Intelijensia Kuhusu Maandamano ya CHADEMA

Intelijensia Kuhusu Maandamano ya CHADEMA

Wageni muhimu kwa nani? Hii tabia ya kutegemea wawekezaji toka nje kwa kufikiri watatuletea maendeleo,ni ya kimaskini sana. No wonder mkwere kwny mahubiri yake ya mwisho wa mwaka alisema nia ya maandamano ya vyama vya upinzani ni kuwachokoza polisi ili katika anga za kimataifa TZ ionekane ni ya kimabavu. Yani mkwere anaogopa anga za kimataifa kuliko kuogopa watu wake?! Ni muda mwafaka kwa kuifanya serikali ianze kuwaogopa wananchi,na si wananchi kuiogopa serikali. Kwa namna iyo,madudu yote yanayotokea sasa hatutayasikia,kwani serikali itakua ikifikiria mara mbili mbili kabla ya kuamua au kutenda jambo. Mi sasa ni actions kwenda mbele...no more talking. Mtanisoma tu.....
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?

wawekezaji kitu gani? kwani wanamsaidia nani hao wawekezaji zaidi ya mafisadi wenu na ccm yenu? mwananchi wa kawaida anafaidika nini na uwekezaji wa kihindi huo? give me a break you can do better than this.
 
Viongozi wa Chadema walilazimisha maandamano yafanyike licha ya kuombwa na Mkuu wa Polisi Tanzania kuwa yasifanyike kwa sababu tu:

Walikuwa na nia ya kuwatisha wawekezaji wakubwa duniani ambao wapo Tanzania, huko huko Arusha kwa sasa.

Wawekezaji hao, wakiongozwa na Dhirubhai Ambani walikuwa Tanzania kwa nia ya mapumziko na biashara na kutazama mandhari ya Tanzania na uwezekano mkubwa wa kuwekeza Tanzania.

Kwa roho mbaya tu na kwa nia isiyoyatakia mema Tanzania, viongozi wa Chadema wakahakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa lazima na hata yangeruhusiwa na polisi basi fujo lazima zingetokea ili kuwatisha hao wawekezaji waone kuwa Tanzania si pa kuwekeza.

Yote hiyo, ni kwa sababu tu, ya chuki zao binafsi walizozijenga baada ya kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi uliopita.

Hakuna mantiki yoyote kwa wana siasa walio mahiri kulazimisha maandamano yafanyike wakati kuna wageni, tena wawekezaji muhimu ambao hakuna nchi katika hii dunia yetu ya sasa isiotaka wawepo au watembelee kwao.

Viongozi wa Chgadema kwa ajili tu ya chuki zao binafsi, wakaona hii ndio fursa ya kuipakaza matope (kama si m*v*) Tanzania. Walijuwa kuwa wawekezaji wakubwa kama hawa wanapokuja tena kwa idadi kubwa kama iliowasili hapa, lazima kuna waandishi wa habari wa kimataifa hususan wa mambo ya kibiashara na pia kuna watu wa intelijensia za kibiashara ambao misafara kama hiyo huwa hawakosekani.

Kwa namna ya maisha tunayoishi wa Tanzania au kwa mpenda amani yoyote, hata kama mna ugomvi wenu wa ndani, ajapo mgeni, tena ambae anaweza kuleta manufaa nyumbani kwenu, huwa mnasitisha ugomvi kwa siku mbili tatu mpaka mgeni aondoke. Haya hutokea hata majumbani mwetu, tukipapurana na bahati nzuri au mbaya mgeni akibisha hodi basi mara nyingi kwa wenye akili husitisha kupapurana kwao, wakamhudumia mgenina ikibidi kupapurana, wataendelea mgeni akisha ondoka.

Leo Chadema wameonyesha sura gani ya nchi yetu, kwa kulazimisha maandamano yaliyositishwa na Mkuu wa Polisi, mbele ya hawa wageni?

Nna uhakika, sura walioionyesha si nzuri, lakini, ni matumaini yangu kuwa wenyeji, waliowaalika hawa wageni, wataweza kuwafahamisha ukweli ulivyo na wataridhia si tu kuja tena kutembelea Tanzania, bali na kuwekeza kwa wingi, kwani kwa sasa bado tunahitaji mitaji ya nje.

Nawaomba wa Tanzania walaani kitendo cha viongozi wa Chadema baada ya kuuelewa huu ukweli wa kwanini hawa viongozi walilazimisha maandamano yafanyike.

Mungu awalaze popote apendapo Marehemu waliofarik.

katika wajinga na wewe ni mmoja wao, tena umeboa kwa ujinga, yaani ukajikunja kuandika ujinga kama huu? na kama wewe ni mmoja wa inteligensia ndo maana serikali nayo ni jinga kama wewe
 
Kichwa chako kimejaa maji tupu. Tangu wamekuja wawekezaji tumefaidika na nini zaidi ya ufisadi na ugawaji wa pesa za walipakodi kwa elephant projects. Amani bila demokrasia ya kweli ni kubaki utumwani katika kipindi tofauti. Hapo bado utaelewa tu maana yake.
 
Akili kama hiyo ya Zomba ndio wanayo Watanzania wengi sana.
kazi yetu iwe ni kuwaelimisha tu jamani ingawa wanakatisha tamaa.
 
Ki msingi mimi nimeonja joto la jiwe la vurugu za kisiasa Arusha. Hapa naeleza kifupi sana, kimsingi askari walikuwa wamejiandaa kwa vita. Maana walichokuwa wamekifanya sio kupambana na waandamaji bali kila binadamu mwenye ngozi nyeusi aliyeonekana mjini Arusha. wakipita wakiwaona mnatembea wawili watatu hapa ni bomu la machozi na taaa!!!!! taaaa!!!!!(lisasi) ili mradi walikuwa wanataka kuua.Kama ulikuwa uko mbali unaweza kusema chadema walikuwa na fujo lakini sivyo ilivyokuwa. ilikuwa ni vurugu akari walizotumwa wafanye wakizania wanakijenga chama cha mapinduzi. Sasa inavyoelekea wamekibomoa. Wamekipa CHADEMnguvu sana hapa. Damu za watu zilizomwagika na ziwe juu yao waliopanga hizi vurugu.
 
Ki msingi mimi nimeonja joto la jiwe la vurugu za kisiasa Arusha. Hapa naeleza kifupi sana, kimsingi askari walikuwa wamejiandaa kwa vita. Maana walichokuwa wamekifanya sio kupambana na waandamaji bali kila binadamu mwenye ngozi nyeusi aliyeonekana mjini Arusha. wakipita wakiwaona mnatembea wawili watatu hapa ni bomu la machozi na taaa!!!!! taaaa!!!!!(lisasi) ili mradi walikuwa wanataka kuua.Kama ulikuwa uko mbali unaweza kusema chadema walikuwa na fujo lakini sivyo ilivyokuwa. ilikuwa ni vurugu akari walizotumwa wafanye wakizania wanakijenga chama cha mapinduzi. Sasa inavyoelekea wamekibomoa. Wamekipa CHADEMnguvu sana hapa. Damu za watu zilizomwagika na ziwe juu yao waliopanga hizi vurugu.
Aftermath yake wataiona kabla ya 2015.
JK alieleza kuwa ni wakati wa kutibu majeraha yaliyozalishwa na uchaguzi, kama kutibu kwenyewe ndio huku, basi ni bora kuwa na kidonda-ndugu!...
Ndio maana wanasiasa si watu wa kuwaamini hata kidogo, wanabadilika badilika mno rangi!...kweeeeee!
 
Viongozi wa Chadema walilazimisha maandamano yafanyike licha ya kuombwa na Mkuu wa Polisi Tanzania kuwa yasifanyike kwa sababu tu:

Walikuwa na nia ya kuwatisha wawekezaji wakubwa duniani ambao wapo Tanzania, huko huko Arusha kwa sasa.

Wawekezaji hao, wakiongozwa na Dhirubhai Ambani walikuwa Tanzania kwa nia ya mapumziko na biashara na kutazama mandhari ya Tanzania na uwezekano mkubwa wa kuwekeza Tanzania.

Kwa roho mbaya tu na kwa nia isiyoyatakia mema Tanzania, viongozi wa Chadema wakahakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa lazima na hata yangeruhusiwa na polisi basi fujo lazima zingetokea ili kuwatisha hao wawekezaji waone kuwa Tanzania si pa kuwekeza.

Yote hiyo, ni kwa sababu tu, ya chuki zao binafsi walizozijenga baada ya kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi uliopita.

Hakuna mantiki yoyote kwa wana siasa walio mahiri kulazimisha maandamano yafanyike wakati kuna wageni, tena wawekezaji muhimu ambao hakuna nchi katika hii dunia yetu ya sasa isiotaka wawepo au watembelee kwao.

Viongozi wa Chgadema kwa ajili tu ya chuki zao binafsi, wakaona hii ndio fursa ya kuipakaza matope (kama si m*v*) Tanzania. Walijuwa kuwa wawekezaji wakubwa kama hawa wanapokuja tena kwa idadi kubwa kama iliowasili hapa, lazima kuna waandishi wa habari wa kimataifa hususan wa mambo ya kibiashara na pia kuna watu wa intelijensia za kibiashara ambao misafara kama hiyo huwa hawakosekani.

Kwa namna ya maisha tunayoishi wa Tanzania au kwa mpenda amani yoyote, hata kama mna ugomvi wenu wa ndani, ajapo mgeni, tena ambae anaweza kuleta manufaa nyumbani kwenu, huwa mnasitisha ugomvi kwa siku mbili tatu mpaka mgeni aondoke. Haya hutokea hata majumbani mwetu, tukipapurana na bahati nzuri au mbaya mgeni akibisha hodi basi mara nyingi kwa wenye akili husitisha kupapurana kwao, wakamhudumia mgenina ikibidi kupapurana, wataendelea mgeni akisha ondoka.

Leo Chadema wameonyesha sura gani ya nchi yetu, kwa kulazimisha maandamano yaliyositishwa na Mkuu wa Polisi, mbele ya hawa wageni?

Nna uhakika, sura walioionyesha si nzuri, lakini, ni matumaini yangu kuwa wenyeji, waliowaalika hawa wageni, wataweza kuwafahamisha ukweli ulivyo na wataridhia si tu kuja tena kutembelea Tanzania, bali na kuwekeza kwa wingi, kwani kwa sasa bado tunahitaji mitaji ya nje.

Nawaomba wa Tanzania walaani kitendo cha viongozi wa Chadema baada ya kuuelewa huu ukweli wa kwanini hawa viongozi walilazimisha maandamano yafanyike.

Mungu awalaze popote apendapo Marehemu waliofarik.

Crap!
 
Pole mkuu...inaonekana nawe ni mhanga! Naamini ili tukio litaleta madabiliko, japo 'cost' yake imekuwa kubwa kupita kiasi.
 
Hebu Google haya majina
1.Andrew James Tice (Canada)
2. Gopalakrishnan Balachandaran (India)
3. Hon Sung Woo (Singapore)
4. Guy Picard (Canada)
5. Sulaiman Al Adawi (Oman)
6. Stanley Munai (Kenya).
 
Kichwa chako kimejaa maji tupu. Tangu wamekuja wawekezaji tumefaidika na nini zaidi ya ufisadi na ugawaji wa pesa za walipakodi kwa elephant projects. Amani bila demokrasia ya kweli ni kubaki utumwani katika kipindi tofauti. Hapo bado utaelewa tu maana yake.

Yeah you got a point there,hivi kama watanzania tumefaidika nini exactly?umeme?sasa hivi tu navyoandika haupo na ni hivihivi for the last 2 weeks i think!Zaidi wanaofaidika na hao wawekezaji ni hao wakubwa wenu mnaowashabikia.Wanatoka vitambi,VX zinabadilishwa daily,Huku kina Zomba mnasota,afu bado kutoka hamtaki,mnawashangilia tu.This is bullshit
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?

wewe unathamini wageni kuliko uhuru wako. Mgeni akija kwako unaweza kumpisha chumba na mkeo kwa ajili ya kuonyesha ukarimu
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?

FIKIRA MBOVU; uchumi wa nchi hii hautajengwa na wawekezaji, hao ni wezi wa mchana. Kaa chonjo ndugu hadi mkeo ataibiwa, we endelea kuwaona kama ni wageni wa maana. Uchumi wa nchi hii tutaujenga wa-TZ wenyewe.
 
Back
Top Bottom