Mkuu wa polisi nchini Said Mwema kusitisha ghafla maandamano ya Chama Cha Chadema huko mjini Arusha ambayo yalishapata kibali kutoka kwa Mkuu wa Polisi mkoa wa Arusha ni dhahiri kuna mkubwa fulani aliyeshinikiza na leo anainamisha kichwa chini kwa kuona matokea ya kutumia zaidi nguvu ya dola kukandamiza haki za wananchi badala ya kutumia utaratibu wa utashi wa mazungumzo ya pande zote mbili kwa amani kama walivyoomba chadema hapo awali au kuyaacha maandamano na mkutano uishe kwa amani.
Mfalme Suleman wa taifa la Waisrael alipoambiwa aombe kitu cho chote kwa Mungu katika utawala wake, yeye aliomba Mungu amjalie kipaji cha hekima na burasa. Aliomba kitu ambacho kwa wengi wa watawala wetu wa leo ni kitu adimu kukifikiria Mungu awajalie. Kwa hakika alichagua fungu lililo bora na adimu sana. Wengi wetu wanaomba usiku na mchana Mungu awajali kupata utajiri na heshima na kutawala bila mipaka. Lakini Mfalme Suleman anaheshimika katika historia ya wafalme wengi kwamba ni mmoja aliyejaliwa hekima na busara sana katika utawala wake licha ya udhaifu wake aliokuwa nao. Naam busara na hekima ndio sifa njema ya kiongozi bora, na yuko makini kufikiria athari zake kabla hajaagiza utumiaji wa nguvu dhidi ya raia wasio na hatia na wanaaoandamana kwa amani.
Maji kadiri ya nature na wataalamu wa fisikia wanajua the force of gravity, maji hayawezi rudi mlimani, na hilo hata kwa mwenye akili changa anajua. Kwa vyo vyote mwenye kulazimisha maji yarudi mlimani yalikotoka kinyume cha nguvu ya asili yake kufuata mreremko basi kwa vyo vyote akili yake haija kaa sawa. Kwa maana busara na hekima inakosekana kwa kiasi kikubwa. Kiongozi mwenye hekima na busara atatumia busara na hekima kutambua nature ya maji kufuata mkondo wake hadi baharini. Busara na hekima kwa pamoja vitaongoza mkondo wa maji yaendelee na safari yake kwa utulivu wote.
Kulazimisha maji yarudi yalikotoka haiwezekani. Inawezekana kuyasimamisha kwa muda mahala fulani na ujue wazi wakati huo yanakusanya nguvu. Yatatoboa njia nyingine ya kupita na pengine nguvu yake ikizidi itavunjilia mbali kizuizi ulichoweka ili mradi safari yake inaendelea. Hapo kutakuwa na athari kubwa kwani mimea na udongo na vitu vingine ambavyo ni kando ya mtu vitaadhirika katika dhoruba itakayoletwa na maji, na baadhi kusombwa katika dhoruba hiyo.
Kama maji hayo yasingezuiwa madhara yanayotokana na nguvu ya kusukuma yaendelee na safari yake yangeepukika. Kwa maana hiyo hapa ni common sense tu ambayo imo ndani ya hekima na busara.
Tuna mifano hai kama ya Mzee Ruksa kwa busara yake alipoona maji kuzidi nguvu katika harakati za kudai mageuzi aliruhusu na kuongoza mageuzi na hakukutokea madhara kama tunayoona sasa katika utawala huu. Sijui tumekulia jeshini hivi tunafikiria siasa ni nguvu badala ya majadiliano ya kupata hoja ya kukubaliana?
Wanafalsafa husema kukaa kimya bila kutolea msimamo wako katika jambo fulani maana yake ni kwamba unakubali au unapinga ila unao woga wa uwazi. Hii ni kasoro kubwa, na ngoja ngoja huumiza matumbo kama wahenga walivyotuachia usemi huu. Hatima ya ngojangoja huumiza matumbo ndo yaliyojilia huko Arusha.
Heshima ya jiji la arusha laweza shuka hadhi yake tokana na kukosa burasa katika mambo ya kawaida tu yanayotaka haki za raia zizingatiwe, kwani jiji hilo linaitangaza Tanzania katika mengi. Hayo yanatokea Arusha kuna mambo ya siri yaliyofichika ili kulinda maslahi ya wachache, si matakwa ya wananchi. Kuibuka ghafla kutafuta makafia ya kusaidia kuongoza jahazi lisiendelee kuzama tokana na dhoruba kali, wakati dalili za dhoruba uliziona na kwa sababu zako binafsi uliidharau hiyo, tunaweza tafsiri kama ni kutapatapa kwa mfa maji.
Hekima na busara huzaa mafanikio ya uongozi bora, lakini machafuko ni udhaifu wa uongozi ambao wanajiona ni watawala. Cha msingi wengi wa viongozi wetu ni watawala badala ya kuwa viongozi. Kiongozi bora ataongoza maji yafuate mtiririko wake yaendako.