Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,148
- 10,571
Hongera sana kwa kuanza ukurasa mpya wa maisha, tazama mbele brother na endelea kusamehe na kusahau yale ambayo yalitokea kipindi ulipojitoa kwa ajili ya Lisa. Karma is a bitch! Nature itakulipia bro wala usisumbuke na yaliyopita, waswahili wanasema YALIYOPITA SI NDWELE tazama mbele kuna maisha unatakiwa kuishi duniani.
Nadhani kila Mtanzania anafahamu kisa chako wewe na aliyewahi kuwa Mke wako, nyakati za furaha pamoja na nyakati mbaya. Ila usione ajabu kupata watanzania wengi wakikuzungumzia kama mfano bora sana, wapo ambao wamekupa jina la GENTLEMAN, wapo wanaokuita MSAMARIA na kuna wengine walikwenda mbali na kuona kuwa haukupaswa kujitoa kiasi kile kwa mwanamke ambaye hakuwahi kuwa na upendo wala hisia kwako.
Nina imani shemeji yetu ni mtu wa kipekee sana kwako, pamoja na familia yako, naweza kusema kuwa una bahati ya kipekee kwa sababu hayupo kwenye vichwa vya habari sio Facebook, Tiktok wala Instagram, ni kupitia picha zenu za harusi watu ndo wamemuona shemeji kwa mara ya kwanza kuwa ndo Mrs. Mabeste.
Mbali na hayo kuna idadi kubwa ya watu kutoka nyumbani Tanzania, Kenya, Uganda na mataifa mengi tunatamani kuona ukirejea kwenye fani ya muziki, japo tuendelee kusikia sauti yako.
HONGERA SANA KWA KUJIPATIA JIKO BORA KAKA MABESTE.
Nadhani kila Mtanzania anafahamu kisa chako wewe na aliyewahi kuwa Mke wako, nyakati za furaha pamoja na nyakati mbaya. Ila usione ajabu kupata watanzania wengi wakikuzungumzia kama mfano bora sana, wapo ambao wamekupa jina la GENTLEMAN, wapo wanaokuita MSAMARIA na kuna wengine walikwenda mbali na kuona kuwa haukupaswa kujitoa kiasi kile kwa mwanamke ambaye hakuwahi kuwa na upendo wala hisia kwako.
Nina imani shemeji yetu ni mtu wa kipekee sana kwako, pamoja na familia yako, naweza kusema kuwa una bahati ya kipekee kwa sababu hayupo kwenye vichwa vya habari sio Facebook, Tiktok wala Instagram, ni kupitia picha zenu za harusi watu ndo wamemuona shemeji kwa mara ya kwanza kuwa ndo Mrs. Mabeste.
Mbali na hayo kuna idadi kubwa ya watu kutoka nyumbani Tanzania, Kenya, Uganda na mataifa mengi tunatamani kuona ukirejea kwenye fani ya muziki, japo tuendelee kusikia sauti yako.
HONGERA SANA KWA KUJIPATIA JIKO BORA KAKA MABESTE.