo yalivyo na yataendelea kuwa hivyo, haturudi karne ya 19 tena
Ngojani nikuoe ukweli wako, si kila mwanamke amefanywa kwa ajili ya kuwa MKE. Wengine kutokana na makuzi yao moja kwa moja wanafit kuwa vyombo vya starehe kwa jamii pana. Tunachoongelea hapa ni wanawake walioandaliwa kuwa wake wa ndoa, hawa imewapasa kuangalia mizania kati ya elimu na ndoa na wachunge mwenendo wao.

Kwa mtazamo wako sidhani kama article hii inakuhusu sana kwani hauenei kwenye misingi yake, wako waliosoma na wamepata mambo mema japo mawili ama matatu, hawa wamehusika moja kwa moja. Sasa waliofanyiwa mind programming sitegemei waichukulie article hii kama changamoto kwao.

Wenye Roho wa Mungu bado wataiona na kujitathmini, watachukua lililo jema nao watatoa michango ya kujenga. Bali wale waliotekwa na fikra potofu za kimagharibi watatumia hoja fhaifu kupinga kila kitu, ndio ukweli wenyewe
 
Umepoteana huelewi maudhui,by the way sina tabia ya kunuku kila kitokacho ulaya. Mmelishwa matango pori nasasa hamna furaha kama ilivyokuwa zamani. Kama unabisha angalia waliokimbilia upepo wa kisulisuli, ni aibu kwa janga mnalotengeneza wenyewe.

Habari ya ulayawaachie wenyewe, tujadili ya kwetu. Elimu haikupaswa kumwondoa mwanamke kwenye majukumu yake ya msingi, lakini kilichopo sasa ni nini? Naamini wazazi wako walikulea vema ingawa wewe hutaki kuwatendea hivyo wanao, ubataka walelewe na dunia. Ni upuuzi usiomithilika.

Kama unadhani mimi nanung'unika basi umepotea, mimi najaribu kushauri kuhusu maadili na sababu ya wanawake kujikuta wakiwa na wanyonge pale ujana wapo unapoondoka. Wanawake ni short sighted hata kama utabisha, wanasombwa hovyo na kila upepo unaokuja na ndio maana ni target kubwa ya kila jambo jipya, iwe fashion, urembo, mavazi, imani mpya n.k. Akili zao zinavutwa kila kinachoonekana ni kitamu machoni hata kama mwisho wake ni mchungu, hawana uwezowa kuchuja mambo. Ndivyo walivyoumbwa.

Starehe na kujidanganya hudumu kwa muda mfupi sana kwa mwanamke wa kizazi kipya, asiyeheshimu kuumbwakwake kama mwanamke, ambaye anadhani ushindani na walioumbwa wanaume ni jambo la kutukuzwa, lakini mwanamke anayeijua nafasi yakeana chance kubwa ya kuwana furaha idumuyo maisha yake yote. Mwanamke hakuumbwakushindana na mwanamume bali kumsaidia kufikia malengo ya maishawakiwa kama familia moja. Sasa wanawake waliojanjaruka kama wewe na kujiona ni wenye kupambana na wanaume hupigana na vivuli vyao wenyewe kwani watacheka mwanzoni, tena kwa muda mfupi sana, lakini mwisho wao huwa ni kilio na majuto makuu.

Elimu ilikusudiwa kumtoa mtu kwenye ujinga na kumpeleka kwenye hekima na busara, lakini badala yake imefanya kinyume chake. Wacha mtumike kwa starehe na kuwaburudisha walioharibika akili pia, lakini usisahau kuwawakati ukuta.

Amina.
Naona maneno mengi ila point kidogo
Wazazi wangu walinilea vizuri hilo ni kweli, walinipa elimu,wakanifundisha nidhamu na kujitegemea, na vimenisaidia sana, sbabu maisha yangu yapo secured. Nami wanangu nitawalea hivyo hivyo
Hao wanawake wanaochukuliwa na upepo sijui wa kisulisuli ndio hao waliolelewa kuwa wakikuwa kazi yao ni kuolewa na kuzaa na kutunza mume, sasa imetokea hawajaolewa, ndio maana wapo vile

Suala la mtu kuendekeza starehe na kuharibikiwa halina uhusiano na jinsia, maana wapo wanaume wengi waliofanya starehe wakaishia kutumia madawa ya kulevya, wengine wapo gerezani, wengine hata wamejiua kwa msongo wa mawazo, wengine wamefia baharini ama porini wakitaka kuzamia nchi za watu. So ni akina nani ambao hawaishi kwa busara ambao starehe inawapelekesha zaidi na kuwagaharimu maisha yao?
 
Gombeni sana na kulalama sana ila mkumbuke mfumo usio wa haki unaoitwa mfumo dume ndiyo uliomfanya mwanamke kutafuta jinsi ya kujikomboa. Mfumo mpya mnaoulilia kuwa ni mbaya siyo mpya bali ni ule ule sema sasa una jinsi zote mbili na mkuki kwa nguruwe unakuwa mchungu. Huyu Mungu tunayemtaja hapa kuwa alimweka mwanaume kuwa mtawala na mwanamke mtawaliwa (if at all maana nakumbuka aliwatuma kutawala/kutiisha nchi) hakusema kumtawala mwanamke ni kumnyanyasa na kumdharau. Angetaka iwe hivyo angeumba mwanamke ambaye hana akili wala vipawa na angeweza kabisa kulea watoto wake kama wafanyavyo hayawani. Lakini kitendo cha kuwapa wote ufahamu na jukumu la kutiisha nchi alitaka hawa watu washirikiane kwa upendo kila mmoja katika nafasi yake na waheshimiane.

Kilichotokea ni mtawala kuwa mbinafsi na kutawala kidikteta - kusahau kuwa mwenzie ni binadamu kamili mwenye utashi na matamanio ya asili ya upendo na uhuru. Vipigo ni vya mwanamke, uduni ni wa mwanamke, kazi duni ni za mwanamke, matusi ya kudhalilisha ni ya kike. Yaani chochote cha mwanamke ni duni. Mwanaume akikosea anaambiwa anafanya mambo ya kike na akiambiwa hivi anaumia; mwanamke akifanya yampasayo mwanadamu kufanya anaambiwa anaigiza uanaume! Mwanaume ni mtu, mwanamke ni kiumbe. Kiumbe dhaifu. Mwanamke si kiumbe cha kufananishwa nacho. Ni fahari kufananishwa na simba au jogoo lakini si mwanamke.

Sasa mambo yamebadilika. Maendeleo ya Sayansi na uchumi yanasukuma mabadiliko katika mahusiano ya kijamii. Mfumo wa sasa hauruhusu mahusiano ya mtawala asiyejitambua na mtawaliwa asiyejitambua. Kujitambua ndo habari yenyewe - mtu mmoja mmoja mpaka taifa. Ukila na kipofu vizuri utakula muda mrefu na yeye ataridhika. Ukimdhulumu utampa fursa ya kujihoji na kuhoji kisha nafasi yako itatikiswa maana hukutumia maarifa bali kiburi cha kumiliki nyenzo za kutawalia (mali na elimu). Sasa huyu mnyonge baada ya kujitambua kuwa hastahili kutendewa vibaya anaanza harakati za kujikomboa. Naye anaanza kutaka kukaa alipo mtawala ili naye apate ahueni. Na ahueni anaipata kweli wala tusidanganyane kuwa mwanamke mwenye uhuru wa kimaarifa na kiuchumi ana tabu kama mwanamke ambaye hana hivi vitu na anajitambua lakini hana jinsi. Asiyejitambua hana shida. Jambo usilolijua halikusumbui. Ndiyo wife material naskia.

Sasa mwanamke akishapata nyenzo za uhuru hawezi kuenenda tofauti na mfumo kandamizi uliopo. Naye atakuwa mkandamizaji. Kwa hiyo mfumo dume na mfumo jike yote ni mifumo kandamizi. Watanyanyasika wanawake na wanaume wote ambao hawana nyenzo za uhuru. Kimsingi wanaume ni waathirika wakubwa zaidi kwani si rahisi kukaa kwenye nafasi ya "mtu duni" kwani anaathirika mara mbili: hana vyenzo za uhuru wala urahisi wa kupata mwenzi kwani nyenzo hizo ni vigezo vikuu. Mwanamke mwenye nyenzo za uhuru akikosa mwenzi anakuwa amekosa kitu moja, si vyote, na kama amevuka kiwango cha kushikiliwa kimaadili na jamii anaweza kutumia nyenzo zake kuwachezea wanaume walio kwenye nafasi duni. Uhuru si sawa na upweke. Sasa mwanaume ukose nyenzo za uhuru - upweke utakuhusu, manyanyaso yatakuhusu maana anayekuweka mjini ndiye anakuendeshea maisha. KILA MWANAMKE NA KILA MWANAUME ATAFUTE SANA KUJITEGEMEA KIAKILI NA KIUCHUMI.

Mwisho, mfumo sahihi wa kijamii ni mfumo wa haki (just). Tunaposema haki sawa kwa wote tunamaanisha binadamu wote ni sawa bila kujali ulemavu au jinsi ya mtu. Mfumo unaoheshimu utu wa mtu kwanza kabla ya kuja kwenye uanamke, ulemavu, utoto au uzee ndiyo mfumo bora. Mwanamke angechukuliwa kama mtu kwanza halafu mwanamke baadae tusingefika hapa. Pia tusichanganye mabadiliko ya kiuchumi na mabadiliko ya nafasi ya mwanamke. Mwanamke miaka mingi huko nyuma na mpaka sasa ni mzalishaji mkuu. Wa wakati ule alikuwa akizalisha karibu na nyumbani na anakwenda shamba na mtoto anamchimbia shimo anamuweka au anamuweka mgongoni. Lakini sasa shughuli za kiuchumi zimepanuka na makazi yamekuwapo ya vijiji na miji. Si jambo geni kwa mwanamke kuacha mtoto nyumbani na kwenda kutafuta. Mimi nina miongo minne sasa na niliachwa sana kwa mama mkubwa mpaka mama atakaporudi toka shambani au sokoni na alipokwenda kujiendeleza kielimu niliachwa kwa babu na bibi. Mama yangu mwenyewe mwenye miongo 7 alianza shule akiwa na miaka 10 kwa kuwa alikuwa akimlea mdogo wake wakati mama yake akizalisha mali. Tusichanganye mada. Kazi ndiyo utu. Tujipange upya zama zimebadilika.
Shawtyyy 😘😘😘ur a 💯💯💯
 
Mkuu Nyenyere kuna mada Fulani ulipost hapo nyuma na kwa kweli nilitofautiana sana na mtizamo wako(na mpaka sasa natofautiana na wewe)

Lakini kwa mada hii ya leo nakuunga mkono asilimia mia moja na naomba niongezee hoja kadhaa hapa chini kuunga mkono mada yako

Mkuu kwa sababu ya mapinduzi yalifofanyika na yanayoendelea kufanyika kila siku,leo hii tunapata familia na vizazi vibovu kuwahi kutokea,kwa nini?

leo hii baba na mama wote ni wafanyakazi kuondoka aubuhi kurudi usiku,watoto wameshakula wamelala,anayeshinda na watoto ni dada wa kazi ambaye haijulikani anashindaje na kuwatendeaje watoto,mama anapoondoka anaacha tu maagizo dada utampa mtoto uji,utamwekea katuni,utahakikisha anafanya homework,mtoto ni wa dada wa kazi?dada wa kazi anajua thamani ya yule mtoto?akiharibika dada ana hasara yeyote?na akiwa mtu mzuri kioo cha jamii,ni kwa namna gani dada wa kazi anafaidika hivi kwamba atajitahidi kwa kadri awezavyo kumlea mtoto ipasavyo?

kwa mfano huo mdogo tu wale ambao wamewahi kuona madhara ya aina hi ya Maisha wataelewa nachokisema ila kwa wale ambao wanaamini njii hii ya Maisha ni sawa si ajabu huko mbeleni watu watakuja kuconfess humu (painful ad regret Confession)

Kiasili na kulingana na uumbaji mwanaume aliumbwa kutafuta kwa maana ya kwamba mke alipaswa akae nyumbani atunze watoto muda wote baba anapokuwa katika mihangaiko ya kutafutia riziki mke na watoto wake,ni aina hii yamaisha iliyofanya familia kadhaa za miaka kadhaa kuwa bora na kutokeza vijana wa kiume na mabinti wa kike wenye kutegemeka na kujiheshimu,mama walikuwa wakitumia muda wao mwingi kutunza watoto wao na kuwafundisha lilo sawa na lilo na kosa pia,haikuwa rahisi kwa binti au kijana kuharibika na mama shindwe kuona mbadiliko hayo na kutoa ripoti kwa baba ambaye angeshughulikia hali hiyo kabla mambo hayajaharibika kabisa

lakini leo poor us kuna uwezekano mtoto kashaharibika sana tu (labda kawa mvuta bangi,katoa mimba za kutosha,kawa shoga,kawa mlevi) na bado mama au baba hajui kuhusu yote hayo,watajua saa ngapi wakati wote wako kazini bize kutafuta pesa?nani atampa mwenzie ripoti kuhusiana na maendeleo ya mtoto? dada wa kazi? dada wa kazi wanawajua vizuri watoto wenu? inauma lakini kutokana na aina yetu ya Maisha ya siku hizi,inakuja kujulikana kuwa mtoto kafikia stage ya point of no return na hakuna kinachoweza kufanyika kumsaidia tena just kwa sababu mama na baba wote walikuwa bize kuzitafuta pesa,what for? Maisha bora,,,,Maisha bora yapi?kupoteza watoto wenu mkiwa mmebaki na pesa zenu nyingi??
Mkuu umenena kweli tupu, tatizo tumeikataa devine order. Dhambi ya uasi ilianzia Edeni ambapo mwanamke alisikiliza sauti ya nyoka na kumwasi Mungu, mwanamume naye akasikiliza sauti ya mwanamke na kumwasi Mungu. Leo hii mwanamke ameasi maagizo ya Mungu kwa kuisikiliza sauti ya nyoka, tena anamfanya mwanamume naye aasi kwa kuisikiliza sauti yake. Ni yale yale, dhambi ya uasi inaendelea na hii ndio sababu Paulo alisema wanawake wasiwe juu ya mwanamume.

Asante kwa bandiko lako murua
 
Yap, nimesema hayo. Na kwakuongezea tu, elimu yamwanamke ilenge kumboresha kwenye kutekeleza majukumu yake ambayo umekiri ni ya kitraditional. Hakuna kilicho juu ya malezi ya watoto, kutokutekeleza hilo ni dhambi kubwa.
Watoto wanalelewa na wazazi wote, mimi nimelewa na wazazi wote sawa tu, baba na mama wote wametumia muda mwingi na mimi. Malezi hakuachiwa mama tu, Wanangu hivyo hivyo, wapo na mama yao na baba yao kwa muda mwingi pia. Ni suala la kujipanga tu.
Mimi naamini familia itakuwa bora zaidi endapo wazazi wakitumia muda mwingi pamoja na pia wakiwa pamoja na watoto wao.
 
Naona maneno mengi ila point kidogo
Wazazi wangu walinilea vizuri hilo ni kweli, walinipa elimu,wakanifundisha nidhamu na kujitegemea, na vimenisaidia sana, sbabu maisha yangu yapo secured. Nami wanangu nitawalea hivyo hivyo
Hao wanawake wanaochukuliwa na upepo sijui wa kisulisuli ndio hao waliolelewa kuwa wakikuwa kazi yao ni kuolewa na kuzaa na kutunza mume, sasa imetokea hawajaolewa, ndio maana wapo vile

Suala la mtu kuendekeza starehe na kuharibikiwa halina uhusiano na jinsia, maana wapo wanaume wengi waliofanya starehe wakaishia kutumia madawa ya kulevya, wengine wapo gerezani, wengine hata wamejiua kwa msongo wa mawazo, wengine wamefia baharini ama porini wakitaka kuzamia nchi za watu. So ni akina nani ambao hawaishi kwa busara ambao starehe inawapelekesha zaidi na kuwagaharimu maisha yao?
Ok, walee hivyo wanao, kwako nimemaliza
 
😂😂😂😂ivi kweli mimi nitake kuwa sawa na mwanaume nianze kufanya kazi ngumu kama za ukuli labda bandarini, nianze kubeba gunia la mahindi begani wakati nimepewa mbavu 01 tuu kati ya mbavu 12
Wacha niendelee na majukumu yangu ya kuzaa kwa uchungu, kupamba nyumba na kupika🤗🤗🤗
 
Watoto wanalelewa na wazazi wote, mimi nimelewa na wazazi wote sawa tu, baba na mama wote wametumia muda mwingi na mimi. Malezi hakuachiwa mama tu, Wanangu hivyo hivyo, wapo na mama yao na baba yao kwa muda mwingi pia. Ni suala la kujipanga tu.
Mimi naamini familia itakuwa bora zaidi endapo wazazi wakitumia muda mwingi pamoja na pia wakiwa pamoja na watoto wao.
Si kweli, hiyo ni maneno ya mdomoni. Tunaposema mama awalee watoto haimaanishi baba si mlezi, tunaongelea mgawanyo wa majukumu na primary responsibility. Baba awapo na watoto hushughulika na masuala mazito wakati muda mwingi watoto huutumia na mama yao. Au hujui kuwa mtoto akitaka jambo kwa baba hupitia kwa mama? Unajua sababu ni ipi? Kama wote mtakuwa nje ya nyumba na mkarudi pamoja huku mna watoto ni saa ngapi mnawalea? Ni suala la kujipanga vipi? Unajua sababu ya mitaa kujaa mapanya road na wavut bangi leo hii? Unajua sababu y watoto kukosa maadili? Usiongee nadharia kuvuti hoja kwako, ongea uhalisia
 
😂😂😂😂ivi kweli mimi nitake kuwa sawa na mwanaume nianze kufanya kazi ngumu kama za ukuli labda bandarini, nianze kubeba gunia la mahindi begani wakati nimepewa mbavu 01 tuu kati ya mbavu 12
Wacha niendelee na majukumu yangu ya kuzaa kwa uchungu, kupamba nyumba na kupika🤗🤗🤗
Wanaume wote wanabeba mizigo kwani?.

Hamna softer works that u can also do uingize kipato?
 
Naona maneno mengi ila point kidogo
Wazazi wangu walinilea vizuri hilo ni kweli, walinipa elimu,wakanifundisha nidhamu na kujitegemea, na vimenisaidia sana, sbabu maisha yangu yapo secured. Nami wanangu nitawalea hivyo hivyo
Hao wanawake wanaochukuliwa na upepo sijui wa kisulisuli ndio hao waliolelewa kuwa wakikuwa kazi yao ni kuolewa na kuzaa na kutunza mume, sasa imetokea hawajaolewa, ndio maana wapo vile

Suala la mtu kuendekeza starehe na kuharibikiwa halina uhusiano na jinsia, maana wapo wanaume wengi waliofanya starehe wakaishia kutumia madawa ya kulevya, wengine wapo gerezani, wengine hata wamejiua kwa msongo wa mawazo, wengine wamefia baharini ama porini wakitaka kuzamia nchi za watu. So ni akina nani ambao hawaishi kwa busara ambao starehe inawapelekesha zaidi na kuwagaharimu maisha yao?
Na kama kweli wazazi wako wamekufundishwa kujitegemea, basi uko sahihi kwa mabandiko yako. Maada hii haina mashiko kwako kwwni ni kwa ajili ya wanaothamini ndoa. Kwenye ndoa hakuna kujitegemea, bali wote watakuwa mwili mmoja, hayo unayoleta ni nje ya ndoa hivyo nje ya mada.
 
Wanaume wote wanabeba mizigo kwani?.

Hamna softer works that u can also do uingize kipato?

Hiyo mizigo sio lazima iwe anafanya ili apate kuongeza kipato ni majukumu waliyopewa na aliyewaumba
Juzi nilikua nahamisha makabati makubwakubwa mbona wanawake4 tulishindwa hadi wakaja wanaume2 na kazi ikaenda fasta
Hapa ndio nasemaga hakuna usawa ila kuna haki sawa
 
Back
Top Bottom