Imetokea loliondo

Imetokea loliondo

jamani mambo ya ngoso tumuachie ngoso, ukweli wa kikombe anao babu, cha msingi kila mtu kaja hapa duniani kwa muda wake, imani alazimishwi mtu, anayeamini kuwa atapona akinywa kikombe akanywe, asioamini basi akae na matatizo yake mpaka hapo atakapooteshwa mwenyewe kuwa dawa ya taizo lako ni hii. kwa upande wangu nipo katikati siwezi sema siamini au naamini.
 
Hata deci ilianza hivihivi. Staili ileile na watu walewale. Tusubiri, time will tell.
 
Taarifa rasmi kutoka Ikulu na sekta husika leo kuanzia saa moja asubuhi ya tarehe 27/03/2011 imesitisha watu wote kwenda Loliondo kwa Mchungaji mstaafu ndugu Ambilikile Mwasapile kwenda kupata tiba hadi hapo tarehe 2/04/2011 kutokana na miundombinu kuwa mibovu hadi kupelekea wananchi kushindwa kufika eneo husika na wananchi wengine kukwama na hadi kuishia kukaa porini kutokana na miondombinu ya kufika kwa mchungaji huyo kuwa ni kitendawili kutokana na mvua za masika zinazoanza kunyesha katika kanda ya kaskazini. Serikali imefikia uamuzi huo baada ya kupata malalamiko na isitoshe baadhi ya watu kushindwa kufika au kurejea kutoka kule Samunge Loliondo kutokana na hali hiyo, serikali imetamka kua haitaweza kustahimili kuona wananchi wanakwama katikati ya pori nene kutokana na kukwama japokua wananchi wanahitaji huduma hiyo ya mchungaji Mwasapile. Kwahiyo serikali imewaomba wananchi kua na subira hadi hapo tamko rasmi litakapotolewa hiyo tarehe 2 ya mwezi wa nne. Lakini serikali pia imesema kua wale walioko kule Loliondo wabakie wakisubiri huduma lakini hakuna magari au Helikopta kwenda huko.
 
Hivi huyu Maggid ndo mwenye blog na alianzisha gazeti akatoa matoleo mawili tu?
Ndiyo maana, kumbe ana mawazo mafupi hivi. Nafikiri utakuwa umetumia nguvu nyingi sana mpaka kufika hapo ulipo kielimu na kimaisha.
 
mbona huelewek kama mufti wako uko upande upi ambao ni sahihi kwako.

only great thinkers wanaweza kunielewa,
an ordinary person like you ni pasua kichwa tu,
nimekueleza ishu ya babu ni ya kiimani zaidi,anayedhan hiyo ndio tiba kwa yanayomsibu na aende tu,apate hicho kikombe, na wale wanaofikiri hiyo ishu haiingii akilini waendelee na mambo yao,
usitake mtu asiamini /aamini kama usivyoamini/unavyoamini wewe, hii ni ishu ya kiimani zaidi.
Yawezekana ni ngumu kwako kunielewa,
usiumize kichwa cna!,
 
No Comments: Kwani TAnzania wakuu kwasasa Ipoje maana tunasikia kwenye media tu sisi tupo nje tupeni ukweli halisi
 
jamani mambo ya ngoso tumuachie ngoso, ukweli wa kikombe anao babu, cha msingi kila mtu kaja hapa duniani kwa muda wake, imani alazimishwi mtu, anayeamini kuwa atapona akinywa kikombe akanywe, asioamini basi akae na matatizo yake mpaka hapo atakapooteshwa mwenyewe kuwa dawa ya taizo lako ni hii. kwa upande wangu nipo katikati siwezi sema siamini au naamini.

aah bana, ngoswe hapo
 
Ndugu Zangu,

JANA usiku muda mfupi kabla ya taarifa ya habari, TBC1, kulikuwa na mahojiano ya mwandishi wa TBC na Babu wa Loliondo.

Kati ya aliyoyaongea, Babu anasema, kuwa Mungu ndiye aliyepanga bei ya tiba ya kikombe iwe shilingi mia tano. Kuwa alimwonyesha mia tano! Na Mungu akamwambia wageni walipe dola moja!

Tafsiri yangu;

Pamoja na kuwa mwandishi hakumuuliza Babu maswali magumu, bado Babu wa Loliondo hakunisogeza hata hatua moja kutoka kwenye msimamo wangu. Kuwa tiba ya Babu ni Abrakadabra.

Tujiulize swali moja tu; hivi Mungu huyo ni Mungu gani anayebagua waja wake. Kuwa wengine walipe mia tano na wengine dola moja?

Jamani, hivi Mungu huyu wa Babu wa Loliondo naye anafuatilia exchange rate kila siku? Itakuwaje basi, shilingi ikipanda au kushuka thamani dhidi ya dola ya Marekani? Babu itabidi aoteshwe haraka ndoto nyingine ili abadilishe bei ya kikombe!

Na kwenye taarifa ya habari iliyofuatia ikaripotiwa, kuwa Serikali imeshindwa kutoa tamko jana juu ya tiba ya Babu kwa vile Babu amesema kamati iliyoundwa iende kwanza Loliondo!

”Mnajua tena mambo haya ya imani!” Alitamka mwanakamati mmoja kwenye TBC1. Na leo imeandikwa kwenye gazeti moja, kuwa Serikali itatoa tamko leo juu ya tiba ya ' Babu'.

Naam. Tamko hili liharakishwe kutolewa kabla ' Babu' hajaoteshwa ndoto, kuwa ' Tamko Lisitishwe hadi itakapotamkwa tena!'. Na nani? Fikiri mwenyewe.

Si ilipata kusemwa, kuwa kila kukicha, kuna kioja kinazuka kutoka Afrika!


Maggid
Iringa,
Jumapili, Machi 27, 2011

leo kidooogo nimekusoma bro. lakini pua zangu zinanusa harufu kwamba kikombe cha babu ni mradi waaaa............... mradi waaaaaaaaaaaaaaa ...... malizia mwenyewe kabla haijafika 2015.
 
Maggid, anasema ukweli. kanisa la kkkt linajua nini maana ya mtu kudai ameoteshwa na mungu.kitheolojia, ina maana gani mtu anaposema amemuona mungu? nimewahi kuanzisha mada hapa ambayo ilishambuliwa pia kuwa jambo hili litaaibisha kkkt.tusubiri tuone. kuna interrogation yoyote imefanyika kuhakiki madai ya babu kuonana na mungu? hakuna. hivyo jambo analodai halina misingi yoyota ya kibiblia, kitheologia, wala kiimani.ni lazima kuchunguza izo roho, maana si zote hutoka kwa mungu.na kuna objective criteria kujudge kama madai ya mtu kuwasiliana na divine beings ni sahihi. hakuna hata mija ambalo limefanywa kwa babu wa loliondo. kuna watakaosema mara moja, hakuna vitu hivyo kupima jielimisheni kwanza kisha mpinge.kuna elimu ya biblia, na hata masuala ya imani zipo elimu zinazoyahusu na mamlaka za kaya regulate. hongera maggid kuwa kati ya watanzania wachache wanaojiuliza kabla ya kutembea gizani
 
Mkuu hii ndio ripoti tunayosubiri toka serekalini leo?

na

Vigogo si watakuwa wamenyimwa haki yao ya kutibiwa ndani ya nchi...sasa waende nje?
 
kama imani yako haba basi hata aje Yesu na Muhamad SAW we utabaki hivyohivyo tu...
 
Kwa nini wanaompinga babu wengi ama ni walokole au wana imani ya dini tofauti na ukrito? Na kwa nini inaonekana kama roho inawauma sana kuhusu kazi ya babu kuliko kujenga hoja zenye mantiki?

Kwa nini hawahoji watu wanaojiita manabii na maaskofu wanaoanzisha makanisa ya kilokole kwa kutumia ushirikina na kuibia watu ili wajitajirishe?
 
Bora vigogo wazuiwe ili hao wanyonge wapate vikombe vyao kwa unafuu zaidi
 
Back
Top Bottom