Imetokea loliondo

Imetokea loliondo

Heshima yako Maggid, Hili suala ni gumu sana kuna interest za watu wazito na linasemekana hili jambo lina mkono wa kifreemasons ndio maana babu anataka mia tano ile namba ina maana kubwa! Hili la dola moja nimelisikia hivi punde limenifanya nianze kuamini kuwa fremasons wanamkono ukiitazama ile dola moja utaona alama zao iangalie kwa makini kuna picha ya piramid juu yake kuna kama jicho! Usihadaike na kuumiza kichwa kuhusu maswala ya exchange rates kwani Mungu wa Isaya na Yakobo ni mwenye mapenzi na wanaadamu hawezi kuwapeleka sehemu inayowadhalilisha na kuishi maisha ya wanyama! Si tunasikia watu wanajisaidia porini na wanateseka kisawasawa kungoja "kikombe"? Upo wapi utu hapo? Kuna wengine humu JF wana miradi yao ya kubeba wanaoenda Loliondo kwa babu kwahiyo tegemea upinzani mkubwa wa hoja zako.

Naona watanzania siku hizi mmeingiliwa na Mambo ya kusema Freemasonry, kitu kidogo Freemasons, fulani kanya -Freemasons, Mbwa kakojoa -Freemasons, mwizi kaiba- Freemasons, babu na kikombe chake -Freemasons, Shekhe Yahya atabiri Kikwete kuwa Fisadi- Freemasons, tanzania ni maskini-Freemasons. Kila kitu mmekiweka kwenye Freemasons. Am sick and tired of this Freemasons songs, its like ccm sing Amani na utulivu
 
Ni kweli hata mimi nilikuwa na mgonjwa wangu aende huko kwa helicopter inayomilikiwa na kampuni ya Firelight ila nimepokea e-mail kwamba wamezuiwa kutua("Unfortunately have just had some bad news last night. TCAA have just informed all air transport to Loliondo that it must stop until further notice")
 
Maggid umeishiwa mambo yakuandika?? kila kukicha unamwandama Babu wa Loliondo na dawa yake, nini shida??.

Acha wanaoamini wakapate tiba, unachonga kwa vile huumwi,ungekuwa una hayo magonjwa sugu sidhani kama ungemkejeli Babu kiasi hiki.

Tuheshimu maamuzi na huduma za watu wengine, siku Maggid ukiwa na kansa au kisukari sugu ndio utaelewa kwa nini watu wanaenda kwa Babu Loliondo.
 
maggid,

hapa utatolewa macho, babu hapa jamvini siyo simple kama unavyofikiria. mbali na imani potofu, kudanganyika na ubishi/ignorance nk baadhi ya watu hapa wana maslahi ya kiuchumi kutokana na hii biashara ya kikombe,

usifikiri ni imani peke yake, wapo wanaotengeneza cash kila siku!

so watch out brother

you have been warned!
 
:juggle::juggle::juggle::juggle::juggle::juggle::juggle:!!!! dola.jpg
 
maggid,

hapa utatolewa macho, babu hapa jamvini siyo simple kama unavyofikiria. mbali na imani potofu, kudanganyika na ubishi/ignorance nk baadhi ya watu hapa wana maslahi ya kiuchumi kutokana na hii biashara ya kikombe,

usifikiri ni imani peke yake, wapo wanaotengeneza cash kila siku!

so watch out brother

you have been warned!

Miss Judy...............

Anyway, am confused.............imani ni kitu kigumu sana.....Nifundishe kuhusu imani Miss Judy tafazali.
 
Ndugu Zangu,

JANA usiku muda mfupi kabla ya taarifa ya habari, TBC1, kulikuwa na mahojiano ya mwandishi wa TBC na Babu wa Loliondo.

Kati ya aliyoyaongea, Babu anasema, kuwa Mungu ndiye aliyepanga bei ya tiba ya kikombe iwe shilingi mia tano. Kuwa alimwonyesha mia tano! Na Mungu akamwambia wageni walipe dola moja!

Tafsiri yangu;

Pamoja na kuwa mwandishi hakumuuliza Babu maswali magumu, bado Babu wa Loliondo hakunisogeza hata hatua moja kutoka kwenye msimamo wangu. Kuwa tiba ya Babu ni Abrakadabra.

Tujiulize swali moja tu; hivi Mungu huyo ni Mungu gani anayebagua waja wake. Kuwa wengine walipe mia tano na wengine dola moja?

Jamani, hivi Mungu huyu wa Babu wa Loliondo naye anafuatilia exchange rate kila siku? Itakuwaje basi, shilingi ikipanda au kushuka thamani dhidi ya dola ya Marekani? Babu itabidi aoteshwe haraka ndoto nyingine ili abadilishe bei ya kikombe!

Na kwenye taarifa ya habari iliyofuatia ikaripotiwa, kuwa Serikali imeshindwa kutoa tamko jana juu ya tiba ya Babu kwa vile Babu amesema kamati iliyoundwa iende kwanza Loliondo!

”Mnajua tena mambo haya ya imani!” Alitamka mwanakamati mmoja kwenye TBC1. Na leo imeandikwa kwenye gazeti moja, kuwa Serikali itatoa tamko leo juu ya tiba ya ' Babu'.

Naam. Tamko hili liharakishwe kutolewa kabla ' Babu' hajaoteshwa ndoto, kuwa ' Tamko Lisitishwe hadi itakapotamkwa tena!'. Na nani? Fikiri mwenyewe.

Si ilipata kusemwa, kuwa kila kukicha, kuna kioja kinazuka kutoka Afrika!


Maggid
Iringa,
Jumapili, Machi 27, 2011

Hata mimi niko PESMISTIC na tiba ya babu. Na, kama alitamka habari ya Dola kwa watu wa nje, tamko hilo linaonyesha kuwa hana Roho wa Mungu wa Kweli. Muda utajasema kama kweli babu ana roho wa Mungu. Wahubiri wote wamekuwa wakitembea, wakisafiri, iweje yeye ni pale pale? Kwa nini awape mateso watu hivyo?Why 500?

Kwa nini isiwe kiasi chochote? Hii inanipa taabu kabisa hadi nimeshindwa kumwezesha ndg yangu mmoja pesa ya kwenda huko kwani SIPAAMINI.
 
Naona watanzania siku hizi mmeingiliwa na Mambo ya kusema Freemasonry, kitu kidogo Freemasons, fulani kanya -Freemasons, Mbwa kakojoa -Freemasons, mwizi kaiba- Freemasons, babu na kikombe chake -Freemasons, Shekhe Yahya atabiri Kikwete kuwa Fisadi- Freemasons, tanzania ni maskini-Freemasons. Kila kitu mmekiweka kwenye Freemasons. Am sick and tired of this Freemasons songs, its like ccm sing Amani na utulivu

Unaongea kama Freemasons,lol,just kidding;point well taken - tuna Freemasonicphobia!
 
na baaaaaaaaaaado hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania tulivyokuwa watu wa kupelekwa pelekwa, yaani mpaka viongozi wetu wanonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na upeo mdogo it means wanaweza kudanganywa muda wowote na kutuweka watanzania matatizoni, hivi je ikatokea yale maji yaje kuleta sumu kwenye miili yetu si inamaaana tutapoteza watanzania wengi ikiwemo viongozi wetu pia. jamani watanzania tuamke na tusikurupuke, tumemsahau mpaka MUNGU sasa tumamuangalia babu. heeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee siamini jamani
 
Maggid anakataa kuwa babu kaoteshwa na Mungu kwa kuwa Biblia inasema "Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake Yohana 5:37" Maggid anathibitisha kuwa Biblia inasema kuwa sisi pamoja na "babu" hatujapata kamwe kusikia sauti ya Mungu wala kuuona uso wake!Nadhani babu ana zaidi ya majini Maimuna Tafakari!

ndo hivi makamba alisoma kumbe hakuelewa kama wewe.
 
Ndugu Zangu,

Hata kama Watanzania wote watahamia kwa ' Babu' wa Loliondo, mimi nitabaki kijijini kwetu Nyeregete, alikozikwa babu yangu. Na itabaki kuwa hivyo, labda waje kunibeba na karandinga la jeshi.

Maggid,
Iringa.
 
Maggid, itakuwa vizuri kwa waandishii wafatilie hali halisi ya mahospitali ili muweze kulinganisha na kabla maswala ya babu yalivyokuwa. Kuna habari za kuaminika kuwa KCMC imefurika watu wanaotoka kupata kikombe cha babu! Hospital za Arusha na Moshi yaani KCMC na Mount Meru kumekuwa na taarifa za kupokea maiti zilizokwisha kuharibika. Waandishi waisaidie jamii kujua hii hali wasitumie jina la babu kujipatia mia tano na wao kwa kuuza magazeti tu!

Utakuwa Mwongo sana kwa Nipo KCMC na hali halisi si hivyo kama unavyosema! most of hao wanaokufa wamekwenda wakiwa wamezidiwa sana wengine wakiwa wametoroshwa hospitalini na ndugu zao in a critical condition (pia madoctor nao wameenda kupata kikombe) cha msingi sana hapa kama hukubaliani na babu waache wanaokwenda na imani zao hulazimishwi! na kucritisize ishu za babu naona mnapoteza muda tu waulize wagonjwa au nenda kawaambie stori zako wagonjwa wanaosubiri kwenda kwa babu uone shughuli utakayoipata..
 
Sitak kuamin kwamba maggid uwezo wa kufikiri ni mdogo. BABU ameoteshwa mia tano kwa kuwa ni hela ya Kitanzania ambayo kila mtz anaiweza kuipata awe maskin au tajiri. na khs 1USD hiyo ni currency maarufu dunian kote na inajulikana kila mahali. Tatizo lako ulitaka BABU aoteshwe Currency za kutoka UARABUNI ndo ungerizika na kuamin kama hutak kuamin kaa kimya waache wenye iman wakatibiwe, SHEIKH YAHYA YUPO KUWATIBU WATU KAMA NINYI BABU HANA MAJIN MAIMUNA.

Hehehehe! .. hapo kwenye brown nafkiri ni ViceVersa ... mawazo yako ni ya walewale ushikirina mtupu

DAH!! U TOTALY POOR n LITTLE KNOWLEDGE IN TORTOLOGY POLE SANA BIBLIA HAISOMWI KWA ANDIKO MOJA MOJA KAMA UFANYAVYO WEWE NENDA KASOME WAKORINTHO UONE MUNGU ANAVYOONYESHA UKWELI WA NDOTO ZA MABABU SIKU ZA MWISHO.

waeva.. did u mean Tautology..?!!

Mtu mzima mwandishi wa habari anachallenge babu kuchagi mia tano na dola I . Hivi ww unataka aishi vipi na hao wanaofanyakazi nae wale mawe? Kwani si sera kuwa wageni walipie huduma in dollers.? Hata huko misikitini kwako mashehe huomba sadaka maana hawafanyi kazi nyingine. I hate such poor way of writting to publoc. Crazzy

kama jina lako linavyothibitisha (Mfamaji)+ you sound jealous
 
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama ufisadi au ujanjaujanja waliokunao viongozi wetu kuna jambo la kihuni linalotokea wakati wa kunywa kikombe cha babu.
Kuna taarifa ya kuwa viongozi kabla ya kufika loliondo huwa wanatuma taarifa inayoambatana na list ya majina ya ndugu zao ambao hawatakaa foleni ya kusubiri kikombe.
Yaani fisadi ni fisadi tu hata kwenye mambo ya ki-imani!?!
 
Nakuunga mkono Maggid! Hiyo si dawa wala miujiza. Ukweli utajulikana muda si mrefu.

Tutakuja kukimbiana hapa jamvini.
 
Maggid,

Utakufa kwa wivu, husuda na kijiba cha roho. Ulianza na CHADEMA yakakushinda, umevagaa Babu pia...yatakushinda.

Mwaka huu lazima ujinyonge tu.

By the way kwa nini usiandike historia ya chama chetu kikkongwe na biograph ya mtabiri wetu mkuu na mtoa ulinzi usioonekana kwa kingozi wetu mkuu?

Bora useme wewe maana nikisema mimi nitatukana
 
Ndugu Zangu,

Hata kama Watanzania wote watahamia kwa ' Babu' wa Loliondo, mimi nitabaki kijijini kwetu Nyeregete, alikozikwa babu yangu. Na itabaki kuwa hivyo, labda waje kunibeba na karandinga la jeshi.

Maggid,
Iringa.

So why bother mkuu??

why dont you shut up! and do your things!

Hii ni imani na mpaka sasa umeishavuna aibu nyingi tu, you cvan not question Imani, after all wewe ni mwislamu na yule ni mkristo hauoni kwa akili ndogo kabisa mko dunia mbili tofauti?

Leo hii mtu akisikia mtume alioa wake 22, aliua, akaoa na kulala na mtoto wa miaka 9, alilala na wanawake wenye edhi, alichukua Quran toka kwenye pango, n.k haviingii akilini! Yet we have mosques kila kona na tunaenda misikitini na kurudi kwetu,...maisha yanaendelea...

Issues za Imani ni nzito sana na next time try your level best kukaa mbali navyo maana utapata aibu, nilifikiri ulipopost ile ya kwanza nilijua umepata somo, unarudia tena??

Kuwa najua mabaya ua islamu then niseme ili iwe nini?? eti babu hajaku-convince! Sheikh yahya nimsemsikia kwa masikio yangu akisema mimi naenda nyie kufeni!!!

Ni swala la mtu na ndio maana wengi wako kule na wa dini na mataifa mbalimbali HATA HIZO ARV kuna wengine hawazitaki, kuna wengine hawatumii panadol bali hedex...list of preferances goes on

sasa wewe kwa nini USEME?? ili iwe nini??
 
na baaaaaaaaaaado hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania tulivyokuwa watu wa kupelekwa pelekwa, yaani mpaka viongozi wetu wanonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na upeo mdogo it means wanaweza kudanganywa muda wowote na kutuweka watanzania matatizoni, hivi je ikatokea yale maji yaje kuleta sumu kwenye miili yetu si inamaaana tutapoteza watanzania wengi ikiwemo viongozi wetu pia. jamani watanzania tuamke na tusikurupuke, tumemsahau mpaka MUNGU sasa tumamuangalia babu. heeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee siamini jamani

we kipanya masoud yule sunrise au? maana amani misana yuko na mchumchu wetu scola studio
 
uwongo tu kikombe kikombee,,,,,bONGO means akiliii,,ujanjaa,huu ndio ujanja wa kutafuta pesa,,,Bongo hakuna kaziii,watu wana kila njia ya kutafuta pesa,serikali imeshindwa kumzibiti huyu mtu kwa sababu wameshaona ameshakubalika kwa jamii na dawa yake tayari ipo sokonii,,,

Hapa kuna kazi kubwa,siasa mbovu nchini iliyongia,na kama serikali wataindilia itachafua amani,kwanza hospitali hakuna dawa,watu hawana uwezooo,na kwa vile watu wame believe kuwa kikombe cha babu ni tima leo serikali wakamuondoee au waharibu ile biashara ,,naona tanzania haitokalika,,,ikifikia wabunge ,,na manaibu kuenda kupata kikombee ujue hapo kuna ulakiniii,,,na hii yote ni believe,,,

Nakumbuka utotoni kwangu alikuwa rafiki yangu mkubwa sana kiumri zaidi ya miaka 13,,,basi kila week akinipitia home kunisalimia,,,siku moja alikuja home alikuwa akiwashwa na nyayo zake,,,zinamsumbua,basi huwezi amini nilimfanyia mambo kwa kutumia majani tu,ya aina mbilii,,nimejua mwenyewe vya kufanya nikampaka miguuni kwake,,na aliniuliza dawa nikamwambia ndiiooo, kumbe ulikuwa usanii tu utoto wanguu,,,

Huwezi amini baada ya muda mchache alijisikia fresh na muasho ulipungua kiasi kukubwa sana hata kiatu aliweza kuvaa tena,na alitaka haya majani nimpatia ili akifika kwake akihitaji ajipake,,baada ya siku mbili akanipitia home na kuniuliza ile dawa kweli,,nimemkomalia macho ndioo,ananiambia imenifaa bwana ,,,sana shukuraniii,,,

kwa kweli nikasema kuwa kitu ni believe,the way yu believe is the way yu succesed,,,,kwa hioo huuooo ni usanii tu,,,
 
Ukimuona mtu na akili zake anaenda kwa babu kutafuta uzima, ujue kahangaika sana muda mrefu sasa hanabudi kuenda kujaribu ili apate uponyaji ambao kautafuta bilamafanikio kwa muda mrefu. Mtu kama maggid na wapambe wake, hawajapatwa na matatizo km ya hiv, kifua kikuu, saratani, na kisukari wakaonja adha yake.pemgine km wangeshapata wangetushuhudia kuwa wao japokuwa wanaumwa hawawezi kwenda ila wanasubiri kuendelea na mateso yao hadi wafe.... Pengine hapo wanganza nishawishi nami kwa hoja zao... Lakini kupayuka tu huku wengine wakipata taaaaaaabu kiafya haiingii akilini mwangu!!!



Kaka hicho ni kipimo kidogo sana cha imani kwako. Kwa wakristo kama umetegeka kiurahisi mtego wa nguvu za giza za babu je wa mnyama namba 666 utauweza? na kwa wale waislam waliosoma dini yao wanajua habari masihi-dajari je kama umeweza kuasi maamlisho ya dini yako je visa vya huyo jamaa utaviweza? maana yeye hatosema kuwa kaoteshwa atasema yeye ndiye mungu na atakuwa na uwezo mkubwa sana wa kufanya miujiza ili umuamini kama yeye ni mungu.
 
Back
Top Bottom