Imetokea loliondo

Imetokea loliondo

Habari za uhakika kutoka moja kati ya Taasisi ya Serikali iliyopo chini ya Wizara ya Afya inayojishughulisha na utafiti wa tiba zimethibitisha kuwa "Dawa ya Babu wa Loliondo" inatibu.

Chanzo cha habari hizi kutoka kwa moja kati ya watafiti wa Taasisi hiyo nyeti ambayo pia inafadhiliwa na Wamarekani ambaye ana shahada ya Uzamifu (Ph.D) na pia ni moja katika ya Wakurugenzi katika Taasisi hiyo zinasema kuwa utafiti wa awali katika maabara kutoka katika Samples za dawa ya "Kikombe Cha Babu" inaonyesha kuwa dawa hiyo ni "ACTIVE" katika kutibu magonjwa yafuatayo:

1. Kisukari - 100% ACTIVE
2. Saratani - 100% ACTIVE
3. Vidonda vya Tumbo - 100% ACTIVE
4. Ukimwi - 99% ACTIVE

Chanzo cha habari kilisema Babu alikubali Serikali kuchukua Samples za dawa hiyo baada ya kuhakikishiwa kuwa hawaendi kuwapa watu vikombe bali ni utafiti. Baada ya kuhakikishiwa Babu alitoa baraka zake.

Hatua hiyo ilikuwa ni muhimu hasa baada ya taarifa za kuthibitika kuonyesha kuwa hata Mkuu wa Kaya alikuwa ni kati ya watu wa Mwanzo kupata kikombe cha Babu mbali ya viongozi wengine wa Juu wa Serikali pamoja na vyama vya Siasa.

Changamoto kubwa kwa sasa ni utafiti juu ya "Madhara" au Side Effects zinazotokana na dawa hiyo na hapo panahitaji umakini. Kama side effects zitakuwa mbaya na Mkuu wa Kaya na viongozi wengine wameshapata kikombe inatubidi kuwa makini katika kuchuja matokeo au findings hizo.

Chanzo hicho pia kilisema Dawa ya Babu iliwahi kufanyiwa utafiti wa Maabara na Wakenya ambao waliipa jina la "KEMRON". Hata hivyo utafiti huo wa Wakenya katika maabara haukuendelea kwa sababu ambazo hazijafahamika.

Akionyesha kuwa Dawa ya Babu inaweza kufaa, alitolea mfano kuwa Dawa ya Chloroquine ambayo iligunduliwa miaka ya 1934 kabla ya hapo ilikuwa inatolewa na "Mtumishi Wa Mungu" ambaye naye alidai pia alionyeshwa na Mungu na ilimpasa mgonjwa yeyote anywee dawa hiyo ya mitishamba akiwa Kanisani. Baadaye mtafiti moja aliichukua dawa hiyo na kuifanyia utafiti na kugundua kuwa ilikuwa inatibu Malaria. Kabla ya hapo wengi waliidharau wakidhani kuwa ilikuwa ni sumu au ina side effects nyingi.

Hata hivyo Serikali inashindwa kwa sasa kutoa taarifa ya awali kwa sababu ya complications za "Hati Miliki" na pia hatma ya muendelezo wa dawa hiyo. Inasemekana kwa kuwa dawa hiyo imechukuliwa mikononi mwa Babu kwa ruhusa yake, hakuna mwenye uwezo wa kisheria wa kufanya chochote bila ridhaa ya Babu.

Huu unaweza kuwa ni Mwanzo wa nuru mpya ya matibabu katika magonjwa haya sugu. Ingawa Babu amekuwa akibezwa na baadhi ya watu, lakini kumekuwa na ushahidi wa kutosha kutoka kwa watumijaii wa dawa yake kuwa inawasaidia na pia imewaponya. Hata hivyo wapo pia Wagonjwa wanaozidiwa njiani na kufariki na pia wapo ambao wamepata Kikombe na kufariki kwa kuwa hali zao zilikuwa mbaya au kutokana na matatizo mengine ya kitabibu.

Ingawa Babu amekuwa akitumia Kikombe maalumu ambacho anadai amepewa na Mungu lakini kwa sasa tafiti za awali za kisayansi na matokeo ya waliopona au kupata nafuu vinaonyesha kuwa dawa yake inatibu.

Ni juu ya Serikali na "Babu wa Loliondo" kukaa chini kwa pamoja na kuangalia ni nini cha kufanya. Wasiwasi mkuu uliopo kwa sasa ni juu ya "Side Effects" za dawa hiyo kama zitakuwepo.

Wadau hii imekaaje? Kazi kwenu!
 
Mkuu ,Mtu ni utu ...

Justfy hii habari!

Habari hii ni ya ukweli na kama ulikua umepanga safari ya kwenda huko basi sitisha mkuu! hata mimi naunga mkono kutokana hali ilikua imeshaanza kuharibika sana na milipuko ya magonjwa yameshaanza.
 
Miss Judy...............

Anyway, am confused.............imani ni kitu kigumu sana.....Nifundishe kuhusu imani Miss Judy tafazali.

babu,

imani ya kikristo sio kitu kigumu ila wengi wanakwepa kui-study na wanatoa hicho kisingizio kuwa ni kitu kigumu. tofauti ya imani ya kikristo na imani nyingine ni kuwa ya kikristo "imefunuliwa" kwa kila mtu na kwa hiyo ukitaka kuijua usome ufunuo wa hiyo imani utajua kila kitu. ufunuo wenyewe unapatikana katika biblia na ni simpe and straight forward. imani nyingine hazijafunuliwa kwa kila mtu, zimefunuliwa kwa wachache tu tena kwa njia zisizo za kawaida na ukitaka kuzijua sharti ukae miguuni kwa hao wachache ujifunze.

tuliza moyo, siku moja nitakufundisha vizuri tu hadi uridhike

yote kwa neema na utukufu wa Mungu
 
Taarifa rasmi kutoka Ikulu na sekta husika leo kuanzia saa moja asubuhi ya tarehe 27/03/2011 imesitisha watu wote kwenda Loliondo kwa Mchungaji mstaafu ndugu Ambilikile Mwasapile kwenda kupata tiba hadi hapo tarehe 2/04/2011 kutokana na miundombinu kuwa mibovu hadi kupelekea wananchi kushindwa kufika eneo husika na wananchi wengine kukwama na hadi kuishia kukaa porini kutokana na miondombinu ya kufika kwa mchungaji huyo kuwa ni kitendawili kutokana na mvua za masika zinazoanza kunyesha katika kanda ya kaskazini. Serikali imefikia uamuzi huo baada ya kupata malalamiko na isitoshe baadhi ya watu kushindwa kufika au kurejea kutoka kule Samunge Loliondo kutokana na hali hiyo, serikali imetamka kua haitaweza kustahimili kuona wananchi wanakwama katikati ya pori nene kutokana na kukwama japokua wananchi wanahitaji huduma hiyo ya mchungaji Mwasapile. Kwahiyo serikali imewaomba wananchi kua na subira hadi hapo tamko rasmi litakapotolewa hiyo tarehe 2 ya mwezi wa nne. Lakini serikali pia imesema kua wale walioko kule Loliondo wabakie wakisubiri huduma lakini hakuna magari au Helikopta kwenda huko.
aliyetangaza ni babu mwenyewe na ameomba serikali iboreshe miundo mbinu na wasimamie wawe wanafika watu 2000 tu kwa siku kijijini samunge
 
Du!
Je ndani ya siku hizi kama 6 tu serikali watafanya kitu gani, hasa kwa upande wa mazingira, ambayo kwa kiasi kikubwa yamedeteriorate huko Samunge?
Au ni show tu kuonyesha kuwa wapo?
 
Kama habari hizi ni za uhakika, basi Serikali isilale, ikae meza moja na Babu na kufanya maafikianoi kwa faida ya Taifa na Wanadamu.

Nasubiri sana kuwasikia akina Kakobe na wengine watareact vipi kwa sasa.
 
Sample size, methodology iliyotumika na imefanyiwa utafiti lini? Inatakiwa matokeo ya dawa hiyo yawe published kwenye recognised journal ili yakubalike.
 
Labda UMBUMBUMBU ni nini? Mkristo yeyote humu JF ambaye ameshawahi kumwona Bwana Yesu, huyo ana haki ya kupinga lolote kuhusu TIBA ya Babu. Lakini sisi tunaoitwa Wakristo kwa kuhubiriwa tu, au kubatizwa na fundishwa tu TUKAAMINI, basi hatuna haki ya kuikataa tiba ya Babu. kama ulibatizwa UKAAMINI, vipi kuhusu hawa walipata kikombe WAKAPONA? Tuache kushikilia dini na kuwa mabingwa wa mistari, huku maisha yetu yakikosa tone moja la ushuhuda wa imani yetu ...huu ni UMBUMBUMBU tu. God Bless!
 
Sample size, methodology iliyotumika na imefanyiwa utafiti lini? Inatakiwa matokeo ya dawa hiyo yawe published kwenye recognised journal ili yakubalike.

Mkuu, umeshaambiwa hizi habari ni za Ki-Inteligensia. Of course hicho ndicho wengi tunachokisubiri. Kama haya ni matokeo ya utafiti wa awali, then something my happen soon . . . .
 
I gues the side effects will be less effective than on the curretive side.

Tumesikia wengi waki confess wamepona, Ila binafsi sijasikia aliyeconfess kupatwa na Madhara.

Ningeshauri serikali iwe strict kidogo kwa hawa wengine wanaojitokeza na kudai wameoteshwa na mama zao.

yaani amini msiamini, Foleni ya Mbeya kama Loliondo, Dogo anadai kaotesha na mama yake aliyekuwa mganga wa kienyeji.

Kuna watu wamepata kikombe cha mbeya na wamepata madhara makubwa sana, The Govt should act soon!!!!

Tumshikuru Mungu kwa kazi yake. Taifa lilikua linaangamia
 
Du!
Je ndani ya siku hizi kama 6 tu serikali watafanya kitu gani, hasa kwa upande wa mazingira, ambayo kwa kiasi kikubwa yamedeteriorate huko Samunge?
Au ni show tu kuonyesha kuwa wapo?

kitumbua kinaanza kuingia mchanga live!

nilijua lazima tu utakuwa sensitive na habari zinazomhusu huyu babu

kazi ipo hapo
 
Kumekuwa na thread nyingi zinazojaribu kuelezea juu ya uwezo wa dawa ya babu kuponyesha magonjwa sugu.lakini hakuna aliwahi kuleta ushuhuda kutoka maabara.
Nimejaribu kuwafuatili wagonjwa ambao walitoka kwa babu na kufika kwenye kituo cha afya ili kujua matokeo ya tiba ya babu.
Jumla ya watu 25 walifika kwenye kituo hiki kwa lengo la kujua kama wamepona au la.kati ya hawa 20 walikua wameathirika na virusi vya ukimwi,watano walikuwa na ugonjwa wa kisukari.
Matokeo:
wagonjwa wote 20 ambao ni HIV positive walionekana bado wako positive.
Wagonjwa wawili wa kisukari walionekana sukari zao kuwa normal au kupungua kulinganisha na mwanzo(4.7mmol/dl and 6.7mmol/dl)
wagonjwa watatu wa kisukari walionekana sukari zao zipo juu kuliko awali(21>27,13>19,7.4>7.6mmol/dl)
wagonjwa wawili kati ya hawa watano wa kisukari walikua na hypertension na wote walionekana pressure zao ziko juu kuliko awali.kwa ufupi haya ndio matokeo ya uchunguzi nilioufanya kwenye kituo hiki cha afya.

Vipimo vilifanywa kwa kutumia SD BIOLINE,GLUCOMETER pamoja na SYPHGMOMANOMETER.
Conclusion:tunahitaji uchunguzi wa kina hasa kwa wagonjwa wanaohudhuria kliniki lakini wakaamua kwend kwa babu,sampuli iliyotumika ni ndogo mno kuweza kueleza iwapo dawa ya babu inatibu au la.hata hivyo ni muhimu kwa wagonjwa kuendelea kutumia tiba zao za hospitali kwani mpaka sasa hakuna ushahidi wa kuridhisha wa kuikubali au kuikataa dawa ya babu.

Shukrani:kwa wagonjwa wote waliokubali kuonyesha siri juu ya magonjwa yao na pia shukrani nyingi zikiendee hiki kituo cha afya kwa kuweka kumbukumbu ya wagonjwa wanaotoka loliondo.

Nawasilisha...
 
Well done Jackbauer! Matokeo yako yanaonyesha before and after the treatment.

Ongezea sample size na hapo utaweza kujua statistically kama kuna improvement yo yote au la.
 
Kuna kazi kubwa saana Tanzania, hapa JF wachangiaji ndio hao wanaonekana kuwa wameenda shule. Hao ambao hawajasoma inakuwaje? Tunalazimisha vitu kutokana na hisia na imani zetu. Hata hiyo chroroquine iliyoitaja nayo pia ilikuja kugundulika kuwa na madhara. Wanaoumwa wana haki ya kuhangaika na tiba kwa kuwa kila ambacho hushauriwa kuwa kitawaponya wangependa kujaribu, lakini kwa hili la kuacha tiba ambazo zilishachunguzwa na kujikita kwenye tiba isiyo na uchunguzi ni kuweka maisha hatarini.
Binafsi ninawasihi wale wanaoumwa waendelea kutumia dawa za kitaalamu kama hii ya babu inaponya wasubiri majibu ya tafiti kisha ndio wataamua la kufanya. Wasiache dozi, Taifa bado linawahitaji.
 
Nimepokea ujumbe kutoka ccm unasema 'TUMEANZA KUTIMIZA ILANI ZA CHAMA CHETU TUMEANZIA SEKTA YA AFYA, NADHANI MNAJIONEA WENYEWE HUKO LOLIONDO'
 
Taarifa rasmi kutoka Ikulu na sekta husika leo kuanzia saa moja asubuhi ya tarehe 27/03/2011 imesitisha watu wote kwenda Loliondo kwa Mchungaji mstaafu ndugu Ambilikile Mwasapile kwenda kupata tiba hadi hapo tarehe 2/04/2011 kutokana na miundombinu kuwa mibovu hadi kupelekea wananchi kushindwa kufika eneo husika na wananchi wengine kukwama na hadi kuishia kukaa porini kutokana na miondombinu ya kufika kwa mchungaji huyo kuwa ni kitendawili kutokana na mvua za masika zinazoanza kunyesha katika kanda ya kaskazini. Serikali imefikia uamuzi huo baada ya kupata malalamiko na isitoshe baadhi ya watu kushindwa kufika au kurejea kutoka kule Samunge Loliondo kutokana na hali hiyo, serikali imetamka kua haitaweza kustahimili kuona wananchi wanakwama katikati ya pori nene kutokana na kukwama japokua wananchi wanahitaji huduma hiyo ya mchungaji Mwasapile. Kwahiyo serikali imewaomba wananchi kua na subira hadi hapo tamko rasmi litakapotolewa hiyo tarehe 2 ya mwezi wa nne. Lakini serikali pia imesema kua wale walioko kule Loliondo wabakie wakisubiri huduma lakini hakuna magari au Helikopta kwenda huko.

Kwa hiyo kwa hizo siku chache miundo mbinu hiyo itaboreshwa na kuwawezesha Wabongo kwenda kupata maji ya uzima bila adha zozote zile zitakazosababishwa na miundo mbinu mibovu! USANII MTUPU!
 
Back
Top Bottom