IKULU: Kikwete si mmiliki DOWANS!

Salva hawezi kumgeuka boss wake, unategemea aseme eti JK ndiye mmiliki? Just a common sense is enough hata akikanusha aseme basi nani mmiliki hadi Ikulu, yaani Ikulu inamwogopa?

Jibu wote mnajua, tunajua, we can't get fooled anymore, the end
 
IKULU INAWEZA IKATUMIA ZA LUGHA ZA KIHUNI KIWANGO HIKI KWELI???

Jamani pamoja na usemi kwamba kamtumikie KAFIRI upate mradi wako, hili la Mwandishi Mwandamizi wa habari wa ngazi yake Dr Salva Rweyemamu kutilia sahihi taarifa yenye matusi ya nguoni na lugha za kihuni kiasi hiki si tu kupaka masizi rekodi yake zuri katika taaluma yake bali zaidi ni kudhalilisha taasisi yenyewe ya urais ambayo taarifa hii ilionekana kutafuta kutetea.

Nani angetegemea taarifa kutoka ikulu iweze kubeba manena yaliouchi kiasi hiki!! Hivi ni kweli kwamba hakukwepo na maneno mengine yenye STAHA zaidi ambazo zingeweza kutumika kukidhi haja ya kutuma ujumbe ule ule bila kutafuta kupunguzia hadhi Dr Slaa mbele ya macho ya jamii??

Kama ni kweli ikulu ilihamaki kiasi hicho kwamba wametajwa wao kumiliki Dowans wakati wao wanamfahamu mtu mwingine kuwa ndiye mmiliki halisi kwa nini wasingechukua tu hatua ya kuanika majina yenyewe ili ndio Dr Slaa apate kuumbuka utamu zaidi. Au waliona vipi uvivu wa kumfikisha mtu huyu muongo mkubwa Dr Slaa Mahakamani ili akachukuliwe hatua za kisheria?

Kwa watu wenye busara zao hawahitaji maneno zaidi mtu kuwaeleza kwa kiwango gani watu WALIVYOGUSWA PABAYA na taarifa ya mwaka mpya ambayo Dr Slaa aliwakarimia Wa-Tanzania wenzake juu ya kampuni bubu la Dowans Tanzania Limited.

Hebu mtu yeyote jisomee kipande hiki cha taarifa inayodaiwa chanzo chake ni ikulu yetu pale Magogoni, ukaipime kisha ukajipe jibu mwenyewe akilini mwako.

... Taarifa kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu
‘aliyechanganyikiwa' na ‘mzabinazabina' ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha...
 
Rweyemamu ndio aliyechanganyikiwa na mzabizabina kwasababu alitakiwa kujibu hoja tu badala ya kuleta matusi na kejeli. Watanzania wa sasa sio wajinga kama anavyodhani yeye, tumempuuza yeye (Rweyemamu) na Ikulu yao. Watwambie nani wamiliki wa Dowans badala ya mipasho!! Shame on you Rweyemamu
 
BTW, watu wa bara bana kwa kujitutumua na kiswahili chao cha kilugha! mzabinazabina ndio mdudu gani ?lolz. Neno sahihi ni kizabizabina.
 
Mwaka huu tataona na kuskia mengi! ila namashaka udikteta utashika kasi karibuni maana kwakuwa wanauficha moto kwa mikono tusishangae ukawaunguza,
Tanzania ya mambumbumbu ilishapita!! leo tunajua mbivu na mbichi.
 
We bwana Rweyemamu, acha kujidhalilisha kwa kukubali kutumika kutoa matamko yasiyo na tija kwa taifa,tena ukome wewe na wenzako kumwita Rais wangu mwongo wakati hutaki kueleza ukweli ni nani mmiliki wa DOWANS.
 
Tumeshatambua kuwa Dr Slaa ndiye mkweli,mzalendo na mwenye uchungu na nchi hii,sio nyinyi mafisadi.madudu yenu yakianikwa hadharani mnaanza kutoa matusi.Bado hamjaweza kufuta kile alichosema rais wangu slaa(PhD),sanasana mmeuchochea moto kwani tutaendelea kumtaja Jk kuwa ndie fisadi namba 1 na mmiliki wa dowans mpaka mtakapomtaja wenyewe....sh*¤n*z!
 
Hizi lugha zinazotumika ikulu ni zilezile za kitchen party kama Sofia Simba. Wanataka kutuaminisha kuwa Dk. Slaa amechanganyikiwa kama walivyojaribu kutuaminisha uongo wa UDINI katika uchaguzi mkuu na baada. Hivi kama mtu amekukashifu na kukuchafulia jina, kwa nini husiende mahakamani ili sheria ichukuwe mkondo wake.

Hii santuri ya kumwita Slaa kichaa tuliwahi kuisikia, watu wakatoa vitisho.......hadi sekunde chache kabla sijatundika hii post HAKUNA mtu ambaye alishakwenda mahakamani kumfungulia Slaa mashtaka. Kama kaumizwa hatutaki porojo za mipasho, fuata haki yako mbele ya vyombo vya sheria.
 
Hii habari kwenye gazeti la Tanzania Daima badala kusema Salvatory Rweyemamu aliwahi kuwa mhariri anayeheshimika, lingesema kuwa Salvatory Rweyemamu aliwahi kuajiriwa na Richmond kufanya kazi ya Public Relations kusaidia kuijenga Richmond/Dowans kwenye media ya Tanzania. Salva pia alihojiwa na kamati ya Bunge iliyoongozwa ya Mwakyembe na kukiri kuwa yeye alitambulishwa kwa Richmond/Dowans na Rostam Aziz. Hizi kumbukumbu zote ziko kwenye ripoti ya Mwakyembe.

Nimekunwa sana na namna unavyotaka attribute ya rweyemamu iandikwe. Hivyo ndivyo inavyopaswa isomeke. Hongera.
 
KIKWETE NI MKURUGENZI MTENDAJI WA DOWANS....Te he te he. Naskia Rostam aziz ni mkurugenz msaidiz, Lowasa ni mweka hazna na Chenge ni mwanasheria wao. Hyo ndio tim ya Dowans
 
JK amekanusha kwamba yeye siyo mmiliki wa dowans, tena katumia maneno makali mweli, ila ukweli unabaki pale kwamba, Kama Rais ana jukumu la kulitaarifu humu kwamba uozo wa Dowans unafanya na nani. Ikiwa ataki kutuambia mmilikiwa Dowans, basi yeye ndo mwenyewe
 
Kama Mkwere siyo mhusika. Kwa nini wahusika hawasemwi?

Au suala bado liko mahakamani?

Si hukumu ilishatolewa? Au nimezuzuka?
 
Kama anakanusha kwamba Kikwete sio mmoja wa wamiliki basi ataje wamiliki halali....kwa nini waseme ati tutafute ni nani wamiliki wakati serikali ndio inaowajua?

Wakanushe weeee kama ilivyokuwa EPA baadaye waanze kuona haya......Go Dr. goooo.....Aluta Continua.....
 
KURUGENZI ya Mawasiliano Ikulu imeelezea kukerwa kwake na hatua ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kumtaja rais Jakaya Kikwete kuwa alihusika katika uzembe uliosababisha taifa kutakiwa kuilipa kampuni ya Dowans sh bilioni 185 kama fidia.
Taarifa kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu ‘aliyechanganyikiwa' na ‘mzabinazabina' ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha.
Rweyemamu katika taarifa yake hiyo iliyoonyesha waziwazi kuandikwa na mtu mwenye hasira, chuki na dharau ama kwa Dk. Slaa, CHADEMA na Tanzania Daima alikwenda mbele na kumwita kiongozi huyo wa kisiasa kuwa ni mtu hatari.
JK hawezi kuukwepa ukweli kuwa ana masilahi mazito ndani ya DOWANS.......na huu hapa ni ushahidi:-

a) Uteuzi wa Dr. Idrissa Rashid kuiongoza Tanesco ulijaa mizengwe kibao..............Dr. Rashid mwenyewe alikiri kuwa pamoja na kuwa nafasi hiyo ilitangazwa magazeti yeye hakuiomba ila JK alimwomba amsaidie kwenye nafasi hiyo...........Hivyo pamoja na sheria ya Tanesco kuweka wazi kuwa Mtendaji Mkuu wa Tanesco atateuliwa na Bodi, JK aliingilia Bodi kinyume na sheria pale alipombandika swahiba wake pale Tanesco..........................Swali la kujiuliza JK alikuwa anatetea masilahi ya nani kwa kuiingilia Bodi ya Tanesco?

b) Kwa vile Dr. Rashid hakuwa ameteuliwa na Bodi ya Tanesco hivyo na yeye hakuona sababu ya kuishirikisha Bodi tajwa katika utoaji wa zabuni ya uzalishaji wa umeme kwa Richmond na hata zabuni hiyo haikupitishwa kwa Bodi ya zabuni na matokeo yake kampuni kivuli ikapewa kazi hiyo..........Kulingana na rekodi zilizopo Brella, Richmond haijawahi kusajiliwa hapa nchini na hivyoufanyaji wake wa kazi ulikuwa ni batili na haikupaswa kupewa zabuni tajwa............Haya ni makosa ya kijinai yaani "criminal negligence" na JK anashindwa nini kumkabidhi swahiba wake Takukuru? Hapa inaonyesha kabisa hoja za Dr. Hosea kwa Wikileaks ni za kweli ya kuwa JK ndicho kikwazo kikuu cha utawala bora hapa nchini...............

c) Baada ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme ikaikabidhi kazi hiyo kwa DOWANS ambao walitumia dola za kimarekani 7.5 milioni kununua mitambo hiyo ya kuzalisha umeme kazi ambayo ilikuwa ndani ya uwezo wa Tanesco.........................na hivyo hawakuhitaji mzabuni yeyote..........................

d) Tanesco kwa matendo yao walimhalalisha Dowans kuwa mzabuni wa kumrithi Richmond bila ya kupata kibali cha Bodi ya zabuni....

e) Baada ya mkataba kuisha Tanesco wakaishinikiza serikali kununua mitambo ya DOWANS kwa bei ambayo ilikuwa ni zaidi ya mara 20 ya bei ambayo Dowans walinunulia mitambo tajwa.......na ili kuishinikiza serikali kuinunua mitambo ya DOWANS, Tanesco wakaamua kuitumia Mahakama Kuu kwa kuwazuia Dowans wasiondoke na mitambo yao kwa amri ya Mahakama.....................bila sababu za kimsingi.........

f) Kutokana na uvunjaji huo wa mkataba kwa kutumia visingizio vya kuwa Dowans hawajalipa kodi, Msuluhishi akaibandika Tanesco jumla ya Tshs 185 Bilioni ikiwa ni zaidi ya mara 18 ya gharama ambazo Dowans walinunulia ile mitambo...............

g) Mwanasheria Mkuu ametoa ushauri Dowans walipwe huku uamuzi huo haujatoa sababu ni maeneo yapi Tanesco ilikuwa imekiuka huo mkataba kitendo ambacho kwa AG makini angeligangamala kuhakikisha analifungua shauri upya hapa Dar kupinga tuzo ambayo hata sababu za Tuzo hiyo hazifahamiki.........................Katika hukumu hiyo Msuluhishi aliahidi kutoa sababu lakini sababu hizo hakuzitoa sasa mdaiwa ataonaje kuwa katendewa haki? Hivi tuna AG au tunambabaishaji ambaye anadai ameipitia hiyo hukumu na ameona ipo beneti na tuilipe tu...............Hawa ndiyo wateule wa JK ambao kazi yao kuu ni kujenga mazingira ya kulipora taifa hili changa..........

h) JK hayuko tayari kumfikisha mahakamani Dr. Idrissa Rashid kwa sababu alimpeleka pale Tanesco kwenda kulipora hilo shirika la umma na hasa ukizingatia ya kuwa JK alivunja sheria za tanesco kuhakikisha Dr. Rashid anakwenda pale tanesco kulifilisi shirika hilo na mzigo wa hasara hizo kutupiwa raia wanyonge ambao kosa letu ni kumvumilia JK ambaye hana sifa ya kuliongoza taifa hili masikini duniani........

i) Haya ni mazingira yanaonyesha ya kuwa JK ni mshiriki kwenye mradi wa Dowans na hata kama jina lake halipo ila linawakilishwa na swahiba wake wa karibu Rostam Aziz kama ushahidi huu kwenye hukumu ya Dowans unavyothibitisha ambao tanesco wenyewe waliutumia ................................

RostamAziz.jpg
 
Hivi inakuwaje nchi inakuwa na watu 'wazushi' na 'vizabizabina' na ambao ni hatari kwa 'usalama wa taifa' lakini wakati huo huo hawakamatwi na vyombo vya usalama? Kama Dr. Slaa ni mtu wa namna hiyo kwa nini hawamkamati? Mimi nashindwa kuelewa hapo! Lakini mkuu wa nchi alipata kusema kuwa 'ukiambiwa kitu jaribu kuchanganya na za kwako'!!
 
Back
Top Bottom