Kwani ww Magid usipobadli msimamo wako kuhusu Babu nani anajali? Who do u think you are btw. It seems unajikweza kwamba una attention saaana kumbe we
only read your trash to laugh out loudly.
Nimekuwa nikisoma criticisms zako kuhusu huyu mzee nikashangaa . For your info. there is no more news from Babu because everybody has succumbed
to his cup including scientist. Halafu eti nawe uko mbele against udini. Funny.
Tumeona wengine "wakitumwa" na Dokta wa kanono Silaa, kwenda kujiangamiza kwa kuwa watapatiwa Simenti ya elfu tano na maisha bora kwa kufumba na kufumbuwa.
Hata hawatazami huyo anaewaambia ana maisha yepi? Na yana ubora upi?
1) Mwenyekiti anadaiwa, kapata mwanya kidogo kaanza kuchota mali ya umma hataki kuirudisha, jee akipewa nchi? Hatuyaoni haya.
2) Mgombea aliebobea (Daktari) mwenye kuzijuwa sheria za kanoni anaenda kinyume kabisa na hizo sheria: a) kwa kuoa akiwa padiri b) kwa kuongeza mke c) ambae hajaachika kwa mume wa kwanza na anaishi nae kama kimada kwa sheria za kanoni. Hatuyaoni haya.
Hivi hawa wakipewa waendeshe nchi, itakuwaje? Jibu: chota mali za umma na kula sheria za "kanono".
Hivyo ndivyo tulivyo. "Wajinga ndio waliwao".
"Reality" huwa hawaioni, hawaisikii wala hawataki kuiona wala kuisikia. Inashangaza kwa wenye kuona.
je na vipi wanaokufa kwa maelfu baada ya kunywa hiko kikombe cha loliondo? Mungu akiponya kaponya!! Tafuteni kitabu kinaitwa PAMBANO KUU
je na vipi wanaokufa kwa maelfu baada ya kunywa hiko kikombe cha loliondo? Mungu akiponya kaponya!! Tafuteni kitabu kinaitwa PAMBANO KUU
kweli slaa anawapa jambajamba sana ccm... Kila kitu kinachozungumziwa hapa nchini sasa anatajwa slaa,,, huyu ndie mpinzani wa kweli,,, hakuna mfano
Heshima yako Maggid, Hili suala ni gumu sana kuna interest za watu wazito na linasemekana hili jambo lina mkono wa kifreemasons ndio maana babu anataka mia tano ile namba ina maana kubwa! Hili la dola moja nimelisikia hivi punde limenifanya nianze kuamini kuwa fremasons wanamkono ukiitazama ile dola moja utaona alama zao iangalie kwa makini kuna picha ya piramid juu yake kuna kama jicho! Usihadaike na kuumiza kichwa kuhusu maswala ya exchange rates kwani Mungu wa Isaya na Yakobo ni mwenye mapenzi na wanaadamu hawezi kuwapeleka sehemu inayowadhalilisha na kuishi maisha ya wanyama! Si tunasikia watu wanajisaidia porini na wanateseka kisawasawa kungoja "kikombe"? Upo wapi utu hapo? Kuna wengine humu JF wana miradi yao ya kubeba wanaoenda Loliondo kwa babu kwahiyo tegemea upinzani mkubwa wa hoja zako.
Ndugu Zangu,
JANA usiku muda mfupi kabla ya taarifa ya habari, TBC1, kulikuwa na mahojiano ya mwandishi wa TBC na Babu wa Loliondo.
Kati ya aliyoyaongea, Babu anasema, kuwa Mungu ndiye aliyepanga bei ya tiba ya kikombe iwe shilingi mia tano. Kuwa alimwonyesha mia tano! Na Mungu akamwambia wageni walipe dola moja!
Tafsiri yangu;
Pamoja na kuwa mwandishi hakumuuliza Babu maswali magumu, bado Babu wa Loliondo hakunisogeza hata hatua moja kutoka kwenye msimamo wangu. Kuwa tiba ya Babu ni Abrakadabra.
Tujiulize swali moja tu; hivi Mungu huyo ni Mungu gani anayebagua waja wake. Kuwa wengine walipe mia tano na wengine dola moja?
Jamani, hivi Mungu huyu wa Babu wa Loliondo naye anafuatilia exchange rate kila siku? Itakuwaje basi, shilingi ikipanda au kushuka thamani dhidi ya dola ya Marekani? Babu itabidi aoteshwe haraka ndoto nyingine ili abadilishe bei ya kikombe!
Na kwenye taarifa ya habari iliyofuatia ikaripotiwa, kuwa Serikali imeshindwa kutoa tamko jana juu ya tiba ya Babu kwa vile Babu amesema kamati iliyoundwa iende kwanza Loliondo!
Mnajua tena mambo haya ya imani! Alitamka mwanakamati mmoja kwenye TBC1. Na leo imeandikwa kwenye gazeti moja, kuwa Serikali itatoa tamko leo juu ya tiba ya ' Babu'.
Naam. Tamko hili liharakishwe kutolewa kabla ' Babu' hajaoteshwa ndoto, kuwa ' Tamko Lisitishwe hadi itakapotamkwa tena!'. Na nani? Fikiri mwenyewe.
Si ilipata kusemwa, kuwa kila kukicha, kuna kioja kinazuka kutoka Afrika!
Maggid
Iringa,
Jumapili, Machi 27, 2011
Kwa yeyote mwenye kutaka kuhakikisha anaweza piga simu any traffic Control Tower haswa Arusha Control Tower!Notam pia imetokaHamna hiyo taarifa me niko loliondo na ni mkaz wa huku kila siku gari zinaflow kwa babu.