Uchaguzi 2020 ITV leo hakuna taarifa ya mikutano ya Lissu?

Wanabodi habari ya majukumu?

Nipo naangalia taarifa ya habari ya ITV naona leo hakuna taarifa ya mikutano ya Lissu. Je, leo Mh Lissu hakufanya mikutano?

ITV ni vizuri muwe mnatupa taarifa mapema siku ambazo hakuna taarifa za Lissu tusiwetunapoteza muda, angalau tuwe tunafanya mambo mengine.
Wakikupa taarifa wanajua hautawaangalia
 
24 October 2020
Songea mjini, Ruvuma
Tanzania

WATU WA SONGEA MAGUFULI NI MBAGUZI,MWIZI NA FISADI MSIMCHAGUE” TUNDU LISSU


Da aisee jamaa anajua kuelimisha huyu!
Watu wanaitikia utadhani wait darasani.
Kutokumpa Urais mtu huyu Ni hasara kwa Taifa.
Anagusa kila sekta.
Aisee kura yangu kwa Lissu.
 
Ukienda pages za ITV wanaweka posts za Lisu kwa sana,na wanapata comments za kushiba saaana. Ila taarifa ya habari wanakuwa kimya
 
Kungekuwa na Uhuru Kama ule wa 2015 jiwe angekubali kushindwa kabla ya uchaguzi. Na kubana KOTEE HUKO lakini bado Tundu Lisu kawa mwiba Ni Jambo la kushangaza.
Mungu hutenda kwa namna hii.
Ili Kuonesha uwezo wake hufanya upande mmoja kuwa dhaifu Kisha kuuinua,na wenye nguvu huuacha utumie nguvu zake Kisha kuushusha.
Mifano Ni mingi
Musa na farao
Daudi na goliati
N.k
 
Back
Top Bottom