Ilikuwa mwaka 1981

Ilikuwa mwaka 1981

Hahaha! Power Mabula kabla ya kuvunjiwa Jiwe kifuani alikua akijinadi "Power Mabula mtoto wa pekee,sina Kaka wala Dada,nilizaliwa peke yangu"

Halafu anapoza Koo kwa juice ya Orange "Squash"(skuash) enzi hizo.
Mkuu unanikumbusha mbali sana, kulikuwa na Juice nyingine ya Black current.
 
Kitambo hiyo MTOTO WA MWENZIO MWANAO. Unaharibu mtaani, mama au baba wa rafiki yako anakucharaza za kutosha,na ukifika home husemi. Ukisema unakula zingine.
Bora ya jirani, hata mpita njia usiyemjua ukiharibu mbele yake atakutandika tena unashukuru kakupiga yeye kuliko lingefika nyumbani
 
Pale tabora tulikuwa na KAUTA, wengine walikuwa na Kagera Retco, Kauma, Shinyanga Retco, Kaudo, Mbeya Retco, sijui nchi hii tulijikwaa wapi tu
Waroho na wabinafsi walipochukua nchi
 
Dah... Mbona alianza mdogo Sana? Enzi hizo kuanza shule ilikuwa uwe na 19 au 20....kutokana na changamoto zake...
Hapana mimi nilianza 72 nilikuwa sijafika 10 hata mkono ulikuwa haugusi sikioni labda vile nilikwenda mwezi baada ya wenzangu kuanza
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu.
Hii ilwahi nitokea pale maeneo ya bamaga miaka ileeeee..... Nilisahau lazimika kununua maziwa (mtindi) pale nilipienda kuzoza, kisha nikamkuta Baba wa binti ndio yupo dukani.
Alafu bahati yangu mbaya, hiyo pesa (ilikua shilingi 10 ya noti) nilikua nimetumwa nikanunue chumvi dukani.....
Dukani kwa mpemba nini? Maana miaka ya nyuma Mwenge nzima maduka yalikuwa miwili tu Mwenge kijijini nyumba No. 1 na kwa mpemba karibu na hongera bar
 
Daaaaaaaaaah basi mkuu apa nakumbuka ndo nilikua natimiza miaka 25 niko na bibi enu suluwali yangu ndefu panaaa af kichwani nina aflo moja atali
Mkuu kumbe ulikuwa Bitoz mimi nilikuwa mwali nikiimbishwa naugua siku tatu nimelala kitandani kila nikiwaza nilichoambiwa ugonjwa unazidi nikiukizwa ninachoumwa sisemi
 
Mkuu kumbe ulikuwa Bitoz mimi nilikuwa mwali nikiimbishwa naugua siku tatu nimelala kitandani kila nikiwaza nilichoambiwa ugonjwa unazidi nikiukizwa ninachoumwa sisemi
Daah zamani raha sana
 
Acheni uongo mie nilikua darasa la sita ukikutana na kidume hata hakijakusemesha unajicheshachekesha kweli nature ni balaa.
Mkuu hapa hakuna muongo ila kumbuka hata malaya walikuwepo tulikuwa nao madarasani na ndio hao waliokuwa wanajichekesha hata kwa walimu pia kuwa darasa la sita si sababu mkuu wengine hadi tunamaliza la saba hatujui vyekundu wala vyeupe hasa uongo uko wapi?
 
Mkuu hapa hakuna muongo ila kumbuka hata malaya walikuwepo tulikuwa nao madarasani na ndio hao waliokuwa wanajichekesha hata kwa walimu pia kuwa darasa la sita si sababu mkuu wengine hadi tunamaliza la saba hatujui vyekundu wala vyeupe hasa uongo uko wapi?
Sikuamanisha vibaya lakini asante kwa matusi na kibaya sikuwa nakujibu wewe.Pia jifunze ustaarabu hatua tuliyofikia tumeshatoka kwenye unyani nahisi wewe tulikusahau huko.
 
Mkuu kumbe ulikuwa Bitoz mimi nilikuwa mwali nikiimbishwa naugua siku tatu nimelala kitandani kila nikiwaza nilichoambiwa ugonjwa unazidi nikiukizwa ninachoumwa sisemi
Unataka kuniambia ulizaliwa mwaka 1964???
 
Back
Top Bottom