Imetokea loliondo

Imetokea loliondo

Maggid kama mwandishi wa habari anao wajibu huo. na wewe kama msomaji una wajibu wa kufuatilia alichokiandika maggid kina ukweli kiasi gani. wewe usiishie kufikiria kuwa tayari dawa ya magonjwa sugu imepatikana, fikiria zaidi ya hapo, tena kupitia imani yako wewe unayoiamini.Shetani ana vitimbi vingi sana vya kuweza kumtoa mtu katika imani yake, huo ni mfano mdogo katika vitimbi vya shetani. Jibu swali kuna mungu anayebagua watu wake katika kuwaponya? katika dawa zinazojulikana za kienyeji na hata za kitaalamu ni dawa gani ambayo ukihama nayo kutoka sehem moja kwenda sehemu nyingine haiwi dawa? hayo ni masheriti ya nguvu za giza.

.
Mkuu ni imani ipi ya kweli? Maana kila kundi lina ya kwao na yeyote aliekinyume nao ni muongo.
Nyoka wa shaba aliyemtengeneza Usa na kumweka juu ya mlima, ilihamishwa milima mingapi ili kurahisishia watu wasielekee mahali pamoja tu?
Hekalu la Mungu lililokuwepo Yerusalemu kwa nini haikuruhusika kujengwa kila nchi ili watu wasisumbuke sana kusafiri mpaka Yerusalemu?
Masuala ya dini sii jambo la kukurupuka na kuyasemea. Kaa chini fikiri kwanza tena kwa mapana, fanya research ya imani husika halafu ndipo utoke na maoni yako.
.
 
Kwa jinsi Ombwe la uongozi lilivyo sasa hapa nchini, jambo hili sintolishangaa!!

Je, yeye Lukuvi siku alipokwenda kamata Kikombe alitumia usafiri gani?
 
pj kwanini kuwa muongo leo siku ya bwana , vyombo vyote vya usafiri vimezuiliwa mpk april mosi
 
Wakati umefika kwa serikali kuchukua hatua za dhati kuleta nidhamu katika safari za kwa babu ili kupunguza tabu wanazopata wagonjwa huko.
 
kuna watu wanadhani hakuna elimu ya dini.kwamba mambo ya imani yanakuja tu hayahitaji elimu. elimu ya imani ni tofauti na kuamini.naweza nikajua khusu usahihi wa imani ila nisiamini.naweza kujua hatari ya sigara lakini nikavuta.sasa basi zipo shule ambazo hutoa hadi shahada za mambo ya imani. naam wapo wanaopata PhD za Theologia.hawa wanaweza kutusaidia kuhusu mambo ya loliondo. nimesoma kidogo elimu hiyo. nakubali na kuamini kuwa Mungu anaweza kumfanya mtu atende miujiza.mungu anaweza yote. lakini najua pia kuwa Mungu hawezi kujipinga.
ikumbukwe ni mungu ametupa akli na utashi.kwa hiyo ni yeye anayeruhusu wanadamu kavumbua tiba za kihospitali na za kienyeji ni mungu. ufunuo umekamilika na yesu kristo.hakuna ufunuo mpya.ni hivi kama muujiza umetoka kwa mungu kweli, mtokewa huwa na utii na unyenyekevu kwa mamlaka ya kanisa na serikali.mungu hawezi kuzuiwa na binadamu kutenda kazi. so mtokewa husikiliza na mungu huleta wepesi kwa wanaozuia kwa kudhihirisha ukweli kwao wote. mamlaka zilizo halali zinaongozwa na mungu, haziwezi kupinga jambo halali ambalo mungu anataka. hivyo anayedai ametumwa na mungu hakatai anapopigwa marufuku kwa uchunguzi kama alivyofanya babu wa liliondo serikali ilipotaka aache kwa ajili ya uchunguzi.
pia, inahitaji muda wa kutosha, kwani jambo la mungu haliwezi kuwa la muda mfupi tu.ndiyo maana mimi natilia shaka uharaka wa kkkt kuunga mkono jambo hili kwani shetani huweza kufanya vitu kama hivyo, na watu wakishaamini anageuka ili kuleta mkanganyiko kwa waamini.
pia kama ni mungu anahusika kutakuwa na manufaa ya kiroho kwa jamii pana. loliondo hilo halipo ni kupata kikombe na kuondoka.mchungaji kuogopa kukiri kuwa huduma yake ni ya yesu kristo ni very questionable,je yesu anaogopa kuwa akitamkwa watu wasioamini ktk yesu hawatakwenda? na je ikiwa wagonjwa wanapona kweli kwa jina la yesu, waislamu watakataa kwenda ili kukwepa jukumu hilo? je loliondo maono yanahusiana na mungu na si yesu? mchungaji ni wa kkkt. ana imani na yesu je, mungu aliyemtokea amemwambia asimhusishe yesu kwenye tiba yake, au kwamba hiyo ingekuwa kikwazo kwa wagonjwa? na jibu lolote kati ya haya lina usahihi gani kiimani, kibiblia, na kitheologia?
pia kama mungu anahusika kusingekuwa na kukataa kupima kimaabara kuthibitisha uponyaji. kwani hata yesu alipoponya watu kila mara ulifuatia ushahidi wa wazi na maradhi yalikuwa yamepona kabisa. mf. vipofu walikuwa wanaona, wakoma wamekuwa kawaida.loliondo wengi wanadai huwezi kuthibitisha mambo ya imani kwa vipimo vya sayansi, huu ni uchawi.
na kwa nini kkkt imemrudisha mchungaji aliyestaafu kwa umri kwenye huduma. kwani asingeweza kuendelea akiwa mstaafu.au ukiwa na uwezo umri wako unapungua?
kwa hiyo mambo ya loliondo, hadi sasa hayajachunguzwa hata kidogo. kwa hiyo nashauri wanaokwenda huko, wasiache kutumia dawa za hospitali.hakuna cha mungu wala cha mchungaji pale ni ujanja tu na kudanganya watu waliojaa hofu na wasoelimu
 
''Ishara na Miujiza zitaambatana na hao waaminio, nanyi mtaweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya'' kwa ufupi ni kwamba, si babu wala si kwa kikombe bali hata kwa kuweka mikono au kutamka tu! Ukimwi, tb, kisukar na mengne yote yanaondoka, lakin kwake anayeamin! Kwa hyo Mungu wetu si mwanadamu, njia zake ni nyingi sana za kutenda makuu na maajabu juu ya kumponya mwanadamu! Ndugu zangu wana JF, tuache marumbano juu ya kazi ya babu katk kutimiza adhima ya Kimungu. Cha maana ambacho nakiangalia na najiulza mara nyingi ni JE WATU WANAOPONA UGONJWA WAO, WANAMKIRI YESU KUWA NI BWANA NA MWOKOZ WA MAISHA YAO? Je baada ya kupona kutoka ktk masumbufu ya magonjwa WANATUBU na kuendelea kuishi ktk utauwa na utakatifu? Wanampa utukufu nani baada ya uponyaji wao? Ndugu zangu naomba mjue kuwa YEYE IOPONYAYE NAFSI YAKE HUIANGAMIZA, Ni akheri kufa ktk KRISTO kuliko kutafuta tiba ya mwili ili uendelee kutenda dhambi na hatimae ufie ktk dhambi! Mwili huu huisha lakin upo UZIMA tena baada ya kifo. Watu wengi tunakimbia KIFO badala ya kuikimbia JEHANAMU YA MILELE! Mwili nayo nafsi vitakoma lakin ROHO itaishi milele. Ningefurahi na kushangilia iwapo nngeona umati mkubwa, watu kusafiri kutoka sehemu mbalimbali za dunia wakikimbilia kupata UZIMA WA MILELE (kutubu dhambi zao). Laiti km angetokea mtu anayeishi ktk Roho yaan aliekufa akatuambia hal halisi kuhusu huko aliko kukoje, nadhani tungeamua wenyewe! Ndiyo sikatai watu kuendelea kupata uponyaji wa miili yao dhidi ya magonjwa lakin UPONYAJI WA ROHO NI BORA MARA MIA KULIKO KUPONYWA MWILI KWANZA! Kumbukeni YESU anasema na HUO UZIMA UTAKUWA NDAN YENU lakin baada ya ROHO kuuhishwa. Wapendwa endeleeni kwenda kwa babu lakin tukisha toka huko na kupona, kitu cha kwanza kabsa kama ulikuwa hujamwamini YESU kuwa ni BWANA na Mwokozi wa maisha yako kwa kutubu, PLEASE tafuta kanisa la KIROHO utubu kwanza ili uweze kuendelea kuwa mzima kiroho na kimwili, na USITENDE DHAMBI TENA! Naamin ukifanya ivo utaendelea vzr na utapeta mpaka! LAKINI kama hutaokoka, magonjwa yatakuwa juu yako mpaka unaenda kaburini, ni vzr tukafaham kuwa magonjwa ni juu ya hao Wasioamini, haijalishi unasali kanisa gan lenye jina zuri la kiroho lakini kama HUAMINI, jua kuwa bado hujaokoka na magonjwa ni halali yako. Ni vzr pia kufahamu kuwa hizi ndizo zile nyakati za mwisho zilzokwisha kutabiriwa! Watu watasafiri kutoka pande kuu nne za dunia wakimbilia miujiza na uponyaji wa miili yao badala ya kuitafuta KWELI yangu(YESU) matetemeko makubwa, Japan, machafuko ya nchi n.k. NI WAKATI WA KUJIWEKA TAYARI NA SIO WAKATI WA KUSHANGAA SHANGAA TENA.
Kila la kheri!
 
na baaaaaaaaaaado hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania tulivyokuwa watu wa kupelekwa pelekwa, yaani mpaka viongozi wetu wanonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na upeo mdogo it means wanaweza kudanganywa muda wowote na kutuweka watanzania matatizoni, hivi je ikatokea yale maji yaje kuleta sumu kwenye miili yetu si inamaaana tutapoteza watanzania wengi ikiwemo viongozi wetu pia. jamani watanzania tuamke na tusikurupuke, tumemsahau mpaka MUNGU sasa tumamuangalia babu.

hapo kwenye red kuna ukweli mzito.
 
Wa Mbeya na Tarakea vp nao....?
...badomacho yako loliondo! wakishaproof failure watarudi mbeya na tarakea!!
Kwa sababu ni mambo ya kiimani... na wasioamini wanakufa wiki moja na ushei baada ya kunywa dawa! na wengine wanaokiuka miiko ya babu ndio hao tunawaona sukari zinavyopanda kuliko awali na madaktari wako katika kazi ya ziada kuwarudisha katika hali ya kawaida!!

FUNUNU zinaponza watanzania!!!

Kiukweli wacheni babu aendelee na "ujasiriamali" maana unainyanyua wilaya aliyomo inachuma chumo ambalo haikuweza kupata kabla toka kwa wawekezaji na wananchi...kama haitoshi, hifadhi ya taifa nayo inachuma! Mwisho wa siku babu hatokuwepo na wenye maradhi yao watakuwa wanasaka tiba kwingineko kwa aliyetokewa na malaika mkuu!
....ni imani! hata ujamaa tuliambiwa ni imani.. sikumbuki kama upo au umeshapotea!!
 
Shida wanaolijadili suala hili hapa JF wanatumia visima tofauti vya maarifa. Kila mmoja anajaribu kutumia kisima cha maarifa ya imani/ dini yake kuhalalisha au kupinga tiba ya babu. Ndo maana kunakuwa na kutokuelewana kwingi. Mi nadhani hatumtendei haki babu na hata tiba yake. Tutafanya haki kama tutalijadili kwa mtizamo wa imani ya babu: yaani Biblia au imani ya kikristo inasemaje juu ya suala hili.
 
mmnh,mi nilidhani ndo utekelezaji wa yale aliyozungumza yule waziri wa kenya!
 
Hamna tiba pale. Ila nimefurahi kwa kuwa anawabatiza waislamu kwa ridhaa yao wenyewe!!!
 
Kama ni uponyaji wa kweli hakuna wa kupingana naye, ila tunachosikia ni kuwa baadhi baada ya kutoka hali imekuwa mbaya zaidi. Kingine ni kuwa waliambiwa baada ya kikombe wapime tena hospitali kuhakikisha kuwa wamepona, wengi hawafanyi hilo.

Tuwaombee basi iwe tiba ya kweli...
 
na baaaaaaaaaaado hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania tulivyokuwa watu wa kupelekwa pelekwa, yaani mpaka viongozi wetu wanonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na upeo mdogo it means wanaweza kudanganywa muda wowote na kutuweka watanzania matatizoni, hivi je ikatokea yale maji yaje kuleta sumu kwenye miili yetu si inamaaana tutapoteza watanzania wengi ikiwemo viongozi wetu pia. jamani watanzania tuamke na tusikurupuke, tumemsahau mpaka MUNGU sasa tumamuangalia babu. heeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee siamini jamani
...ikiwa hivyo babu atakuwa amesaidia sana! maana tutaanza na kizazi kipya kitakachoogopa ushirikina na vitu visivyotafitiwa!
Itasaidia kuondosha kizazi ambacho hakifikirii kesho yao,
Itasaidia sana kupata wapiga kura makini...
Itasaidia kuondosha wanaofuata mkumbo na kila aina ya fununu....
kwa hilo ntaunga mkono babu aendelee kuwepo!
 
Bado hujaumwa wewe ukaenda hospitalini na kuambiwa umeshindwa kutibika. Siku moja uugue, ushindwe kupona huko unakoamini sana, na Babu awe ameshasitisha kutibu watu. Nahisi uamwomba sana akuhudumie, unacheza na kifo!?
 
Haina haja ya kugombana kuhusu babu wa loliondo, kama ilivyosemwa ni suala la imani, hivyo anayeamini aende kwa babu asiyeamini asiende. Hayo majibu ya serikali hayatasaidia kitu kwa sababu vyovyote watakavyosema, hali itabaki ileile, kwamba wenye imani na dawa hiyo watakwenda kwa babu, wasio na imani na dawa hiyo hawatakwenda.
 
Hamna tiba pale. Ila nimefurahi kwa kuwa anawabatiza waislamu kwa ridhaa yao wenyewe!!!
Mawenzi furaha uliyopata kwasababu uliyoitoa haitakusaidia! Kuna msemo kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe. Kwa misingi hiyo hata watu wote humu duniani waamue kufuata imani sawa na yakwako bado kama wewe matendo yako machafu umati huo hautakua na msaada kwako.

This is the home of great thinkers! Are you real the one?
 
Bado hujaumwa wewe ukaenda hospitalini na kuambiwa umeshindwa kutibika. Siku moja uugue, ushindwe kupona huko unakoamini sana, na Babu awe ameshasitisha kutibu watu. Nahisi uamwomba sana akuhudumie, unacheza na kifo!?

Mfumu mwingine mkali zaidi yuko Mbeya mkuu. Huko foleni bado si kubwa sana.
 
Hamna tiba pale. Ila nimefurahi kwa kuwa anawabatiza waislamu kwa ridhaa yao wenyewe!!!

mpendwa huyu habatizi watu, labda kama anawasilimisha mimi sijui! yeye anawasokomezea midomoni likikombe lake tu basi!
 
Back
Top Bottom