Ilikuwa mwaka 1981

Ilikuwa mwaka 1981

Good old days...napenda sana enzi hizo, kabla dunia haijawa digitalised na internet..maisha yalikuwa magumu, ila sijui kwa nini nayaona mazuri ...
Hata movie napendelea za zamani kuliko sasa, au za sasa ila matukio ya zamani
 
Shule za Sekondari zilikuwa za aina mbili tu, za SERIKALI na za KULIPIA. Na walionda hizo za KULIPIA tuliwaona......!
Kwani siku hizi zipo za aina ngapi? Kuna ya tatu imeongezeka au kuna moja imepungua?
 
Naona humu ni wa miaka ya 50 na 60. Ngoja wa 2000_
 
Sikuzile Bima Lee ilikuwa ikimilikiwa na Shirika La Bima La Taifa ( National Insurance Corporation, NIC), bendi hii ilitikisa vilivyo enzi zake, ilikuwa inakusanya nguli wengi wenye uwezo wa hali ya juu na waliochangia mafanikio makubwa katika bendi hiyo.
Miongoni mwa nguli hao, kulikuwa na waimbaji kama vile, Shaaban Dede ‘Super Motisha’, Othman Momba ‘Sauti ya Chuma’, Jerry Nashon ‘Dudumizi’ na Roy Bashekanako, na wenigine wengi.
Kwa upande wa ala, Bima lee ilikuwa imekusanya ‘mafundi’ kemkemu, kama akina Joseph Mulenga ’Spoiler’, Abdallah Gama, Suleiman Mwanyiro ‘Computer’, Hamis Mnyupe, Shaaban Lendi pamoja na Ally Rashid.
Na kama walikuwa na bendi ya taarabu vile, Bima modern taarab
 
Ahaa! Wewe ndiyo ulikuwa unanipiga makwenzi nikinyoa kipara eh? Halafu nikivaa safari buti zangu unanifanyia Wow wow kama mbwa! Nimeshakujua!! Sasa hivi mi msoja,njoo tena!

Ha ha ha aise hivyo viatu ilikuwa ni shida,
Ila sasa ukivaa heshima!
 
Miaka hiyo nilikua na ndoto ya kuwa rais wa Tanzania ila ndio hivyo tena baba wa taifa aliendelea kuvaa viatu.
 
Hapo bado hata karanga zilizo liwa nifanyike mbegu bado hazijapandwa
 
Back
Top Bottom