Siku ya Sheria nchini: Jaji Mkuu wa Tanzania asema sasa basi Mahakimu kuandika kwa mkono

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,177
7,750
IMG-20240201-WA0248.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2024.

Jaji Mkuu Profesa Ibrahim ameyasema hayo leo tarehe 1/2/2024 kwenye maadhimisho ya siku ya sheria yaliyo fanyika Jijini Dodoma.

Jaji Mkuu amesema kufuatia kwa teknolojia ya kisasa kufungwa kwenye mahakama zote itasaidia kuandika na kutafasiri kwenye lugha mbalimbali hivyo kazi za Mahimu na Majaji itakuwa ni ndogo tu nayo ni kutoa maamuzi.

Hatua hii ya matumizi ya tehama itasaidia kuharakisha usikilizwaji wa kesi na kutolewa kwa hukumu kwa wakati.

Pongezi kwa mahakama kwa kupiga hatua kubwa, sasa wananchi wanacho subiri ni utekelezaji.
 
Hongera sana Mahakama.....hatua hii kubwa...tupate haki kwa wakati...na pia mahakama iwe huru kweli
 
Nawaambia vijana elimu ni rahisa hata kazi zitakuwa rahisi...Binadamu kapewa akili aweze kutawala mazingira kwa namna yeyote binadamu ni mjanja ... Lazima atafanya kila mbinu kurahisisha maisha..

Kuna watu hawajakuta zile FAX zenye typing ya kusogeza kama unashona nguo hapo hapo...Masekretari yalikona mpaka vidole vinatoka sugu kama wapiga vinanda..
 
haki iko kwa Mungu tu Mahakamani ni ushetani wa kudhurumu haki za Watu unaoendelea huko
 
Back
Top Bottom