Ilikuwa mwaka 1981

Ilikuwa mwaka 1981

Na umeliweka kwenye wanga... mgongoni kuna malinda ya mraba, na mabegani pia....

Kuna wakati BLUEE ILIKUWA INAHUSIKA
Usisahau na Buibui!! Ila sisi wa mjini tulikuwa tunatumia karatasi flani hivi za kupasia!! Basi unakuta ina picha ya kijimaua,unanyunyiza maji kidogo kwenye shati Kisha unabandikia kipicha chako na kukipasi!! Oow! Those good old days!
 
Dah... Ulisalimika na kichapo siku hiyo??
Ilibidi nirudi home mbio huku nikiwa nahema kwanguvu, nilipo ulizwa tatizo, nikasema nimeijia tochi nikatafute pesa imeanguka. Tena nikajifanya nina haraka isije tokea mpintanjia akaiokota....
Ndipo mama akanipa pesa nyingine na akasema sio rahisi kuipata pesa ilio anguka usiku ule....
 
Enzi hizo miaka ya 1977 pale ukumbi wa Savannah maeneo ya Ubungo, ukimilikiwa na Mzee Makao, Maquis Du Zaire walikua wakipiga mitindo ya Sanifu na Ogelea piga mbizi baadaye ukumbi huo ukaitwa White House. Nakumbuka siku zele Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge. Ukumbi wa Mpakani baadaye ulibadilishwa jina kuwa Silent Inn. Kisha baadae pakaja kua Kanisa.
Shikamoo mzee!
 
Hapana mwaka huo hao walikuwa hawajaja. Alikuwapo mtu anaitwa Belesa Kakere. Hao walikuja kunako 1984

Mkuu Belesa Kakere wakati huo yuko na Marehemu Marijani Rajab namkumbuka kwenye kipande hiki cha wimbo nadhani unajua,
"Shangazi yakooo nae kakusihi sanaaaaaa, uje kumuona mama Magreti ukapuuza ". Aaah acha tu nyimbo zilikuwa zamani siku hizi kelele tu Mkuu!
 
Mkuu Belesa Kakere wakati huo yuko na Marehemu Marijani Rajab namkumbuka kwenye kipande hiki cha wimbo nadhani unajua,
"Shangazi yakooo nae kakusihi sanaaaaaa, uje kumuona mama Magreti ukapuuza ". Aaah acha tu nyimbo zilikuwa zamani siku hizi kelele tu Mkuu!


Hiyo ilikuwa DAR INTERNATIONAL wana SUPER BOMBOKA na sio BIMA LEE. Hapo walikuwa pia na Cosmas na Fresh Jumbe...
 
J
marijani rajabu marijani.jpg

Marijan Rajab aka Doza
 
Back
Top Bottom