Kubenea anatupatia sana watanzania na gazeti lake. Ila ni ukweli usiyopingika kuwa hana uwezo wa kupangilia uongo wake. Mara anakuja na habari ya uhakika kuhusu afisa wa Polisi kuwa ndiye aliyemteka Ulimboka mara aje na jina Rama. Angalia hata kwenye taarifa yake anasema Rama alikuwa anasisitiza kuwa Ulimboka atamke kama alitumwa na CDM wakati huo huo anasema taarifa toka ndani ya TISS ni kwamba chombo hicho kinaamini Ulimboka alitumwa na CDM. Unaona Kubenea anavyojaribu kuupotosha Umma wa Watanzania kuwa TISS wanaamini kuwa Ulimboka alitumiwa na CDM katika sakata la Mgomo kwa kumtaka Rama kuwa alikuwa akisisitiza hilo. Kwa akili ya haraka haraka najiuliza swali hili, "TAMKA KAMA CDM WALIKUTUMA" hiyo sentensi Mwanalalisi waiipata kutoka kwa nani? Ulimboka mwenyewe au mtumishi kutoka dara hiyo ya Usalama wa Taifa?