Ilikuwa mwaka 1981

Ilikuwa mwaka 1981

Dah... Enzi hizo mie Suka wa daladala.... Nabadilisha tu madem wa jangwani.... Hata ndom zilikuwa zinapatikana kwa shida sana
Enzi hizo miaka ya 1977 pale ukumbi wa Savannah maeneo ya Ubungo, ukimilikiwa na Mzee Makao, Maquis Du Zaire walikua wakipiga mitindo ya Sanifu na Ogelea piga mbizi baadaye ukumbi huo ukaitwa White House. Nakumbuka siku zele Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge. Ukumbi wa Mpakani baadaye ulibadilishwa jina kuwa Silent Inn. Kisha baadae pakaja kua Kanisa.
 
Enzi hizo miaka ya 1977 pale ukumbi wa Savannah maeneo ya Ubungo, ukimilikiwa na Mzee Makao, Maquis Du Zaire walikua wakipiga mitindo ya Sanifu na Ogelea piga mbizi baadaye ukumbi huo ukaitwa White House. Nakumbuka siku zele Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge. Ukumbi wa Mpakani baadaye ulibadilishwa jina kuwa Silent Inn. Kisha baadae pakaja kua Kanisa.
Vijana jazz usiwasahau. Pia unawakumbuka wakina Bichuka, Shabani Dede.
 
Vijana jazz usiwasahau. Pia unawakumbuka wakina Bichuka, Shabani Dede.
Mkuu....,
Sikuzile Kinondoni ilkuwa inawaka moto kwa Vijana siku ya Jumapili. Lang'ata ambayo baadae ilikuja kuwa Club ASET na sasa kanisa, palikuwa ndo ukumbi wa Dansi za kuanzia mchana kwa Bendi ya Maquis. Ukija hapa mbele Vijana Jazz Pambamoto awamu ya pili chini ya uongozi wa Hemed Maneti walikuwa nao kila Jumapili mchana wanaporomosha Dansi, na siku hiyo ilipewa jina Vijana Day. Kwa kweli Maquis walikuwa wanajaa watu na Vijana wanajaa watu. Kulikuweko na wapenzi wa kudumu wa Vijana kama ilivyokuwa Maquis. Wakati huo nyimbo kama Ngalula, Makumbele zilikuwa zinalia Lang'ata huku Vijana wanateremsha Shingo feni, Ngapulila, Azda. Ushindani huu ulilazimisha bendi kujitahidi kupiga vizuri na kwa displine au la wapenzi wanahamia bendi jirani. Kuna wakati Vijana Jazz walikuwa wanaanza muziki saa kumi na moja jioni na kupumzika saa tatu na nusu usiku kisha kumaliza dansi saa nne. Maquis wakawa wanaanza saa kumi na kumaliza saa tano usiku. Na wakaanza kuruhusu mtu yeyote atakayekuwa kapigwa muhuri wa kuruhusu kutoka nje ya ukumbi Vijana Jazz,aliruhusiwa kuingia Maquis bure. Vijana wakabadili ratiba na kuanza kupiga saa 9 mchana, kwa mtindo wa bandika bandua, yaani muziki nonstop. Na kufuta kupumzika hadi saa tano. Hiyo ndo ilikuwa raha kwa wapenzi. Vijana haikuwa na show wakati wa Maneti, Lakini show ilikuja baadae katika kukabili show ya Maquis ambayo ilikuwq nzuri sana chini ya mwalimu wao Wabangoi. Majina makubwa yalitawala madansi hayo Maquis kulikuwa na Dekula Vumbi kwenye solo,second solo Mbwana Cox (aliyetoka Vijana Jazz), banza Mchafu Bass, Nguza Viking, Adios, Tshimanga Assossa,Parashi Lukumbule Vijana Jazz kulikwa Shaaban Wanted, Hemed Maneti, Eddy Sheggy, Adam Bakari, Kida Waziri, Abou Semhando, Rashid Pembe na wengine wengi, basi raha kila jumapili ilikuwa kama tamasha
 
Mkuu....,
Sikuzile Kinondoni ilkuwa inawaka moto kwa Vijana siku ya Jumapili. Lang'ata ambayo baadae ilikuja kuwa Club ASET na sasa kanisa, palikuwa ndo ukumbi wa Dansi za kuanzia mchana kwa Bendi ya Maquis. Ukija hapa mbele Vijana Jazz Pambamoto awamu ya pili chini ya uongozi wa Hemed Maneti walikuwa nao kila Jumapili mchana wanaporomosha Dansi, na siku hiyo ilipewa jina Vijana Day. Kwa kweli Maquis walikuwa wanajaa watu na Vijana wanajaa watu. Kulikuweko na wapenzi wa kudumu wa Vijana kama ilivyokuwa Maquis. Wakati huo nyimbo kama Ngalula, Makumbele zilikuwa zinalia Lang'ata huku Vijana wanateremsha Shingo feni, Ngapulila, Azda. Ushindani huu ulilazimisha bendi kujitahidi kupiga vizuri na kwa displine au la wapenzi wanahamia bendi jirani. Kuna wakati Vijana Jazz walikuwa wanaanza muziki saa kumi na moja jioni na kupumzika saa tatu na nusu usiku kisha kumaliza dansi saa nne. Maquis wakawa wanaanza saa kumi na kumaliza saa tano usiku. Na wakaanza kuruhusu mtu yeyote atakayekuwa kapigwa muhuri wa kuruhusu kutoka nje ya ukumbi Vijana Jazz,aliruhusiwa kuingia Maquis bure. Vijana wakabadili ratiba na kuanza kupiga saa 9 mchana, kwa mtindo wa bandika bandua, yaani muziki nonstop. Na kufuta kupumzika hadi saa tano. Hiyo ndo ilikuwa raha kwa wapenzi. Vijana haikuwa na show wakati wa Maneti, Lakini show ilikuja baadae katika kukabili show ya Maquis ambayo ilikuwq nzuri sana chini ya mwalimu wao Wabangoi. Majina makubwa yalitawala madansi hayo Maquis kulikuwa na Dekula Vumbi kwenye solo,second solo Mbwana Cox (aliyetoka Vijana Jazz), banza Mchafu Bass, Nguza Viking, Adios, Tshimanga Assossa,Parashi Lukumbule Vijana Jazz kulikwa Shaaban Wanted, Hemed Maneti, Eddy Sheggy, Adam Bakari, Kida Waziri, Abou Semhando, Rashid Pembe na wengine wengi, basi raha kila jumapili ilikuwa kama tamasha
Umenikumbusha mbali sana Manet, jamaa alikuwa na talent, nikakumbuka sherehe ya kuadhimisha miaka kumi ya umoja wa Vijana ilifanyika Moshi, nilikuwa Weruweru basi tulipata bahati ya kukaa mbele, nilimuoana Manet kwa mara ya mwisho.
 
Enzi hizo miaka ya 1977 pale ukumbi wa Savannah maeneo ya Ubungo, ukimilikiwa na Mzee Makao, Maquis Du Zaire walikua wakipiga mitindo ya Sanifu na Ogelea piga mbizi baadaye ukumbi huo ukaitwa White House. Nakumbuka siku zele Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge. Ukumbi wa Mpakani baadaye ulibadilishwa jina kuwa Silent Inn. Kisha baadae pakaja kua Kanisa.
Dah... Yaani kama juzi tu chief...
 
Back
Top Bottom