Idara ya Usalama wa Taifa yakanusha tuhuma

Idara ya Usalama wa Taifa yakanusha tuhuma

Status
Not open for further replies.
Eti "tushirikiane kuhakikisha nchi yetu iendelee kuwa salama" lini tumekuwa salama kama kikundi cha watu kinaweza kwenda hazina na kuchota kiasi cha fedha watakazo, ndege tena za jeshi zina ingia na kutoka huku ziki beba lasilimali za taifa. Hayo ni baadhi ya matukio yanayofanyika mbele ya wanaojiita usalama wa taifa!
 
Yakanusha kuwa haikupanga kumuua Dr. Ulimboka na kwamba kinachotangazwa na vyombo vya habari ni vipande vya taarifa visivyo na ukweli wowote na wananchi wapuuze.

TAMKO RASMI KUHUSU TUHUMADHIDI YA IDARA YA USALAMA WATAIFA

Matukio yaliyotajwa katikatuhuma hizo yanachunguzwa na Jeshi la Polisi ambacho ndicho Chombo ChenyeDhamana, na kwa Maslahi ya Taifa si vizuri kuachia upotoshaji huo uendelee.

Imetolewa na Idara ya Usalama wa Taifa,

Hapo kwenye red, polisi nadhani wameshamaliza uchunguzi wao, na wamempeleka mtuhumiwa mahakamani na tumeambiwa tusiongee tena hili jambo kwa sababu liko mahakamani, sasa sijui uchunguzi gani anaongelea ni upi. La msingi hapa watuambie (with evidence) Rama sio mtu wao na hakupata kuwasiliana na DR. uli.
 
Yakanusha kuwa haikupanga kumuua Dr. Ulimboka na kwamba kinachotangazwa na vyombo vya habari ni vipande vya taarifa visivyo na ukweli wowote na wananchi wapuuze.

Tunaolalamika ni wananchi wenyewe, kama wanaufahamu ukweli watumie taaluma yao kututoa mashaka
 
Hivi nchii hii inausalama wa taifa kweli,taasisi nyeti kama ile inatapatapa kutoa ukweli,badala yake inazidi kushusha heshima yake kwa kutoa majibu dhaifu na ya kilevi.bora wangesema ukweli ila walipewa maelekezo.tungewaelewa vizuri.
 
Ya charles teila yatawakuta wengi,tusubiri mda,siku na mwaka.
 
Si wawafungulie mashtaka Mwanahalisi!
Kama kweli hawakuhusika wanakazana nini kukanusha na si kuchukua hatua?
 
tamko fupi lakini lenye maneno mazito.ni vyema mwanahalisi lipelekwe mahakamani likaeleze vizuri na kwa ufasaha


Duh!!! Unasipidi ya kuandikaaa!!! Tatizo post nyingiii, pumba za kufa mtu!! Wewe kama sio Zoka basi utakuwa Msangi!!
 
Kwa hali ya Kawaida tu Ukimwagiwa Tindikali huwezi kurudisha uwezo wako wa kufikiri tena kama awali..

Mwanahalisi wasamehewe tu.. Nadhani hawako normal kbs!!

Mimi (bila hata kutumia taaluma yangu ya kiDaktari)....nina wasi wasi na 'uwezo wako wa kufukiri'. Tindikali inamwagwa mwilini, effect zake zinaishia kwenye ngozi na macho...hainyonywi kusababisha 'systemic effect'....inahusiana vipi na uwezo wa kufikiri wa Kubenea? Tungekuwa na CT scan hospitalini kwetu ningeshauri ufanyiwe CT scan ya ubongo..unaweza kukuta tope tu limejaa huko, huku we ukiamini kuna ubongo!
 
Yakanusha kuwa haikupanga kumuua Dr. Ulimboka na kwamba kinachotangazwa na vyombo vya habari ni vipande vya taarifa visivyo na ukweli wowote na wananchi wapuuze.
Wakuu hawa sio usalama wa taifa bali ni usalama wa (M)dhaifu, hoja dhaifu, matendo dhaifu kila kitu dhaifu, ...........................dhaifu.
Had they been strong they would have come out very early on this obvious issue, all the same none expected them to own their shameful act(s)
 
It is pathetic! kwa Idara kufikia kiwango cha kutoa statement ambayo ni extremely weak!.......reform kwenye Idara is long overdue........ili kulinda heshima ya Idara........Ni wakati muafaka wa ku-reshufle na kustaafisha baadhi ya key positions.......

Ogah umenena.......
 
it is pathetic! Kwa idara kufikia kiwango cha kutoa statement ambayo ni extremely weak!.......reform kwenye idara is long overdue........ili kulinda heshima ya idara........ni wakati muafaka wa ku-reshufle na kustaafisha baadhi ya key positions.......
sio ku-reshufle, ni kui-dissolve kuanza upya!
 
Jamani mimi sielewwi haya masuala yanakwendaje. Kila siku tunaambiwa hili suala liko mahakamani sasa inakuwaje hawa watu tena wanalijadili? Hata muheshimiwa spika aliwaonya wale wote walokuwa wakilizungumzia suala hili bungeni. Sasa sijui nani atawaonya hawa jamaa kwa kukiuka taratibu za kimahakama kwani kila nikisoma hii thread naona kabisa wanaingilia au wanaweza 'kuinfuluence' maamuzi ya kimahakama.
 
shame on you tiss, nawashauri kama si kweli basi wapelekeni mwanahalisi mahakamani@@@!!!
 
Kwani kukanusha tuu ndio kunaweka facts hadharani??

Haya kama ni hivi na sie watanzania tunakanusha basi taarifa ya Usalama wa Taifa kutohusika, kwa hio what is the final stand??

Mie nina suggestion moja kuwa kikao kijacho cha bunge kisiwe na swala jingine la kujadili zichambuliwe report zote zilizoundiwa tume kuanzia 3yrs ago!! Then agenda ya mwisho iwe Analysis ya value for Money katika kuunda tume kwa matukio yanayotokea Tanzania, kama vipi iundwe Organ kama Sumatra, Ewura iwe ni maalamu kwa kuchunguza matukio ya Ki-Tanzania kama Migomo ya madaktari, utekaji, migomo ya waalimu,mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, ili tu apply kwa vigezo.... Pesa za walipa kodi jamani!!!!!
 
...usalama wanasema kuwa kuna watu wanalitumia gazeti kwa lengo lao, kwa kuwa wao ni usalama wa Taifa watueleze ni watu gani hao? namna nyingine zinabaki kuwa inteligensia za Wilson...
 
Mbona hiyo taarifa yenyewe haijasainiwa na yeyote?, wanaogopa kusaini ili siku ukweli ukijulikana wairuke taarifa yao so will be no responsible person
 
Yakanusha kuwa haikupanga kumuua Dr. Ulimboka na kwamba kinachotangazwa na vyombo vya habari ni vipande vya taarifa visivyo na ukweli wowote na wananchi wapuuze.

Wangekuwa wamenena vyema kama wangeorodhesha 'sifa zao nzuri' ili kuepuka kuchafuliwa jina lao. Tatizo sifa za usalama wa taifa ni nzuri machoni mwao na watawala lakini ni mbaya na za kutisha machoni pa wananchi. Naamini sifa nzuri ya mwizi ni kuiba sana bila kushikwa, sifa nzuri ya mwanafunzi ni kufaulu mitihani yake kwa kiwango cha juu sana; sasa kati ya hao wawili na yuko tayari kutangaza sifa zake? Tafakari!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom