In DEFENCE of LOWASSA (Warioba & Butiku on it)

Kama serikali yetu inataka kufanya kweli, Lowasa na tapeli Rostam lazima washitakiwe kuhusu RICHMONDULI la sivyo yatakua yale yale ya JK mwache mzee wa watu apumumzike vizuri kwa kujipongeza kula mabilioni aliyotuibia. Kutoshitakiwa na kufilisiwa ni sawa na kuendeleza ufisadi.
Lowasa anajua fika ni mhusika mkuu na anajua hana cha kujitetea.
 
Jamani wanaCCM wale wabunge wa Arusha waliosemeka wamepokea rusha mliwatemesha uanachama mara moja.Sasa sijui mna mpango gani na hawa akina El na wenzake ambao wameliibia Taifa? Au ndo mnatuhakikishia kuwa kweli CCM ni chama cha majambazi??!!
 
Nyangumi,
Maneno yako kweli tupu hata yule wa CUF aliyekuwa akisafirisha watu nje yalimkuta hayohayo leo vipi CCM bado wanawakumbatia hawa jamaa?...

Kutokana na hali hii naomba mtu afungue mada inayozungumzia BUNGE letu na yanayotokea huko ili watu wapate kufahamu kinachoendelea... leo hii ktk pita pita zangu nimeona kitu hiki ndani ya IPPmedia kidogo kinanipa tumaini kuwa ngoma hii bado kabisaaaa!..
Nimenukuu kipande hiki:-

Akinukuu kifungu cha 57(2)E, Spika alisema iwapo Waziri Mkuu atajiuzulu, Waziri au Naibu Waziri naye anakoma kushika wadhifa wake.
"Sasa baada ya kuwa mheshimiwa Waziri Mkuu amemuandikia Rais barua kwamba anajiuzulu na jioni hiyo hiyo ombi lake kukubaliwa na kwa mujibu wa Katiba kwa kutumia kifungu hicho cha 57(2)E ni dhahiri kwamba Bunge hili sasa hatuna serikali.

Sasa waheshimiwa wabunge kwa kuwa serikali imebaki na Rais na Makamu wake ambao nao hawamo ndani ya Bunge, ibara ya 63 (2) ya Katiba inatamka kazi zetu kama Bunge ni kuishauri na kuisimamia serikali, ikiwa ni pamoja na kuwahoji maswali Mawaziri lakini sasa hawapo,`` alisema Spika na kupigiwa makofi yaliyoambatana na vicheko.

Akizungumia hoja ya kujadili ripoti ya mkataba wa Richmond alisema: ``Kushauri huko ni pamoja na kuendelea kuyajadili haya mapendekezo ya kamati teule ili tukishauri yale yatakayokubalika wawepo wa kuyatekeleza� Sasa hawapo, kwa msingi huo natangaza kuahirisha Bunge nipate nafasi ya kushauriana na taasisi mbalimbali,``

Asubuhi bungeni jana, Bw. Lowassa, hakuonekana hali kadhalika Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika naye hakuonekana.
Hata hivyo, Bw. Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha, walikuwepo. Baadhi ya Mawaziri walivikimbia viti vyao na kujiunga na wabunge wa kawaida kwenye viti vya nyuma.

Lakini kwa upande wake, aliyekuwa Waziri wa Miundombinu Bw. Andrew Chenge ambaye ni mbunge wa Bariadi Magharibi mara baada ya kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge huku akijua kabisa hana tena wadhifa wake wa uwaziri, hakusumbuka kwenda kwenye kiti anachokalia siku zote ambacho kiko mbele. Badala yake Bw. Chenge alikwenda nyuma kabisa ya viti vya wabunge ambako hakuna viti akaamua kuketi chini ya zulia.

Hata hivyo, muda mfupi baadaye, Bw. Chenge aliangaza na kubaini kuwepo kwa viti kadhaa vikiwa havina wabunge waliovikalia, aliinuka na kwenda kukalia kiti cha Mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz ambaye hakuwepo ndani ya ukumbi.

Nje ya Bunge zilisikika dua zisemazo ``kaka, dada nakuombea Mungu, Mwenyezi Mungu atakurudisha. Tutakuona na safari hii utapanda ngazi.`

Asubuhi kabla ya kuanza kikao cha Bunge, Mawaziri `waliotimuliwa` waliingia eneo la bunge kinyonge, tena kwa miguu baada ya kuegesha magari yao binafsi nje ama ya serikali yaliyokuwa na namba za STK. Utaratibu uliozoeleka ni vigogo hao kuingia na `mashangingi` yao na kuyaegesha katika eneo maalum la magari ya viongozi.
Wengi hao walionekana wanyonge, wakitembea kwa makundi makundi huku wakijadili hili na lile, hali ambayo ilidhihirisha hofu ya kutemwa kwenye baraza jipya linalosubiriwa kwa hamu.

Haya haya Simba na Yanga uwanjani....fainali ndio hiyooooo!
 
Wakampeleka kwa SPIKA,

Wakamuuliza wewe ndiye RICHMOND?

Hakujibu neno.

SPIKA akaomba MUONGOZO

Ndipo LOWASA akasema NAJIUZULU.

Wabunge wakapiga kelele wakisema ASULUBIWE.

Spika akasema mpelekeni Golgota.

Hata yapata saa 11 wakamsulubisha LOWASA; kulia KARAMAGI kushoto
MSABAHA.

KARAMAGI akamwambia tumefanya usanii mwingi, jiokoe nafsi yako na sisi pia.

LOWASA akalia kwa Kimasai OONGAI PAPALAI yaana RAIS mbona umeniacha?
Kisha akakata roho.
 
Jamani naomba kuuliza na kuelimishwa

.....Kujiuzulu kwa Lowassa.....je atapata marupurupu kama akina Warioba, Salim et al? i.e. Ulinzi, Gari, Safari na mapochopocho mengine??
 
303217440.jpg

Mwenzetu ana fani nyingi labda kabla ya kumfunga tumpeleke kwenye Olympic anaweza kutuletea medali.
 
Jamani,

"Kifo" cha Uwaziristan Mkuu wa Lowassa was in making for a long time. It is not about Richmond issue that led for public rallying and even Wabunge wenzake kumkebehi. Ni arrogance, stupidity, heavy handedness na worse enough ruling generating fear!

Nchi inashangilia si kwa kuwa amebainika ni mwizi au alihusika na wizi, bali ni kwa kuwa alitawala kibabe na kutaka aogopewe na kila mtu. Alikuwa mtemi flani hivi aliyejiamini kupita kiasi na aliliburuza mpaka Bunge.

Alifukuza mhandisi wa Serikali kwa kosa la mkandarasi, alimfokoea DC John Mongela wakati jamaa ndio anaanza kutoa takwimu na hotuba! he was a bully!

There is 50% chance kuwa hakupata mshiko wa RDC (let's assume), lakini ni jinsi alivyokiuka protocol zote za kizabuni na kutumia madaraka kushinikiza mradi huu ufanikiwe. That is why it appears he had part in Uhujumu. Worse enough is that he failed to do a due dilligence on RDC ending up handling contract to a phony company.

Sasa hili atalikwepa vipi wakati Taifa linaangamia kutokana na uzembe wake?

Tuendelee kuongozwa na mtu mzembe na mwenye kushindwa kufuata sheria kama yeye? Kama yeye hakufuata sheria na kanuni, akakosa maadili, je walio chini yake wafanyeje?

Angalia Pinda alichosema
Akizungumzia kashfa ya Richmond, Pinda alisema imetokana na kutokuwepo utawala bora, hivyo yeye ameahidi kusimamia dhana hiyo kwa kuamini kwamba, umma wa Watanzania una matarajio makubwa sana kutoka katika serikali hii mpya.
this should tell you how Lowassa was horrible as Prime Minister.

The worst leader in History of Tanzania!
 
Wakampeleka kwa SPIKA,

Wakamuuliza wewe ndiye RICHMOND?

Hakujibu neno.

SPIKA akaomba MUONGOZO

Ndipo LOWASA akasema NAJIUZULU.

Wabunge wakapiga kelele wakisema ASULUBIWE.

Spika akasema mpelekeni Golgota.

Hata yapata saa 11 wakamsulubisha LOWASA; kulia KARAMAGI kushoto
MSABAHA.

KARAMAGI akamwambia tumefanya usanii mwingi, jiokoe nafsi yako na sisi pia.

LOWASA akalia kwa Kimasai OONGAI PAPALAI yaana RAIS mbona umeniacha?
Kisha akakata roho.


Na kabla ya kikao cha Bunge, alienda kuonana na Rais Kikwete kuhusu ripoti ya tume (kwani alishaiona tayari).Alitaka ripoti isisomwe kwani ingemuumbua, kumbuka Rais ndiye aliunda tume ichunguze kashfa hii.

Guess what?????? EL Akamwambia JK, mheshimiwa Rais, "Kama itawezekana, kikombe hiki kiniepuke, sio kama nipendavyo mimi bali mapenzi yako yatimizwe"
 
Ogah,
Hii ndiyo hofu yetu kubwa kwa sababu hawa jamaa wanapewa sifa ya kujiuzuru kwao, sioni kidole cha mtu wala kiongozi mmoja isipokuwa mama yetu.
Kumbuka wakati wa Nyerere, Mwinyi na kama sikosei Mrema walijiuzuru lakini walibadilishwa madaraka na Mwinyi kuwa hata rais wa nchi..Kifupi watawala wote toka tupate Uhuru wamekuwa ktk payroll yetu hadi walipoaga dunia ni wachache sana tena basi labda wale waliokiuka maadili ya chama sio nchi nzima....
Msomo wa wengi... Tik..... tak...tik... tak, time will tell.
 
Mkandara

Mimi nakubaliana na wewe kabisa.

Watu watashangaa watakaposikia Waziri wa Maji: Edward Lowassa.
Na baada ya JK kumtangaza atawatuliza wananchi kwa kusema. " ah ah nimeamua kumrudisha Lowassa kwenye wizara hii kwani naamini n wananchi wanaamini utendaji wake kwenye wizara hii ulisaidia kumwondoa CityWater waliokuwa wanataka wananchi wakose maji. Pili nadhani makosa yaliyomkumba kama waziri mkuu yalishirikisha baraza nzima la mawaziri, mimi nikiwa mwenyekiti wao, kwa hiyo mnataka na mimi nijiuzulu jamani. tumpeni nafasi..

Just predicting.
 
Mkandara na Al-Jazeera,

Mwinyi na Natepe waliwahi kujiuzulu nafasi zao za uwaziri kutokana na kashfa zilizozikumbwa wizara zao kutokana na makosa yaliyofanywa na subordinates wao siyo wao wenyewe; yaani walichukua mizigo ya wizara zao ingawa makosa hayakuwa yao binafsi.

Tatizo la Lowasa ni kuwa amejiuzulu kwa sababu ya makosa aliyofanya yeye binafsi, siyo kwa sababu ya makosa yalioyofanywa subordinates wake. Nasubiri nisikie eti amepewa madaraka mengine, ndipo mbingu na dunia zitakapopasuka tuone kati ya Kikwete na wananchi ni nani zaidi.

Kwanza alipoumbuliwa mwaka 1995 na Nyerere, sikutegemea kuwa angerudi madarakani na kupewa madaraka makubwa hivi. Lakini ndiyo hivyo, ila sasa tumeng'aka.
 
..AKIHOJIWA na tido muhando jana ..waziri mkuu mstaafu jaji joseph warioba akiungwa mkono na mwenyekiti wa taasisi ya mwalimu nyerere ..joseph butiku..,warioba ameongelea sakata la richmond..na kusema ripoti haikuwa mbaya ..

hata hivyo warioba ameelezwa kusikitishwa kwake na kitendo kwa utaratibu wa haki kukiukwa kwa ripoti kubwa kama hiyo kuonesha udhaifu wa kutomuhoji MTUHUMIWA MKUU.,amesema hilo kiutaratibu si sawa na kisheria imesababisha haki isionekane kutendeka..alimlaumu mbunge lucas dseleli na mwakyembe kwa hilo..HATA hivyo seleli alijitetea kuwa wao walikuwa wakijiuliza kama wamuite wakaona anaweza kukataa..wakafikiria kumuuliza rais kama wamuite ..pia wakaacha na mwisho wakaamua bora tu wapeleke ripoti bungeni,..hata hivyo warioba aliwaambia kwa kuwa walikuwa hawakumuita..jambo la busara lingeweza kuwa kupeleka ripoti bungeni NA KUTOPENDEKEZA LOLOTE KWA WAZIRI MKUU KWA KUWA YEYE HAKUHOJIWA ..HIVYO BUNGE LINGEFANYA KAZI YA MWISHO YA KUSIKILIZA UTETEZI WAKE ..NA KUAMUA PENDEKEZO AU AZIMIO LA KUTOA KWA RAIS KUHUSU WAZIRI MKUU..ALIMALIZIA KWA KUSEMA KWA KUWA KOSA LA KISHERIA LIMESHAFANYIKA ..IWE FUNZO KWA TUME NYINGINE ZITAKAZOFUATA...KUTOMUHUKUMU MTU BILA KUMSIKILIZA!
 
Mkandara na Al-Jazeera,

Tatizo la Lowasa ni kuwa amejiuzulu kwa sababu ya makosa aliyofanya yeye binafsi, siyo kwa sababu ya makosa yalioyofanywa subordinates wake. Nasubiri nisikie eti amepewa madaraka mengine, ndipo mbingu na dunia zitakapopasuka tuone kati ya Kikwete na wananchi ni nani zaidi.

Kwanza alipoumbuliwa mwaka 1995 na Nyerere, sikutegemea kuwa angerudi madarakani na kupewa madaraka makubwa hivi. Lakini ndiyo hivyo, ila sasa tumeng'aka.

Kichuguu,'
Nasikia hata kule Musoma watu walikuwa wanasherehekea kuondolewa kwa Lowassa.
Watu walijua jeuri na ulafi wake.
 
Phil tunaomba source kwa sababu unachosema haki make sense, kwamba walishauri ripoti iwekwe bungeni bila kupendekeza chochote is hogwash because technically Mwakyembe hakusema Lowassa ajiuzulu (not in so many words anyway) ila alishauri Waziri Mkuu atumie busara zake, ambayo inaacha wazi option ya rebuttal.

Watu wote walio objective, Warioba included according to the above post, na wanaojua misingi ya sheria wanajua kwamba haki inapoonekana kuwa haikutendeka haki haikutendeka, kwamba siyo tu muhimu kwa haki kutendeka, inabidi haki itendeke na pia haki ionekane kutendeka.Tatizo ni kuwa nikisema hilo hapa naonekana Lowassa apologist which is a very narrow minded outlook.

Watu hawawezi ku reconcile facts kwamba one might be appalled by Lowassa's clear corruption and also be dissapointed that the Mwakyembe Committee did not question Lowassa.

There is this euphoria now that everybody should be happy now that Lowassa is out, and nobody should question the tenets of the procedures.I beg to differ on principle.That Lowassa had to go is as they say a "no brainer" but it would have been nicer to see Lowassa denied any reason to say he was not given a chance to clarify things.I understand the logistics may have been challenging for Mwakyembe but we have to set high standards and care about precedents.
 
..AKIHOJIWA na tido muhando jana ..waziri mkuu mstaafu jaji joseph warioba akiungwa mkono na mwenyekiti wa taasisi ya mwalimu nyerere ..joseph butiku..,warioba ameongelea sakata la richmond..na kusema ripoti haikuwa mbaya ..

hata hivyo warioba ameelezwa kusikitishwa kwake na kitendo kwa utaratibu wa haki kukiukwa kwa ripoti kubwa kama hiyo kuonesha udhaifu wa kutomuhoji MTUHUMIWA MKUU.,amesema hilo kiutaratibu si sawa na kisheria imesababisha haki isionekane kutendeka..alimlaumu mbunge lucas dseleli na mwakyembe kwa hilo..HATA hivyo seleli alijitetea kuwa wao walikuwa wakijiuliza kama wamuite wakaona anaweza kukataa..wakafikiria kumuuliza rais kama wamuite ..pia wakaacha na mwisho wakaamua bora tu wapeleke ripoti bungeni,..hata hivyo warioba aliwaambia kwa kuwa walikuwa hawakumuita..jambo la busara lingeweza kuwa kupeleka ripoti bungeni NA KUTOPENDEKEZA LOLOTE KWA WAZIRI MKUU KWA KUWA YEYE HAKUHOJIWA ..HIVYO BUNGE LINGEFANYA KAZI YA MWISHO YA KUSIKILIZA UTETEZI WAKE ..NA KUAMUA PENDEKEZO AU AZIMIO LA KUTOA KWA RAIS KUHUSU WAZIRI MKUU..ALIMALIZIA KWA KUSEMA KWA KUWA KOSA LA KISHERIA LIMESHAFANYIKA ..IWE FUNZO KWA TUME NYINGINE ZITAKAZOFUATA...KUTOMUHUKUMU MTU BILA KUMSIKILIZA!

Naona hii ni mbinu tu ya kumtafutia Lowassa sympathy ili asifuatiliwe tena zaidi ya hapo, ionekane kuwa ameshajiuzulu (licha ya "kuonewa") kwa hiyo inatosha! Au labda ilipangwa kuwa ataachia ngazi, lakini mazingira yajengwe ionekane alionewa, ili hatua zaidi zisifuate, ndipo aweze kujipanga vizuri kuendelea na ulaji katika nafasi alizobaki nazo, na aweze kuendelea kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. Na kwa kuwa Lowassa ile mizengwe aliyoianza imepita, sasa itapinda!
 
..AKIHOJIWA na tido muhando jana ..waziri mkuu mstaafu jaji joseph warioba akiungwa mkono na mwenyekiti wa taasisi ya mwalimu nyerere ..joseph butiku..,warioba ameongelea sakata la richmond..na kusema ripoti haikuwa mbaya ..

hata hivyo warioba ameelezwa kusikitishwa kwake na kitendo kwa utaratibu wa haki kukiukwa kwa ripoti kubwa kama hiyo kuonesha udhaifu wa kutomuhoji MTUHUMIWA MKUU.,amesema hilo kiutaratibu si sawa na kisheria imesababisha haki isionekane kutendeka..alimlaumu mbunge lucas dseleli na mwakyembe kwa hilo..HATA hivyo seleli alijitetea kuwa wao walikuwa wakijiuliza kama wamuite wakaona anaweza kukataa..wakafikiria kumuuliza rais kama wamuite ..pia wakaacha na mwisho wakaamua bora tu wapeleke ripoti bungeni,..hata hivyo warioba aliwaambia kwa kuwa walikuwa hawakumuita..jambo la busara lingeweza kuwa kupeleka ripoti bungeni NA KUTOPENDEKEZA LOLOTE KWA WAZIRI MKUU KWA KUWA YEYE HAKUHOJIWA ..HIVYO BUNGE LINGEFANYA KAZI YA MWISHO YA KUSIKILIZA UTETEZI WAKE ..NA KUAMUA PENDEKEZO AU AZIMIO LA KUTOA KWA RAIS KUHUSU WAZIRI MKUU..ALIMALIZIA KWA KUSEMA KWA KUWA KOSA LA KISHERIA LIMESHAFANYIKA ..IWE FUNZO KWA TUME NYINGINE ZITAKAZOFUATA...KUTOMUHUKUMU MTU BILA KUMSIKILIZA!



Walichozungumzia Warioba na Butiku ni technicallity of the issue. Lakini kuna tuhuma za kutosha katika ripoti hiyo ku-warrant kujiuzulu kwa waziri mkuu. Labda wangempa muda atoe maoni yake kabla ya ripoti kuwasilishwa lakini kilichonishtua ni jinsi watu wizarani walivyokuwa na uwoga wa kuzungumza. Wengine wanapeleka mafaili lakini wanafungua kurasa mbili tatu na si kuonyesha faili zima. Mkono wa Lowassa umeonekana katika kila sura ya kashfa hii.
 
Watu wote walio objective na wanaojua misingi ya sheria wanajua hilo na wamelisema.Tatizo ni kuwa nikisema hilo hapa naonekana Lowassa apologist which is a very narrow minded outlook.

Watu hawawezi ku reconcile facts kwamba one might be appalled by Lowassa's clear corruption and also be dissapointed that the Mwakyembe Committee did not question Lowassa.

There is this euphoria now that everybody should be happy now that Lowassa is out, and nobody should question the tenets of the procedures.I beg to differ on principle.That Lowassa had to go is as they say a "no brainer" but it would have been nicer to see Lowassa denied any reason to say he was not given a chance to clarify things.I understand the logistics may have been challenging for Mwakyembe but we have to set high standards and care about precedents.

Mwakyembe sio mjinga. judge warioba ana act kama tume ni mahakama. no tume imetoa hoja kuwa lowassa kibaka na aangalie cha kufanya. palepale bungeni lowassa angeleta ushaidi kuwa hana makosa na wabunge wangejadili na kufikia uamuzi. kwa nini hakufanya hivyo ///

kulikuwa hamna ulazima wa lowassa kuresign lakini jambo ambalo lowassa hakusema ni kuwa jk alimwita chamwino na kumuambia either u resign or navunja baraza kesho.

buzwagi, epa, richmond zote mzee edo ndani. ahahaha

mama kilango na kina Mwakyembe wanasubiri zifike bungeni mtaona mengi mwaka huu.
 
Walichozungumzia Warioba na Butiku ni technicallity of the issue. Lakini kuna tuhuma za kutosha katika ripoti hiyo ku-warrant kujiuzulu kwa waziri mkuu. Labda wangempa muda atoe maoni yake kabla ya ripoti kuwasilishwa lakini kilichonishtua ni jinsi watu wizarani walivyokuwa na uwoga wa kuzungumza. Wengine wanapeleka mafaili lakini wanafungua kurasa mbili tatu na si kuonyesha faili zima. Mkono wa Lowassa umeonekana katika kila sura ya kashfa hii.

Jasusi technicality hii inahusu "rule of law" na precedents.Ni muhimu watu kama Warioba waseme hivi ili lisirudiwe ama sivyo ndiyo itakuwa default standard.

Nimekuwa nikisema hivi all along.Watu wanabisha.Sasa leo wanasema ni technicality.Guess what, technicalities are what acquit Mafia bosses, kwa hiyo we have to be really careful with technicalities ama sivyo tunawapa kina Lowassa msemo sasa.Kama isingekuwa ukweli kwamba Lowassa hawezi kupush the envelope on his defense, basi angeweza kui-discredit ripoti kichizi kwa sababu hakuitwa kuhojiwa.Uzuri ni kwamba the evidence is overwhelming and Lowassa cannot risk exposing himself anymore.

Hongera sana Warioba kwa kusema hivyo.It takes a person of great integrity to say that hasa kwa sababu Lowassa is down and out now and to narro minded people mtu ukisema hivyo unapewa all sorts of conspiracy theories kuwa unamtete a Lowassa ili asiwe prosecuted.

Lowassa hawezi kuwa prosecuted anyway kwa sababu anajua too much about wrongdoings in the government, including the presidents.
 
Mheshimiwa Lowassa akiwa kiongozi mkuu wa serikali alikuwa na opportunity nyingi kwenda mbele ya kamati na kujieleza maana mamlaka na maamuzi ya mwisho ya Richmond ni ofisi yake. Hii habari ya kuonewa na sijui hakupewa nafasi ni nonsense, na kwanini alimuandikia Spika kuhusu involvement yake in January wakati alijua kamati ilimaliza muda wake December mwakajana. He had all the opportunity kujieleza bungeni. Lowassa ilibidi awajibishwe kwa kusema kamati imetumia udaku na maneno ya mtaani...hapo alidanganya bunge maana Kamati haikutumia hata kielelezo kimoja kutoka kwenye gazeti.
It is ridiculous kusema he wasnt given the opportunity when the comittee had an open door policy. There was no need for him to be interviewed as there was already a paper trail pointing to his involvement, all he had to do as prime minister (who knew there was a trail leading to him) was to speak out in Parliament and explain how he wasnt involved. Period.
 
Mwakyembe sio mjinga. judge warioba ana act kama tume ni mahakama. no tume imetoa hoja kuwa lowassa kibaka na aangalie cha kufanya. palepale bungeni lowassa angeleta ushaidi kuwa hana makosa na wabunge wangejadili na kufikia uamuzi. kwa nini hakufanya hivyo ///

kulikuwa hamna ulazima wa lowassa kuresign lakini jambo ambalo lowassa hakusema ni kuwa jk alimwita chamwino na kumuambia either u resign or navunja baraza kesho.

buzwagi, epa, richmond zote mzee edo ndani. ahahaha

mama kilango na kina Mwakyembe wanasubiri zifike bungeni mtaona mengi mwaka huu.

Moe,

Judge Warioba anachosema ni kuwa regardless whether hii ni tume au mahakama, concept ya kila mtu kupewa nafasi ya kujitetea is so basic and universal kiasi kwamba huwezi kutoa report objective bila kumuhoji mtuhumiwa, period.

The same applies kama tunaongelea high court, parliamentaly commitee au mashtaka ya wanafunzi wawili wa primary kwa mwalimu.
 
Back
Top Bottom