Jaji Chande: Washiriki wa ghasia walibeba silaha mbalimbali jambo ambalo haliruhusiwi kisheria kwenye maandamano ya amani

Jaji Chande: Washiriki wa ghasia walibeba silaha mbalimbali jambo ambalo haliruhusiwi kisheria kwenye maandamano ya amani

Sijapewa username bado

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,659
Reaction score
2,621

.......tatu, washiriki wa ghasia za wakati na baada ya uchaguzi mkuu walibeba silaha za aina mbalimbali, zikiwemo mawe, nondo, mkuki, sururu, fimbo, marungu, visu, vibiriti, vipulizi, bunduki, manati, kombeo, rato, mapanga; jambo ambalo haliruhusiwi kisheria katika maandamano ya amani.

Hii ni kinyume cha sheria na taratibu za kimataifa; Ibara ya 21 ya Mkataba wa Haki za Binadamu na Raia na Kisiasa mwaka 1966, Haki kando Ibara ya 11 ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na za Watu mwaka 1981, na Ibara ya 10 na 11 ya Mkataba wa Ulaya wa Haki za Binadamu mwaka 50.

Na kitaifa, Ibara ya 18 na 21 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haviruhusu maandamano ya watu waliobeba silaha. Jaji Chande
 
Hao wauaji hawana aibu. Hizo sheria za kimataifa zinaruhusu mauaji ya maelfu ya wananchi, hata walio ndani ya nyumba zao??

Mwenye video ya yule mama wa Arusha aliyepigwa risasi mgongoni na kuuawa huku akikimbia atuwekee hapa tuone kama alikuwa na silaha yoyote
 
Chande Choko you're part and parcel of tyrant system that killed thousands of Tanganyikans.
 
Kwa kuzingatia sheria na kanuni zinazotawala maandamano ya amani kimataifa, kikanda na kitaifa pamoja na ushahidi uliowasilishwa mbele ya Tume, ni maoni ya Tume kuwa kilichotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025 hakikuwa maandamano ya amani. Matukio hayo yalikuwa nje ya kinga zote za sheria na kanuni hizo. Tume inasisitiza kuwa tofauti kati ya maandamano halali na ghasia iliyopangwa ni muhimu kwa utawala wa sheria na amani ya taifa. Ushahidi unaonyesha wazi hatua zilizochukuliwa #RipotiYaTumeImefichua
#TumeYaUchunguziReport


Wafanya Vurugu Walilipwa
IMG-20260426-WA0041.jpg
 
Ripoti original mmeichoma moto mkaisoma ya Kabudi ndio maana msomaji akashindwa kuisoma kwa ufasaha.
Mfanano wa ripoti na hotuba ni kiashiria cha kuandaliwa na mtu mmoja ambaye ni kabudi.
Body language ya msomaji inajielekeza kuwa alikuwa kwenye kitisho cha kuuliwa na alikuwa kwenye maeneo mawili tofauti na double tasks yaani mwili ulikuwa ikulu na nafsi ilikuwa kwenye sala hivyo kukosa kujiamini.
Jiandaeni tu kuelekea the Hague hakuna namna. Na kabudi atawachoma tu.
 
Back
Top Bottom