ITV yaanika kila kitu na ushahidi wa kutosha kuhusu mauaji ya mwandishi huko Iringa

Mkuu majebere naomba nikuulize maswala haya
1. Nipe majibu ya tume iliyoundwa juu ya wale watu waliouwa pale songea wakati walipokuwa wakienda kwa rc
2. Niambie umeanza lini kusikia malalamiko ya watu wa nyamongo juu ya polisi kufanya mauaji ya watanzania wenzetu na hata kufikia hatua ya polisi hao kutupa miili ya marehemu barabarani? Je ni hatua gani zilichukuliwa hata baada ya kamati kuundwa?
3. Niambie jana jimbo la bubu-zanzibar makamu wa rais alikuwa na mkutano wa hadhara je zanzibar hakuana sensa? Au zanzibar si tanzania au hizi sheria zinalimitation
4. Jana kulikuwa na tamasha la fiesta mwanza mpaka sa 3 usiku, je mwanza sio tanzania? Hakuna sensa?/
5. Unafahamu kuwa morogoro wilaya ya mvomero amos makala (mb) anaendelea na mikutano yake kama kawaida je mvomero sio tanzania hakuna sensa? Hakuna sensa?
6. Unafahamu kwamba polisi na chadema walikubaliana kutokufanya mikutano lakini waliruhusiwa kufanya mikutano ya ndani na kufungua matawi, je tukio lile lilitokea katika mkutano upi?
7. Niambie ni polisi gani aliyechukuliwa hatua tangu mwakyembe alipoanza kulipoti juu ya mkakati wa baadhi ya watu kutaka kumuua hata kutaka kumuua kwa sumu, na ndipo baadaye mwanahalisi kuja kueleza kwa upana wake, je ni nini kilifanyika?
Nijibu hayo kwanza maana nona unaleta masihala hapa

Unadhani hawakuelewi, wanaelewa sana, nafsi zinawauma pia, Mtu hawezi kufanya uchunguzi kwa jambo linalomhusu mwenyewe. na hivi wanajua sisi watanzania ni watu wa kuburuzwa tu, utasikia " ... jambo hilo liko mahakamani, ... Uchunguzi umekamilka, ... Police wametoa maelezo ya kina ... nk" Nimeona picha iliyotumwa CNN, nimeona picha ambazo mwana JF ameweka humu JF, hakuna haja ya tume. Walioua wameonekana hadharani, aliyeshika Limashine la kuulia ameonekana. sasa habari za kutuuliza kama ni bomu tuseme ni la aina gani, sasa huo ni utani. Ni kwamba Police wameua mwandishi wa habari, na haikuwa sawa kufanya hivyo kwasababu mwandishi huyo hakuwa na kinga yoyote, alikuwa anahangaika tu kujiokoa.Nina mashaka pia na akili au mafunzo wanayopata hao "POLISI JAMII, ULINZI SHIRIKISHI, UTII BILA SHURUTI ... " na mbwembwe kibao wanazotuletea siku hizi. Hivi wanaambiwa mashine hizo ni za kufanyia nini ? Maana ni lazima kuna boss wao anayewapatia mashine na maelekezo ! so Mheshimiwa commited, waambie issue hapa siyo kuwa nani ameua, NO, aliyeua kajulikana, labda mtu ajitetee kwa kusema Mashine ile ilijilipua nk, na hakuna msamaha, KWANINI ALIMLENGESHA MTU TUMBONI ??
 
nimeiona hii taarifa itv. wale waandishi ni mashahidi wazuri kwenye tume HURU lkn sio tume iliyoundwa na polisi. hawa ndo mashahidi wanaohitajiwa na fatou bensouda in case shauri hili linakwenda the hague. how comes wewe ni mtuhumiwa na wewe uunde tume ya kujichunguza? this is only in tanzania under ccm gov. oooh WARIOBA, i hope that you and your commission w'll never let us down in this matter.

Inabidi watake care sana la sivyo sasa hivi utasikia mmoja ameteleza chooni na kuvunjika uti wa mgogo na mwingi amepata ugonjwa unaofanana na ebola kisha wametangulizwa mbele ya haki. Chochote kitakachowatokea jueni wamewakolimba.
 
naona bongo CSI mko wengi.

Hili halihitaji utaalam wowote kuliona.Ndo maana inatia gadhabu mnapoleta ubishi kitu kiko wazi na raia mwema ameuwawa kinyama with the very same people who are supposed to be protecting him!

Kweli kuna watu na kuna viatu.You fit the latter!duuh!
 
:flypig:WAMEAMUA KUUA MMOJA MMOJA KILA KWENYE TUKIO,TUNAKOELEKEA WATAFANYA MAUAJI YA MAKUNDI KWA MAKUNDI.
WANAHARAKATI WA HAKI ZA BINADAMU MKO WAPI??????????????
 
mimi nikuulize, hakimu akifanya kosa hapelekwi mahakamani, au wao kesi zao zinasikilizwa na mtu tofauti? Kama kuna polisi wameua kwa kukusudia basi watashitakiwa, hii ndio kazi ya polisi hata kama watuhumiwa pia ni polisi.

SIYO Tanzania ! siku utakaposoma hiyo report ya hao Police ndiyo utaelewa tunalokuambia !
 
Hili halihitaji utaalam wowote kuliona.Ndo maana inatia gadhabu mnapoleta ubishi kitu kiko wazi na raia mwema ameuwawa kinyama with the very same people who are supposed to be protecting him!

Kweli kuna watu na kuna viatu.You fit the latter!duuh!

majebere Amesema anaenda kunywa bia baridi. I afraid huenda wakati tunajadili naye tayari alikuwa TWO IN ONE ! bora ametushitua, mimi pia napumzika mkuu, TUNATWANGA MAJI.
 
Tatizo sio polisi, tatizo hiki chama kisichotii sheria za nchi. kifo ni just matokeo ya huu ukaidi.

Nahisi akili yako imeganda. Hivi, hicho chama ndo kiliwaambia polisi wamburute na kumuua pembeni? Picha inaonesha walimdhibiti, kwa nini hakufungwa pingu na kupelekwa polisi kama walivyofanya kwa wale viongozi wa cdm?
Kumbe mtu mwenyewe ukimueleza ni kama kumpigia mbuzi gitaa, haya baki na njozi zako wenzio wenye akili washa kimbia.
 
hao mashahidi wamepandikizwa, na unaposema alipigwa bomu kwa nyuma utumbo ukatoka na akakatika vipande vipande,hilo ni bomu gani,la machozi au rpg. Mimi nashaka sana na hao mashahidi wako, lazima watakua wametumwa kudanganya umma. Sisi tunasubiri uchunguzi ufanyike kwanza.

nina mashaka sana na uelewa wako! Na kama umesoma, basi shule haijakusaidia!
 
JF Senior Expert Member unasumbuliwa na udini wewe , watu wanajadili mambo ya kitaifa wewe umekazana waislamu kugoma sensa, mbona walihesabiwa?unafiki wako utakuponza
 
akili za majebere ni za kutilia mashaka hazinatofauti na huyu mwenyekiti wa oyesterbay
 

Attachments

  • sensa (1).jpg
    sensa (1).jpg
    80 KB · Views: 72
Mkuu kauli zake huyu mwandishi ndio zinafahamika, huyu ni mwanachama mtiifu wa CDM na hilo linafahamika. Kwa hiyo uandishi ilikuwa just cover tu.

tell us if by being so he deserve this, pls say YES and possibly whose minds do you represent!
 
watu wanajifanya hawaoni yote yatakuwa wazi siku moja na siasa zenu za ubaguzi zilizoasisiwa na c.c.m. sensa ilikuwepo tangu wakati wa nyerere na chadema haikuwepo. ulitaka chadema iwaambie watu wasihesabiwe? chadema hawana muda kujadili mambo ya dini, hayo waachie mashehe na wachungaji. hapa lete siasa tu.
 
Hao mashahidi wamepandikizwa, na unaposema alipigwa bomu kwa nyuma utumbo ukatoka na akakatika vipande vipande,hilo ni bomu gani,la machozi au RPG. Mimi nashaka sana na hao mashahidi wako, lazima watakua wametumwa kudanganya umma. Sisi tunasubiri uchunguzi ufanyike kwanza.
Acheni U-TUPOI Ninyi vichwa maji,
POLICCM ambao ni vibaraka wa CHAMA CHA MABWEPANDE tangu lini walitoa taarifa ya uchunguzi ya kweli?,
Uzoefu unaonesha wamezoea kubambikia WATU kesi,issue ya mabwepande waliibuka na raia wa kenya hii huenda wakaibuka na mkongoman,
Kwa maelezo na picha zilizopo ni wazi kabisa kuwa POLICCM ndo wahusika wa uharamia huo(watajichunguza wenyewe?),Nyie ma-FIRAHUNI MNAO WASAPOTI MABWEPANDE NA UDHALIMU WAO MLAANIWE.
 
Majibu karibu yote utayapata baada ya tume kufanya uchunguzi, vuta subira. Lakini kumbuka kuwa matukio yote yamefanyiwa uchunguzi lakini watanzania wanatabia ya kusahau haraka sana, hata hili tukio litasahaulika pamoja na kwamba uchunguzi utaisha na maelezo yote yatakuwepo.

wewe majebere ni **** tu huna tofauti na hiyo
 
Duh!! Bongo BADO SANA aisee. Yaani mwenzenu katolewa utumbo nyie 'kwa ujasiri' mnasusia kutangaza habari zao? Mna tofauti gani na walimu walivyotishia nyau kwa eti kugomea sensa? Tz tuna tatizo kubwa.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom