Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Hell no, wanawake wanaamini hela ndio kila kitu kwenye maisha yao.

Mnaamini hela ni mbdala wa mwanaume na chochote kimuhusisho mwanaume.

Ni mara nyingi sana utawaskia wanawake wakisema "nina kazi yangu inaniingizia kipato kinachotosheleza mahitaji yangu yote, sasa mwanaume wa nini?"

Sasa ni mara ngapi ngapi umewahi kuskia mwanaume akiwa na hela anatamka maneno kama haya!? Kwamba akiwa na hela basi hata umuhimu wa mwanamke kwake unapungua?
Umeenda to the extreme

Na si wanawake wote wako hivyo

Ndo mana bado wanawake wana mahusiano na wanaume na wataendelea kuwa nayo
 
kabla hujabisha hii hoja jiulize kwanza kwanini wanawake wengi wenye vipato hawajaolewa au ni masingle mother
 
Mkuu huu Uzi wako una hoja lakin haya yachukulie kama mabadiliko ya dunia. Ulishafikiria miaka elfu kumi mbele dunia itakuaje yan miaka ya 7019 au 7020 huko. Keep calm enjoy the show
 
Najua mada kama hizi ni ngumu lakini lazima tuangalie ni wapi tulipojikwaa. Feminism ilipaswa kuboresha majukumu ya mwanamke, badala yake imefanya mwanamke awe kama mwanamume.
Ukiwauliza hivi huwa mnataka haki sawa au kufanana haki ? Kwao wanaona kufanana kwa haki ndio haki sawa. Wamesahau ya kuwa haki sawa huwa zinazingatia maumbile na hali za wahusika.

Naendelea kusoma maoni ya wadau ...
 
Na hiki kinachoendelea hapa ni stress za mfumo unaopingwa kama mfa maji kutapata.
Nashauri wanaume wajipange kuwaandaa vijana wa kiume maana sasa ulimwengu unampendelea mwanamke na kama ilivyo kwa wanaume sasa mambo yanaweza kubadilika.
Sasa,hivi ushawahi kujiuliza kwanini huu ulimwengu unampendelea Mwanamke kama unavyodai ?
 
Asante mkuu kwa kulitambua hilo.

Hawa wanaamini pesa na mali ndio kusudio la wanawake wengi kuolewa, kwa hiyo akiwa navyo hivyo basi hata mwanaume/kuolewa kwake sio suala muhimu tena.

Yaani iko hivi pesa/mali=mwanaume

Ukiwa navyo hivyo basi tayari una mwanaume ndani. Inafurahisha na inasikitisha.

Si umeona kuna mmoja kule mwanzo kasema ukishakuwa na uhuru wa kiuchumi tu(pesa) unaweza hata kumnunua mwanaume, haya ndio mawazo ya wanawake wa kileo kwamba tafuta pesa mambo mengine yatakuwa ni ya ziada tu.

Cha kushangaza pamoja na pesa zao lakini kuna mambo mbali mbali ya Kijamii kama malezi wamefeli vibaya mno.
Mkuu hakika hili ni janga la ki dunia, tunakoelekea sio kuzuri, hatusemi mwanamke asipatiwe elimu la hasha, ila shida inakuja pale elimu inapotumika kumfanya mwanamke ajione ameshafanikiwa ki maisha coz anao uwezo wa kupata anachokitaka hata km hana mume,
Lakini ifahamike kuwa bado mwanume atabaki kuwa kichwa, nukuu za maandiko ya vitabu vitakatifu ukiangalia kwa sehemu kubwa hata walipokuwa wakitoa hesabu za idadi ya watu (sensa) waliainisha kundi la wanaume fulani eidha walioenda vitani ama kufanya jambo fulani hii tu inatosha kudhihirisha kuwa mwanaume kuwa kichwa ni mpango toka kuumbwa kwa ulimwengu.
 
Hicho unachokisema ndio ukengeufu wenyewe. Jukumu la mwanamke ni kuzaa na kulea, hizo kazi mmepewa na wajanja na iko sababu ya kibiashara na kimapato ya serikali. Mwanamke anagawana majukumu na mune, mmoja nyumbani mwingine kazini. Ndio maana watoto wa siku hizi hawana malezi bora, kwa sababu mama anarudi saa nne usiku na baba pia. Wanawake mmejitwisha jukumu la wanaume, mkaacha jukumu lenu.

Kwamba wasio na kazi wana maisha mabaya si kweli, inategemea unatazasha vipi maisha. Wanawake wasio na waume nilioongea nao mimi hawana furaha wala amani hata kama wana kazi. Kazi sio kila kitu kwa mwwnamke ila dunia imejaribu kumwaminisha hivyo. Kwa mfumo sasa hakuna mwanamke tena, wote ni watafutaji tu. Mwanamke halisi atawazia malezi ya famikia bora kuliko kutafuta mali binafsi ndani ya ndoa.

Ukahaba kuwepo tangu kale ni kwa sababu wako wachache ambao hawakuzingatia maonyo. Na hiyo sio sababu ya kuendeleza ukahaba, misingi ya zama hizo haikushabikia ukahaba bali ilipinga kabisa, hivyo kauli yako ni mfu. Wanawake wengi wanaji expose kwenye system ya elimu, wanajikuta wameingia kwenye vitendo vya ukahaba kwani wanaanza kujitegemea wakiwa bdo hawako tayari.
What a Genius!!
 
Umeenda to the extreme

Na si wanawake wote wako hivyo

Ndo mana bado wanawake wana mahusiano na wanaume na wataendelea kuwa nayo
Mahusiano yapo ndiyo na ni kweli yataendelea kuwepo kwa sababu hakuna mbala wa hizi gender mbili. Kama kungekuwa na mbadala wa gender hizi mbili nina uhakika kuna watu wangeshajaribisha hiyo alternative kama inafaa zaidi ya me/ke. Uenda pia kiasi flani sitonfahamu kati ya ke na me inachangia kuongezeka kwa lesbianism hadi baadhi ya nchi na madhehebu ya dini wameshindwa kuhimili mishindo yao wakawaruhusu.
 
Mkuu umeongea mambo halisia yanaendelea kwenye baadhi ya familia zetu. Binafsi sometimes huwa na-regret kuoa mke msomi, maana sioni faida yake kiukweli masaa mengi yuko bize na mambo yake hana muda hata na watoto. Lakini pia mwisho wa siku faida ya kazi zake hizo kwa familia ni very negligible.

Yaani kwa uzembe wake kwa watoto ilifika pahala nikahamua kuwa narudi nyumbani mwenyewe mapema ili nikague school works na kuwasimamia watoto wafanye homeworks.

Nilifikia uhamuzi huu baada ya kumsihi afanye hivyo yeye bila mafanikio, wakati huo mimi navipenda kweli vitoto vyangu hivi vi3 na pia ninavilipia hela yangu nyingi ninayopata kwa shida ili visome!

Nikaona bora nijitoe tu muhanga nivisaidie maana kwa upande wangu kama ni kukosea/kupatia maisha kidogo kuna muelekeo ila kwa hawa watoto bado sana kulijua hilo hivyo inabidi kuwasaidia kadri iwezekanavyo hata kama ushirikiano wa bibie ni mdogo.
Pole sana hao itabidi tu ulee mwenyewe kushindwa majukumu kunapelekea ku oa wanawake wenye pesa ili watusaidie hayo ndo madhara yake jitahidi usimkorofishe mana atakuhama mpaka chumba
 
Pole sana hao itabidi tu ulee mwenyewe kushindwa majukumu kunapelekea ku oa wanawake wenye pesa ili watusaidie hayo ndo madhara yake jitahidi usimkorofishe mana atakuhama mpaka chumba
Sioni dalili za yeye kuhama mkuu. Nilishamwambia akijisikia kuondoka milango iko wazi mimi siyo mtu wa kuji-stress sana na hayo mambo. Lakini abanduki mkuu na mara nyingi tunatibuana lakini anakuwa mwepesi wa kushuka na kuomba samahani.

Labda malengo yake kwangu hayajatimia au anaogopa asije akawa muanga wa kisulisuli cha mama lwakatare maana ki- umri bado tunadai kidogo mimi na yeye. Yuko kwenye early 30s wakati mimi niko late 30s.
 
Back
Top Bottom