#COVID19 Ifike mahali Askofu Gwajima na wengine wa jinsi yake wadhibitiwe kiserikali na kichama kuhusu chanjo ya UVIKO-19

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Serikali yetu imekata shauri la kuleta na kutoa chanjo ya UVIKO kwa watanzania/wananchi wake. Imeweka wazi kabisa kuwa chanjo ipo na ni ya HIARI. Yaani, mtanzania atakayeridhia kuchanjwa atachanjwa.

Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.

Haipendezi na wala si jambo la kufurahiwa kuona mwananchi au kiongozi wa kiserikali, kisiasa au kidini akijitokeza hadharani kupinga na kukejeli chanjo ya UVIKO kama afanyavyo Askofu Gwajima. Askofu Gwajima ni kiongozi wa kidini na kisiasa.

Kuendelea kukosoa chanjo ya UVIKO hadharani kwa Askofu Gwajima ni kuonyesha jinsi anavyoikosoa hadharani Serikali na hata msimamo wa chama chake cha Mapinduzi kinachounda serikali husika. Lazima adhibitiwe kiserikali na kichama.

Kama kuna yeyote wa kupinga chanjo, afanye hivyo kwa kufaidi haki yake ya HIARI ya chanjo husika. Hakuna maana wala faida kujipambanua kwa umma na kuleta suitafahamu isiyo na mantiki. Serikali iheshimiwe!
 
Hayo ni mawazo ya kidiktekta, kwani serikali haiwezi kukosolewa ?

Msimamo wa serikali sio lazima uwe msimamo wa wananchi.

Muacheni Gwajima ateme yake, serikali ifanye kazi yake kuwashawishi wananchi waamini hizo chanjo, sio kila anayepingana mawazo na serikali apigwe rungu.

Japokuwa sikubaliani na Gwajima , lakini naheshimu haki yake ya kutoa mtazamo wake.
 
Wasomi wa nchi hii bure kabisa!

Acheni watu wawe huru kusema mradi hawavunji sheria.

Wewe bado primitive kabisa licha ya kujiita/kuwa Mwanasheria.

Akili hizi za kijimaa ndio zinafanya watu wenye fikra na mitazamo tofauti na serikali au watawala watekwe, wauwawe, wabambikiziwe makesi, n.k.

Serikali ni kikundi cha watu ambacho kinaweza kuwa sahihi au laa juu ya jambo fulani, hivyo usitake wote tuwaze kama wao.

Usisahau ni hawa hawa walikuwa sehemu ya serikali ya Magufuli iliyopinga chanjo ile leo wamegeuka.

Tumia akili yako kutafuta msimamo sahihi kuhusu hili jambo na usiwe bendera fuata upepo.
 
Serikali yetu imekata shauri la kuleta na kutoa chanjo ya UVIKO kwa watanzania/wananchi wake. Imeweka wazi kabisa kuwa chanjo ipo na ni ya HIARI. Yaani, mtanzania atakayeridhia kuchanjwa atachanjwa.

Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.

Haipendezi na wala si jambo la kufurahiwa kuona mwananchi au kiongozi wa kiserikali, kisiasa au kidini akijitokeza hadharani kupinga na kukejeli chanjo ya UVIKO kama afanyavyo Askofu Gwajima. Askofu Gwajima ni kiongozi wa kidini na kisiasa.

Kuendelea kukosoa chanjo ya UVIKO hadharani kwa Askofu Gwajima ni kuonyesha jinsi anavyoikosoa hadharani Serikali na hata msimamo wa chama chake cha Mapinduzi kinachounda serikali husika. Lazima adhibitiwe kiserikali na kichama.

Kama kuna yeyote wa kupinga chanjo, afanye hivyo kwa kufaidi haki yake ya HIARI ya chanjo husika. Hakuna maana wala faida kujipambanua kwa umma na kuleta suitafahamu isiyo na mantiki. Serikali iheshimiwe!
Nimeishia hapa.

"Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu."

Nani kasema huo ni Msimamo wa Serikali..?
 
KATIBA INASEMAJE? NCHI HII INAHITAJI WASOMI KULIKO WAPUMBAVU. YAANI LEO HII TUNAKATAZA GWAJIMA ASISEME ANACHOAMINI? TUKABISHANA NAYE KWA HOJA MNATAKA AKAMATWE?AZUIWE? AITWE GAIDI? SIVYO?

Serikali yetu imekata shauri la kuleta na kutoa chanjo ya UVIKO kwa watanzania/wananchi wake. Imeweka wazi kabisa kuwa chanjo ipo na ni ya HIARI. Yaani, mtanzania atakayeridhia kuchanjwa atachanjwa.

Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.

Haipendezi na wala si jambo la kufurahiwa kuona mwananchi au kiongozi wa kiserikali, kisiasa au kidini akijitokeza hadharani kupinga na kukejeli chanjo ya UVIKO kama afanyavyo Askofu Gwajima. Askofu Gwajima ni kiongozi wa kidini na kisiasa.

Kuendelea kukosoa chanjo ya UVIKO hadharani kwa Askofu Gwajima ni kuonyesha jinsi anavyoikosoa hadharani Serikali na hata msimamo wa chama chake cha Mapinduzi kinachounda serikali husika. Lazima adhibitiwe kiserikali na kichama.

Kama kuna yeyote wa kupinga chanjo, afanye hivyo kwa kufaidi haki yake ya HIARI ya chanjo husika. Hakuna maana wala faida kujipambanua kwa umma na kuleta suitafahamu isiyo na mantiki. Serikali iheshimiwe!
 
Hayo ni mawazo ya kidiktekta, kwani serikali haiwezi kukosolewa ?

Msimamo wa serikali sio lazima uwe msimamo wa wananchi.

Muacheni Gwajima ateme yake, serikali ifanye kazi yake kuwashawishi wananchi waamini hizo chanjo, sio kila anayepingana mawazo na serikali apigwe rungu.

Japokuwa sikubaliani na Gwajima , lakini naheshimu haki yake ya kutoa mtazamo wake.
Umeongea jambo ambalo wote wameingia kwenye mtego wapinzani na ccm. Sababu Gwajima anachukiwa na wengi. Mimi sikubaliani naye kimawazo lakini nmempenda sababu mbili.
1. Hajataka kuwa mnafiki
2. Anatumia haki yake kikatiba
 
Nimetafuta jibu zuri la kukujibu lakini nimekosa baada ya kugundua kuwa wewe ni punguani Kama punguani wengine. Nimeshia tu kusema mtak.....o wako!
 
Wasomi wa nchi hii bure kabisa!

Acheni watu wawe huru kusema mradi hawavunji sheria.

Wewe bado primitive kabisa licha ya kujiita/kuwa Mwanasheria.
Nchi hii haina wasomi. Ina wapuuzi flani ambao hawajielewi. Gwajima sioni kosa lake.... Serikali yenyewe imesema ni hiyari. Na Gwajima ana hoja zake. Marekani wanapinga kwa kila namna hakuna wanaokamatwa au kufungwa
 
Malizia....

"Kama wanavyodhibitiwa wapinzani kiserikali na kichama kwa kukiuka msimamo wa Serikali juu ya katiba mpya?"
 
Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.
Maswali ya Askofu Gwajima yangejibiwa kwa ufasaha na hao wataalamu wetu, bila shaka tusingefika huku

Serikali imeyataka haya. Tulizoea kuona watu wakijazishwa consent form kwenye operations ambazo chances of ending up dead ni 50%. Unapowambia watu wajaze form kabla ya kuchanjwa na kwamba hutahusika na litakalompata mtu baada ya kudungwa, then watu wana haki ya kurelate chanjo na potential outcome ya operation - 50% chances of dying early.

Huko ulaya nako zinakotoka chanjo, watu “wanahongwa” $100 ili wakubali kudungwa chanjo🙂
 
Serikali hiyo hiyo ndio ilikuwa inasema tujifukize na mpaka mawaziri wengine kufikia kutwambia corona ni scam.

Na kwasababu Gwajima ni CCM acha wararuane
 
Serikali yetu imekata shauri la kuleta na kutoa chanjo ya UVIKO kwa watanzania/wananchi wake. Imeweka wazi kabisa kuwa chanjo ipo na ni ya HIARI. Yaani, mtanzania atakayeridhia kuchanjwa atachanjwa.

Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.

Haipendezi na wala si jambo la kufurahiwa kuona mwananchi au kiongozi wa kiserikali, kisiasa au kidini akijitokeza hadharani kupinga na kukejeli chanjo ya UVIKO kama afanyavyo Askofu Gwajima. Askofu Gwajima ni kiongozi wa kidini na kisiasa.

Kuendelea kukosoa chanjo ya UVIKO hadharani kwa Askofu Gwajima ni kuonyesha jinsi anavyoikosoa hadharani Serikali na hata msimamo wa chama chake cha Mapinduzi kinachounda serikali husika. Lazima adhibitiwe kiserikali na kichama.

Kama kuna yeyote wa kupinga chanjo, afanye hivyo kwa kufaidi haki yake ya HIARI ya chanjo husika. Hakuna maana wala faida kujipambanua kwa umma na kuleta suitafahamu isiyo na mantiki. Serikali iheshimiwe!
Kesho anaibuka tena kivingine kama Delta Variant subirini kumsikia
 
Serikali yetu imekata shauri la kuleta na kutoa chanjo ya UVIKO kwa watanzania/wananchi wake. Imeweka wazi kabisa kuwa chanjo ipo na ni ya HIARI. Yaani, mtanzania atakayeridhia kuchanjwa atachanjwa.

Msimamo wa Serikali ni msimamo wetu watanzania. Serikali ni yetu na inatupasa kuiheshimu na kufuata uamuzi wake hasa ule ambao unagusa masuala ya afya na umetanguliwa na masuala ya kitaalamu.

Haipendezi na wala si jambo la kufurahiwa kuona mwananchi au kiongozi wa kiserikali, kisiasa au kidini akijitokeza hadharani kupinga na kukejeli chanjo ya UVIKO kama afanyavyo Askofu Gwajima. Askofu Gwajima ni kiongozi wa kidini na kisiasa.

Kuendelea kukosoa chanjo ya UVIKO hadharani kwa Askofu Gwajima ni kuonyesha jinsi anavyoikosoa hadharani Serikali na hata msimamo wa chama chake cha Mapinduzi kinachounda serikali husika. Lazima adhibitiwe kiserikali na kichama.

Kama kuna yeyote wa kupinga chanjo, afanye hivyo kwa kufaidi haki yake ya HIARI ya chanjo husika. Hakuna maana wala faida kujipambanua kwa umma na kuleta suitafahamu isiyo na mantiki. Serikali iheshimiwe!
Kwa hiyo serikali ina dhamana hadi kuwafanya wananchi kuwa panya wa majaribio, na wewe unajiita lawyer.....
 
Wakati mkitaka Askofu atolewe roho, wenzenu wanagawa noti kwa watu wao wanaoipinga chanjo.
20210731_155359.jpg
 
Back
Top Bottom