Kuna Sister nilikutana naye kwenye basi kwa jinsi nilivyopauka kwa vumbi la mkaa akajua labda nina ngoma,akanipa kikaratasi akitangaza wanayo hospital inatoa tiba mdabala,inatibu magonjwa sugu na bla bla bla kibao,cha kushangaza huyo siter alikuwa anakohoa kinoma,nikajiuliza mbona na yeye hajitibu kwa hizo tiba mbadala?
Utakutana na hawa watu wanaouza mafuta sijui yanaondoa chunnusi na bla bla kibao,yeye anayeuza hayo mafuta uso wake una chunusi utafikiri fenesi au wanauza dawa za meno kwa kusema zinangarisha meno na bla bla kibao,ukiyacheck meno ya huyo muuzaji utafikiri ni Shabiki wa yanga.
Huwa sinaga upuuzi wa kusikiliza watu wa type hizo.