GE2025 If not lip services, Lissu anaachiwa, Chadema inashiriki uchaguzi, TAL Mgombea Urais, tunafanya uchaguzi mkuu huru na wa haki kweli

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,722
Wanabodi
Kufuatia mazungumzo ya rais wa TLS juzi kuomba kuonana na Rais Samia,kumuomba pamoja na mambo mengine,ni kuomba Lissu aachiwe,kanuni za uchaguzi zirekebishwe,Chadema ishiriki uchaguzi.

Kiukweli,sijawahi kuona rais msikivu kama Samia!,siku ya Jumanne mtu aombe kumuona rais,kesho yake Jumatano nafasi ikapatikana Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Rais Samia ni msikivu, apewe maua yake. Vipi Serikali yake, Bunge na mahakama ni wasikivu? Kama sio inamanisha

Siku zote nimekuwa nikilalamika humu kuwa wasaidizi wa Rais Samia sheria hawamsaidii,wanamuogopa na kushindwa kumwambia ukweli,hii kesi ya uhaini ya Lissu ni hakuna kitu pale! Pre GE2025 - Wazalendo Wapenda Haki, Msiwe na Wasiwasi, Uhaini ni Matendo na Mipango Mkakati wa Kuutenda, Sio Maneno!, Maneno ni Sedition tuu na Sio Treason!

TLS ni wasaidizi wa Samia wa sheria,hivyo alipoingia tuu,Rais Samia akatoa msimamo wake atafanya kazi na TLS ya aina gani Tujikumbushe Kauli hii ya Rais Samia Atafanya Kazi na TLS ya Aina Gani? Hizi ni Salaam kwa Mwabu,. Swali ni is He A Bow Down Type or a Stand Firm?. hii kwa lugha nyingine ni atafanya kazi na TLS puppets!。

Hivyo Mabukusi aliposhinda urais wa TLS, tulimshauri Hakuna Ubishi Mwabukusi ni Mwanaharakati, Je TLS Yake Iwe ya Kiharakati, Au Asilete Harakati Zake kwenye TLS Yetu, Ibaki Kuwa Profesheno Body?

TLS ilipoanza kwenda na jinsi ile Samia anataka,tuliipongeza Pongezi TLS Kumpongeza Rais Samia kwa Hatua Alizochukua Ngorongoro, TLS Imeonyesha Professionalism na Sio Unaharakati! Big Up Rais wa TLS

Sisi TLS kama TLS, individual members wa TLS, hatumuogopi Rais Samia hivyo nilishauri tumweleze ukweli Rais Samia Mgeni Rasmi AGM ya TLS: Wanasheria Tumweleze Ukweli Kuhusu Ubatili wa Katiba Yetu na Sheria Zetu, Turudishe Haki Kuu ya Msingi

Na mimi individually,nimemshauri sana Rais Samia Pre GE2025 - Je, Wajua bila minimum Reforms za Katiba, Uchaguzi Mkuu wote utakuwa ni batili?Sababu,INEC,Katiba ya ZnZ na Sheria Mpya ya Uchaguzi Zote ni Batili

  1. Rais Samia alianza vizuri kwa kuunda kikosi kazi na tukampongeza ila akaja kujichanganya Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.
  2. Pre GE2025 - Maoni yangu kwenye Mkutano wa Vyama vya Siasa kuhusu Muswada wa Sheria Mpya ya Uchaguzi. Muswada sio batilifu, ni Muswada batili
  3. Nilibahatika kupata fursa kuchangia kwenye vikao vitatu
    Mchango wangu kikao cha kwanza JNICC DSM
    View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=8EEhNkNVlONuph1bMchango wangu mkutano wa pili JNICC DSM
    View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=ky_DyqMycv_SBH7IMchango wangu Kamati ya Bunge,Bungeni Dodoma
    View: https://youtu.be/lBC3xKODSvY?si=fbeeEcbqtBYjuyrJ
  4. Tukasisisitiza Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
  5. Rais Samia alipotimiza miaka miwili madarakani, tukamoingeza na kumshauri Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!
  6. Ngoma ilipotua tuu Bungeni,tukakimbilia kupongeza bila kujua kilichomo!Lile fupa lililowashinda marais wanaume 4, rais mwanamke 1 aligegeda kama mlenda!. Miswada 3 ya ukombozi mpya wa taifa letu yatua bungeni asubuhi hii
  7. Kuja kujua, kumbe ni kiini macho!,wakatuletea mvinyo wa zamani kwenye chupa mpya Je, wajua Muswada Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2023 ni batili? Ni mvinyo wa zamani, kwenye chupa mpya? Why ubatili huu?
  8. Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa
  9. Kwa mujibu wa Katiba yetu ya 1977 katiba ya Zanzibar inayotambuliwa ni ile ya 1984,ambayo sasa imefutwa na toleo la 2010 liliunda GNU Zanzibar,katiba hiyo ni batili,kwa Zanzibar ni halali lakini kwa JMT hii ni katiba ya uhaini dhidi ya serikali ya JMT Tanzania Nchi 1 ya JMT, Zanzibar Kujiita Nchi, Sio Uhaini?. Zanzibar Iadabishwe Kuondoa Ubatili wa Katiba Yake ili Tuitambue au Tumchelee Mwana Kulia? Uchaguzi wa Zanzibar ni halali kwa katiba yao na batili kwa katiba ya JMT!,bila kufanya minimum reforms uchaguzi wa Zanzibar ni batili!
  10. Zanzibar wana serikali ya mseto,katiba ya JMT,haina serikali ya mseto,rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT,hata ACT ishinde kwa asilimia 99%,atakayetangazwa kushinda lazima awe CCM, ili upinzani uweze kushinda Zanzibar na kutangazwa,lazima upinzani ushinde bara kwasababu katiba yetu JMT ya 1977 ni katiba ya CCM enzi za chama kushika hatamu,hivyo ni katiba ya mfumo wa chama kimoja!Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Ushauri wote huo,haikusaidia kitu,ila
jana hili limetokea kama zali, TLS imekutana na Samia,na tumemweleza hili la Lissu Rais wa TLS: Tumezungumza mengi na Rais Samia

Kama hoja hizi za TLS ni za kweli, na sio Lip Services, then Tundu Lissu anakwenda kuachiwa, kanuni za uchaguzi zinarejewa, Chadema inafuta NRNE ,Inashiriki Uchaguzi, TAL Mgombea Urais wa Chadema, Tunafanya Uchaguzi Mkuu Huru na wa Haki Kweli!

NB:Angalizo,isije kuwa TLS wamepigwa tuu sound,lip services!Je, kuna uwezekano baadhi ya Viongozi wetu wanatoa baadhi ya Ahadi kwa "Paying lip Services"?

Rais Samia, yeye kama Samia,hana shida na mtu!,alimnasua Mbowe toka kwenye ile kesi mbaya,akafanya nae maridhiano,akawaahidi watagawana nusu mkate!,wahafidhina wa CCM wakawa ni tatizo Nimemwelewa sana Mbowe, usipoteze imani na Rais Samia. Alivyo kwa Kauli na Matendo hawezi kuwa ni yeye! hivyo hili pia wanaweza kumgomea Mama!

Hili la watu kupigwa sound, niliwahi kumshauri Mama Mama don't preach. I think we've had enough of Preaching about law, justice & human rights. Would you Please just Practice what you Preach?

Pia tulimsisitiza Mama Ombi kwa Rais Samia, tunakushukuru kwa mahubiri mazuri kuhusu haki, tunakuomba utende unachohubiri yasibaki kuwa maneno tuu lakini vitendo ni tofauti

Kuhusu kuachiliwa kwa haka ka simba ka Kizimkazi, Pongezi Rais Samia kwa Tanzania kuwa Kinara Uhuru wa Habari, EAC, Vipi Kale ka 'Simba ka Kizimkazi' Mnaonaje Kaachiwe?, Kanatuvurugia Sana Amani?

Japo Chadema walitaka minimum reforms za katiba,lakini baada ya Bunge kuvunjwa,there is nothing that can be done kwenye katiba!, wabunge wote wa Chadema walipatikana kwa katiba hii hii, hivyo tumewashauri Pre GE2025 - Hata Kusipofanyika Reforms, 2025 CHADEMA Ina Fursa!, Ila They Are Just Too Blind to See!, Hawajitambui! No Election ni Utopia!. Wake Up!

Mungu Ibariki Tanzania

Paskal
 
Kwanini nyote mnasema hivyo baada ya Mwabukusi kumwona Rais? Mayalla, Rostam and Kikwete are the Kingpins of the "atrocities" we are going through as a nation!! Huyu Mamam hana kauli tena!
 
Akiachiwa na marekebisho ya sheria yakafanyika kwa kiasi kikubwa na wakashiriki uchaguzi,hii itakua changamoto kubwa kwa ACT na CHAUMMA,naona itakua ni kinyume na matarajio yao na CHADEMA itapata wabunge wengi sana kuonyesha mabadiliko yalifanyika.
 
BIla shinikizo CCM hawawezi kukubali reforms zifanyike sasa ambazo wamezigomea kuanzia miaka 2 nyuma. walikuwa na maana yao kuzigomea toka mwanzo. Hilo watanzania tusahau.
Na wanajua endapo watakubali Refroms nini kitatokea, si wajinga.

At comfort zone, CCM hawawezi kukubali reforms.
 
Itakuwa miracle ya kwanza kutokea Tanzania warekebishe kanuni Kwa hiari kama inavyotaka...It's purely a lip service...Wenzio wameshajipanga kuanza campaign na hakuna wakuzuia ndiyo lugha Yao and it is true!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…