Jaji David Maraga asikitishwa na kauli ya Rais Samia

Jaji David Maraga asikitishwa na kauli ya Rais Samia

Parabolic

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2013
Posts
2,852
Reaction score
3,094
Jaji mkuu mstaafu wa Kenya, David Maraga ameandika katika ukurasa wake wa X akieleza masikitiko yake kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Mei 4 wakati akimpokea Rais wa Kenya, William Ruto jijini Dar es Salaam.
Endelea....

"Kama Jaji Mkuu, nilithamini udugu uliopo ndani ya Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki na nilifanya kazi kwa karibu na wenzangu katika mahakama ya Tanzania katika jitihada za pamoja za kutafuta haki na kulinda utawala wa sheria.

Kwa hiyo, nimeshtushwa sana na kauli zinazodaiwa kutolewa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu wakati wa hotuba ya Rais Ruto katika Bunge la Tanzania.

Inasikitisha kwamba marais hao wawili wanaripotiwa kujadili kuratibu juhudi za “kuchapa mikwajo” dhidi ya kizazi cha Gen Z nchini Kenya na Tanzania.

Kauli hizi zinachukiza.

Zinakuja takriban wiki moja tu baada ya Rais Suluhu kupokea ripoti ya Tume ya Uchunguzi kuhusu mauaji yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Tanzania wa tarehe 29 Oktoba 2025, ambapo zaidi ya watu 518 walipoteza maisha yao, wengi wao kutokana na majeraha ya risasi.

Hadi sasa, hakuna mtu hata mmoja aliyewajibishwa.

Pia hatupaswi kusahau kwamba mwenzetu Boniface Mwangi, pamoja na Agather Atuhaire wa Uganda, waliteswa wakiwa katika ardhi ya Tanzania. Wahusika bado wako huru.

Wananchi wa Afrika Mashariki wanapaswa kuzungumza. Muungano wa udikteta ambao Marais Suluhu na Ruto wanaunda unatishia kurudisha ukanda wetu kwenye utawala wa kiimla.

Kama nilivyoonesha kupitia uwepo wangu wa mshikamano jijini Dar es Salaam tarehe 19 Mei 2025, niliposimama pamoja na kiongozi wa upinzani Tundu Lissu, Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki haiwezi kupiga hatua wakati viongozi wanakandamiza upinzani na kukiuka haki za msingi za watu wetu.

#UkatibaMovement #UkatibaNdioTiba
 
Jaji mkuu mstaafu wa Kenya, David Maraga ameandika katika ukurasa wake wa X akieleza masikitiko yake kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Mei 4 wakati akimpokea Rais wa Kenya, William Ruto jijini Dar es Salaam.
Endelea....

"Kama Jaji Mkuu, nilithamini udugu uliopo ndani ya Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki na nilifanya kazi kwa karibu na wenzangu katika mahakama ya Tanzania katika jitihada za pamoja za kutafuta haki na kulinda utawala wa sheria.

Kwa hiyo, nimeshtushwa sana na kauli zinazodaiwa kutolewa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu wakati wa hotuba ya Rais Ruto katika Bunge la Tanzania.

Inasikitisha kwamba marais hao wawili wanaripotiwa kujadili kuratibu juhudi za “kuchapa mikwajo” dhidi ya kizazi cha Gen Z nchini Kenya na Tanzania.

Kauli hizi zinachukiza.

Zinakuja takriban wiki moja tu baada ya Rais Suluhu kupokea ripoti ya Tume ya Uchunguzi kuhusu mauaji yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Tanzania wa tarehe 29 Oktoba 2025, ambapo zaidi ya watu 518 walipoteza maisha yao, wengi wao kutokana na majeraha ya risasi.

Hadi sasa, hakuna mtu hata mmoja aliyewajibishwa.

Pia hatupaswi kusahau kwamba mwenzetu Boniface Mwangi, pamoja na Agather Atuhaire wa Uganda, waliteswa wakiwa katika ardhi ya Tanzania. Wahusika bado wako huru.

Wananchi wa Afrika Mashariki wanapaswa kuzungumza. Muungano wa udikteta ambao Marais Suluhu na Ruto wanaunda unatishia kurudisha ukanda wetu kwenye utawala wa kiimla.

Kama nilivyoonesha kupitia uwepo wangu wa mshikamano jijini Dar es Salaam tarehe 19 Mei 2025, niliposimama pamoja na kiongozi wa upinzani Tundu Lissu, Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki haiwezi kupiga hatua wakati viongozi wanakandamiza upinzani na kukiuka haki za msingi za watu wetu.

#UkatibaMovement #UkatibaNdioTiba
Ngoja tusubiri na wastaafu wetu tuwasikie, watasemaje.
 
Jaji mkuu mstaafu wa Kenya, David Maraga ameandika katika ukurasa wake wa X akieleza masikitiko yake kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Mei 4 wakati akimpokea Rais wa Kenya, William Ruto jijini Dar es Salaam.
Endelea....

"Kama Jaji Mkuu, nilithamini udugu uliopo ndani ya Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki na nilifanya kazi kwa karibu na wenzangu katika mahakama ya Tanzania katika jitihada za pamoja za kutafuta haki na kulinda utawala wa sheria.

Kwa hiyo, nimeshtushwa sana na kauli zinazodaiwa kutolewa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu wakati wa hotuba ya Rais Ruto katika Bunge la Tanzania.

Inasikitisha kwamba marais hao wawili wanaripotiwa kujadili kuratibu juhudi za “kuchapa mikwajo” dhidi ya kizazi cha Gen Z nchini Kenya na Tanzania.

Kauli hizi zinachukiza.

Zinakuja takriban wiki moja tu baada ya Rais Suluhu kupokea ripoti ya Tume ya Uchunguzi kuhusu mauaji yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Tanzania wa tarehe 29 Oktoba 2025, ambapo zaidi ya watu 518 walipoteza maisha yao, wengi wao kutokana na majeraha ya risasi.

Hadi sasa, hakuna mtu hata mmoja aliyewajibishwa.

Pia hatupaswi kusahau kwamba mwenzetu Boniface Mwangi, pamoja na Agather Atuhaire wa Uganda, waliteswa wakiwa katika ardhi ya Tanzania. Wahusika bado wako huru.

Wananchi wa Afrika Mashariki wanapaswa kuzungumza. Muungano wa udikteta ambao Marais Suluhu na Ruto wanaunda unatishia kurudisha ukanda wetu kwenye utawala wa kiimla.

Kama nilivyoonesha kupitia uwepo wangu wa mshikamano jijini Dar es Salaam tarehe 19 Mei 2025, niliposimama pamoja na kiongozi wa upinzani Tundu Lissu, Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki haiwezi kupiga hatua wakati viongozi wanakandamiza upinzani na kukiuka haki za msingi za watu wetu.

#UkatibaMovement #UkatibaNdioTiba
Tukisema IQ ya Samia ni ndogo sana wanakasirika na wanatuteka.
 
Kwani Kasongo yeye kasemaje
HHkNnLrXcAAO_BU.jpeg
 
Itakuwa kweli walijadili, lakini huo mjadala ulikuwa kati ya mtu mwenye akili na mtu asiyekuwa na akili. Mwenye akili anajua ni maneno gani anaweza kusema in public na maneno gani hawezi. Asiyekuwa na akili, filter hana—yeye anabwatuka tu!
Kama umemsikiliza ruto leo kasema ajira na umaskini ndio tatizo na sio kenya au tanzania
 
Huyu maza siku akianguka au mtu wake wa karibu akaanguka; hakika kuna kundi kubwa la wananchi litafanya sherehe.
 
Kama umemsikiliza ruto leo kasema ajira na umaskini ndio tatizo na sio kenya au tanzania
Pamoja na mapungufu yake huko nchini kwake, bado mwamba alitoa hotuba bora sana. Bibi mipasho kuna kitu anatakiwa ajifunze kutoka kwa watu wenye akili kubwa, badala ya kuendelea kusikiliza matope ya chawa wake lukuki waliomzunguka.
 
Kama umemsikiliza ruto leo kasema ajira na umaskini ndio tatizo na sio kenya au tanzania
Ndiyo maana nilisema, mjadala huo ulikuwa kati ya mtu mwenye akili na mtu asiyekuwa na akili. Ruto ana akili—anajua biashara ya bangi haina matangazo! Na kwenye hotuba yake alihakikisha ametumia fursa hiyo vizuri kujitenga na tangazo la biashara ya bangi alilolitoa mshirika wake, ambalo tayari lilikuwa limeshalaaniwa vikali na watu mbalimbali ndani ya EAC.
 
Mtu yoyote mwenye akili timamu lazima amshangae na kumsikitikia mtu kama Samia.

Bahati nzuri Kenya katiba yao ina uhuru mkubwa ndio maana unaona jaji mkuu mstaafu kama Maraga anatoka wazi kukemea serikali ikifanya upuuzi hata Willy Mutunga nae huwa hayupo nyuma akiona uvunjifu wa katiba maana sio wateule wa rais walipata ujaji mkuu kwa interview kutokana na taaluma zao hivyo hata mafao yao hawagopi yatapotezwa maana rais hana mamlaka kuyagusa yako kisheria.

Huku kwetu jaji mkuu mstaafu ndio kama Chande na Ibrahim waliokubali kuwa toilet paper kwenye tume uchwara kwa ajili ya kulinda mafao yao na mali walizochuma wanaogopa kupaza sauti maana utashangaa kesho mafao yanafutwa au wanatekwa na kufilisiwa.
 
Wakenya wanaongoza kwa kulalamika na kumpa majina mabovu rais wao ila kila kukicha anakuja na mbinu za kuwakwamua kwenye ubepari wapate ajira tatizo la Kenya ni watu wachache kumiliki ardhi kwa hotuba za Ruto ni Rais bora sana..
Kuhusu Upande wa hotuba za Tanzania nadhani Washauri wa Rais hawapo vizuri kabisa na pia Rais pia hataki kubadili msimamo wake kwenye mambo ya kijamii anawaona Watanzania ni adui kumbe sio..
 
Back
Top Bottom