ITV yaanika kila kitu na ushahidi wa kutosha kuhusu mauaji ya mwandishi huko Iringa

mwinukai

JF-Expert Member
May 3, 2011
1,447
630
ITV imetoa habari iliyokamilika kuhusu mauaji ya mwandishi wa habari, waandishi wa habari walioshuhudia tukio hilo wameeleza bayana tukio hilo kwa kubainisha chazo cha mauaji hayo, na huku wakitoa ushahidi kuhusu jinsi gani marehemu alivyouawa kikatili na jeshi la polisi.

Mwandishi wa kwanza aliyeshuhudia amesema aliona marehemu akipigwa na askari kama nane, na baada ya hapo alioneakana askari mwenye nyota tatu akamkumbatia mwandishi wa habari ili kumnusuru lakini askari Mwingine alimrushia bomu tumboni na kusambatisha tumbo la mwandishi.

Mwandishi wa pili aliyeshudia amesema kuwa aliona marehemu akipigwa na polisi na baada ya hapo alienda kwa RPC kuomba amsaidie kumnusuru yule marehemu na kumuambia yule anayepigwa ni mwandishi wa habari, RPC hakmjibu ila alifungua kioo cha gari na kukifunga tena.

Hata hivyo moja wa ndugu wa marehemu amesema kuwa ni vizuri kila chama kikawa huru kujieleza kwa Wananchi ili Wanainchi wapate fursa ya kuchagua chama wanachokitaka.

Hata hivyo waandishi wa habari wametangaza kusususia shughui zote za polisi kuanzia ile NENDA KWA USALAMA.
 
kuna mashahidi wawili ambao ni waandishi wa habari waliokuwa na marehemu MWANGOSI (JANA- KATIKA UVUNGUZI WA TAWI LA CHADEMA-IRINGA, MUFINDI) wakati anakamatwa na mapolisi shahidi walikuwa wanaelezea tukio zima itv news usiku huu (sa 2 ) wa kwanza anasema
"marehemu alikamatwa na mapolisi 8, wakampiga sana na marungu kwa mda mrefu kila upande wa mwili wake, akatokea polisi wa nyota tatu akawasihi hao polisi 8 wamwachie marehemu lakini haikufaa kitu akatokea polisi mmoja akaja kwa nyuma ya yule aliyekuwa akiwazuia wasiendelee kumpiga marehe akamfyatulia risasi marehemu na kumtawanya utumbo na bomu hilo likamvunja mguu hata huyo polisi aliyekuwa akiwazuia wasimuue.

Shahidi wa pili anasema
Yeye (huyo shahidi-ambaye pia ni mwandishi wa habari)alipoona marehemu anapigwa alikimbilia kutoa taarifa kwa mkuu wa mapolisi waliokuwa katika eneo hilo la tukio huyo mkuu wao alikuwa katika gari akiwa kafunga viooo huyo shuhuda ambaye naye ni mwandishi alipofika hapo akagonga kioo cha gari ili huyo afisa wa polisi afungue, alipofungua huyo mwandishi akamweleza tafadhali naomba msaada wako mkuu yule anayepigwa pale ni mwandishi wa habari, tafadhali naomba msaaada wako huyo afisa hakumsikiliza akarock kiooo.

Ndio maaana nawahuliza hao (Majebere, mwiba na wengineo) wapenda uozo na mauaji ya polisi wameyasikia haya (Ushahidi toka kwa watu wailiokuwa eneo la tukio)? na kuangalia tv... maana wao sijui wanamioyo gani hawa watu ni zaidi ya wanyama kila wakati wao ni kuwatetea polisi hata uweke ushahidi wazi kiasi gani.

Imeniuma sana wakuu SORRY KWA ALIYEKWAZIKA JINSI NILIVYOLIPOTI NI HASIRA JUU YA HAO WATU
 
Safi waandishi msi ishie hapo fungueni na kesi kabisa haya majambazi yafungwe!
 
...Mkuu hii tume uchwara inayoongozwa na Mwema kamwe haitawaita hao jamaa wawili watoe ushahidi na si ajabu wanaweza kabisa kunyamazishwa ili kuficha ukweli wa kile kilichojiri katika mauaji ya Mwangosi.
 
Kususia haitoshi, tuwekeeni sura zao ktk kurasa za mbele tusifanye makosa kulipiza kisasi. Waandishi wa habari elekezeni camera zenu kwenye makazi ya Police na andikeni habari yeyote, we want to know where we can find them.
 
Nimeiona hii taarifa ITV. Wale waandishi ni mashahidi wazuri kwenye tume HURU lkn sio tume iliyoundwa na polisi. hawa ndo mashahidi wanaohitajiwa na fatou bensouda in case shauri hili linakwenda the hague.

How comes wewe ni mtuhumiwa na wewe uunde tume ya kujichunguza?

This is only in tanzania under ccm gov. oooh WARIOBA, i hope that you and your commission w'll never let us down in this matter.
 
Kuna waandishi wengine nimeona kama wameonyesha RPC hakuwepo pale alikuwa kwenye gari, na picha zinaonyesha alikuwa amekumbatiwa na marehemu...sasa unajua baadi ya waandishi tena waliowengi ni walarushwa na mara nyingi huwa wanatumiwa na selikali, unaweza kuona hata kwenye hii habari hadi mwisho itatetewa sana na waandishi ili kuwasafisha polisi hasa RPC aliyekuwa anatoa command pale kwenye tukio...

Mapandikizi mmejaa kwenye hiyo taaluma yenu, wala rushwa kama kina muro mmejaa vilevile...mfano mdogo tu huo...sasa mwandishi mwenzenu ameuawa lakini wenyewe mtashuhudia kabisa baadhi ye waandishi wenzenu wakiwa kinyume na marehemu wakitetea serikali na polisi ili at the end of the day wasafishike.....si ajabu ukasikia bom hilo lilirushwa na chadema hapo...wakati tumeona kila kitu, nimesikia RPC huyo alisema bom lilirushwa na waandamanaji na sio kwamba lilitoka kwa polisi..

Pamoja na kusema kuwa bom hilo lilikuwa ni lile la kutoa machozi, bado tu wanajichanganya kuwa bom lilitoka kwa wananch....nafikiri mabom ya machozi siku hizi wananchi wanaenda kuyachukua kule kwenye boma la silaha la field force unit kule kihesa iringa...hahaha.ajabu kweli...

Polisi kama mlikuwa mnaongea uongo mara nyingi..kwa hili itabidi watu waajibike au waadibishwe haraka kwasababu wananchi wamejua ukweli kabla ninyi hamjaunda uongo mlioutangaza.
 
mwiba , majebere n.k! hamtoishi milele kamwe, na mungu alivyo wa maajabu anaweza akaja kuwaonesha haya waziwazi kupitia mazingira yenu, namaanisha uwenda yakawakuta na nyinyi haya ya marehemu au lah nduguzenu wa karibu! msiwe kama hamjazaliwa! ila ninawasiwasi na uwepo wa hawa watu jf humu, sio watu wa kawaida ni wa system ya huko huko kwenye uozo! mwisho wa yote mlaaanie.
 
Damu ya Mwangosi kumwagika kwake kuwe chachu ya mshikamano wenu waandishi..
This is the time ya kumchapa adui yenu kwa nguvu zenu zote using your respected taaluma..
Ni nyie tu mnaoweza kujikomboa na kujijengea heshima..
The time is now, I mean now..
 
nimeiona hii taarifa itv. wale waandishi ni mashahidi wazuri kwenye tume HURU lkn sio tume iliyoundwa na polisi. hawa ndo mashahidi wanaohitajiwa na fatou bensouda in case shauri hili linakwenda the hague. how comes wewe ni mtuhumiwa na wewe uunde tume ya kujichunguza? this is only in tanzania under ccm gov. oooh WARIOBA, i hope that you and your commission w'll never let us down in this matter.
Shauri hili halina hadhi ya kwenda the hague, kosa hili halijadondokea kwenye any of the four crimes under the ICC statute...can you say this is a widespread and systematic attack against civilian population within the meaning of the icc statute? ili tuseme hii ni crime against humanity?

Bado haijafikia hadhi hiyo, halafu hata hivyo, bado nchi yetu inayo room kupelekea watu mahakamani kwa at least mwaka mmoja ndio reasonable before the ICC gets in...kuna principle kweney article 17 of the icc statute inaeleza principel ya complimentarity, na kama watu watapelekwa mahakamani kwa nia ya kuwashield tu au kama selikali itakuwa serious etc...kwa hili, hawa wataangukia kwenye mahakama zetu hizihizi tu bro.
 
mwiba , majebere n.k! hamtoishi milele kamwe, na mungu alivyo wa maajabu anaweza akaja kuwaonesha haya waziwazi kupitia mazingira yenu, namaanisha uwenda yakawakuta na nyinyi haya ya marehemu au lah nduguzenu wa karibu! msiwe kama hamjazaliwa! ila ninawasiwasi na uwepo wa hawa watu jf humu, sio watu wa kawaida ni wa system ya huko huko kwenye uozo! mwisho wa yote mlaaanie.

Mkuu markj sijui hawa jamaa wanaakili gani hata kifo jamaaa wanashabikia....aghraaaa! Lakini Mungu atawajibu tu siku moja.
 
Hawa waandishi inatakiwa wawe na msimamo wao wenyewe. Wasiwe kama kina Ulimboka.
Kipigo alichopata Uli si cha kitoto ni robo tatu ya Kifo lazima atulie kwanza kusahahu machungu na kama wamemuahidi Compensation atulie basi wasipomtimizia ndio anaweza kuendeleza msimamo wake...

Police kwa hili Wamechemsha hadi wametokota Shame kabisa Dunia itawakataa
 
Mkuu ukaidi upi tena watu wamekwambia haukuwa mkutano wa nje na hata hivyo yule hakuwa muandamanaji ni mwandishi na anajulikana?


Mkuu kauli zake huyu mwandishi ndio zinafahamika, huyu ni mwanachama mtiifu wa CDM na hilo linafahamika. Kwa hiyo uandishi ilikuwa just cover tu.
 
Hao mashahidi wamepandikizwa, na unaposema alipigwa bomu kwa nyuma utumbo ukatoka na akakatika vipande vipande,hilo ni bomu gani,la machozi au RPG. Mimi nashaka sana na hao mashahidi wako, lazima watakua wametumwa kudanganya umma. Sisi tunasubiri uchunguzi ufanyike kwanza.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom