Mimi siyo kama nakuringia, yaani ndivyo nilivyo kama sikujuwi hata habari yangu hautaisikia....ila ukinisalimia nitakujibu. Mimi niliachana kusalimia kina dada miaka 7 iliyopita kwani ilikuwa kila nikiwasalimia dada habari yako, wao wanarudisha kwa kuniambia wanangu hawajala jana, au nataka pango la nyumba la mwaka mzima. Nimeuliza tu habari nashushiwa mizigo ndiyo maana nikaacha kusalimu. Tafadhali nisamehe, yaani ni uamuzi wangu tu wa kuuchuna kwani sitaki mizigo ya kujitakia wakati kula wanakula wengine vyombo nioshe mie.