I don’t wanna marry him, what should I do?

I don’t wanna marry him, what should I do?

Nilianzisha mahusiano na huyu mwanaume miaka miwili na nusu ilopita. Baada ya miezi 6 ya mahusiano nilishtuka kajihamishia kwangu. Sikuweza kumfukuza i just decided to play along though sikupendezwa. Akachukua majukumu ya kulipia rent na matumizi mengine ya ndani.

Kuhusu mambo ya matumizi yuko vizuri tu, japo nafanya kazi na nina biashara zangu pia ila bado hunipa pesa za matumizi. Amenitambulisha nafikiri karibia kwa ndugu zake wote na wanajua tunaishi pamoja, lakini mimi anawafahamu marafiki zangu wawili tu.

Sikuwa tayari kumtambulisha sana kwa upande wangu maana i was having second thoughts. Amekuwa akihitaji mtoto tangu tunaanza mahusiano hivyo nikawa na mtihani wa kujitahidi nisishike mimba kwa kipindi chote hicho.

Amekazania sana issue ya kutaka tufunge ndoa, nimeshalikwepa sana ili ajiongeze lakini naona haelewi somo. Naogopa kumwambia direct kuwa siko tayari kuolewa na yeye, i never fell in love with him. We rushed into this, didnt give me time to digest this. Now i feel like am suffocating. Nimejaribu sana kumpenda nimeshindwa.

Nitumie njia gani ambayo haitomuumiza sana, au itakayomfanya yeye aniache? Nisaidieni maana am tired living a lie.
Una hamu ya kufa wewe
 
Hicho kilikuwa ni kidokezo tu tena cha nyongeza. Ushauri wangu na wa wadau wengine hapa bila shaka utakusaidia katika maamuzi yako...na always akili za kuambiwa changanya na zako !!!
Kwa kifupi kuna member wengi wamempa ushauri mzuri sana kazi ni kwa ke kuufanyia kazi
 
Pole. Basi tafuta kisababu kitakachomfanya akereke na akuache kabisa,au mtengenezee fumanizi either la sms au namna yoyote ili iwe sababu ya ww ku walk out. Ila usithubutu kumuacha maana unaweza kujikuta huolewi Maisha yako yote,ila mngekua hamjawahi kuishi pamoja ingekua simple sana. Ila miaka miwili si mchezo
Ki sheria huyo ni mke wake tayari
 
Just tell him the truth face to face. Yes he’ll be hurt but the truth will set him free and look elsewhere for a wife to be.

If you don’t mind is there any specific reason(s) why you’re unable to fall in love with him!?

Nilianzisha mahusiano na huyu mwanaume miaka miwili na nusu ilopita. Baada ya miezi 6 ya mahusiano nilishtuka kajihamishia kwangu. Sikuweza kumfukuza i just decided to play along though sikupendezwa. Akachukua majukumu ya kulipia rent na matumizi mengine ya ndani.

Kuhusu mambo ya matumizi yuko vizuri tu, japo nafanya kazi na nina biashara zangu pia ila bado hunipa pesa za matumizi. Amenitambulisha nafikiri karibia kwa ndugu zake wote na wanajua tunaishi pamoja, lakini mimi anawafahamu marafiki zangu wawili tu.

Sikuwa tayari kumtambulisha sana kwa upande wangu maana i was having second thoughts. Amekuwa akihitaji mtoto tangu tunaanza mahusiano hivyo nikawa na mtihani wa kujitahidi nisishike mimba kwa kipindi chote hicho.

Amekazania sana issue ya kutaka tufunge ndoa, nimeshalikwepa sana ili ajiongeze lakini naona haelewi somo. Naogopa kumwambia direct kuwa siko tayari kuolewa na yeye, i never fell in love with him. We rushed into this, didnt give me time to digest this. Now i feel like am suffocating. Nimejaribu sana kumpenda nimeshindwa.

Nitumie njia gani ambayo haitomuumiza sana, au itakayomfanya yeye aniache? Nisaidieni maana am tired living a lie.
 
..Baada ya miezi 6 ya mahusiano nilishtuka kajihamishia kwangu......

Hapo umedanganya. Kuna vitu vilivyokufanya umpende mpaka ukakubali ahamie kwako. Pengine vitu hivyo kwa sasa havipo au vimebadilika. Au pengine ulitaka tu akusaidie katika hayo mambo ya rent na mengineyo na sasa umefikia melengo yako unamwona hafai. Kizungumkuti cha dunia: wenzio wanahaha kutafuta waume wa kuwaoa.

Ili kuzuia mikanganyiko jikaze tu umwambie ukweli. Toa sababu zako. Hata kama umepata mwanaume mwingine unayedhani anakufaa zaidi we mwambie tu. Hii ni bora kuliko kuanza kumfanyia visa na mambo mengine ya kitoto. Kama anakupenda kikweli atakuelewa na hatakulazimisha lakini lifanye hili kwa heshima, utashi mwema, uwazi na unyenyekevu. Kama unaona ni vyema unaweza kumwambia mbele ya mchungaji wenu au mtu mwingine mwenye mamlaka kama mama yako...Ukifanya vinginevyo si ajabu tutakuja kukusoma ukiwa kama mwathirika wa hawa wanaocharangwa mapanga na kuchomwa visu na wapenzi wao baada ya wapenzi wao kuwekeza sana tena kwa muda mrefu halafu wanakuja kuwafanyia visa vya kijinga mwishoni mwishoni huku...

Mungu Akuhekimishe katika hili
Naomba nimtetee, inawezekana ukajikuta mtu keshajihamishia bila makubaliano mbona hata ninyi hili huwa mnalalamika kuwa tunajihamishia? Mtu anaweza kulala leo, kesho anakuja na nguo ya kulalia, keshokutwa anakuja na nguo plus viatu vya kubadilisha pamoja na vitu vyake anavyotumia, kumbuka muda huo anabebelea hivyo vitu vile alivyoleta mwanzo havirudishi. Anaanza kulala siku moja baadae siku mbili, tatu, baadae unakuta kamaliza wiki bila kurudi kwake ndipo hapo anaanza kufahamu hata mambo ya kodi, mboga n.k. Ni hapo tu ndio nimetofautiana na wewe vinginevyo naungana na wewe
 
Uvelia my daughter.., unajua mapenzi ni jambo linalo beba hisia kubwa sana,mtu anapoangukia katika haya hata kama ni mtu mwenye umri mkubwa unaweza muonea huruma pale yakimshika pabaya

Sawa uyo mtu umetokea kumkinai pengine hata sababu ya msingi unaweza usiwe nayo,unaweza nambia hana future uitakayo,he is not romantic,n.k ambayo ni nonsense iyo ipo hata mimi ishanitokea ivo kwa mwanamke wa ujana wangu alinichoka tu

Alivyokuja kuniambia live kwamba hajisikii kuwa nami yani anatokea kunichukia kuliko kawaida muda mwingine hatamani hata kunisikia alinambia live

Mwanzo nikahisi ni utani au labda ananipima n.k ila ulikua ni ukweli dhahiri


Sasa Uvelia huyo bwana ako tambua fika utakapo mwambia atajua mawazoni mwake ni utan au unampima na kama unavyojua sisi viumbe ni wagumu kuamin

Njia nzuri ya kujitoa kwake watafute watu wenye busara uwaelezee hata kama si wazazi basi wawe ni wanandoa alafu ndo mkae myamalize


Amua moja indecision si nzuri
 
Naomba nimtetee, inawezekana ukajikuta mtu keshajihamishia bila makubaliano mbona hata ninyi hili huwa mnalalamika kuwa tunajihamishia? Mtu anaweza kulala leo, kesho anakuja na nguo ya kulalia, keshokutwa anakuja na nguo plus viatu vya kubadilisha pamoja na vitu vyake anavyotumia, kumbuka muda huo anabebelea hivyo vitu vile alivyoleta mwanzo havirudishi. Anaanza kulala siku moja baadae siku mbili, tatu, baadae unakuta kamaliza wiki bila kurudi kwake ndipo hapo anaanza kufahamu hata mambo ya kodi, mboga n.k. Ni hapo tu ndio nimetofautiana na wewe vinginevyo naungana na wewe
Mwanaume usiyempenda kweli anaweza kufanya hivyo na ukamwachia tu ukaendelea kuishi naye kwa miaka miwili na nusu anakukula na kukuhudumia we umeuchuna tu? Khantwe siamini !!!
 
Sometimes namwelewa mtoa mada sometimes simuelewi.

Namuelewa kwa sababu najua huwezi lazimisha kupenda.

Nashindwa kumuelewa kwa sababu naona ana ego flani hivi, maana sentensi tatu anatamka, "biashara zangu". Sitaki kuendelea kufanya profiling, lakini, a brother is in a very difficult situation.

Yote kwa yote, Lazima ufanye uamuzi kwa faida yako, faida yake, na faida ya Jamhuri.
 
dont treat her like a cerebrity ,coz if u do she treat u as fan,

aliawahi sema mwana jf mmoja siku zilizopita

Hahaha Soo True

Mazee hii kweli kabisa. Hata dem awe mpole mkarimu mtaratibu vp...unavyozidi kumtukuza tu ndio unazidi kuharibu.

Ishanikuta sanaa hii.

Na zile tongoza za kubembeleza ndio kabisaaa
 
Mwanaume usiyempenda kweli anaweza kufanya hivyo na ukamwachia tu ukaendelea kuishi naye kwa miaka miwili na nusu anakukula na kukuhudumia we umeuchuna tu? Khantwe siamini !!!
Inawezekana kabisa, hivi wewe hufahamu kuwa kuna watu wanaolewa na watu wasiowapenda kabisa huku wakiwa na matumaini kuwa watawapenda taratibu. Lakini pia huenda bibie alikuwa na kaupendo kwa jamaa kidogo ila alipoishi nae akagundua vitu fulani asivyovipenda kutoka kwake, (sio lazima aviseme maana vingine vinakuwaga vya kipuuzi tu ila vinapunguza sana mvuto). Au labda bibie alijikuta amemchoka tu na akajikuta hana hamu nae tena japo mwanzo alikuwa na mapenzi naye (hii pia huwa inatokea)
 
Sometimes namwelewa mtoa mada sometimes simuelewi.

Namuelewa kwa sababu najua huwezi lazimisha kupenda.

Nashindwa kumuelewa kwa sababu naona ana ego flani hivi, maana sentensi tatu anatamka, "biashara zangu". Sitaki kuendelea kufanya profiling, lakini, a brother is in a very difficult situation.

Yote kwa yote, Lazima ufanye uamuzi kwa faida yako, faida yake, na faida ya Jamhuri.
Hahaha kwa hiyo mtu kusema biashara zangu ni kosa? Katika eneo hilo alitakiwa asemeje eti, biashara zetu? Wanaume watu wa ajabu sana ninyi
 
Hahahaha, sijataka kuendelea kufanya profiling.

Ila mtoa mada alikuwa anamaanisha anaweza kusimama kwa miguu yake.

Nadhani angekuwa hana biashara zake, hii mada tusingeiona.
Hahaha kwa hiyo mtu kusema biashara zangu ni kosa? Katika eneo hilo alitakiwa asemeje eti, biashara zetu? Wanaume watu wa ajabu sana ninyi
 
Back
Top Bottom